2 Nyakati 34 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Nyakati 34:1-33

Yosia Afanya Matengenezo

(2 Wafalme 22:1-2)

134:1 1Nya 3:14; Sef 1:1; 1Fal 3:7-9; 13:2; 2Nya 35:25Yosia alikuwa na miaka minane alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka thelathini na mmoja. 234:2 2Nya 29:2Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana na kuenenda katika njia za Daudi baba yake, hakugeuka upande wa kuume wala wa kushoto.

334:3 1Fal 13:2; 1Sam 1:24; 1Nya 16:11; Mit 8:17; Za 119:9; 2Tim 3:15; 2Nya 15:2; 1Fal 13:2Katika mwaka wa nane wa utawala wake, alipokuwa angali bado mdogo, alianza kumtafuta Mungu wa Daudi baba yake. Katika mwaka wake wa kumi na mbili alianza kusafisha mahali pa juu pa kuabudia miungu pa Yuda na Yerusalemu, akiondoa nguzo za Ashera, sanamu za kuchonga na vinyago vya kusubu. 434:4 Kut 34:13; 2Fal 23:11; Mik 1:5; Kut 32:30; Law 26:30Mbele ya macho yake, wakazibomoa madhabahu za Mabaali, wakazivunja madhabahu za kufukizia uvumba zilizokuwa zimesimama juu yake, wakazivunja nguzo za Ashera, sanamu na vinyago. Hivi alivivunja vipande vipande na kuvisambaza juu ya makaburi ya waliokuwa wamevitolea kafara. 534:5 1Fal 13:2Akachoma mifupa ya makuhani wao juu ya madhabahu zao na kwa njia hiyo akaitakasa Yuda na Yerusalemu. 6Katika miji ya Manase, Efraimu na Simeoni, hadi Naftali na kwenye magofu yanayoizunguka, 734:7 Kut 32:20; Kum 9:21; 2Nya 31:1akavunja madhabahu na nguzo za Ashera na kuzipondaponda hizo sanamu hadi zikawa unga na kukata vipande vipande madhabahu zote za kufukizia uvumba katika Israeli yote. Kisha akarudi Yerusalemu.

834:8 2Fal 22:3Katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Yosia, ili kutakasa nchi na Hekalu, akawatuma Shafani, mwana wa Azalia na Maaseya mtawala wa mji, pamoja na Yoa mwana wa Yoahazi, mwandishi ili kukarabati Hekalu la Bwana Mungu wake.

934:9 1Nya 6:13; 2Nya 35:8; 2Fal 12:4Wakamwendea Hilkia kuhani mkuu na kumpa fedha ambazo zilikuwa zimeletwa ndani ya Hekalu la Bwana ambazo Walawi waliokuwa mabawabu walikuwa wamezikusanya kutoka kwa watu wa Manase, Efraimu na mabaki wote wa Israeli kutoka kwa watu wote wa Yuda na Benyamini na wakazi wa Yerusalemu. 10Kisha wakazikabidhi hizo fedha kwa watu waliowekwa ili kusimamia kazi ya Hekalu la Bwana. Hawa watu waliwalipa wafanyakazi waliokarabati na kutengeneza Hekalu lipate kurudi katika hali yake. 1134:11 2Nya 24:12; 33:4-7Wakawapa pia mafundi seremala na waashi fedha ili kununua mawe yaliyochongwa, mbao kwa ajili ya kufungia na boriti kwa ajili ya majengo ambayo wafalme wa Yuda walikuwa wameyaacha yakawa magofu.

1234:12 2Nya 12:15; 1Nya 25:1; Neh 7:2; 1Kor 4:2; 2Fal 12:15; 22:7; Mt 28:20Watu wakafanya kazi kwa uaminifu. Waliokuwa wamewekwa juu yao ili kuwaelekeza ni Yahathi na Obadia, Walawi wa uzao wa Merari, Zekaria na Meshulamu, waliotoka kwenye uzao wa Kohathi. Walawi wote waliokuwa na ufundi wa kupiga ala za uimbaji, 1334:13 1Nya 23:4; Ezr 7:6; Yer 8:8; Mt 26:3wakawa wasimamizi wa vibarua na kuwaongoza wale waliofanya kila aina ya kazi. Baadhi ya Walawi walikuwa waandishi, maafisa na mabawabu.

