2 Wafalme 25 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Wafalme 25:1-30

Kuanguka Kwa Yerusalemu

(2 Nyakati 36:13-21; Yeremia 52:3-30)

125:1 Yer 21:2; Eze 21:22Hivyo katika mwaka wa tisa wa utawala wa Sedekia, katika siku ya kumi ya mwezi wa kumi, Nebukadneza mfalme wa Babeli, akiwa na jeshi lake lote, alifanya vita dhidi ya Yerusalemu. Akapiga kambi nje ya mji na kuuzunguka mji pande zote. 2Mji ulizungukwa na jeshi mpaka mwaka wa kumi na moja wa utawala wa Mfalme Sedekia. 325:3 Law 26:26; Mao 2:20Ilipowadia siku ya tisa ya mwezi wa nne, njaa ikazidi kuwa kali sana ndani ya mji, hadi hapakuwa na chakula kwa ajili ya watu. 425:4 Ay 30:14; Eze 33:21Kisha ukuta wa mji ukavunjwa, na jeshi lote likakimbia. Wakaondoka mjini usiku kupitia lango lililokuwa kati ya kuta mbili karibu na bustani ya mfalme, ingawa Wakaldayo walikuwa wameuzunguka mji. Wakakimbia kuelekea Araba. 525:5 Law 26:36; Eze 12:14Lakini jeshi la Wakaldayo likamfuatia mfalme na kumpata katika sehemu tambarare za Yeriko. Askari wake wote wakatengwa naye na kutawanyika, 625:6 Isa 22:3; Hes 34:11naye akakamatwa. Akapelekwa kwa mfalme wa Babeli huko Ribla, mahali ambapo hukumu yake ilitangazwa. 725:7 Kum 28:36; Eze 40:1Wakawaua wana wa Sedekia mbele ya macho yake. Kisha wakayangʼoa macho yake, wakamfunga kwa pingu za shaba na kumpeleka Babeli.

8Mnamo siku ya saba ya mwezi wa tano, katika mwaka wa kumi na tisa wa utawala wa Nebukadneza mfalme wa Babeli, Nebuzaradani jemadari wa askari walinzi wa mfalme, afisa wa mfalme wa Babeli, alikuja Yerusalemu. 925:9 Za 74:3-8; Amo 2:5Alichoma moto Hekalu la Bwana, jumba la kifalme, na nyumba zote za Yerusalemu. Aliteketeza kila jengo muhimu. 1025:10 Yer 50:15Jeshi lote la Wakaldayo, chini ya jemadari wa askari walinzi wa mfalme, walivunja kuta zilizoizunguka Yerusalemu. 1125:11 Law 26:44; 2Fal 24:14Nebuzaradani jemadari wa askari walinzi akawapeleka uhamishoni watu waliokuwa wamebaki katika mji, pamoja na mabaki ya watu wa kawaida, na wale waliojisalimisha kwa mfalme wa Babeli. 1225:12 2Fal 24:14Lakini yule jemadari wa askari walinzi akawaacha baadhi ya wale watu maskini kabisa ili watunze mashamba ya mizabibu na mashamba mengine.

13Wakaldayo walivunja vipande zile nguzo za shaba, vile vishikilio vya shaba vilivyohamishika, na ile Bahari ya shaba, ambavyo vyote vilikuwa katika Hekalu la Bwana. Hivyo wakaichukua hiyo shaba na kuipeleka Babeli. 1425:14 Hes 7:14; Ezr 1:7Wakachukua pia vyungu, masepetu, mikasi ya kusawazishia tambi, sahani na vyombo vyote vya shaba vilivyotumika katika huduma ya Hekalu. 1525:15 2Fal 24:13; Yer 15:13Jemadari wa askari walinzi wa mfalme akachukua vile vyetezo na yale mabakuli ya kunyunyizia, vitu vyote vile vilivyokuwa vimetengenezwa kwa dhahabu safi au fedha.

