2 Samweli 22 – NEN & KLB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Samweli 22:1-51

Wimbo Wa Daudi Wa Sifa

(Zaburi 18)

122:1 Kut 15:1; Amu 5:1; Za 18:2-50Daudi alimwimbia Bwana maneno ya wimbo huu wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli. 222:2 1Sam 2:2; Za 31:3; 91:2; 71:3; 144:2; Kum 32:4; Za 18:2; Mit 18:10; Mt 18:10Akasema:

Bwana ni mwamba wangu,

ngome yangu na mwokozi wangu,

322:3 Mit 10:29; Yoe 3:16; Kum 23:15; 32:37; Za 14:6; 31:2; 59:16; 71:7; 91:2; 94:22; Isa 25:4; Yer 16:19; Mwa 15:1; Kum 33:17; Lk 1:69; Za 9:9; 52:7Mungu wangu ni mwamba wangu,

ambaye kwake ninakimbilia,

ngao yangu na pembe ya wokovu wangu.

Yeye ni ngome yangu, kimbilio langu

na mwokozi wangu,

huniokoa kutoka kwa watu wenye jeuri.

422:4 Za 48:1; 96:4; 145:3Ninamwita Bwana, anayestahili kusifiwa,

nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.

522:5 Za 69:14-15; Yon 2:3“Mawimbi ya mauti yalinizunguka,

mafuriko ya maangamizi yalinilemea.

622:6 Za 116:3; Mdo 2:24Kamba za kuzimu22:6 Kuzimu kwa Kiebrania ni Sheol, maana yake ni Shimo lisilo na mwisho. zilinizunguka,

mitego ya mauti ilinikabili.

722:7 Mwa 35:3; Amu 2:15; 2Nya 15:4; Za 4:1; 77:2; 120:1; Isa 26:16; Za 34:15; 116:4; 116:4; Kut 3:7Katika shida yangu nalimwita Bwana,

nilimlilia Mungu wangu.

Kutoka Hekaluni mwake alisikia sauti yangu,

kilio changu kikafika masikioni mwake.

822:8 Amu 5:4; Za 97:4; Kut 19:18; Za 68:8; 77:18; Yer 10:10; Ay 9:6; 26:11; Za 75:3“Dunia ilitetemeka na kutikisika,

misingi ya mbingu ikatikisika,

vilitetemeka kwa sababu

alikuwa amekasirika.

922:9 Za 50:3; 97:3; Ebr 12:29; Ufu 11:5; Isa 6:6; Eze 1:13; 10:2; Hab 3:5Moshi ukapanda kutoka puani mwake,

moto uteketezao ukatoka kinywani mwake,

makaa ya moto yawakayo

yakatoka ndani mwake.

1022:10 Kut 19:9; Law 16:2; Kum 33:26; 1Fal 8:12; Ay 26:9; Za 104:3; Isa 19:1; Yer 4:13; Nah 1:3; Isa 64:1Akazipasua mbingu akashuka chini,

mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.

1122:11 Mwa 3:24; Kut 25:22; Za 104:3Alipanda juu ya kerubi akaruka,

akapaa juu kwa mbawa za upepo.

1222:12 Kut 19:9Alifanya giza hema lake la kujifunika:

mawingu meusi ya mvua ya angani.

1322:13 Ay 37:3; Za 77:18Kutokana na mwanga wa uwepo wake

mawingu yalisogea,

ikanyesha mvua ya mawe

na umeme wa radi.

1422:14 1Sam 2:10; Isa 30:30Bwana alinguruma kutoka mbinguni,

sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.

1522:15 Kum 32:23; Za 7:13; 77:7; Hab 3:11Aliipiga mishale na kutawanya adui,

umeme wa radi na kuwafukuza.

1622:16 Za 6:1; 50:8, 21; 106:9; Nah 1:4; Isa 30:33; 40:24; Kut 14:21Mabonde ya bahari yalifunuliwa,

na misingi ya dunia ikawa wazi

kwa kukaripia kwake Bwana,

kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwake.

1722:17 Za 144:7; Kut 2; 10“Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika;

alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.

