2 Nyakati 25 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Nyakati 25:1-28

Amazia Mfalme Wa Yuda

(2 Wafalme 14:2-20)

125:1 2Fal 14:1Amazia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka ishirini na tisa. Mama yake aliitwa Yehoadani kutoka Yerusalemu. 225:2 1Fal 8:61; Isa 29:13; 2Fal 14:4; Isa 29:13; Hos 10:2Akatenda yaliyo mema machoni pa Bwana, lakini sio kwa moyo wake wote. 325:3 2Fal 14:5Baada ya ufalme kuimarika mikononi mwake, aliwaua maafisa waliomuua mfalme baba yake. 425:4 Kum 28:61; Hes 26:11; Kum 24:16; Eze 18:20; 2Fal 14:6; Yer 31:30Hata hivyo hakuwaua watoto wao, lakini akafanya sawasawa na ilivyoandikwa katika Sheria, katika Kitabu cha Mose, ambako Bwana aliamuru: “Baba hawatauawa kwa ajili ya watoto wao, wala watoto hawatauawa kwa ajili ya baba zao. Kila mmoja atakufa kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe.”

525:5 2Sam 24:2; Kut 30:14; 1Nya 21:1Amazia akawaita watu wa Yuda pamoja, akawaweka chini ya majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia kufuatana na jamaa zao katika Yuda yote na Benyamini. Kisha akawahesabu wale wenye umri wa miaka ishirini au zaidi na akakuta kwamba walikuwa wanaume 300,000 watu walio tayari kwa utumishi wa jeshi, walio na uwezo wa kutumia mkuki na ngao. 6Akawaajiri pia watu 100,000 wapiganaji kutoka Israeli kwa talanta 100 za fedha.25:6 Talanta 100 za fedha ni sawa na tani 3.75.

725:7 2Nya 16:2-9; 19:1-3; Hos 4:6-19; 1Fal 12:28; Isa 28:1-3; Hos 5:6-15; 9:11-17Lakini mtu wa Mungu akamjia na kumwambia, “Ee mfalme, haya majeshi kutoka Israeli kamwe usiyaruhusu yaende pamoja na wewe kwa kuwa Bwana hayuko pamoja na Israeli, wala hayupo pamoja na yeyote wa watu wa Efraimu. 825:8 2Nya 14:11; 20:6; Mwa 18:14; Amu 7:7; 1Sam 14:6; 1Nya 29:11; Ay 5:18; Za 20:7; 118:6; Yer 32:17; Mt 19:26; Rum 8:31Hata kama ukienda na kupigana kwa ujasiri katika vita, Mungu atakufanya ukimbie mbele ya adui, kwa kuwa Mungu anao uwezo wa kusaidia au wa kuangusha.”

925:9 Kum 8:18; Mit 10:22; Hag 2:8; 2Nya 1:12Amazia akamuuliza yule mtu wa Mungu, “Lakini itakuwaje kwa zile talanta 100 za fedha nilizolipa kwa ajili ya haya majeshi ya Israeli?”

Yule mtu wa Mungu akajibu, “Bwana aweza kukupa zaidi sana ya hizo.”

10Hivyo Amazia akayaondoa yale majeshi yaliyokuwa yamekuja kutoka Efraimu na kuyarudisha nyumbani. Waliwakasirikia sana Yuda, nao wakarudi nyumbani wakiwa na hasira kali.

1125:11 2Fal 14:7Ndipo Amazia akajitia nguvu na kuliongoza jeshi lake kwenye Bonde la Chumvi, ambako aliua watu 10,000 wa Seiri. 1225:12 Za 141:6; Oba 1:3Jeshi la Yuda pia likawateka watu 10,000 wakiwa hai, likawapandisha juu ya jabali na kuwatupa chini kwa nguvu hata wote wakavunjika vipande vipande.

13Wakati huo yale majeshi Amazia aliyoyarudisha na ambayo hakuyaruhusu kushiriki katika vita, yalivamia miji ya Yuda kuanzia Samaria hata Beth-Horoni. Yakawaua watu 3,000 na kuchukua kiasi kikubwa sana cha mateka.

1425:14 Kut 20:3; Isa 36:20; 2Nya 28:23Amazia aliporudi kutoka kuwachinja Waedomu, alileta pia kutoka huko miungu ya watu wa Seiri. Akaisimamisha kama miungu yake mwenyewe, akaisujudia na kuitolea kafara za kuteketezwa. 1525:15 Yer 10:3-5; Mdo 19:26; Za 96:5; 115:3-8; Isa 46:1-2; 1Kor 8:4Hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya Amazia, naye akamtuma nabii kwake, ambaye alisema: “Kwa nini unauliza kwa miungu ya hawa watu, ambayo haikuweza kuwaokoa watu wake wenyewe kutoka mkononi mwako?”

