2 Samweli 2 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Samweli 2:1-32

Daudi Atiwa Mafuta Kuwa Mfalme Wa Yuda

12:1 1Sam 23:2, 11-12; Mwa 13:18; 23:19; 1Sam 30:31; Hes 27:21; 1Sam 23:2-9; 1Fal 2:11Ikawa baada ya mambo haya, Daudi akamuuliza Bwana, “Je, nipande kwenda katika mojawapo ya miji ya Yuda?”

Bwana akasema, “Panda.”

Daudi akauliza, “Je, niende wapi?”

Bwana akajibu, “Nenda Hebroni.”

22:2 1Sam 25:42-43; 30:5Basi Daudi akakwea kwenda huko pamoja na wake zake wawili, Ahinoamu wa Yezreeli na Abigaili, mjane wa Nabali wa Karmeli. 32:3 1Sam 27:2; 1Nya 12:22; Mwa 13:18; 23:2; 37:14Pia Daudi akawachukua watu waliokuwa pamoja naye, kila mmoja na jamaa yake, nao wakaishi huko Hebroni na miji yake. 42:4 1Sam 30:31; 2:35; 2Sam 5:3-5; 1Nya 12:23-40; Amu 21:8; 1Sam 11:1; 31:11-13Ndipo watu wa Yuda wakaja Hebroni, huko wakamtia Daudi mafuta awe mfalme juu ya nyumba ya Yuda.

Daudi alipoambiwa kuwa ni watu wa Yabeshi-Gileadi waliomzika Sauli, 52:5 Amu 17:2; 1Sam 23:21; 2Tim 1:16; Za 115:15akatuma wajumbe kwa watu wa Yabeshi-Gileadi kuwaambia, “Bwana awabariki kwa kuonyesha wema huu kwa kumzika Sauli bwana wenu. 62:6 Kut 34:6; 2Tim 1:16; Mt 5:44Sasa Bwana na awaonyeshe wema na uaminifu, nami pia nitawaonyesha wema ule ule kwa kuwa mmefanya jambo hili. 72:7 Yos 1:6; Amu 5:21Sasa basi, kuweni hodari na mashujaa, kwa maana bwana wenu Sauli amekufa, nayo nyumba ya Yuda imenitia mafuta niwe mfalme juu yao.”

Vita Kati Ya Nyumba Ya Daudi Na Sauli

82:8 1Sam 14:50; 2Sam 3:27; 4:5; 1Nya 8:33; 9:36-39; Mwa 32:2; 1Sam 17:55; 2Sam 17:27Wakati huo Abneri mwana wa Neri, jemadari wa jeshi la Sauli, alikuwa amemchukua Ish-Boshethi mwana wa Sauli na kumleta hadi Mahanaimu. 92:9 Hes 32:26; Yos 19:24-31; 1Nya 12:29; Amu 1:32Akamweka awe mfalme juu ya nchi ya Gileadi, Waasheri,2:9 Waasheri hapa ni kabila moja la Israeli. Yezreeli, Efraimu, Benyamini na Israeli yote.

10Ish-Boshethi2:10 Ish-Boshethi maana yake Mtu wa Aibu, pia anaitwa Esh-Baali maana yake Mtu wa Baali (1Nya 8:33; 9:39). mwana wa Sauli alikuwa na umri wa miaka arobaini alipoanza kutawala Israeli, naye akatawala miaka miwili. Hata hivyo, nyumba ya Yuda ikamfuata Daudi. 112:11 2Sam 5:5Muda ambao Daudi alikuwa mfalme juu ya nyumba ya Yuda huko Hebroni ilikuwa miaka saba na miezi sita.

122:12 Yos 9:3; 18:25; Isa 28:21Abneri mwana wa Neri, pamoja na watu wa Ish-Boshethi mwana wa Sauli, wakatoka Mahanaimu kwenda Gibeoni. 132:13 2Sam 8:16; 19:13; 1Fal 1:17; 1Nya 2:16; 22:6; 27:34; Yer 41:12Yoabu mwana wa Seruya na watu wa Daudi wakatoka na kukutana nao kwenye bwawa la Gibeoni. Kikundi kimoja kiliketi upande mmoja wa bwawa, na kikundi kingine upande wa pili.

142:14 Mit 10:23; 13:10Ndipo Abneri akamwambia Yoabu, “Tuwaweke baadhi ya vijana wasimame na wapigane ana kwa ana mbele yetu.”

Yoabu akasema, “Sawa, na wafanye hivyo.”

