2 Samweli 22 – NEN & HOF

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Samweli 22:1-51

Wimbo Wa Daudi Wa Sifa

(Zaburi 18)

122:1 Kut 15:1; Amu 5:1; Za 18:2-50Daudi alimwimbia Bwana maneno ya wimbo huu wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli. 222:2 1Sam 2:2; Za 31:3; 91:2; 71:3; 144:2; Kum 32:4; Za 18:2; Mit 18:10; Mt 18:10Akasema:

Bwana ni mwamba wangu,

ngome yangu na mwokozi wangu,

322:3 Mit 10:29; Yoe 3:16; Kum 23:15; 32:37; Za 14:6; 31:2; 59:16; 71:7; 91:2; 94:22; Isa 25:4; Yer 16:19; Mwa 15:1; Kum 33:17; Lk 1:69; Za 9:9; 52:7Mungu wangu ni mwamba wangu,

ambaye kwake ninakimbilia,

ngao yangu na pembe ya wokovu wangu.

Yeye ni ngome yangu, kimbilio langu

na mwokozi wangu,

huniokoa kutoka kwa watu wenye jeuri.

422:4 Za 48:1; 96:4; 145:3Ninamwita Bwana, anayestahili kusifiwa,

nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.

522:5 Za 69:14-15; Yon 2:3“Mawimbi ya mauti yalinizunguka,

mafuriko ya maangamizi yalinilemea.

622:6 Za 116:3; Mdo 2:24Kamba za kuzimu22:6 Kuzimu kwa Kiebrania ni Sheol, maana yake ni Shimo lisilo na mwisho. zilinizunguka,

mitego ya mauti ilinikabili.

722:7 Mwa 35:3; Amu 2:15; 2Nya 15:4; Za 4:1; 77:2; 120:1; Isa 26:16; Za 34:15; 116:4; 116:4; Kut 3:7Katika shida yangu nalimwita Bwana,

nilimlilia Mungu wangu.

Kutoka Hekaluni mwake alisikia sauti yangu,

kilio changu kikafika masikioni mwake.

822:8 Amu 5:4; Za 97:4; Kut 19:18; Za 68:8; 77:18; Yer 10:10; Ay 9:6; 26:11; Za 75:3“Dunia ilitetemeka na kutikisika,

misingi ya mbingu ikatikisika,

vilitetemeka kwa sababu

alikuwa amekasirika.

922:9 Za 50:3; 97:3; Ebr 12:29; Ufu 11:5; Isa 6:6; Eze 1:13; 10:2; Hab 3:5Moshi ukapanda kutoka puani mwake,

moto uteketezao ukatoka kinywani mwake,

makaa ya moto yawakayo

yakatoka ndani mwake.

1022:10 Kut 19:9; Law 16:2; Kum 33:26; 1Fal 8:12; Ay 26:9; Za 104:3; Isa 19:1; Yer 4:13; Nah 1:3; Isa 64:1Akazipasua mbingu akashuka chini,

mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.

1122:11 Mwa 3:24; Kut 25:22; Za 104:3Alipanda juu ya kerubi akaruka,

akapaa juu kwa mbawa za upepo.

1222:12 Kut 19:9Alifanya giza hema lake la kujifunika:

mawingu meusi ya mvua ya angani.

1322:13 Ay 37:3; Za 77:18Kutokana na mwanga wa uwepo wake

mawingu yalisogea,

ikanyesha mvua ya mawe

na umeme wa radi.

1422:14 1Sam 2:10; Isa 30:30Bwana alinguruma kutoka mbinguni,

sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.

1522:15 Kum 32:23; Za 7:13; 77:7; Hab 3:11Aliipiga mishale na kutawanya adui,

umeme wa radi na kuwafukuza.

1622:16 Za 6:1; 50:8, 21; 106:9; Nah 1:4; Isa 30:33; 40:24; Kut 14:21Mabonde ya bahari yalifunuliwa,

na misingi ya dunia ikawa wazi

kwa kukaripia kwake Bwana,

kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwake.

1722:17 Za 144:7; Kut 2; 10“Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika;

alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.

1822:18 Lk 1:71Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi,

kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.

1922:19 Za 23:4Walinikabili siku ya msiba wangu,

lakini Bwana alikuwa msaada wangu.

