2 Nyakati 25 – NEN & BDS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Nyakati 25:1-28

Amazia Mfalme Wa Yuda

(2 Wafalme 14:2-20)

125:1 2Fal 14:1Amazia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka ishirini na tisa. Mama yake aliitwa Yehoadani kutoka Yerusalemu. 225:2 1Fal 8:61; Isa 29:13; 2Fal 14:4; Isa 29:13; Hos 10:2Akatenda yaliyo mema machoni pa Bwana, lakini sio kwa moyo wake wote. 325:3 2Fal 14:5Baada ya ufalme kuimarika mikononi mwake, aliwaua maafisa waliomuua mfalme baba yake. 425:4 Kum 28:61; Hes 26:11; Kum 24:16; Eze 18:20; 2Fal 14:6; Yer 31:30Hata hivyo hakuwaua watoto wao, lakini akafanya sawasawa na ilivyoandikwa katika Sheria, katika Kitabu cha Mose, ambako Bwana aliamuru: “Baba hawatauawa kwa ajili ya watoto wao, wala watoto hawatauawa kwa ajili ya baba zao. Kila mmoja atakufa kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe.”

525:5 2Sam 24:2; Kut 30:14; 1Nya 21:1Amazia akawaita watu wa Yuda pamoja, akawaweka chini ya majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia kufuatana na jamaa zao katika Yuda yote na Benyamini. Kisha akawahesabu wale wenye umri wa miaka ishirini au zaidi na akakuta kwamba walikuwa wanaume 300,000 watu walio tayari kwa utumishi wa jeshi, walio na uwezo wa kutumia mkuki na ngao. 6Akawaajiri pia watu 100,000 wapiganaji kutoka Israeli kwa talanta 100 za fedha.25:6 Talanta 100 za fedha ni sawa na tani 3.75.

725:7 2Nya 16:2-9; 19:1-3; Hos 4:6-19; 1Fal 12:28; Isa 28:1-3; Hos 5:6-15; 9:11-17Lakini mtu wa Mungu akamjia na kumwambia, “Ee mfalme, haya majeshi kutoka Israeli kamwe usiyaruhusu yaende pamoja na wewe kwa kuwa Bwana hayuko pamoja na Israeli, wala hayupo pamoja na yeyote wa watu wa Efraimu. 825:8 2Nya 14:11; 20:6; Mwa 18:14; Amu 7:7; 1Sam 14:6; 1Nya 29:11; Ay 5:18; Za 20:7; 118:6; Yer 32:17; Mt 19:26; Rum 8:31Hata kama ukienda na kupigana kwa ujasiri katika vita, Mungu atakufanya ukimbie mbele ya adui, kwa kuwa Mungu anao uwezo wa kusaidia au wa kuangusha.”

925:9 Kum 8:18; Mit 10:22; Hag 2:8; 2Nya 1:12Amazia akamuuliza yule mtu wa Mungu, “Lakini itakuwaje kwa zile talanta 100 za fedha nilizolipa kwa ajili ya haya majeshi ya Israeli?”

Yule mtu wa Mungu akajibu, “Bwana aweza kukupa zaidi sana ya hizo.”

10Hivyo Amazia akayaondoa yale majeshi yaliyokuwa yamekuja kutoka Efraimu na kuyarudisha nyumbani. Waliwakasirikia sana Yuda, nao wakarudi nyumbani wakiwa na hasira kali.

1125:11 2Fal 14:7Ndipo Amazia akajitia nguvu na kuliongoza jeshi lake kwenye Bonde la Chumvi, ambako aliua watu 10,000 wa Seiri. 1225:12 Za 141:6; Oba 1:3Jeshi la Yuda pia likawateka watu 10,000 wakiwa hai, likawapandisha juu ya jabali na kuwatupa chini kwa nguvu hata wote wakavunjika vipande vipande.

