2 Wafalme 12 – NEN & NRT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Wafalme 12:1-21

Yoashi Anakarabati Hekalu

112:1 2Fal 11:2Katika mwaka wa saba wa utawala wa Yehu, Yoashi alianza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka arobaini. Jina la mama yake aliitwa Sibia, kutoka Beer-Sheba. 212:2 Kum 12:25; 2Sam 8:15Yoashi akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana miaka yote ambayo Yehoyada kuhani alikuwa akimwelekeza. 312:3 2Fal 18:4Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.

412:4 Hes 18:19; Kut 30:12Yoashi akawaambia makuhani, “Kusanyeni fedha zote ambazo zitaletwa kama sadaka takatifu kwenye Hekalu la Bwana, yaani fedha zilizokusanywa kama kodi, fedha zilizopokelewa kutokana na nadhiri za watu binafsi, na fedha zilizoletwa kwa hiari hekaluni. 5Kila kuhani na apokee fedha kutoka kwa mmoja wa watunza hazina, nazo zitumike kukarabati uharibifu wowote unaoonekana katika Hekalu.”

6Lakini ikawa kufikia mwaka wa ishirini na tatu wa utawala wake Mfalme Yoashi, makuhani walikuwa bado hawajalikarabati Hekalu. 7Kwa hiyo Mfalme Yoashi akamwita Yehoyada kuhani na makuhani wengine, akawauliza, “Kwa nini hamtengenezi uharibifu uliofanyika hekaluni? Msichukue fedha zaidi kutoka kwa watunza hazina wenu kwa ajili ya matumizi yenu, lakini kuanzia sasa ni lazima fedha yote itumike kwa ajili ya kukarabati Hekalu.” 8Makuhani wakakubali kuwa hawatakusanya tena fedha kutoka kwa watu na kwamba hawatakarabati Hekalu wenyewe.

912:9 Yer 35:4; Mk 12:41Yehoyada kuhani akachukua kisanduku na akatoboa tundu kwenye kifuniko chake. Akakiweka kando ya madhabahu upande wa kulia unapoingia hekaluni mwa Bwana. Makuhani waliolinda ingilio wakaweka ndani ya kisanduku fedha zote ambazo zililetwa katika Hekalu la Bwana. 1012:10 2Sam 8:17Kila mara walipoona kuwa kuna kiasi kikubwa cha fedha ndani ya kisanduku, mwandishi wa mfalme na kuhani mkuu walikuja, wakazihesabu fedha hizo zilizoletwa katika Hekalu la Bwana, na kuziweka katika mifuko. 11Wakiisha kuthibitisha kiasi cha hizo fedha, waliwapa watu walioteuliwa kusimamia kazi katika Hekalu. Kwa fedha hizo, wakawalipa wale watu waliofanya kazi katika Hekalu la Bwana: yaani, maseremala na wajenzi, 1212:12 2Fal 22:5-6waashi na wakata mawe. Walinunua mbao na mawe ya kuchongwa kwa ajili ya ukarabati wa Hekalu la Bwana, na kulipia gharama nyingine zote za kulitengeneza.

1312:13 1Fal 7:51Fedha zilizoletwa kwenye Hekalu hazikutumiwa kutengenezea masinia ya fedha, mikasi ya kusawazishia tambi, mabakuli ya kunyunyizia, tarumbeta wala vyombo vingine vyovyote vya dhahabu au fedha kwa ajili ya Hekalu la Bwana; 14zililipwa kwa wafanyakazi, ambao walizitumia kwa kukarabati Hekalu. 1512:15 2Fal 22:7; 1Kor 4:2Wao hawakudai kupewa hesabu ya fedha kutoka kwa wale waliowapa ili kuwalipa wafanyakazi, kwa sababu walifanya kwa uaminifu wote. 1612:16 Law 5:14-19Fedha zilizopatikana kutokana na sadaka za hatia na sadaka za dhambi hazikuletwa katika Hekalu la Bwana; zilikuwa mali ya makuhani.

1712:17 2Fal 8:12Wakati huu Hazaeli mfalme wa Aramu akapanda kuishambulia Gathi, akaiteka. Kisha akageuka ili kuishambulia Yerusalemu. 1812:18 1Fal 15:18; 2Fal 15:20Lakini Yoashi mfalme wa Yuda akavichukua vyombo vyote vitakatifu vilivyowekwa wakfu na baba zake, yaani Yehoshafati, Yehoramu na Ahazia, wafalme wa Yuda, zawadi ambazo yeye mwenyewe alikuwa ameziweka wakfu pamoja na dhahabu yote iliyokutwa katika hazina za Hekalu la Bwana na katika jumba la kifalme, akazipeleka kwa Hazaeli mfalme wa Aramu, ambaye hatimaye aliondoka Yerusalemu.