1822:18 Lk 1:71Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi,

kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.

1922:19 Za 23:4Walinikabili siku ya msiba wangu,

lakini Bwana alikuwa msaada wangu.

2022:20 Ay 36:16; Za 31:8; 118:5; 22:8; Isa 42:1; Mt 12:18; 2Sam 15:26Alinileta nje mahali penye nafasi tele,

akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.

2122:21 1Sam 26:23; Za 26:6; Ay 17:9; 22:30; 42:7-8; Za 24:4Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu;

sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.

2222:22 Mwa 18:19; Za 128:1; Mit 8:32Kwa maana nimezishika njia za Bwana;

sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.

2322:23 Kum 6:4-9; Za 119:30-32, 102; Kum 7:12Sheria zake zote zi mbele yangu,

wala sijayaacha maagizo yake.

2422:24 Mwa 6:9; Efe 1:4; Yn 1:47Nimekuwa sina hatia mbele zake,

nami nimejilinda nisitende dhambi.

2522:25 1Sam 26:23Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu,

sawasawa na usafi wangu machoni pake.

2622:26 Mt 5:7“Kwa yeye aliye mwaminifu unajionyesha kuwa mwaminifu,

kwa asiye na hatia unajionyesha kutokuwa na hatia,

2722:27 Mt 5:8; Law 26:23-2422:27 1Nya 27:9-10kwa aliye mtakatifu unajionyesha kuwa mtakatifu,

lakini kwa aliyepotoka unajionyesha kuwa mkaidi.

2822:28 Kut 3:8; 1Sam 2:8-9; Za 72:12-13; Mit 30:13; Dan 4:31; Sef 3:11; Isa 2:12-17; 5:15; Za 12:5; Mt 5:3Wewe huwaokoa wanyenyekevu,

lakini macho yako ni juu ya wenye kiburi

ili uwashushe.

2922:29 Za 27:1; Isa 2:5; Mik 7:8; Ufu 21:23; 22:5Wewe ni taa yangu, Ee Bwana.

Bwana hulifanya giza langu

kuwa mwanga.

30Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi,

nikiwa pamoja na Mungu wangu

nitaweza kuruka ukuta.

3122:31 Kum 32:4; Mt 5:48; Za 12:6; 119:140; Mit 30:5-6; Mwa 15:1; Dan 4:37; Ufu 15:3“Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu;

neno la Bwana halina dosari.

Yeye ni ngao kwa wote

wanaokimbilia kwake.

3222:32 Kut 32:31; 1Sam 2:2; Isa 45:5-6Kwa maana ni nani aliye Mungu

zaidi ya Bwana?

Ni nani aliye Mwamba

isipokuwa Mungu wetu?

3322:33 1Sam 2:2; 2Sam 7:22; Za 27:1; Kum 18:13Mungu ndiye anivikaye nguvu

na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.

3422:34 Isa 35:6; Hab 3:19; Kum 32:13Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu,

huniwezesha kusimama mahali palipo juu.

3522:35 Za 144:1; 7:12; 11:2; Zek 9:13Huifundisha mikono yangu kupigana vita;

mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.

3622:36 Efe 6:16Hunipa ngao yako ya ushindi,

unajishusha chini ili kuniinua.

3722:37 Mit 4:11Huyapanua mapito yangu,

ili miguu yangu isiteleze.

38“Niliwafuatia adui zangu na nikawaseta,

sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.

3922:39 Za 44:5; 110:6; Mal 4:3Niliwaseta kabisa, nao hawakuweza kuinuka tena;

walianguka chini ya miguu yangu.

4022:40 Yos 10:24; 1Fal 5:3; Za 44:5Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita;

uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.

4122:41 Kut 23:27Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia,

nami nikawaangamiza adui zangu.

4222:42 Isa 1:15; Za 50:22; 1Sam 14:37; 28:6; Ay 27:6; Mit 1:28Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa;

walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.

4322:43 1Fal 20:10; 2Fal 13:7; Isa 41:2; Amo 1:3; Za 7:5; Isa 41:25; Mik 7:10; Zek 10:5; Isa 5:25; 10:6; 22:5Niliwaponda kama mavumbi ya nchi;

niliwaponda na kuwakanyaga kama tope barabarani.