2022:20 Ay 36:16; Za 31:8; 118:5; 22:8; Isa 42:1; Mt 12:18; 2Sam 15:26Alinileta nje mahali penye nafasi tele,

akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.

2122:21 1Sam 26:23; Za 26:6; Ay 17:9; 22:30; 42:7-8; Za 24:4Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu;

sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.

2222:22 Mwa 18:19; Za 128:1; Mit 8:32Kwa maana nimezishika njia za Bwana;

sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.

2322:23 Kum 6:4-9; Za 119:30-32, 102; Kum 7:12Sheria zake zote zi mbele yangu,

wala sijayaacha maagizo yake.

2422:24 Mwa 6:9; Efe 1:4; Yn 1:47Nimekuwa sina hatia mbele zake,

nami nimejilinda nisitende dhambi.

2522:25 1Sam 26:23Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu,

sawasawa na usafi wangu machoni pake.

2622:26 Mt 5:7“Kwa yeye aliye mwaminifu unajionyesha kuwa mwaminifu,

kwa asiye na hatia unajionyesha kutokuwa na hatia,

2722:27 Mt 5:8; Law 26:23-2422:27 1Nya 27:9-10kwa aliye mtakatifu unajionyesha kuwa mtakatifu,

lakini kwa aliyepotoka unajionyesha kuwa mkaidi.

2822:28 Kut 3:8; 1Sam 2:8-9; Za 72:12-13; Mit 30:13; Dan 4:31; Sef 3:11; Isa 2:12-17; 5:15; Za 12:5; Mt 5:3Wewe huwaokoa wanyenyekevu,

lakini macho yako ni juu ya wenye kiburi

ili uwashushe.

2922:29 Za 27:1; Isa 2:5; Mik 7:8; Ufu 21:23; 22:5Wewe ni taa yangu, Ee Bwana.

Bwana hulifanya giza langu

kuwa mwanga.

30Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi,

nikiwa pamoja na Mungu wangu

nitaweza kuruka ukuta.

3122:31 Kum 32:4; Mt 5:48; Za 12:6; 119:140; Mit 30:5-6; Mwa 15:1; Dan 4:37; Ufu 15:3“Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu;

neno la Bwana halina dosari.

Yeye ni ngao kwa wote

wanaokimbilia kwake.

3222:32 Kut 32:31; 1Sam 2:2; Isa 45:5-6Kwa maana ni nani aliye Mungu

zaidi ya Bwana?

Ni nani aliye Mwamba

isipokuwa Mungu wetu?

3322:33 1Sam 2:2; 2Sam 7:22; Za 27:1; Kum 18:13Mungu ndiye anivikaye nguvu

na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.

3422:34 Isa 35:6; Hab 3:19; Kum 32:13Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu,

huniwezesha kusimama mahali palipo juu.

3522:35 Za 144:1; 7:12; 11:2; Zek 9:13Huifundisha mikono yangu kupigana vita;

mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.

3622:36 Efe 6:16Hunipa ngao yako ya ushindi,

unajishusha chini ili kuniinua.

3722:37 Mit 4:11Huyapanua mapito yangu,

ili miguu yangu isiteleze.

38“Niliwafuatia adui zangu na nikawaseta,

sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.

3922:39 Za 44:5; 110:6; Mal 4:3Niliwaseta kabisa, nao hawakuweza kuinuka tena;

walianguka chini ya miguu yangu.

4022:40 Yos 10:24; 1Fal 5:3; Za 44:5Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita;

uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.

4122:41 Kut 23:27Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia,

nami nikawaangamiza adui zangu.

4222:42 Isa 1:15; Za 50:22; 1Sam 14:37; 28:6; Ay 27:6; Mit 1:28Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa;

walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.

4322:43 1Fal 20:10; 2Fal 13:7; Isa 41:2; Amo 1:3; Za 7:5; Isa 41:25; Mik 7:10; Zek 10:5; Isa 5:25; 10:6; 22:5Niliwaponda kama mavumbi ya nchi;

niliwaponda na kuwakanyaga kama tope barabarani.

4422:44 Kut 11:3; 2Sam 3:1; 8:1-14; Isa 55:3-5; Kum 28:13“Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu wangu;

umenihifadhi mimi kama kiongozi wa mataifa.