13Wakati huo yale majeshi Amazia aliyoyarudisha na ambayo hakuyaruhusu kushiriki katika vita, yalivamia miji ya Yuda kuanzia Samaria hata Beth-Horoni. Yakawaua watu 3,000 na kuchukua kiasi kikubwa sana cha mateka.

1425:14 Kut 20:3; Isa 36:20; 2Nya 28:23Amazia aliporudi kutoka kuwachinja Waedomu, alileta pia kutoka huko miungu ya watu wa Seiri. Akaisimamisha kama miungu yake mwenyewe, akaisujudia na kuitolea kafara za kuteketezwa. 1525:15 Yer 10:3-5; Mdo 19:26; Za 96:5; 115:3-8; Isa 46:1-2; 1Kor 8:4Hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya Amazia, naye akamtuma nabii kwake, ambaye alisema: “Kwa nini unauliza kwa miungu ya hawa watu, ambayo haikuweza kuwaokoa watu wake wenyewe kutoka mkononi mwako?”

1625:16 2Nya 16:10; Mit 9:7-8; 1Sam 2:25Wakati nabii alipokuwa angali anazungumza, mfalme akamwambia, “Je, wewe tumekuchagua kuwa mshauri wa mfalme? Nyamaza, ya nini uuawe?”

Hivyo nabii akanyamaza lakini akasema, “Najua kuwa Mungu ameazimia kukuangamiza kwa sababu umefanya jambo hili na hukusikiliza shauri langu.”

1725:17 2Fal 14:8-9Baada ya Amazia mfalme wa Yuda kushauriana na washauri wake akatuma ujumbe kwa Yehoashi, mwana wa Yehoahazi mwana wa Yehu, mfalme wa Israeli kusema: “Njoo tukabiliane uso kwa uso.”

1825:18 Amu 9:8-15Lakini Yehoashi mfalme wa Israeli akamjibu Amazia mfalme wa Yuda, “Mbaruti uliokuwa Lebanoni ulituma ujumbe kwa mwerezi uliokuwa Lebanoni, ‘Mtoe binti yako aolewe na mwanangu.’ Kisha mnyama wa mwituni aliyekuwa Lebanoni akaja na kuukanyaga ule mbaruti. 1925:19 2Nya 35:21; Mit 18:9; 12:15Wewe unasema moyoni mwako kwamba umemshinda Edomu, nawe sasa unajigamba na kujivuna. Lakini kaa nyumbani kwako! Kwa nini utafute matatizo na kujiletea anguko lako mwenyewe na la Yuda pia?”

2025:20 1Fal 12:15; 2Nya 22:7Hata hivyo, Amazia hakutaka kusikia, kwa kuwa Mungu alifanya hivyo ili awatie mikononi mwa Yehoashi, kwa sababu waliitafuta miungu ya Edomu. 21Hivyo Yehoashi mfalme wa Israeli akakwea kuwashambulia. Yeye na Amazia mfalme wa Yuda wakakabiliana uso kwa uso huko Beth-Shemeshi katika Yuda. 22Yuda ikashindwa na Israeli na kila mtu akakimbilia nyumbani kwake. 2325:23 2Fal 14:13; Neh 8:16; 2Nya 26:9; Yer 31:38; 2Nya 21:17; 22:1, 6Yehoashi mfalme wa Israeli akamteka Amazia mfalme wa Yuda, mwana wa Yoashi, mwana wa Ahazia, huko Beth-Shemeshi. Kisha Yehoashi akamleta Yerusalemu na kuubomoa ukuta wa Yerusalemu kuanzia lango la Efraimu hadi Lango la Pembeni, sehemu yenye urefu wa kama dhiraa 400.25:23 Dhiraa 400 ni sawa na mita 180. 2425:24 1Nya 26:15Akachukua dhahabu yote, fedha na vyombo vyote vilivyopatikana katika Hekalu la Mungu, ambavyo vilikuwa chini ya uangalizi wa Obed-Edomu, pamoja na hazina za jumba la mfalme na mateka, kisha akarudi Samaria.