4422:44 Kut 11:3; 2Sam 3:1; 8:1-14; Isa 55:3-5; Kum 28:13“Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu wangu;

umenihifadhi mimi kama kiongozi wa mataifa.

Watu ambao sikuwajua wananitumikia,

4522:45 Za 66:3; 81:15; Kum 33:29nao wageni huja wakininyenyekea,

mara wanisikiapo, hunitii.

4622:46 Mik 7:17Wote wanalegea,

wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.

4722:47 Kut 15:2; Kum 32:15; Za 18:31; 89:26; 95:1Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu!

Atukuzwe Mungu,

Mwamba, Mwokozi wangu!

4822:48 Hes 31:3; Za 144:2; 1Sam 25:39; Za 94:1Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi,

ayawekaye mataifa chini yangu,

4922:49 Za 140:1; 27:6aniwekaye huru toka kwa adui zangu.

Uliniinua juu ya adui zangu;

uliniokoa toka kwa watu wajeuri.

5022:50 Za 9:11; 47:6; 68:4; Rum 15:9Kwa hiyo nitakusifu, Ee Bwana,

katikati ya mataifa;

nitaliimbia sifa jina lako.

5122:51 Za 21:1; 144:9-10; 1Sam 16; 13; Za 89:20; Mdo 13:23; 2Sam 7:13; Za 89:24, 29Humpa mfalme wake ushindi mkuu;

huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake,

kwa Daudi na wazao wake milele.”

Korean Living Bible

사무엘하 22:1-51

다윗의 노래

1다윗은 여호와께서 그의 모든 원수들과 사울의 손에서 자기를 구원해 주셨을 때 여호와께 이렇게 노래하였다.

2“여호와는 나의 반석,

나의 요새, 나의 구원자이시며

3내 하나님은 내가 피할 바위이시요

내 방패가 되시고

22:3 원문에는 ‘나의 구원의 뿔’나를 구원하는 힘이시다.

그가 나의 높은 망대와

피난처와 구원자가 되셔서

모든 원수들에게서

나를 구원하셨네.

4내가 여호와께 부르짖으면

그가 나를 원수들에게서 구원하시니

여호와는 찬양을 받으실 분이시다.

5“사망의 물결이 나를 에워싸고

파멸의 홍수가 나를 덮쳤으며

622:6 또는 ‘음부의 줄’죽음의 위험이 나를 두르고

사망의 덫이 내 앞에 놓였을 때

7내가 고통 중에서

여호와께 부르짖었더니

그가 성소에서 내 음성을 들으시고

내가 부르짖는 소리에

귀를 기울이셨네.

8“그때 땅이 떨고 진동하였으며

하늘의 터전이 흔들렸으니

그가 분노하셨음이라.

9그 코에서 연기가 나오고

그 입에서 소멸하는 불이 나와

그 불에 숯불이 피었네.

10그가 하늘을 굽히고 내려오시니

그의 발 아래

어두운 구름이 깔렸구나.

11그가 22:11 히 ‘그룹을’하늘 마차를 타고 나시며

바람 날개로 다니시고

12흑암과 빽빽한 비구름으로

휘장을 삼으셨네.

13그 앞의 광채로 숯불이 피었구나.

14하늘에서 뇌성을 발하시므로

전능하신 하나님의 음성이 들렸다.

15그가 화살을 쏘아

원수들을 흩으시며

번개로 그들을 쳐부쉈네.

16여호와의 꾸지람과 콧김으로

바다 밑이 드러나고

땅의 기초가 나타났구나.

17“그가 높은 곳에서 나를 붙들어

깊은 물에서 나를 건져내셨네.

18여호와께서 나를 강한 대적과

나를 미워하는 원수들에게서

구하셨으니

그들은 나보다 강한 자들이었다.

19내가 곤경에 처했을 때

그들이 나를 덮쳤으나

여호와께서는 나를 보호하셨다.

20그가 나를

안전한 곳으로 인도하시고

나를 기쁘게 여겨 구원해 주셨네.

