2 Nyakati 27 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Nyakati 27:1-9

Yothamu Mfalme Wa Yuda

(2 Wafalme 15:32-38)

127:1 1Fal 15:5, 32; 1Nya 3:12; Isa 1:1; Hos 1:1; Mik 1:1Yothamu alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na sita. Mama yake aliitwa Yerusha binti Sadoki. 227:2 2Nya 26:16-21; Za 119:120; 2Fal 15:35Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana kama Uzia baba yake alivyokuwa amefanya, lakini tofauti na yeye, hakuingilia huduma za hekaluni mwa Bwana. Lakini hata hivyo, watu wakaendelea na desturi zao mbaya. 327:3 2Nya 26:16-21; 33:14; Neh 3:26Yothamu akajenga upya Lango la Juu la Hekalu la Bwana na kufanya kazi kubwa kwenye ukuta katika kilima cha Ofeli. 4Akajenga miji katika vilima vya Yuda pamoja na ngome na minara mwituni.

527:5 2Nya 26:8; Mwa 19:36; Yer 49:1-6; 2Fal 3:4Yothamu akafanya vita na mfalme wa Waamoni na kumshinda. Mwaka ule Waamoni wakamlipa talanta 10027:5 Talanta 100 za fedha ni sawa na tani 3.75. za fedha, kori 10,00027:5 Kori 10,000 za ngano ni sawa na tani 2.2. za ngano na kori 10,000 za shayiri. Waamoni wakamletea kiasi hicho hicho mwaka wa pili na wa tatu.

627:6 2Nya 26:5; 1Sam 2:30; 1Nya 12:14; 19:3; Za 34:8; 40:4Yothamu akaendelea kuwa na nguvu kwa sababu alienenda kwa ukamilifu mbele za Bwana Mungu wake.

7Matukio mengine ya utawala wa Yothamu, pamoja na vita vyake vyote na vitu vingine alivyofanya, vimeandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli na Yuda. 8Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na sita. 9Yothamu akalala na baba zake na akazikwa katika Mji wa Daudi. Naye Ahazi mwanawe akawa mfalme baada yake.

King James Version

2 Chronicles 27:1-9

1Jotham was twenty and five years old when he began to reign, and he reigned sixteen years in Jerusalem. His mother’s name also was Jerushah, the daughter of Zadok. 2And he did that which was right in the sight of the LORD, according to all that his father Uzziah did: howbeit he entered not into the temple of the LORD. And the people did yet corruptly. 3He built the high gate of the house of the LORD, and on the wall of Ophel he built much.27.3 Ophel: or, the tower 4Moreover he built cities in the mountains of Judah, and in the forests he built castles and towers.

5¶ He fought also with the king of the Ammonites, and prevailed against them. And the children of Ammon gave him the same year an hundred talents of silver, and ten thousand measures of wheat, and ten thousand of barley. So much did the children of Ammon pay unto him, both the second year, and the third.27.5 So…: Heb. This 6So Jotham became mighty, because he prepared his ways before the LORD his God.27.6 prepared: or, established

7¶ Now the rest of the acts of Jotham, and all his wars, and his ways, lo, they are written in the book of the kings of Israel and Judah. 8He was five and twenty years old when he began to reign, and reigned sixteen years in Jerusalem.

9¶ And Jotham slept with his fathers, and they buried him in the city of David: and Ahaz his son reigned in his stead.