2 Wafalme 14 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Wafalme 14:1-29

Amazia Mfalme Wa Yuda

(2 Nyakati 25)

1Katika mwaka wa pili wa utawala wa Yehoashi mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli, Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda alianza kutawala. 2Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka ishirini na tisa. Mama yake aliitwa Yehoadani, kutoka Yerusalemu. 3Akatenda yaliyo mema machoni pa Bwana, lakini sio kama Daudi baba yake alivyokuwa amefanya. Katika kila kitu alifuata mfano wa Yoashi baba yake.

414:4 2Fal 12:3Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.

514:5 2Fal 12:20Baada ya ufalme kuimarika mikononi mwake, aliwaua maafisa waliomuua mfalme baba yake. 614:6 Yer 31:30; Eze 18:4, 20Hata hivyo, hakuwaua wana wa wale wauaji, sawasawa na ilivyoandikwa katika Kitabu cha Sheria ya Mose ambako Bwana aliamuru, “Baba hawatauawa kwa ajili ya watoto wao, wala watoto kwa ajili ya baba zao. Kila mmoja atakufa kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe.”

714:7 2Sam 8:13; Amu 1:36Ndiye aliwashinda Waedomu elfu kumi katika Bonde la Chumvi, na akauteka Sela katika vita, naye akauita Yoktheeli, jina ambalo mji huo unalo hadi leo.

8Kisha Amazia akatuma wajumbe kwa Yehoashi mwana wa Yehoahazi, mwana wa Yehu, mfalme wa Israeli, akisema, “Njoo, tuonane uso kwa uso.”

914:9 Amu 9:8-15Lakini Yehoashi mfalme wa Israeli akamjibu Amazia mfalme wa Yuda: “Mbaruti uliokuwa Lebanoni ulituma ujumbe kwa mwerezi uliokuwa Lebanoni, ‘Mtoe binti yako aolewe na mwanangu.’ Kisha mnyama wa mwituni aliyekuwa Lebanoni akaja na kuukanyaga ule mbaruti. 1014:10 2Nya 26:16Hakika umeishinda Edomu, na sasa unajivuna. Jisifu katika ushindi wako, lakini kaa nyumbani kwako! Kwa nini unachokoza na kujiletea anguko lako mwenyewe na la Yuda pia?”

1114:11 Yos 15:10Hata hivyo, Amazia hakusikia, hivyo Yehoashi mfalme wa Israeli akashambulia. Yeye na Amazia mfalme wa Yuda wakakutana uso kwa uso huko Beth-Shemeshi katika Yuda. 1214:12 1Fal 22:36Yuda ikashindwa na Israeli, na kila mtu akakimbilia nyumbani kwake. 1314:13 Neh 8:16; Yer 31:38; Zek 14:10Yehoashi mfalme wa Israeli akamteka Amazia mfalme wa Yuda, mwana wa Yoashi, mwana wa Ahazia, huko Beth-Shemeshi. Kisha Yehoashi akaenda Yerusalemu na kuubomoa ukuta wa Yerusalemu kuanzia Lango la Efraimu hadi Lango la Pembeni, sehemu yenye urefu wa kama dhiraa 400.14:13 Dhiraa 400 ni sawa na mita 180. 14Akachukua dhahabu yote na fedha na vyombo vyote vilivyopatikana ndani ya Hekalu la Bwana na katika hazina zote za jumba la mfalme. Akachukua pia mateka na akarudi Samaria.

1514:15 2Fal 13:12Matukio mengine ya utawala wa Yehoashi, aliyoyafanya na mafanikio yake, pamoja na vita vyake dhidi ya Amazia mfalme wa Yuda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli? 16Yehoashi akalala pamoja na baba zake, akazikwa Samaria pamoja na wafalme wa Israeli, naye Yeroboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.

17Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda aliishi miaka kumi na mitano baada ya kifo cha Yehoashi mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli. 18Matukio mengine ya utawala wa Amazia, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?

1914:19 2Fal 12:20; Yos 10:3Wakafanya shauri baya dhidi ya Amazia huko Yerusalemu, naye akakimbilia Lakishi, lakini wakawatuma watu wamfuatilie huko Lakishi, nao wakamuulia huko. 20Akarudishwa kwa farasi na akazikwa huko Yerusalemu pamoja na baba zake katika Mji wa Daudi.

2114:21 2Nya 26:23; Amo 1:1Kisha watu wote wa Yuda wakamchukua Azaria14:21 Azaria pia aliitwa Uzia. aliyekuwa na umri wa miaka kumi na sita, na kumfanya mfalme mahali pa baba yake Amazia. 22Ndiye aliijenga tena Elathi na kuirudisha kwa Yuda baada ya Amazia kulala pamoja na baba zake.

Yeroboamu Wa Pili Mfalme Wa Israeli

2314:23 2Fal 13:13; 1Nya 5:17Katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda, Yeroboamu mwana wa Yehoashi mfalme wa Israeli alianza kutawala huko Samaria, naye akatawala kwa miaka arobaini na mmoja. 24Akafanya maovu machoni pa Bwana, na hakuacha dhambi hata moja ya Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda. 2514:25 Hes 13:21; Mt 12:39Ndiye alirudishia mipaka ya Israeli kuanzia Lebo-Hamathi hadi Bahari ya Araba, sawasawa na neno la Bwana, Mungu wa Israeli, lililosemwa kupitia mtumishi wake Yona mwana wa Amitai, nabii kutoka Gath-Heferi.