21“여호와께서

나의 의로움에 대하여 갚아 주시고

나의 깨끗한 삶을 보상해 주셨으니

22이것은 내가 여호와의 법을 지키고

내 하나님을 떠나

악을 행하지 않았음이라.

23나는 그의 모든 법을 지키고

그의 명령을 어기지 않았으며

24그 앞에서 흠 없이 살고

내 자신을 지켜 죄를 짓지 않았다.

25그래서 나의 의로운 행위대로,

내가 그 앞에서 깨끗하게 산 그대로,

여호와께서 나에게 갚아 주셨네.

26“여호와여,

주는 자비로운 자에게

주의 자비를,

흠 없는 자에게

주의 완전하심을,

27깨끗한 자에게

주의 깨끗하심을,

악한 자에게

주의 분노를 보이시는 분이십니다.

28주는 22:28 또는 ‘곤고한 백성’겸손한 자를 구원하시고

교만한 자를 낮추십니다.

29“여호와여,

주는

나의 등불이 되셔서 나의 어두움을 밝혀 주시니

30내가 주의 도움으로

적진을 향해 달려갈 수 있으며

주의 힘으로 적의 방어벽을

뛰어넘을 수 있습니다.

31“하나님의 22:31 또는 ‘도는’행위는 완전하고

여호와의 말씀은 참되니

그는 자기에게 피하는 모든 자에게

방패가 되신다.

32여호와 외에

하나님이 어디 있으며

우리 하나님 외에

반석이 어디 있는가?

33하나님은 나의 튼튼한 요새가 되어

나를 안전한 곳으로 인도하시는구나.

34그가 내 발을 사슴 발 같게 하여

나를 높은 곳에서도 서게 하시며

35나를 훈련시켜 싸우게 하시니

내가 놋활도 당길 수 있게 되었네.

36“여호와여, 주는 나에게

구원의 방패를 주시고

나를 도우셔서 크게 하셨으며

37내 길을 넓게 하셔서

내가 넘어지지 않게 하셨습니다.

38내가 원수들을 추격하여

그들을 쳐죽이기 전에는

돌아서지 않았습니다.

39내가 그들을 쳐서 쓰러뜨리자

그들이 다시 일어나지 못하고

내 발 아래 엎드러졌습니다.

40주께서 전쟁을 위해

나를 힘으로 무장시키시고

내 대적들을 내 발 앞에

굴복하게 하셨으며

41내 원수들이

등을 돌려 달아나게 하셨으므로

내가 나를 미워하는 자들을

모조리 없애 버렸습니다.

42“그들이 도와 달라고 외쳐도

그들을 구해 줄 자가 없었으며

그들이 여호와께 부르짖어도

그가 대답하지 않으셨다.

43내가 그들을 쳐서

땅의 먼지처럼 되게 하였고

그들을 짓밟아

거리의 진흙처럼 뭉개 버렸네.

44“주께서 나를

반역하는 백성에게서 구하시고

나를 보존하여

모든 민족의 머리가

되게 하셨으므로

내가 알지 못하는 백성이

나를 섬기며

45외국인들이 내 소문을 듣고

내 앞에 굽실거리며 복종합니다.

46그들이 모두

용기를 잃고

숨어 있던 곳에서 떨며 나옵니다.

47“여호와는 살아 계신다!

나의 반석 되시는 분을 찬양하세.

내 구원의 바위 되시는

하나님을 높이세.

48그는 내 원수를 갚으시고

여러 민족을 나에게 복종시키시며

49나를 원수들에게서

구하신 하나님이시다!

“여호와여, 주는 나를

내 대적 위에 높이 드시고

난폭한 자들의 손에서

나를 구해 주셨습니다.

50여호와여, 그러므로 내가

여러 민족 가운데서

주께 감사하며

주의 이름을 찬양합니다.

51“여호와께서 자기 왕에게

큰 승리를 주시고

자기가 기름 부어 세운 자에게

한결같은 사랑을 베푸시니

나와 내 후손이

영원히 누릴 축복이구나!”

다윗의 마지막 말