2 Wafalme 16 – NEN & BDS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Wafalme 16:1-20

Ahazi Mfalme Wa Yuda

(2 Nyakati 28)

116:1 Isa 1:1; Hos 1:1Katika mwaka wa kumi na saba wa utawala wa Peka mwana wa Remalia, Ahazi mwana wa Yothamu mfalme wa Yuda alianza kutawala. 2Ahazi alikuwa na miaka ishirini alipoanza kutawala, akatawala huko Yerusalemu kwa miaka kumi na sita. Tofauti na Daudi baba yake, hakufanya yaliyo mema machoni pa Bwana, Mungu wake. 316:3 Law 18:21; Kum 9:4Akaenenda katika njia za wafalme wa Israeli, na hata akamtoa mwanawe kafara katika moto, akifuata njia za machukizo za mataifa ambayo Bwana alikuwa ameyafukuza mbele ya Waisraeli. 416:4 Kum 12:2; Eze 6:13Akatoa kafara na kufukiza uvumba katika mahali pa juu pa kuabudia miungu, juu ya vilima, na chini ya kila mti uliotanda.

516:5 2Fal 15:37Kisha Resini mfalme wa Aramu na Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli wakaondoka kwenda kupigana dhidi ya Yerusalemu na kumzunguka Ahazi kwa jeshi, lakini hawakuweza kumshinda. 616:6 Isa 9:12; 1Fal 9:26Wakati ule, Resini mfalme wa Aramu akaurudisha Elathi kwa Aramu kwa kuwafukuza watu wa Yuda. Kisha Waedomu wakahamia Elathi, nao wanaishi huko mpaka leo.

716:7 2Fal 15:29; Hos 10:6Ahazi akatuma wajumbe kumwambia Tiglath-Pileseri mfalme wa Ashuru kwamba, “Mimi ni mtumishi na mtumwa wako. Njoo na uniokoe kutoka mkononi mwa mfalme wa Aramu na wa mfalme wa Israeli, ambao wananishambulia.” 816:8 2Fal 12:18; 12:18Naye Ahazi akachukua fedha na dhahabu zilizopatikana ndani ya Hekalu la Bwana na katika hazina ya jumba la mfalme, na kuzituma kama zawadi kwa mfalme wa Ashuru. 916:9 Mwa 14:15; Amo 1:5Mfalme wa Ashuru akamwitikia kwa kushambulia Dameski na kuiteka. Akawahamishia wenyeji wake huko Kiri, na kumuua Resini.

1016:10 Isa 6:2Kisha Mfalme Ahazi akaenda Dameski kukutana na Tiglath-Pileseri wa Ashuru. Akaona madhabahu huko Dameski, naye akamtumia Uria kuhani mchoro wa hayo madhabahu, pamoja na maelezo ya mpango kamili wa ujenzi wake. 11Kwa hiyo Uria kuhani akajenga madhabahu kulingana na mipango yote ambayo Mfalme Ahazi alikuwa ameituma kutoka Dameski, na akamaliza ujenzi kabla ya Mfalme Ahazi kurudi. 1216:12 2Nya 26:16Mfalme aliporudi kutoka Dameski na kuona hayo madhabahu, akayasogelea na kutoa sadaka juu yake. 13Akatoa sadaka yake ya kuteketezwa na sadaka ya nafaka, akamimina sadaka ya kinywaji na kunyunyizia damu ya sadaka zake za amani juu ya hayo madhabahu. 1416:14 Kut 40:6; 1Fal 8:64Mfalme Ahazi akayaondoa madhabahu ya zamani ya shaba kutoka hapo mbele ya Hekalu la Bwana, yaliyokuwa yamesimama kati ya ingilio la Hekalu na hayo madhabahu mapya, naye akayaweka upande wa kaskazini mwa hayo madhabahu mapya.

1516:15 Kut 29:38-41Ndipo Mfalme Ahazi akatoa amri zifuatazo kwa Uria kuhani: “Juu ya hayo madhabahu kubwa mapya, toa sadaka ya asubuhi ya kuteketezwa na sadaka ya jioni ya nafaka, sadaka ya mfalme ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya nafaka, sadaka ya kuteketezwa ya watu wote wa nchi, pamoja na sadaka yao ya nafaka na sadaka yao ya kinywaji. Unyunyize juu ya hayo madhabahu damu yote ya sadaka za kuteketezwa na dhabihu. Lakini mimi nitatumia hayo madhabahu ya zamani ya shaba kwa ajili ya kutafuta uongozi.” 16Naye Uria kuhani akafanya kama Mfalme Ahazi alivyoagiza.

1716:17 1Fal 7:27Mfalme Ahazi akaondoa mbao za pembeni na kuondoa masinia kwenye vile vishikilio vilivyohamishika. Akaondoa ile Bahari kutoka kwenye mafahali wa shaba walioishikilia, na kuiweka kwenye kitako cha jiwe. 1816:18 Eze 16:28Kwa heshima ya mfalme wa Ashuru, akaliondoa pia pazia la Sabato lililokuwa limewekwa ndani ya Hekalu, na akaondoa ile njia ya kifalme ya kuingia kwenye Hekalu la Bwana.

19Matukio mengine ya utawala wa Ahazi na yale aliyoyafanya, je hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda? 2016:20 Isa 14:28Ahazi akalala na baba zake, naye akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi. Naye Hezekia mwanawe akawa mfalme baada yake.