16Shaba iliyotokana na zile nguzo mbili, ile Bahari na vile vishikilio vilivyohamishika, ambavyo Solomoni alikuwa ametengeneza kwa ajili ya Hekalu la Bwana, ilikuwa na uzito usioweza kupimika. 1725:17 1Fal 7:15-22Kila nguzo ilikuwa na urefu wa dhiraa kumi na nane.25:17 Dhiraa 18 ni sawa na mita 8.2. Sehemu ya shaba juu ya nguzo moja ilikuwa na urefu wa dhiraa tatu25:17 Dhiraa 3 ni sawa na mita 1.35. na ilikuwa imepambwa kwa wavu na makomamanga ya shaba kuizunguka kote. Ile nguzo nyingine pamoja na wavu wake ilifanana na hiyo ya kwanza.

1825:18 1Nya 6:14; Yer 21:1Yule jemadari wa askari walinzi akawachukua kama wafungwa Seraya kuhani mkuu, kuhani Sefania aliyefuata kwa cheo, na mabawabu watatu. 19Miongoni mwa wale watu waliokuwa wamesalia katika mji, alimchukua afisa kiongozi wa wapiganaji, na washauri watano wa mfalme. Akamchukua pia mwandishi aliyesimamia uandikishaji wa watu wa nchi, pamoja na watu wake sitini waliopatikana ndani ya mji. 20Nebuzaradani jemadari akawachukua hao wote na kuwapeleka kwa mfalme wa Babeli huko Ribla. 2125:21 Hes 34:11Huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, mfalme wa Babeli akaamuru wanyongwe.

Hivyo Yuda wakaenda utumwani, mbali na nchi yao.

2225:22 Yer 40:5, 7; 2Fal 22:12Nebukadneza mfalme wa Babeli akamteua Gedalia mwana wa Ahikamu, mwana wa Shafani, awe msimamizi wa watu aliowaacha Yuda. 23Maafisa wote wa jeshi na watu wao waliposikia kwamba mfalme wa Babeli amemteua Gedalia kuwa mtawala, wakamjia Gedalia huko Mispa. Hawa walikuwa Ishmaeli mwana wa Nethania, Yohanani mwana wa Karea, Seraya mwana wa Tanhumethi Mnetofathi, na Yezania mwana wa Mmaaka, pamoja na watu wao. 24Gedalia akaapa ili kuwatia moyo wao na watu wao. Akasema, “Msiwaogope maafisa wa Kikaldayo. Kaeni katika nchi na kumtumikia mfalme wa Babeli, na itakuwa vyema kwenu.”

2525:25 2Fal 12:20; Zek 7:5Hata hivyo, katika mwezi wa saba Ishmaeli mwana wa Nethania mwana wa Elishama, aliyekuwa wa uzao wa mfalme, akaja pamoja na watu kumi, nao wakamuua Gedalia, na pia watu wa Yuda, pamoja na Wakaldayo waliokuwa naye huko Mispa. 2625:26 Isa 30:2; Yer 43:7Baada ya haya, watu wote kuanzia aliye mdogo sana hadi aliye mkubwa kabisa, pamoja na maafisa wa jeshi, wakakimbilia Misri kwa kuwaogopa Wakaldayo.

Yehoyakini Anaachiwa

(Yeremia 52:31-34)

2725:27 2Fal 24:12Katika mwaka wa thelathini na saba tangu Yehoyakini mfalme wa Yuda apelekwe uhamishoni, katika mwaka ule ambao Evil-Merodaki25:27 Pia aliitwa Ameli-Mariduki. alifanyika mfalme wa Babeli, alimwacha huru Yehoyakini kutoka gerezani siku ya ishirini na saba ya mwezi wa kumi na mbili. 2825:28 Ezr 5:5; Dan 2:48Alizungumza naye kwa upole na kumpa kiti cha heshima zaidi kuliko wale wafalme wengine aliokuwa nao huko Babeli. 2925:29 2Sam 9:7Hivyo Yehoyakini akayavua mavazi yake ya mfungwa, na siku zote za maisha yake zilizobaki alikula mezani mwa mfalme. 3025:30 Mwa 43:34; Es 9:22Siku kwa siku mfalme alimpa Yehoyakini posho siku zote za maisha yake.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

