2 Nyakati 26 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Nyakati 26:1-23

Uzia Mfalme Wa Yuda

(2 Wafalme 14:21-22; 15:1-7)

126:1 1Fal 14:21; 2Nya 22:1Kisha watu wote wa Yuda wakamtwaa Uzia, aliyekuwa na umri wa miaka kumi na sita, nao wakamfanya mfalme mahali pa Amazia baba yake. 2Ndiye alijenga upya Elathi kuirudisha kwa Yuda baada ya Amazia kulala pamoja na baba zake.

3Uzia alikuwa na umri wa miaka kumi na sita alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka hamsini na miwili. Mama yake aliitwa Yekolia wa Yerusalemu. 4Akatenda yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Amazia baba yake alivyofanya. 526:5 2Nya 15:2; Mwa 41:15; Dan 1:17; 2Nya 7:2; Dan 2:9; 10:1Akamtafuta Mungu katika siku za Zekaria, aliyemwelekeza kumcha Mungu. Wakati wote alipomtafuta Bwana, Mungu alimfanikisha.

626:6 Isa 2:6; Yer 25:20; Amo 3:9; Isa 14:29; 1Nya 21:16Alipigana vita dhidi ya Wafilisti na kubomoa kuta za Gathi, Yabne na Ashdodi. Kisha akajenga upya miji karibu na Ashdodi na mahali pengine katikati ya Wafilisti. 726:7 2Nya 21:16; 1Nya 5:20; 2Nya 20:1; 14:11; Mdo 26:22Mungu akamsaidia dhidi ya Wafilisti na dhidi ya Waarabu walioishi Gur-Baali na dhidi ya Wameuni. 826:8 Mwa 19:38; 2Nya 17:11; 1Sam 11:1; 2Sam 8:2Waamoni wakamletea Uzia ushuru, umaarufu wake ukaenea hadi kwenye mpaka wa Misri, kwa sababu alikuwa amekuwa na nguvu sana.

926:9 2Fal 14:13; 2Nya 25:23; Neh 2:13; 3:13; Zek 14:10Uzia akajenga minara huko Yerusalemu katika Lango la Pembeni, katika Lango la Bondeni na katika pembe, mahali kuta zikutanapo, kisha akaijengea ngome. 1026:10 2Nya 21:16Akajenga pia minara jangwani na kuchimba visima vingi vya maji, kwa sababu alikuwa na mifugo mingi chini ya vilimani na kwenye nchi tambarare. Alikuwa na watu wanaofanya kazi katika mashamba yake na kwenye mashamba yake ya mizabibu huko vilimani na katika ardhi zenye rutuba, kwa kuwa aliupenda udongo.

11Zaidi ya hayo, Uzia alikuwa na jeshi lililofunzwa vizuri, lililokuwa tayari kwenda vitani kwa vikosi kufuatana na idadi yao kama walivyokusanywa na Yeieli mwandishi na Maaseya msimamizi chini ya maelekezo ya Hanania, mmojawapo wa maafisa wa mfalme. 12Idadi yote ya viongozi wa jamaa waliowaongoza hawa wapiganaji walikuwa 2,600. 13Chini ya uongozi wao kulikuwa na jeshi la askari 307,500 watu waliofundishwa kwa ajili ya vita, jeshi lenye nguvu la kumsaidia mfalme dhidi ya adui zake. 1426:14 Yer 46:4Uzia akalipatia jeshi lote ngao, mikuki, chapeo, dirii, pinde na mawe ya kombeo. 15Huko Yerusalemu watu wenye utaalamu mkubwa wakatengeneza mitambo iliyotumika katika minara na kwenye pembe za ulinzi ili kurusha mishale na kuvurumisha mawe makubwa. Sifa zake zikaenea mbali sana kwa sababu alisaidiwa mno mpaka akawa na nguvu sana.

1626:16 2Fal 14:10; Kum 32:15; 2Nya 25:19; 1Nya 5:25; 2Fal 16:12-13; Hab 2:4; Kol 2:18; Kum 8:14Lakini baada ya Uzia kuwa na nguvu sana, majivuno yake yakamsababishia kuanguka. Alikosa uaminifu kwa Bwana Mungu wake, naye akaingia hekaluni mwa Bwana ili afukize uvumba kwenye madhabahu ya kufukizia uvumba. 1726:17 1Nya 6:10; 1Fal 4:2; Mdo 26:22Azaria kuhani akiwa pamoja na makuhani wengine themanini wa Bwana wenye ujasiri wakamfuata huko ndani. 1826:18 Hes 16:39; 18:1-7; Kut 30:7; Yer 13:18; 1Nya 6:49; 2Nya 19:2; Mt 14:4; Gal 2:21Wakamkabili na kumwambia, “Siyo sawa kwako, Uzia, kumfukizia Bwana uvumba. Hiyo ni kazi ya makuhani, wazao wa Aroni, ambao wamewekwa wakfu ili kufukiza uvumba. Ondoka mahali patakatifu, kwa kuwa umekosa uaminifu nawe hutaheshimiwa na Bwana.”