15Kwa hiyo vijana wakasimama, wakahesabiwa: watu wa Benyamini na wa Ish-Boshethi mwana wa Sauli kumi na wawili, na upande wa Daudi kumi na wawili. 162:16 Amu 3:21Kisha kila mtu akakamatana na mpinzani wake kichwani na kuchomana kwa upanga, nao wakaanguka chini pamoja. Kwa hiyo mahali pale katika Gibeoni pakaitwa Helkath-Hasurimu.2:16 Helkath-Hasurimu maana yake Uwanja wa Mapambano.

172:17 2Sam 3:1; 1Sam 17:8; 1Fal 20:11Siku hiyo vita vilikuwa vikali sana, naye Abneri na watu wa Israeli wakashindwa na watu wa Daudi.

182:18 2Sam 3:39; 16:10; 19:22; 3:30; 10:7; 11:1; 14:1; 18:14; 20:8; 24:3; 1Fal 1:7; 2:5, 34; 1Sam 26:6; 2Sam 23:24; 2Nya 2:16; 1Nya 11:26; 27:1; 12:8; Za 6:5; Wim 2:9Wana watatu wa Seruya walikuwako huko: nao ni Yoabu, Abishai na Asaheli. Basi huyo Asaheli alikuwa na mbio kama paa. 19Asaheli akamfukuza Abneri, pasipo kugeuka kulia wala kushoto wakati akimfuata. 20Abneri akaangalia nyuma na kumuuliza, “Ni wewe, Asaheli?”

Akamjibu, “Ndiyo.”

212:21 1Sam 17:42Ndipo Abneri akamwambia, “Geuka upande wa kulia au kushoto. Mchukue mmoja wa vijana wa kiume na umvue silaha zake.” Lakini Asaheli hakuacha kumfukuza.

222:22 2Sam 3:27Abneri akamwonya tena Asaheli akimwambia, “Acha kunifukuza! Kwa nini nikuue? Je, nitawezaje kumtazama ndugu yako Yoabu usoni?”

232:23 2Sam 3:27; 4:6; 20:17Lakini Asaheli alikataa kuacha kumfuatia, kwa hiyo Abneri akamchoma Asaheli tumboni kwa ncha butu ya mkuki wake, mkuki ukamtoboa ukatokea mgongoni mwake. Akaanguka na kufa papo hapo. Ikawa kila mtu alisimama alipofika mahali pale Asaheli alipoanguka na kufa.

242:24 Yos 9:3; 10:2Lakini Yoabu na Abishai walimfuata Abneri, na jua lilipokuwa linatua, wakafika kwenye kilima cha Ama, karibu na Gia kwenye njia ya kuelekea kwenye nyika ya Gibeoni. 25Ndipo watu wa kabila la Benyamini wakakusanyika tena nyuma ya Abneri. Wakaunda kikosi na kujiimarisha juu ya kilima.

262:26 Kum 32:42; Yer 46:10, 14; Nah 2:13; 3:15; Ay 18:2; 19:2; Za 4:2; Mdo 7:16Abneri akamwita Yoabu, akamwambia, “Je, ni lazima upanga uendelee kuangamiza milele? Hutambui kwamba jambo hili litaishia katika uchungu? Utaacha kuwaagiza watu wako waache kuwafuatilia ndugu zao hata lini?”

272:27 Mit 17:14; 20:18; Lk 14:31-32Yoabu akajibu, “Hakika kama aishivyo Mungu, kama hukusema, hawa watu wangeendelea kuwafuatia ndugu zao mpaka asubuhi.”

282:28 2Sam 18:16; 20:23; Amu 3:27Basi Yoabu akapiga tarumbeta, nao watu wote wakasimama, hawakuwafuata Israeli tena, wala hawakuwapiga tena.

292:29 Kum 3:17; Mwa 32:2; Wim 2:17; Yos 21:38; 2Sam 17:24Usiku ule wote Abneri na watu wake wakatembea kupitia Araba. Wakavuka Mto Yordani, wakaendelea wakipitia nchi yote ya Bithroni wakafika Mahanaimu.

30Basi Yoabu akarudi kutoka kumfuatia Abneri, na kuwakusanya watu wake wote. Pamoja na Asaheli, watu kumi na tisa wa Daudi walikuwa wamepotea. 31Lakini watu wa Daudi walikuwa wamewaua watu wa kabila la Benyamini 360 waliokuwa pamoja na Abneri. 322:32 Mwa 49:29; 47:29-30; Amu 8:32; 2Sam 17:24Wakamchukua Asaheli, wakamzika katika kaburi la baba yake huko Bethlehemu. Kisha Yoabu na watu wake wakatembea usiku kucha na kufika huko Hebroni wakati wa mapambazuko.