Watu ambao sikuwajua wananitumikia,

4522:45 Za 66:3; 81:15; Kum 33:29nao wageni huja wakininyenyekea,

mara wanisikiapo, hunitii.

4622:46 Mik 7:17Wote wanalegea,

wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.

4722:47 Kut 15:2; Kum 32:15; Za 18:31; 89:26; 95:1Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu!

Atukuzwe Mungu,

Mwamba, Mwokozi wangu!

4822:48 Hes 31:3; Za 144:2; 1Sam 25:39; Za 94:1Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi,

ayawekaye mataifa chini yangu,

4922:49 Za 140:1; 27:6aniwekaye huru toka kwa adui zangu.

Uliniinua juu ya adui zangu;

uliniokoa toka kwa watu wajeuri.

5022:50 Za 9:11; 47:6; 68:4; Rum 15:9Kwa hiyo nitakusifu, Ee Bwana,

katikati ya mataifa;

nitaliimbia sifa jina lako.

5122:51 Za 21:1; 144:9-10; 1Sam 16; 13; Za 89:20; Mdo 13:23; 2Sam 7:13; Za 89:24, 29Humpa mfalme wake ushindi mkuu;

huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake,

kwa Daudi na wazao wake milele.”

Hoffnung für Alle

2. Samuel 22:1-51

Davids Danklied

(Psalm 18)

1David sang das folgende Danklied, nachdem der Herr ihn aus der Gewalt aller Feinde und auch aus der Hand von Saul befreit hatte:

2Der Herr ist mein Fels, meine Festung und mein Erretter,

3mein Gott, meine Zuflucht, mein sicherer Ort.

Er ist mein Schild, mein starker Helfer,22,3 Wörtlich: das Horn meines Heils. – Das Horn steht sinnbildlich für Stärke und Kraft.

meine Burg auf unbezwingbarer Höhe.

Du, Gott, bewahrst mich vor den Angriffen meiner Feinde.

4Gepriesen seist du, Herr!

Wenn ich zu dir um Hilfe rufe,

dann werde ich vor meinen Feinden gerettet.

5Ich war schon umgeben von den Fluten des Todes,

er drohte mich zu verschlingen wie eine mächtige Woge.

6Hilflos musste ich zusehen,

wie die tödliche Falle zuschnappte.

7In äußerster Bedrängnis schrie ich zum Herrn.

Ja, zu meinem Gott rief ich um Hilfe.

Da hörte er mich in seinem Tempel,

mein Schreien drang durch bis an sein Ohr.

8Plötzlich erbebte die Erde,

selbst der Himmel geriet ins Wanken,

denn glühender Zorn hatte Gott gepackt.

9Schwarzer Rauch quoll aus seiner Nase,

aus seinem Mund loderten Flammen,

und glühende Kohlen wurden herausgeschleudert.

10Er riss den Himmel auf

und kam auf dunklen Wolken zur Erde herunter.

11Auf einem Kerub flog er daher

und schwebte herab, vom Sturm getragen.

12Er hüllte sich in Finsternis,

verbarg sich in dichten, dunklen Regenwolken.

13Dann ging ein Lichtglanz von ihm aus,

und glühende Kohlen prasselten nieder.

14Der Herr ließ einen Donnerschlag auf den anderen folgen,

vom Himmel dröhnte die Stimme des höchsten Gottes.

15Er schoss seine Pfeile ab,

und die Feinde stoben auseinander.

Grelle Blitze zuckten und verwirrten das feindliche Heer.

16Sogar den Meeresboden konnte man sehen;

offen lagen die Fundamente der Erde da,

als der Herr meine Feinde bedrohte

und vor Entrüstung schnaubte.

17Er streckte mir seine Hand von oben entgegen

und riss mich aus den tosenden Fluten.

18Er befreite mich von der Übermacht meiner Feinde,

von allen, die mich hassten und so viel stärker waren als ich.

19Sie hatten mich überfallen, als ich schon im Unglück steckte.

Aber der Herr gab mir sicheren Halt

20und führte mich aus der Not hinaus in die Freiheit.

Er rettete mich. So viel bedeute ich ihm!