Kitabu Cha Sheria Chapatikana

(2 Wafalme 22:3-20)

1434:14 Kum 31:24-26; 2Fal 22:8Wakati walikuwa wakizitoa nje fedha zilizokuwa zimetolewa kwenye Hekalu la Bwana, kuhani Hilkia akakipata kile Kitabu cha Sheria ya Bwana kilichokua kimetolewa kwa mkono wa Mose. 1534:15 2Fal 22:8; Neh 8:1Hilkia akamwambia Shafani mwandishi, “Nimekipata Kitabu cha Sheria ndani ya Hekalu la Bwana.” Akampa Shafani kile Kitabu.

16Kisha Shafani akakipeleka kile Kitabu kwa mfalme na kumwambia, “Maafisa wako wanafanya kila kitu kama walivyokabidhiwa kufanya. 17Wamelipa fedha zilizokuwa katika Hekalu la Bwana na wamewakabidhi wasimamizi na wafanyakazi.” 1834:18 Kum 17:19; Yos 1:8Kisha Shafani mwandishi akamwarifu mfalme kuwa, “Kuhani Hilkia amenipa Kitabu.” Naye Shafani akakisoma mbele ya mfalme.

1934:19 Kum 28:3-68; Yos 7:6; Gal 2:19; 3:10-11; Rum 7:7-14; Hab 3:16; Rum 3:20; 2Fal 19:1; Neh 8:9; Za 94:12-13; 119:120; Yer 23:9; Yoe 2:13Mfalme aliposikia yale maneno ya Sheria, akayararua mavazi yake. 2034:20 2Fal 22:3-12Akatoa maagizo haya kwa Hilkia, Ahikamu mwana wa Shafani, Abdoni mwana wa Mika, Shafani mwandishi na Asaya mtumishi wa mfalme, 2134:21 Mao 2:4; 4:11; Eze 36:18; 2Fal 17:6“Nendeni mkamuulize Bwana kwa ajili yangu na kwa ajili ya mabaki walioko Israeli na Yuda kuhusu yale yaliyoandikwa ndani ya kitabu hiki ambacho kimepatikana. Hasira ya Bwana ni kubwa mno ambayo imemwagwa juu yetu kwa sababu baba zetu hawakulishika neno la Bwana wala hawajatenda kulingana na yale yote yaliyoandikwa katika Kitabu hiki.”

2234:22 Kut 15:20; Lk 2:36; Mdo 21:9; Neh 6:14; Amu 4:4; 2Fal 22:14Hilkia pamoja na wale wote mfalme aliokuwa amewatuma pamoja naye wakaenda kuzungumza na nabii mke aitwaye Hulda, aliyekuwa mke wa Shalumu mwana wa Tokhathi, mwana wa Hasra mtunzaji wa chumba cha mavazi. Hulda aliishi Yerusalemu, katika Mtaa wa Pili.

23Akawaambia, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana, Mungu wa Israeli: Mwambieni yule mtu aliyewatuma ninyi kwangu, 2434:24 Mit 16:4; 2Nya 36:14-20; Kum 28:15-68; Dan 9:11-16; Yos 23:16; 2Fal 21:12; 23:26-27; Isa 5:5; Yer 25:9; Amo 3:6; Zek 1:6‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana: Nitaleta maafa juu ya mahali hapa na watu wake, laana zote zilizoandikwa ndani ya hicho kitabu ambazo zimesomwa mbele ya mfalme wa Yuda. 2534:25 2Nya 33:3-6; Yer 22:9Kwa sababu wameniacha mimi na kufukiza uvumba kwa miungu mingine na kunighadhibisha kwa kazi yote ya mikono yao, hivyo hasira yangu itamwagwa juu ya mahali hapa, wala haitatulizwa.’ 26Mwambieni mfalme wa Yuda, ambaye amewatuma kumuuliza Bwana, ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana, Mungu wa Israeli kuhusu maneno uliyoyasikia: 2734:27 2Nya 12:7; 32:26; Za 86:5Kwa kuwa moyo wako ulikuwa msikivu na ulijinyenyekeza mbele za Mungu uliposikia kile nilichosema dhidi ya mahali hapa na watu wake na kwa sababu ulijinyenyekeza mbele zangu na uliyararua mavazi yako na kulia mbele zangu, nimekusikia, asema Bwana. 2834:28 2Nya 35:20-25; 32:26Basi nitakukusanya kwa baba zako, nawe utazikwa kwa amani. Macho yako hayataona maafa yote nitakayoleta juu ya mahali hapa na juu ya wote wanaoishi hapa.’ ”

Kwa hiyo wakampelekea mfalme jibu lake.