1625:16 2Nya 16:10; Mit 9:7-8; 1Sam 2:25Wakati nabii alipokuwa angali anazungumza, mfalme akamwambia, “Je, wewe tumekuchagua kuwa mshauri wa mfalme? Nyamaza, ya nini uuawe?”

Hivyo nabii akanyamaza lakini akasema, “Najua kuwa Mungu ameazimia kukuangamiza kwa sababu umefanya jambo hili na hukusikiliza shauri langu.”

1725:17 2Fal 14:8-9Baada ya Amazia mfalme wa Yuda kushauriana na washauri wake akatuma ujumbe kwa Yehoashi, mwana wa Yehoahazi mwana wa Yehu, mfalme wa Israeli kusema: “Njoo tukabiliane uso kwa uso.”

1825:18 Amu 9:8-15Lakini Yehoashi mfalme wa Israeli akamjibu Amazia mfalme wa Yuda, “Mbaruti uliokuwa Lebanoni ulituma ujumbe kwa mwerezi uliokuwa Lebanoni, ‘Mtoe binti yako aolewe na mwanangu.’ Kisha mnyama wa mwituni aliyekuwa Lebanoni akaja na kuukanyaga ule mbaruti. 1925:19 2Nya 35:21; Mit 18:9; 12:15Wewe unasema moyoni mwako kwamba umemshinda Edomu, nawe sasa unajigamba na kujivuna. Lakini kaa nyumbani kwako! Kwa nini utafute matatizo na kujiletea anguko lako mwenyewe na la Yuda pia?”

2025:20 1Fal 12:15; 2Nya 22:7Hata hivyo, Amazia hakutaka kusikia, kwa kuwa Mungu alifanya hivyo ili awatie mikononi mwa Yehoashi, kwa sababu waliitafuta miungu ya Edomu. 21Hivyo Yehoashi mfalme wa Israeli akakwea kuwashambulia. Yeye na Amazia mfalme wa Yuda wakakabiliana uso kwa uso huko Beth-Shemeshi katika Yuda. 22Yuda ikashindwa na Israeli na kila mtu akakimbilia nyumbani kwake. 2325:23 2Fal 14:13; Neh 8:16; 2Nya 26:9; Yer 31:38; 2Nya 21:17; 22:1, 6Yehoashi mfalme wa Israeli akamteka Amazia mfalme wa Yuda, mwana wa Yoashi, mwana wa Ahazia, huko Beth-Shemeshi. Kisha Yehoashi akamleta Yerusalemu na kuubomoa ukuta wa Yerusalemu kuanzia lango la Efraimu hadi Lango la Pembeni, sehemu yenye urefu wa kama dhiraa 400.25:23 Dhiraa 400 ni sawa na mita 180. 2425:24 1Nya 26:15Akachukua dhahabu yote, fedha na vyombo vyote vilivyopatikana katika Hekalu la Mungu, ambavyo vilikuwa chini ya uangalizi wa Obed-Edomu, pamoja na hazina za jumba la mfalme na mateka, kisha akarudi Samaria.

2525:25 2Fal 14:17Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda aliishi miaka kumi na mitano baada ya kifo cha Yehoashi mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli. 26Kwa habari ya matukio mengine katika utawala wa Amazia, kuanzia mwanzo hadi mwisho, je, hayakuandikwa katika kitabu cha wafalme wa Yuda na wa Israeli? 2725:27 Yos 10:3Kuanzia wakati ule Amazia alipogeuka na kuacha kumfuata Bwana walifanya shauri baya dhidi yake huko Yerusalemu naye akakimbilia Lakishi, lakini wakawatuma watu wamfuatilie huko Lakishi nao wakamuulia huko. 2825:28 2Fal 14:20Akarudishwa kwa farasi na akazikwa pamoja na baba zake katika Mji wa Yuda.

Swedish Contemporary Bible

2 Krönikeboken 25:1-28

Amasja regerar i Juda

(2 Kung 14:1-6)

1Amasja var tjugofem år gammal när han blev kung, och han regerade i tjugonio år i Jerusalem. Hans mor hette Joaddan och var från Jerusalem. 2Han gjorde det som var rätt i Herrens ögon, dock inte helhjärtat.

3När hans kungamakt var säkrad, avrättade han de män som mördat hans far kungen. 4Men han dödade inte deras barn, utan handlade i enlighet med Herrens befallning i Moses lagbok: ”Föräldrarna får inte dödas för sina barns synder, och barn ska inte dödas för synder som deras föräldrar har begått. Var och en ska dö för sitt eget brott.”