19Kwa matukio mengine ya utawala wa Yoashi na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda? 2012:20 2Fal 14:5; Amu 9:6Maafisa wake wakafanya shauri baya dhidi yake, nao wakamuulia Yoashi huko Beth-Milo, kwenye barabara iteremkayo kuelekea Sila. 21Maafisa waliomuua walikuwa Yozabadi mwana wa Shimeathi, na Yehozabadi mwana wa Shomeri. Akafa na akazikwa pamoja na baba zake katika Mji wa Daudi. Naye Amazia mwanawe akawa mfalme baada yake.

New Russian Translation

4 Царств 12:1-21

1На седьмом году правления Ииуя Иоаш стал царем и правил в Иерусалиме сорок лет. Его мать звали Цивья; она была родом из Вирсавии. 2Иоаш делал то, что было правильным в глазах Господа, все время, пока его наставлял священник Иодай. 3Только святилища на возвышенностях не были убраны, и народ продолжал приносить там жертвы и возжигать благовония.

Иоаш восстанавливает храм

(2 Пар. 24:4-14)

4Иоаш сказал священникам:

– Соберите все деньги, что приносятся как священный дар в дом Господа, – деньги, собранные по переписи, деньги, полученные по обетам, и деньги, которые были добровольно пожертвованы на дом. 5Пусть возьмут деньги у каждого из жертвующих и используют их на восстановление дома Господа там, где найдется повреждение.

6Но к двадцать шестому году правления царя Иоаша священники все еще не восстановили дом. 7И вот царь Иоаш призвал священника Иодая и прочих священников и спросил их:

– Почему вы не чините дом? Не берите больше денег у жертвователей, а передайте их на починку дома.

8Тогда священники согласились, что не будут больше ни принимать от народа денег, ни отвечать за восстановление дома.

9Священник Иодай взял ящик и проделал в его крышке дыру. Он поставил его у жертвенника, с правой стороны от входа в дом Господа, и священники, которые охраняли вход, клали в ящик все деньги, приносимые в дом Господа. 10Всякий раз, когда они видели, что в ящике много денег, приходили царский писарь и первосвященник, считали деньги, принесенные в дом Господа, и клали их в мешки. 11Когда деньги были пересчитаны, они отдавали их тем, кто смотрел за работами в доме. А они платили тем, кто работал в доме Господа, – плотникам и строителям, 12тем, кто клал стены, и тем, кто тесал камни. Они также покупали дерево и тесаные камни для восстановления дома Господа и оплачивали все прочие расходы на восстановление дома.

13Но ни серебряных кубков, ни ножниц для фитилей, ни кропильных чаш, ни труб, ни иных вещей из золота или серебра для дома Господа не изготовляли на деньги, приносимые в дом. 14Деньги платили рабочим, которые восстанавливали дом. 15От тех, кому отдавали деньги для выплаты рабочим, не требовали отчета, потому что они действовали честно. 16Деньги от жертв повинности и жертв за грех не вносились в дом Господа – они шли священникам.

Иоаш спасает Иерусалим от Хазаила

(2 Пар. 24:23-24)

17В то время Хазаил, царь Арама, напал на город Гат и захватил его. Затем он решил идти на Иерусалим. 18Но Иоаш, царь Иудеи, взял все священные вещи, посвященные его отцами Иосафатом, Иорамом и Охозией, царями Иудеи, дары, которые посвятил он сам, и все золото, которое нашлось в сокровищницах дома Господа и царского дворца, и послал их Хазаилу, царю Арама, который после этого отошел от Иерусалима.

Смерть Иоаша

(2 Пар. 24:25-27)

19Что же до прочих событий правления Иоаша и всего, что он сделал, то разве не записаны они в «Книге летописей царей Иудеи»? 20Его приближенные составили против него заговор и убили его в Бет-Милло, на дороге, которая спускается к Силле. 21Иозавад, сын Шимеаты, и Иегозавад, сын Шомеры, – вот те приближенные, которые сразили его до смерти. Он был похоронен со своими предками в Городе Давида. Амасия, его сын, стал царем вместо него.