Yosia Afanya Agano La Kutii

(2 Wafalme 23:1-20)

2934:29 2Fal 23:1Kisha mfalme akawaita pamoja wazee wote wa Yuda na Yerusalemu. 30Akapanda kwenda hekaluni mwa Bwana pamoja na watu wa Yuda, watu wa Yerusalemu, makuhani na Walawi, watu wote, wakubwa kwa wadogo. Akasoma wakiwa wanasikia maneno yote ya Kitabu cha Agano, ambacho kilikuwa kimepatikana katika Hekalu la Bwana. 3134:31 1Fal 7:15; 2Fal 11:14-17; 2Nya 29:10; Kum 13:4Mfalme akasimama karibu na nguzo yake na kufanya upya Agano mbele za Bwana ili kumfuata Bwana na kuzishika amri zake, maagizo na sheria kwa moyo wake wote na kwa roho yake yote na ili kuyatii maneno ya Agano yaliyoandikwa katika kitabu hiki.

3234:32 Yer 3:10; 2Nya 14:2Ndipo akamtaka kila mmoja katika Yerusalemu na Benyamini kuweka ahadi zao wenyewe kwa hilo Agano, watu wa Yerusalemu wakafanya hivyo kwa kufuata Agano la Bwana, Mungu wa baba zao.

3334:33 1Fal 11:5; Yer 3:10; 2Nya 24:2Yosia akaondoa machukizo yote ya sanamu kutoka nchi yote iliyokuwa mali ya Waisraeli na akawataka wale wote waliokuwako katika Israeli wamtumikie Bwana Mungu wao. Kwa muda wote alioishi, hawakushindwa kumfuata Bwana, Mungu wa baba zao.

Swedish Contemporary Bible

2 Krönikeboken 34:1-33

Josia regerar i Juda

(34:1—36:1)

(2 Kung 22:1-2; 23:4-20)

1Josia var åtta år gammal när han blev kung, och han regerade i Jerusalem i trettioett år. 2Han gjorde det som var rätt i Herrens ögon, och han följde sin förfader Davids exempel utan att vika åt något håll.

3I sitt åttonde regeringsår, medan han fortfarande var ung, började han söka sin far Davids Gud, och under sitt tolfte år började han rena Juda och Jerusalem från offerplatser, asherapålar och snidade och gjutna gudabilder. 4Man rev ner baalsaltarna inför honom, högg i stycken rökelsealtarna som stod på dem och bröt sönder asherapålarna, och de snidade och gjutna gudabilderna krossade han till stoft och strödde ut över deras gravar som hade offrat åt dem. 5Sedan brände han upp prästernas ben på deras egna altaren och renade på så sätt Juda och Jerusalem. 6Också i städerna i Manasse, Efraim, Simon och ända bort till Naftali och områdena34:6 Kan också betyda ruiner, hus eller tempel. Översättningen här grundar sig på Septuaginta. runt dem, 7rev han ner altarna, asherapålarna, och gudabilderna krossade han till stoft och högg ner rökelsealtarna i stycken i hela Israel. Sedan vände han tillbaka till Jerusalem.

Josia renar landet och templet

(2 Kung 22:3-7)

8Under det artonde året av sin regering, sedan han renat landet och templet, skickade han Shafan, Asaljas son, och Maaseja, stadskommendanten i Jerusalem, och kanslern Joach, Joachas son, för att reparera Herrens, sin Guds, hus.

9De gick då till översteprästen Hilkia med det silver som samlats in i Guds hus, som de leviter som höll vakt där hade samlat från Manasse, Efraim och resten av Israel, liksom av Juda och Benjamin och av folket i Jerusalem. 10De överlämnade det åt de män som var utsedda för att övervaka arbetet i Herrens hus, så att de kunde betala till dem som arbetade med att reparera det. 11De betalade snickarna och byggnadsarbetarna, så att de kunde köpa byggnadssten och timmer till bjälkar och till att timra upp de byggnader som kungarna i Juda hade låtit förfalla.

