2 Wafalme 22 – NEN & BDS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Wafalme 22:1-20

Yosia Mfalme Wa Yuda

(2 Nyakati 34; 35:20-27)

122:1 Yer 1:2; Yos 15:39Yosia alikuwa na miaka minane alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka thelathini na mmoja. Mama yake aliitwa Yedida binti Adaya, kutoka Boskathi. 222:2 Kum 5:32Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana na kuenenda katika njia zote za Daudi baba yake. Hakugeuka upande wa kuume wala wa kushoto.

322:3 2Nya 34:20; Yer 39:14Katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wake, Mfalme Yosia akamtuma mwandishi Shafani mwana wa Azalia, mwana wa Meshulamu, kwenda katika Hekalu la Bwana. Akasema: 422:4 Ezr 7:1; 2Fal 12:4-5“Panda uende kwa Hilkia, kuhani mkuu, umwambie ahesabu zile fedha ambazo zimeletwa katika Hekalu la Bwana, ambazo mabawabu wamekusanya kutoka kwa watu. 522:5 2Fal 12:5Waambie waikabidhi kwa watu walioteuliwa kusimamia kazi ya Hekalu. Waamuru watu hawa wawalipe wafanyakazi ambao wanakarabati Hekalu la Bwana: 622:6 2Fal 12:11-12wale maseremala, wajenzi na waashi. Waambie pia wanunue mbao na mawe yaliyochongwa ili kukarabati Hekalu. 722:7 2Fal 12:15Lakini hawahitajiki kutoa hesabu ya fedha walizokabidhiwa, kwa sababu wanafanya kwa uaminifu.”

822:8 Kum 31:24; Gal 3:10Hilkia kuhani mkuu akamwambia Shafani mwandishi, “Nimekipata Kitabu cha Sheria ndani ya Hekalu la Bwana.” Akampa Shafani, ambaye alikisoma. 9Kisha Shafani mwandishi akamwendea mfalme na kumpa taarifa akisema: “Maafisa wako wametoa ile fedha ambayo ilikuwa ndani ya Hekalu la Bwana na imekabidhiwa mikononi mwa wasimamizi wa marekebisho ya Hekalu.” 1022:10 Yer 36:21Ndipo Shafani mwandishi akampasha mfalme habari kwamba: “Hilkia kuhani amenipa kitabu hiki.” Naye Shafani akakisoma kile kitabu mbele ya mfalme.

11Mfalme aliposikia maneno ya kile Kitabu cha Sheria, akararua mavazi yake. 1222:12 2Fal 25:22; Isa 8:14Akatoa maagizo haya kwa Hilkia kuhani, Ahikamu mwana wa Shafani, Akbori mwana wa Mikaya, Shafani mwandishi, na Asaya mtumishi wa mfalme: 1322:13 Kum 29:24-28; Amo 2:4“Nendeni mkamuulize Bwana kwa ajili yangu, na kwa ajili ya watu na Yuda wote kuhusu yale yaliyoandikwa ndani ya kitabu hiki ambacho kimepatikana. Hasira ya Bwana ni kubwa inayowaka dhidi yetu kwa sababu baba zetu hawakuyatii maneno ya kitabu hiki. Hawajatenda kulingana na yale yote yaliyoandikwa humo kutuhusu sisi.”

1422:14 Kut 15:20Hilkia kuhani, Ahikamu, Akbori, Shafani na Asaya wakaenda kuongea na nabii mke Hulda, ambaye alikuwa mke wa Shalumu mwana wa Tikwa, mwana wa Harhasi mtunzaji wa chumba cha mavazi. Hulda aliishi Yerusalemu katika Mtaa wa Pili.

15Akawaambia, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana, Mungu wa Israeli: Mwambieni yule mtu aliyewatuma ninyi kwangu, 1622:16 Yos 23:15; Dan 9:11‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana: Nitaleta maafa juu ya mahali hapa na watu wake, kulingana na kila kitu kilichoandikwa katika kitabu hicho mfalme wa Yuda alichosoma. 1722:17 1Fal 9:9Kwa sababu wameniacha mimi na kufukiza uvumba kwa miungu mingine, na kunighadhibisha kwa sanamu zote zilizotengenezwa kwa mikono yao, hasira yangu itawaka dhidi ya mahali hapa, wala haitatulizwa.’ 1822:18 Yer 21:2Mwambieni mfalme wa Yuda, ambaye amewatuma kumuuliza Bwana, ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana, Mungu wa Israeli, kuhusu maneno uliyoyasikia: 1922:19 Isa 37:15; Yer 26:6; Law 26:31Kwa kuwa moyo wako ulikuwa msikivu na ulijinyenyekeza mbele za Bwana uliposikia kile nilichosema dhidi ya mahali hapa na watu wake, kwamba wangelaaniwa na kuachwa ukiwa, basi kwa sababu uliyararua mavazi yako na kulia mbele zangu, nimekusikia, asema Bwana. 2022:20 Isa 47:11; 1Fal 21:29Kwa hiyo nitakukusanya kwa baba zako, nawe utazikwa kwa amani. Macho yako hayataona maafa yote nitakayoleta juu ya mahali hapa.’ ”

Basi wakapeleka jibu lake kwa mfalme.