La Bible du Semeur

2 Rois 16:1-20

Le règne d’Ahaz sur Juda

(2 Ch 28.1-27)

1La dix-septième année du règne de Péqah, fils de Remalia, Ahaz, fils de Yotam, roi de Juda, devint roi16.1 Le règne d’Ahaz a sans doute commencé par une corégence avec son père Yotam en 735 av. J.-C. (voir note 17.1).. 2Il était âgé de vingt ans à son avènement et il régna seize ans à Jérusalem16.2 La durée totale du règne d’Ahaz (avec la corégence) fut de 20 ans (735 à 715 av. J.-C.). Le règne personnel après la mort de Yotam a dû commencer en 732, d’où l’indication des 16 ans (cf. note 15.33).. Il ne fit pas ce que l’Eternel son Dieu considère comme juste, contrairement à son ancêtre David. 3Mais il suivit l’exemple des rois d’Israël. Il alla même jusqu’à brûler son propre fils pour l’offrir en sacrifice aux idoles, commettant ainsi la même abomination que les peuples étrangers que l’Eternel avait dépossédés en faveur des Israélites16.3 Sur les sacrifices d’enfants, voir Lv 20.2-5 ; Dt 12.31 ; 18.10.. 4Il offrait des sacrifices et brûlait des parfums sur les hauts lieux, sur les collines et sous chaque arbre verdoyant.

L’Assyrie au secours de Juda

5Alors Retsîn, roi de Syrie, et Péqah, fils de Remalia, roi d’Israël, vinrent pour attaquer Jérusalem. Ils assiégèrent Ahaz, mais ils ne purent pas engager le combat16.5 Voir Es 7.1-17 ; 2 Ch 28.16-21. Retsîn voulait remplacer Ahaz par le fils de Tabeél pour avoir un nouvel allié dans sa politique anti-assyrienne.. 6Vers la même époque, Retsîn, roi de Syrie, ramena Eilath16.6 Eilath était un port sur le golfe d’Aqaba qui donnait aux Judéens l’accès aux mers du sud du pays d’Israël. sous la domination des Syriens16.6 Les deux noms : Syriens et Edomites se ressemblent beaucoup en hébreu, d’où la proposition de certains de mettre ici Edomites. Certains manuscrits ajoutent plus loin : et des Syriens vinrent s’y installer. ; il en chassa les Judéens, et des Edomites vinrent s’y installer. Ils l’ont occupée jusqu’à aujourd’hui. 7Ahaz envoya des messagers à Tiglath-Piléser, roi d’Assyrie, pour lui dire : Je suis ton vassal et ton fils16.7 Jérusalem perdit ainsi son indépendance.. Viens me délivrer du roi de Syrie et du roi d’Israël qui sont venus m’attaquer.

8Ahaz prit l’argent et l’or qui se trouvaient dans le temple de l’Eternel et dans le trésor du palais royal et il l’envoya comme présent au roi d’Assyrie. 9Le roi d’Assyrie répondit à sa demande : il attaqua Damas, prit la ville et en déporta la population à Qir. Quant à Retsîn, il le fit mettre à mort.

Des modifications sacrilèges dans le Temple

10Le roi Ahaz se rendit à Damas pour rencontrer Tiglath-Piléser, le roi d’Assyrie. Là il vit le grand autel qui se trouvait dans cette ville et il en fit parvenir au prêtre Urie une reproduction et un plan détaillé pour qu’il en fasse une copie16.10 Probablement un autel dédié à Tiglath-Piléser.. 11Le prêtre Urie construisit un autel en tous points conforme aux indications que le roi Ahaz lui avait envoyées depuis Damas, et il l’acheva avant que le roi soit rentré de Damas. 12Lorsque celui-ci fut de retour, il vit l’autel, s’en approcha et y monta ; 13il y offrit lui-même un holocauste et une offrande de farine, il y répandit une libation et aspergea l’autel avec le sang des sacrifices de communion. 14Quant à l’autel de bronze qui se trouvait devant l’Eternel, il l’ôta de sa place devant le Temple, entre le nouvel autel et le Temple, et le fit mettre sur le côté du nouvel autel, vers le nord16.14 Voir 1 R 8.64.. 15Le roi Ahaz ordonna au prêtre Urie : Désormais, tu feras brûler sur le grand autel l’holocauste du matin et l’offrande du soir, l’holocauste du roi et son offrande ainsi que l’holocauste et l’offrande de tout le peuple du pays avec leurs libations, et tu l’aspergeras de tout le sang des holocaustes et des autres sacrifices. En ce qui concerne l’autel de bronze, je déciderai moi-même de son usage.

16Le prêtre Urie exécuta tous les ordres du roi.

17D’autre part, Ahaz fit démonter les plaques de bronze des châssis des chariots16.17 Voir 1 R 7.27-39. du Temple et en fit enlever les bassins. Il ôta la grande cuve qui reposait sur les bœufs de bronze16.17 Voir 1 R 7.23-26. et il la fit déposer directement sur le sol pavé. 18Enfin, à cause du roi d’Assyrie, il supprima aussi dans le temple de l’Eternel la galerie du sabbat, que l’on avait construite à l’intérieur et la porte par laquelle les rois pénétraient dans la cour du Temple.

19Les autres faits et gestes d’Ahaz sont cités dans le livre des Annales des rois de Juda. 20Il rejoignit ses ancêtres décédés et fut enterré à leurs côtés dans la Cité de David. Son fils Ezéchias lui succéda sur le trône.