2525:25 2Fal 14:17Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda aliishi miaka kumi na mitano baada ya kifo cha Yehoashi mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli. 26Kwa habari ya matukio mengine katika utawala wa Amazia, kuanzia mwanzo hadi mwisho, je, hayakuandikwa katika kitabu cha wafalme wa Yuda na wa Israeli? 2725:27 Yos 10:3Kuanzia wakati ule Amazia alipogeuka na kuacha kumfuata Bwana walifanya shauri baya dhidi yake huko Yerusalemu naye akakimbilia Lakishi, lakini wakawatuma watu wamfuatilie huko Lakishi nao wakamuulia huko. 2825:28 2Fal 14:20Akarudishwa kwa farasi na akazikwa pamoja na baba zake katika Mji wa Yuda.

La Bible du Semeur

2 Chroniques 25:1-28

Les actes d’obéissance et la victoire militaire

(2 R 14.1-6)

1Amatsia avait vingt-cinq ans lorsqu’il devint roi et il régna vingt-neuf ans à Jérusalem25.1 De 796 à 767 av. J.-C.. Sa mère s’appelait Yehoaddân, elle était de Jérusalem. 2Il fit ce que l’Eternel considère comme juste, mais non pas d’un cœur sans partage25.2 Il a maintenu les hauts lieux (2 R 14.4) et adopté des dieux édomites (voir v. 14).. 3Dès qu’Amatsia eut affermi son autorité royale, il fit exécuter les ministres qui avaient assassiné son père. 4Mais il ne fit pas mourir leurs fils, conformément aux ordres donnés par l’Eternel dans la Loi, dans le livre de Moïse, lorsqu’il dit : « Les pères ne seront pas mis à mort pour les fils et les fils ne seront pas mis à mort pour les pères ; mais chacun sera mis à mort pour son propre péché25.4 Cité en Dt 24.16.. »

La guerre contre les Edomites

5Amatsia rassembla Juda et établit, pour chaque groupe familial, des chefs de « milliers » et de « centaines » pour tout Juda et Benjamin. Il recensa ceux qui avaient au moins vingt ans ; il trouva trois cent mille hommes aptes à la guerre, et sachant manier la lance et le grand bouclier. 6Il enrôla encore pour trois tonnes et demie d’argent, cent mille mercenaires dans le royaume d’Israël du Nord. 7Un homme de Dieu vint lui dire : O roi, qu’une armée d’Israël n’aille pas combattre avec toi, car l’Eternel n’est pas avec le royaume du Nord, avec tous ces Ephraïmites. 8Si tu vas au combat avec eux, tu auras beau te battre vaillamment, Dieu te fera succomber devant l’ennemi, car Dieu a le pouvoir de secourir ou de faire succomber.

9Amatsia demanda à l’homme de Dieu : Mais qu’adviendra-t-il de ces trois tonnes et demie d’argent que j’ai donné aux troupes d’Israël ?

L’homme de Dieu répondit : L’Eternel peut te donner bien plus que cela.

10Alors Amatsia renvoya chez eux les soldats qui étaient venus d’Ephraïm. Mais ceux-ci furent très en colère contre Juda et ils rentrèrent chez eux furieux.

(2 R 14.7)

11Amatsia rassembla son courage, prit la tête de son armée et se dirigea vers la vallée du Sel où il battit dix mille habitants de Séir25.11 Des Edomites (2 R 14.7) du désert situé au sud de la mer Morte.. 12Les Judéens capturèrent vivants dix mille hommes qu’ils emmenèrent au sommet d’une falaise25.12 falaise: (en hébreu : séla) peut-être de la ville de Séla, capitale des Edomites (2 R 14.7). d’où ils les précipitèrent tous dans le vide, de sorte qu’ils se rompirent les os.