列王紀下 25:1-30

1西底迦執政第九年十月十日,巴比倫尼布甲尼撒率領全軍攻打耶路撒冷,在城外安營,修築圍城的高臺。 2城一直被圍困到西底迦執政第十一年。 3那年四月九日,城裡饑荒非常嚴重,百姓無糧可吃。 4城被攻破,城裡的所有士兵便在夜間穿過御花園,從兩城牆中間的門逃往亞拉巴。當時迦勒底人仍四面包圍著城。 5迦勒底軍隊追趕西底迦,在耶利哥平原追上了他,他的軍隊都四散而逃。 6迦勒底人擒住西底迦,把他押到利比拉巴比倫王,在那裡審判他。 7巴比倫王在西底迦面前殺了他的眾子,又剜去他的雙眼,把他用銅鏈鎖著押往巴比倫

聖殿被毀

8巴比倫尼布甲尼撒執政第十九年五月七日,他的臣僕——護衛長尼布撒拉旦來到耶路撒冷9放火焚燒耶和華的殿、王宮及城內所有的房屋。他燒毀了所有重要建築。 10他率領的迦勒底軍隊拆毀了耶路撒冷四圍的城牆。 11護衛長尼布撒拉旦擄去城裡剩下的百姓、投降巴比倫王的人以及其他人, 12只留下一些最貧窮的人,讓他們照料葡萄園、耕種田地。

13迦勒底人打碎耶和華殿中的銅柱、盆座和銅海,把銅運往巴比倫14並帶走了盆、鏟、蠟剪、碟子及一切獻祭用的銅器。 15護衛長還帶走了火鼎、碗等一切金銀器具。

16所羅門為耶和華的殿所造的兩根銅柱、一個銅海和一些盆座,用的銅多得無法計算。 17銅柱高八米,柱頂有柱冠,高一點三五米。柱冠周圍裝飾著銅網和銅石榴。兩根柱子都一樣。

18護衛長尼布撒拉旦擄走祭司長西萊雅、副祭司長西番亞和三名殿門守衛, 19還從城中拿住一名統管士兵的將領、王的五個親信、一名負責招兵的書記和六十名平民。 20護衛長尼布撒拉旦把他們帶到利比拉去見巴比倫王, 21巴比倫王在那裡處死了他們。猶大人就這樣被擄去,離開了家園。

基大利做猶大省長

22巴比倫尼布甲尼撒任命基大利治理猶大的餘民。基大利沙番的孫子、亞希甘的兒子。 23猶大眾將領和他們的下屬聽到巴比倫王委任基大利治理猶大的消息後,便都到米斯巴基大利。他們是尼探雅的兒子以實瑪利加利亞的兒子約哈難尼陀法單戶篾的兒子西萊雅瑪迦雅撒尼亞24基大利向他們和他們的下屬發誓,說:「你們不用害怕那些迦勒底官員。你們住在這地方服侍巴比倫王,就會平安無事。」 25七月,王室後裔以利沙瑪的孫子、尼探雅的兒子以實瑪利帶著十個人在米斯巴刺殺了基大利以及跟他一起的猶大人和迦勒底人。 26因為害怕迦勒底人報復,猶大眾人不論貴賤,都和眾將領一起逃往埃及

約雅斤獲釋

27巴比倫以未·米羅達在他執政的元年十二月二十七日,即猶大約雅斤被擄後第三十七年,施恩釋放了約雅斤28並好言相待,使他的地位高過被擄到巴比倫的其他各王。 29約雅斤脫去了囚衣,終生與巴比倫王一起吃飯。 30在他有生之年,巴比倫王供應他每天的需用。