Swedish Contemporary Bible

2 Samuelsboken 2:1-32

Juda kröner David till kung

1Efter en tid frågade David Herren: ”Ska jag flytta tillbaka till Juda?” ”Ja”, svarade Herren. ”Till vilken stad ska jag flytta?” frågade David. Herren svarade: ”Till Hebron.”

2David flyttade då dit med sina båda hustrur, Achinoam från Jisreel och Avigajil, Navals änka från Karmel. 3Han tog också med sig sina män och deras familjer och de bosatte sig i städerna runt Hebron. 4Männen i Juda kom sedan dit och smorde David till kung över hela Juda.

När David hörde att männen i Javesh i Gilead hade begravt Saul, 5skickade han dem detta budskap: ”Herren ska välsigna er för den trohet ni visat mot er herre Saul genom att begrava honom. 6Herren ska vara nådig och trofast mot er. Också jag ska belöna er, eftersom ni handlat som ni gjort. 7Fortsätt vara starka och modiga! Saul är död, men Juda har smort mig till sin kung.”

David blir kung över Israel

8Men Avner, Ners son och Sauls överbefälhavare för hären, hade fört Sauls son Ish-Boshet till Machanajim 9och gjort honom till kung över Gilead, Asher, Jisreel, Efraim, Benjamins stam och över hela Israel. 10Han var fyrtio år gammal när han blev kung och han regerade i två år. Under denna tid förblev endast Judas stam trogen David 11och han regerade över Juda i Hebron i sju år och sex månader.

Inbördeskrig

12Avner, Ners son, drog ut med Sauls son Ish-Boshets trupper från Machanajim till Givon. 13Joav, Serujas son, drog ut med Davids trupper. De möttes vid Givons damm och slog sig ner på var sin sida om dammen. 14Då sa Avner till Joav: ”Vi låter några av våra unga soldater mötas man mot man inför oss!”2:14 Tvekamp, eller kamp mellan ett begränsat antal soldater, var ett vanligt sätt att avgöra strider i det här området. Se 1 Sam 17:4, där David mötte Goljat.

Joav gick med på det, 15och tolv män ställde upp från Benjamins stam för Ish-Boshet och tolv män för David. 16Var och en grep sin motståndare i huvudet och stack sitt svärd i hans sida. Samtliga dog. Denna plats i Givon har sedan dess kallats Svärdseggarnas åker.

17Striden som då började blev mycket hård, men Avner och Israels män besegrades av Davids trupper. 18Serujas tre söner, Joav, Avishaj och Asael, var också med i striden. Asael kunde springa snabbt som en gasell på fältet, 19och han förföljde Avner utan att vika från honom åt något håll. 20Avner vände sig om och ropade: ”Är det du, Asael?”

”Ja, det är det”, ropade Asael tillbaka. 21”Jaga någon annan, angrip någon av de yngre och ta hans rustning!” skrek Avner. Men Asael fortsatte att förfölja honom.

22Då ropade Avner: ”Ge dig iväg härifrån! Jag skulle aldrig kunna se din bror Joav i ögonen om jag var tvungen att döda dig!”

23Men Asael vägrade vända om och då genomborrade Avner honom i buken med bakänden av sitt spjut. Det gick rakt igenom hans kropp och kom ut i ryggen. Asael föll till marken och dog omedelbart. Alla stannade upp när de passerade platsen där han låg.

24Men Joav och Avishaj förföljde Avner. Solen höll just på att gå ner när de kom till Ammakullen nära Giach längs vägen till Givons öken. 25Avners trupper från Benjamins stam grupperade sig bakom honom på kullens topp 26och Avner ropade ner till Joav: ”Måste vi fortsätta att döda varandra i all evighet? Förstår du inte att det kommer att sluta med katastrof? Hur länge ska du vänta innan du befaller dina män att sluta döda sina bröder?”

27Joav ropade tillbaka: ”Så sant Gud lever, om du inte hade sagt något skulle de ha fortsatt att jaga sina bröder ända till morgonen!”

28Han blåste sedan i sitt horn och hans män slutade jaga Israels trupper och striden upphörde.

29Den natten återvände Avner och hans män genom Jordandalen och gick över floden. De marscherade hela förmiddagen ända till Machanajim. 30Joav och hans män återvände också hem och när de räknade styrkorna saknades bara nitton man, förutom Asael. 31Men själva hade de dödat 360 män från Benjamins stam som hade varit med Avner.

32Joav och hans män tog med sig Asaels kropp till Betlehem och begravde honom i hans fars grav. Sedan gick de hela natten och nådde fram till Hebron i gryningen.