L’idolâtrie et le refus d’écouter un prophète

13Mais, pendant ce temps, les soldats de la troupe qu’Amatsia avait renvoyés, pour qu’ils ne participent pas à son expédition, envahirent les villes de Juda depuis Samarie jusqu’à Beth-Horôn. Ils massacrèrent trois mille habitants et emportèrent un butin considérable.

14Lorsque Amatsia fut de retour après sa victoire sur les Edomites, il rapporta les statues de leurs dieux et en fit ses propres dieux ; il se prosterna devant elles et leur offrit des parfums. 15Alors l’Eternel se mit en colère contre lui et il lui envoya un prophète qui lui demanda : Pourquoi t’es-tu tourné vers les dieux de ce peuple qui n’ont même pas été capables de délivrer leur propre peuple de ton pouvoir ?

16Mais le roi l’interrompit en lui répliquant : Est-ce qu’on t’a nommé conseiller du roi ? Tais-toi ! Inutile de te faire tuer !

Le prophète n’insista pas, mais avant de se retirer, il dit cependant : Parce que tu as agi comme tu l’as fait et que tu as refusé d’écouter mes conseils, je reconnais que Dieu a décidé dans son conseil de te détruire.

La défaite devant Israël

(2 R 14.8-20)

17Amatsia, roi de Juda, prit l’avis de ses conseillers, puis il envoya des messagers à Joas, fils de Yoahaz et petit-fils de Jéhu, roi d’Israël, pour lui faire dire : Allons nous affronter !

18Joas lui fit répondre : Un jour, le chardon du Liban envoya dire au cèdre du Liban : « Donne ta fille en mariage à mon fils ! » Mais les bêtes sauvages du Liban passèrent par là et piétinèrent le chardon. 19Tu te dis que tu as vaincu les Edomites, alors l’orgueil t’est monté à la tête et tu te glorifies ! Maintenant, tu ferais mieux de rester chez toi : pourquoi veux-tu t’engager dans une entreprise malheureuse et courir au-devant d’un désastre pour toi et pour le royaume de Juda ?

20Mais Amatsia n’écouta pas son avertissement, car Dieu faisait en sorte que lui et son peuple subissent la défaite parce qu’ils s’étaient tournés vers les dieux d’Edom. 21Alors Joas, roi d’Israël, se mit en campagne. Les deux rois s’affrontèrent à Beth-Shémesh au pays de Juda. 22L’armée de Juda fut battue par celle d’Israël, et les soldats de Juda s’enfuirent chacun chez soi. 23A Beth-Shémesh, Joas, roi d’Israël, fit prisonnier Amatsia, roi de Juda, fils de Joas et petit-fils de Yoahaz. Il l’emmena à Jérusalem et démolit le rempart de la ville sur une longueur de cent quatre-vingts mètres, depuis la porte d’Ephraïm jusqu’à la porte de l’Angle. 24Il prit tout l’or et l’argent et tous les objets précieux qui se trouvaient dans le temple de Dieu, sous la garde d’Obed-Edom25.24 Famille à laquelle avait été confiée la garde du sanctuaire et de l’argent de l’alliance (voir 1 Ch 13.13-14 ; 26.4-15)., ainsi que les trésors du palais royal. Il prit en plus des otages, puis retourna à Samarie.

L’assassinat d’Amatsia

25Amatsia, fils de Joas, roi de Juda, vécut encore quinze années après la mort de Joas, fils de Yoahaz, roi d’Israël. 26Les autres faits et gestes d’Amatsia, des premiers aux derniers, sont cités dans le livre des rois de Juda et d’Israël. 27A partir du moment où Amatsia se détourna de l’Eternel, on trama contre lui un complot à Jérusalem. Il s’enfuit à Lakish. Mais ses ennemis envoyèrent des gens jusque-là pour le faire assassiner. 28On ramena son corps à dos de cheval à Jérusalem et on l’enterra aux côtés de ses ancêtres dans la cité de Juda.