La Bible du Semeur

2 Rois 22:1-20

Le règne de Josias sur Juda

(2 Ch 34.1-2, 8-28)

1Josias avait huit ans à son avènement et il régna trente et un ans à Jérusalem22.1 De 640 à 609 av. J.-C.. Sa mère s’appelait Yedida, elle était fille d’Adaya de Botsqath. 2Il fit ce que l’Eternel considère comme juste et suivit en tout l’exemple de son ancêtre David sans jamais s’en écarter ni d’un côté ni de l’autre.

La découverte du livre de la Loi

3La dix-huitième année de son règne22.3 C’est-à-dire en 622 av. J.-C. A 16 ans, il commença à servir fidèlement le Seigneur et à 20 ans, il entreprit de purifier le pays des pratiques idolâtres (2 Ch 34.3)., Josias envoya son secrétaire Shaphân22.3 Partisan de la Réforme de Josias, protecteur de Jérémie (Jr 26.24), père de Guedalia qui sera le futur gouverneur de Juda nommé par Nabuchodonosor (25.22 ; Jr 39.14)., fils d’Atsalia et petit-fils de Meshoullam, au temple de l’Eternel. Il lui dit : 4Va trouver le grand-prêtre Hilqiya22.4 Père d’Azaria et grand-père de Seraya, le grand-prêtre exécuté au temps de la destruction de Jérusalem par les Babyloniens (25.18-20). et demande-lui de compter tout l’argent qui a été apporté dans le temple de l’Eternel et que les portiers ont recueilli. 5Que l’on remette cet argent aux entrepreneurs qui ont la responsabilité des travaux dans le temple de l’Eternel. Ceux-ci paieront les ouvriers qui effectuent les réparations dans le Temple : 6les charpentiers, les ouvriers du bâtiment, les maçons. Ils achèteront aussi le bois et les pierres de taille pour consolider l’édifice. 7On ne leur demandera pas de compte pour l’argent qui leur est confié, car ce sont des gens honnêtes.

8A cette occasion, le grand-prêtre Hilqiya annonça à Shaphân, le secrétaire : J’ai trouvé le livre de la Loi dans le temple de l’Eternel22.8 Ce qui révèle la gravité de la révolte contre l’Eternel sous Manassé. Le livre retrouvé était, soit l’ensemble du Pentateuque, soit uniquement le livre du Deutéronome..

Et Hilqiya remit le livre à Shaphân. Celui-ci le lut, 9puis il se rendit auprès du roi pour lui faire un rapport : Tes serviteurs, dit-il, ont versé l’argent qui se trouvait dans le Temple aux entrepreneurs responsables des travaux dans le Temple. 10Puis il ajouta : Le prêtre Hilqiya m’a remis un livre.

Et Shaphân se mit à en faire la lecture devant le roi.

L’intervention de la prophétesse Houlda

11Lorsque Josias entendit le contenu du livre de la Loi, il déchira ses vêtements. 12Puis il convoqua le prêtre Hilqiya, Ahiqam, fils de Shaphân, Akbor, fils de Michée, Shaphân, le secrétaire et Asaya, l’un des ministres.

13– Allez consulter l’Eternel pour moi, leur dit-il, ainsi que pour le peuple et pour tout Juda, au sujet des enseignements de ce livre que l’on vient de retrouver. Car la colère de l’Eternel est bien grande. Elle s’est enflammée contre nous, parce que nos ancêtres n’ont pas obéi aux paroles de ce livre et n’ont pas appliqué tout ce qui y est écrit.

14Alors le prêtre Hilqiya, Ahiqam, Akbor, Shaphân et Asaya se rendirent chez la prophétesse Houlda, femme de Shalloum, fils de Tiqva, petit-fils de Harhas, responsable du vestiaire du Temple. Elle habitait à Jérusalem dans le nouveau quartier. Ils lui exposèrent la situation. 15Alors Houlda leur dit : Voici ce que déclare l’Eternel, le Dieu d’Israël : « Annoncez à l’homme qui vous a envoyés à moi : 16L’Eternel dit : Je vais faire venir un malheur sur cette contrée et sur ses habitants : tout ce qui est prévu dans le livre que vient de lire le roi de Juda. 17En effet, parce qu’ils m’ont abandonné et qu’ils ont fait brûler des parfums à d’autres dieux, et parce qu’ils m’ont ainsi irrité par toute leur conduite, ma colère s’est enflammée contre ce lieu et elle n’est pas près de s’apaiser. 18Mais vous direz au roi de Juda qui vous a envoyés pour consulter l’Eternel : Voici ce que déclare l’Eternel, le Dieu d’Israël : Tu as entendu les paroles contenues dans ce livre. 19Ton cœur s’est laissé toucher, tu t’es humilié devant moi en entendant ce que j’ai décrété contre ce lieu et contre ses habitants, à savoir la dévastation et la malédiction. Tu as déchiré tes vêtements et tu as pleuré devant moi. De mon côté, moi aussi, j’ai entendu ta prière – l’Eternel le déclare ! 20C’est pourquoi je te ferai rejoindre tes ancêtres décédés et tu seras déposé paisiblement dans l’un de tes tombeaux, sans avoir vu tout le malheur que je vais amener sur cette contrée. »

Les envoyés rapportèrent cette réponse au roi.