5Amasja samlade judéerna och ställde upp dem familjevis under befäl av högre och lägre officerare från hela Judas och Benjamins stammar. Han mönstrade dem som var tjugo år eller äldre och fann att det var 300 000 utvalda vapenföra män som kunde hantera spjut och sköld. 6Dessutom lejde han 100 000 tappra soldater från Israel för tre och ett halvt ton25:6 Ordagrant: 100 talenter. silver.

7Men då kom en gudsman till honom och sa: ”O kung, låt inte den israelitiska hären dra ut tillsammans med dig, för Herren är inte med Israel, inte med några från Efraim. 8Gå du frimodigt ut i strid, men Gud ska överlämna dig åt fienden, för Gud har makt att både hjälpa och stjälpa.”

9”Men vad händer med de tre och ett halvt ton silver jag betalade för den israelitiska styrkan?” frågade Amasja gudsmannen. Gudsmannen svarade: ”Herren har makt att ge dig mycket mer än så!”

10Amasja skickade alltså hem den trupp som kommit till honom från Efraim. De blev ursinniga på Juda och gav sig iväg kokande av vrede. 11Men Amasja tog mod till sig och ledde sin armé till Saltdalen och dödade där 10 000 man från Seir. 12Ytterligare 10 000 togs till fånga levande av judéerna. De förde dem upp på toppen av en klippa och störtade ner dem, så att de alla krossades.

13Men männen i den styrka som Amasja hade skickat hem och som inte fått följa med honom till kriget, anföll Judas städer från Samaria till Bet Horon. De dödade 3 000 där och tog med sig ett stort byte.

14När Amasja vände tillbaka efter att ha slagit edoméerna, förde han med sig de gudar som folket hade i Seir. Han satte upp dem som sina egna gudar, bad till dem och tände rökelse till dem. 15Då blev Herren vred på Amasja, och han sände en profet till honom som frågade: ”Varför rådfrågar du gudar som inte ens kunde rädda sitt eget folk undan dig?”

16Men medan han fortfarande talade, frågade Amasja honom: ”När gjorde vi dig till kungens rådgivare? Sluta genast, annars blir du dödad!” Profeten slutade men sa: ”Jag vet att Gud har bestämt sig för att förgöra dig, därför att du har gjort så här och inte lyssnat till mitt råd.”

Amasjas krig med Israel

(2 Kung 14:8-14)

17Kung Amasja i Juda höll rådslag och sände bud till Israels kung Joash, Joachas son och Jehus sonson, och utmanade honom: ”Kom, låt oss mötas öga mot öga!”

18Israels kung Joash skickade detta svar till Juda kung Amasja: ”En törnbuske på Libanon sände bud till en ceder på Libanon: ’Ge din dotter till hustru åt min son.’ Men ett vilddjur på Libanon kom och trampade ner busken. 19Du säger stolt att du har erövrat Edom, du är högmodig och vill vinna mer ära. Stanna hemma! Varför söka efter olycka och riskera att du går under och Juda med dig?” 20Men Amasja ville inte lyssna. Det kom nämligen från Gud, för att de skulle ges i fiendens hand, därför att de hade sökt Edoms gudar.

21Då attackerade Israels kung Joash, och han och Juda kung Amasja möttes öga mot öga vid Bet Shemesh i Juda. 22Juda blev besegrat av Israel, och var och en flydde hem till sig. 23Israels kung Joash tog till fånga Juda kung Amasja, son till Joash, son till Joachas, vid Bet Shemesh och förde honom till Jerusalem. Där rev han ner tvåhundra meter av stadsmuren, från Efraimsporten till Hörnporten. 24Han tog allt guld och silver och alla föremål som fanns i Guds hus hos Oved-Edom, liksom alla skatter från kungapalatset. Han tog också gisslan och återvände sedan till Samaria. 25Men Juda kung Amasja, Joashs son, överlevde kung Joash av Israel, Joachas son, med femton år.

26Amasjas historia i övrigt är nedtecknad i boken om Judas och Israels kungar. 27Från den tid då Amasja vände sig bort från Herren, anstiftades en sammansvärjning mot honom i Jerusalem, och han flydde till Lakish, men de skickade dit män efter honom och dödade honom. 28De hämtade honom sedan med häst tillbaka till Jerusalem och begravde honom bland sina fäder i Judas25:28 Enligt en del handskrifter och tidiga översättningar, bl.a. Septuaginta och Vulgata: Davids. stad.