21Der Herr tat mir Gutes für meine Treue,

meine Rechtschaffenheit hat er belohnt.

22Denn stets bin ich dem Herrn gefolgt

und habe meinem Gott nie den Rücken gekehrt.

23Seine Gebote hielt ich mir immer vor Augen,

und seine Befehle schlug ich nicht in den Wind.

24Ich lebte vollkommen nach seinem Willen

und ging jedem Unrecht aus dem Weg.

25Ja, der Herr belohnte meine Treue,

meine Rechtschaffenheit übersah er nicht.

26Wer zu dir steht, Herr, dem stehst auch du zur Seite;

wer nach deinem Willen lebt, den enttäuschst du nicht.

27Wer ein reines Herz hat, kann sich ganz auf dich verlassen,

doch falsche Menschen führst du hinters Licht.

28Du hilfst denen, die sich selbst nicht überschätzen22,28 Oder: die sich selbst nicht helfen können..

Die Überheblichen aber stößt du von ihrem Thron.

29Herr, du machst die Finsternis um mich hell,

du bist mein Licht.

30Mit dir kann ich die Feinde angreifen;

mit dir, mein Gott, kann ich über Mauern springen.

31Was für ein Gott!

Sein Handeln ist vollkommen,

und was er sagt, ist durch und durch wahr.

Er beschützt alle, die zu ihm flüchten.

32Der Herr allein ist Gott!

Wer außer ihm ist so stark und unerschütterlich wie ein Fels?

33Gott allein ist meine Burg, in der ich Zuflucht finde.

Er ebnet mir meinen Weg.

34Er beflügelt meine Schritte,

lässt mich laufen und springen wie ein Hirsch.

Selbst auf steilen Felsen gibt er mir festen Halt.

35Er lehrt mich, die Waffen zu gebrauchen,

und zeigt mir, wie ich auch den stärksten Bogen spannen kann.

36Herr, deine Hilfe war für mich wie ein schützender Schild.

Du beugst dich zu mir herab und machst mich groß.

37Du räumst mir alle Hindernisse aus dem Weg,

noch nie bin ich beim Laufen gestürzt.

38Ich jagte meinen Feinden nach und überwältigte sie,

ich kehrte erst um, als auch der Letzte von ihnen gefallen war.

39Mit Wucht schlug ich sie nieder,

bis sie nicht mehr aufstehen konnten

und tot zu meinen Füßen lagen.

40Du, Herr, hast mich mit Kraft für diesen Kampf ausgerüstet,

du hast mir zum Sieg über meine Gegner verholfen.

41Dass sie fliehen mussten, verdanke ich dir;

alle, die mich hassten, konnte ich umbringen.

42Sie suchten nach Hilfe, doch weit und breit war kein Retter.

Sie schrien zum Herrn, aber er hörte nicht auf sie.

43Ich rieb sie auf, zermalmte sie zu Staub,

ich zertrat sie wie Dreck auf der Straße.

44Als ein Aufstand meines Volkes mich bedrohte,

hast du mir geholfen,

und mich zum Herrscher über viele Nationen gemacht.

Sogar Völker, die ich nicht kannte, haben sich mir unterworfen.

45Fremde ergaben sich, sobald sie nur von mir hörten,

und gingen gehorsam vor mir auf die Knie.

46Zitternd kamen sie aus ihren Festungen heraus

und hatten keine Kraft mehr zum Widerstand.

47Der Herr lebt! Er ist mein schützender Fels – ich preise ihn!

Ihn allein will ich rühmen,

denn er ist mein Gott, mein Fels, bei dem ich Rettung fand.

48Er ist es, der sich an meinen Feinden gerächt hat;

ganze Völker hat er mir unterworfen

49und mich der Gewalt meiner grausamen Gegner entrissen.

Du, Gott, gabst mir den Sieg über meine Feinde,

von diesen brutalen Menschen hast du mich befreit.

50Darum will ich dich loben, Herr.

Alle Völker sollen es hören!

Deinen Namen will ich preisen mit meinem Lied.

51Du hast deinen auserwählten König aus großen Gefahren errettet.

Ja, du erweist mir, David, deine Liebe,

und auch meine Nachkommen dürfen für alle Zeit darauf zählen.