2614:26 Kum 32:36; 2Fal 13:4; Mao 1:7Bwana alikuwa ameona jinsi kila mmoja katika Israeli, awe mtumwa au aliye huru, alivyoteseka kwa uchungu; hapakuwepo na yeyote wa kuwasaidia. 2714:27 Kum 29:20; Amu 6:14Kwa kuwa Bwana alikuwa hajasema kuwa atafuta jina la Israeli chini ya mbingu, akawaokoa kwa mkono wa Yeroboamu mwana wa Yehoashi.

2814:28 2Sam 8:5; 1Fal 15:31Kwa matukio mengine ya utawala wa Yeroboamu, yote aliyoyafanya na mafanikio yake ya kijeshi, ikiwa ni pamoja na jinsi alivyorudisha Dameski na Hamathi kwa Israeli, ambayo ilikuwa mali ya Yuda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli? 29Yeroboamu akalala pamoja na baba zake, wafalme wa Israeli. Naye Zekaria mwanawe akawa mfalme baada yake.

New International Version – UK

2 Kings 14:1-29

Amaziah king of Judah

1In the second year of Jehoash14:1 Hebrew Joash, a variant of Jehoash; also in verses 13, 23 and 27 son of Jehoahaz king of Israel, Amaziah son of Joash king of Judah began to reign. 2He was twenty-five years old when he became king, and he reigned in Jerusalem for twenty-nine years. His mother’s name was Jehoaddan; she was from Jerusalem. 3He did what was right in the eyes of the Lord, but not as his father David had done. In everything he followed the example of his father Joash. 4The high places, however, were not removed; the people continued to offer sacrifices and burn incense there.

5After the kingdom was firmly in his grasp, he executed the officials who had murdered his father the king. 6Yet he did not put the children of the assassins to death, in accordance with what is written in the Book of the Law of Moses where the Lord commanded: ‘Parents are not to be put to death for their children, nor children put to death for their parents; each will die for their own sin.’14:6 Deut. 24:16

7He was the one who defeated ten thousand Edomites in the Valley of Salt and captured Sela in battle, calling it Joktheel, the name it has to this day.

8Then Amaziah sent messengers to Jehoash son of Jehoahaz, the son of Jehu, king of Israel, with the challenge: ‘Come, let us face each other in battle.’

9But Jehoash king of Israel replied to Amaziah king of Judah: ‘A thistle in Lebanon sent a message to a cedar in Lebanon, “Give your daughter to my son in marriage.” Then a wild beast in Lebanon came along and trampled the thistle underfoot. 10You have indeed defeated Edom and now you are arrogant. Glory in your victory, but stay at home! Why ask for trouble and cause your own downfall and that of Judah also?’

11Amaziah, however, would not listen, so Jehoash king of Israel attacked. He and Amaziah king of Judah faced each other at Beth Shemesh in Judah. 12Judah was routed by Israel, and every man fled to his home. 13Jehoash king of Israel captured Amaziah king of Judah, the son of Joash, the son of Ahaziah, at Beth Shemesh. Then Jehoash went to Jerusalem and broke down the wall of Jerusalem from the Ephraim Gate to the Corner Gate – a section about four hundred cubits long.14:13 That is, about 180 metres 14He took all the gold and silver and all the articles found in the temple of the Lord and in the treasuries of the royal palace. He also took hostages and returned to Samaria.

15As for the other events of the reign of Jehoash, what he did and his achievements, including his war against Amaziah king of Judah, are they not written in the book of the annals of the kings of Israel? 16Jehoash rested with his ancestors and was buried in Samaria with the kings of Israel. And Jeroboam his son succeeded him as king.

17Amaziah son of Joash king of Judah lived for fifteen years after the death of Jehoash son of Jehoahaz king of Israel. 18As for the other events of Amaziah’s reign, are they not written in the book of the annals of the kings of Judah?

19They conspired against him in Jerusalem, and he fled to Lachish, but they sent men after him to Lachish and killed him there. 20He was brought back by horse and was buried in Jerusalem with his ancestors, in the City of David.

21Then all the people of Judah took Azariah,14:21 Also called Uzziah who was sixteen years old, and made him king in place of his father Amaziah. 22He was the one who rebuilt Elath and restored it to Judah after Amaziah rested with his ancestors.

Jeroboam II king of Israel

23In the fifteenth year of Amaziah son of Joash king of Judah, Jeroboam son of Jehoash king of Israel became king in Samaria, and he reigned for forty-one years. 24He did evil in the eyes of the Lord and did not turn away from any of the sins of Jeroboam son of Nebat, which he had caused Israel to commit. 25He was the one who restored the boundaries of Israel from Lebo Hamath to the Dead Sea,14:25 Hebrew the Sea of the Arabah in accordance with the word of the Lord, the God of Israel, spoken through his servant Jonah son of Amittai, the prophet from Gath Hepher.

26The Lord had seen how bitterly everyone in Israel, whether slave or free, was suffering;14:26 Or Israel was suffering. They were without a ruler or leader, and there was no-one to help them. 27And since the Lord had not said he would blot out the name of Israel from under heaven, he saved them by the hand of Jeroboam son of Jehoash.

28As for the other events of Jeroboam’s reign, all he did, and his military achievements, including how he recovered for Israel both Damascus and Hamath, which had belonged to Judah, are they not written in the book of the annals of the kings of Israel? 29Jeroboam rested with his ancestors, the kings of Israel. And Zechariah his son succeeded him as king.