1926:19 2Fal 5:25-27; Hes 12:10Uzia, ambaye alikuwa na chetezo mkononi mwake tayari kufukiza uvumba, akakasirika. Alipokuwa anawaghadhibikia makuhani mbele ya madhabahu ya kufukizia uvumba katika Hekalu la Bwana, ukoma ukamtokea penye kipaji chake cha uso. 2026:20 Es 6:12Azaria kuhani mkuu pamoja na makuhani wengine wote walipomtazama wakaona kwamba alikuwa na ukoma penye kipaji chake cha uso wakaharakisha kumtoa nje. Naam, hata yeye mwenyewe alikuwa anatamani kuondoka kwa sababu Bwana alikuwa amempiga.

2126:21 Law 13:46; 14:8; Kut 4:6; 2Fal 15:5; Hes 5:2Mfalme Uzia alikuwa na ukoma mpaka siku ya kufa kwake. Akatengwa katika nyumba ya pekee akiwa mwenye ukoma, naye akawa ametengwa kutoka Hekalu la Bwana. Yothamu mwanawe akawa msimamizi wa jumba la mfalme, pia akawaongoza watu wa nchi.

2226:22 2Fal 15:1; Isa 6:1Matukio mengine ya utawala wa Uzia, kuanzia mwanzo mpaka mwisho, yameandikwa na nabii Isaya mwana wa Amozi. 2326:23 2Fal 15:7; Isa 6:1Uzia akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa karibu nao katika shamba la kuzikia lililokuwa mali ya wafalme, kwa kuwa watu walisema, “Alikuwa na ukoma.” Yothamu mwanawe akawa mfalme baada yake.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

历代志下 26:1-23

犹大王乌西雅

1全体犹大人立十六岁的乌西雅为王,继承他父亲亚玛谢的王位。 2亚玛谢与祖先同眠后,乌西雅犹大收复了以禄城,并重新修建。 3乌西雅十六岁登基,在耶路撒冷执政五十二年。他母亲叫耶可利雅,是耶路撒冷人。 4他效法他父亲亚玛谢,做耶和华视为正的事。 5撒迦利亚在世之日,乌西雅寻求上帝,撒迦利亚教导他敬畏上帝。当他寻求上帝时,上帝就使他亨通。

6他出兵攻打非利士人,把迦特雅比尼亚实突的城墙夷平后,在亚实突境内及非利士人的其他地区兴建城邑。 7上帝帮助他攻打非利士人和住在姑珥·巴力阿拉伯人及米乌尼人。 8亚扪人向他进贡,乌西雅的名声传到埃及,因他极其强大。

9乌西雅耶路撒冷的角门、谷门和城墙拐角的地方建造城楼,并加固城楼, 10又在旷野建造瞭望塔,挖了许多水井,因为他在高原和平原有很多牲畜。他雇人在山区和沃野为他耕种和照料葡萄园,因为他喜爱农耕。

11乌西雅有支可以随时列队出战的军兵,归书记耶利和官长玛西雅召集,由王的将军哈拿尼雅统领。 12率领战士的族长有两千六百名, 13他们手下有三十万七千五百精兵,随时帮助王攻打敌人。 14乌西雅为全军备有盾牌、矛枪、头盔、铠甲、弓箭和投石器用的石头, 15又让巧匠在耶路撒冷设计和制造兵器,安放在城楼和角楼上,用来发射弓箭和石头。乌西雅威名远扬,因为他得到非常的帮助,极其强盛。

16乌西雅强盛后,便心高气傲,以致走向灭亡。他干犯他的上帝耶和华,擅自进入耶和华的殿在香坛上烧香。 17祭司亚撒利雅率领八十位耶和华勇敢的祭司跟着进殿, 18阻止乌西雅王,说:“乌西雅啊,给耶和华烧香不是你可以做的事,乃是承受圣职做祭司的亚伦子孙的事。离开圣所吧!你已干犯耶和华上帝,必不能从祂那里得荣耀。” 19手拿香炉要烧香的乌西雅大怒,正当他在耶和华殿里的香坛旁向众祭司发怒的时候,他额头上突然患了麻风病。 20亚撒利雅大祭司和众祭司见状,就催促他出殿,他急忙出去了,因为耶和华降灾给他。 21乌西雅王到死一直有麻风病。他被隔离在别的宫中,不得进耶和华的殿。他儿子约坦管理王室,治理国家。

22乌西雅其他的事迹,自始至终都是亚摩斯的儿子以赛亚先知记载的。 23乌西雅与祖先同眠后,葬在他祖坟附近、王室的坟场,因为他有麻风病。他儿子约坦继位。