12Männen arbetade plikttroget under ledning av Jachat och Obadja, leviter av Meraris släkt, och Sakarja och Meshullam av Kehats släkt. Leviter, som var skickliga musiker, 13övervakade och ledde de olika arbetena. Andra leviter var sekreterare, tillsyningsmän och dörrvaktare.

En bokrulle med Guds lag hittas

(2 Kung 22:8-20)

14När man tog fram silvret som samlats in vid Herrens hus, hittade prästen Hilkia boken med Herrens lag, som hade getts genom Mose. 15Hilkia talade om för kungens sekreterare Shafan: ”Jag har hittat boken med lagen i Herrens hus.” Och han gav Shafan boken.

16Shafan tog den med sig till kungen när han skulle rapportera till honom: ”Dina tjänare gör allt de har fått i uppdrag att göra. 17Silvret som har funnits i Herrens hus har betalats ut och överlämnats till tillsyningsmännen och arbetarna.” 18Sedan talade sekreteraren Shafan om för kungen att Hilkia hade gett honom en bokrulle och läste ur den för kungen.

19När kungen hörde vad lagen föreskrev, rev han sönder sina kläder. 20Han befallde Hilkia och Achikam, Shafans son, Avdon, Mikas son, sekreteraren Shafan och sin assistent Asaja: 21”Gå och fråga Herren för mig och för den rest som finns kvar av Israel och Juda om det som står i den bok som nu upptäckts! Herrens vrede är stor och har vällt ut över oss därför att våra förfäder inte har följt Herrens ord och inte handlat så som det står i denna bok.”

22Hilkia och kungens män gick då till profetissan Hulda, hustru till Shallum, föreståndaren för klädkammaren, Tokhats son och Hasras sonson. Hon bodde i Jerusalem i Nya Staden. När de talade med henne om detta, 23svarade hon dem: ”Så säger Herren, Israels Gud: ’Säg till den man som skickade er till mig: 24Så säger Herren: Jag kommer att låta olycka drabba denna plats och dess invånare, alla de förbannelser som är skrivna i boken och som har lästs för kungen av Juda. 25De har övergett mig och tänt offereld åt andra gudar och väckt min vrede genom allt de gjort, och därför ska min vrede drabba denna plats, och den kan inte släckas.’ 26Säg till kungen av Juda, som skickade er hit för att fråga Herren: ’Så säger Herren, Israels Gud, om de ord du har hört: 27Därför att du är bedrövad i ditt inre och har ödmjukat dig inför Gud, sedan du fått höra hans ord mot denna plats och dess invånare, och du har ödmjukat dig inför mig och rivit sönder dina kläder och gråtit inför mig, därför har jag hört dig, säger Herren. 28Jag ska låta dig dö och bli begravd bland dina fäder i ro. Du får slippa se allt det onda som jag ska låta komma över denna plats och dess invånare.’ ”

De återvände till kungen med detta svar.

Josia reformerar gudstjänsten. Hans påskfirande

(2 Kung 23:1-3)

29Då kallade kungen samman alla de äldste i Juda och Jerusalem. 30Han gick upp till Herrens hus tillsammans med alla män i Juda och invånarna i Jerusalem, präster och leviter och allt folk, både stora och små. Han läste för dem allt som stod i förbundsboken som upptäckts i Herrens hus. 31Kungen stod vid sin på sin plats och förnyade inför Herren förbundet, för att de skulle hålla sig till Herren, lyda hans bud, förordningar och föreskrifter och med hela sitt hjärta och hela sin själ och fullgöra bestämmelserna som boken föreskrev. 32Sedan lät han alla i Jerusalem och Benjamin träda in i förbundet, och invånarna i Jerusalem gjorde så, i enlighet med Guds, sina fäders Guds, förbund.

33Sedan avlägsnade Josia alla avskyvärda gudar från israeliternas alla områden och fick alla som fanns i Israel att tjäna Herren, sina fäders Gud.

Så länge han levde vände de sig inte bort från Herren, sina fäders Gud.