2 Nyakati 22 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Nyakati 22:1-12

Ahazia Mfalme Wa Yuda

(2 Wafalme 8:25-29; 9:21-28)

122:1 2Nya 33:25; 23:20-21; 21:16-17; 26:1; 1Fal 8:24Watu wa Yerusalemu wakamfanya Ahazia, mdogo wa wote wa wana wa Yerohamu, kuwa mfalme mahali pa baba yake, kwa sababu washambuliaji wa ghafula waliokuwa wameingia kambini pamoja na Waarabu, walikuwa wamewaua wana wakubwa wote wa Yehoramu. Kwa hiyo Ahazia mwana wa Yehoramu mfalme wa Yuda akaanza kutawala.

222:2 1Fal 16:28; 2Fal 8:26; 2Nya 21:6Ahazia alikuwa na umri wa miaka ishirini na miwili alipoanza kutawala, naye akatawala katika Yerusalemu kwa mwaka mmoja. Mama yake aliitwa Athalia, mjukuu wa Omri.

322:3 2Nya 18:1; 21:6Ahazia naye akaenenda katika njia za nyumba ya Ahabu, kwa sababu mama yake alimshawishi katika kutenda maovu. 422:4 2Nya 24:17; Mit 1:10; 19:27Akafanya yaliyo maovu machoni pa Bwana kama walivyokuwa wamefanya nyumba ya Ahabu, kwa kuwa baada ya kufa kwa baba yake nyumba ya Ahabu ndio waliokuwa washauri wake, kwa uangamivu wake. 522:5 2Nya 18:11, 34; 2Fal 8:28Pia akafuata shauri lao alipokwenda pamoja na Yoramu mwana wa Ahabu mfalme wa Israeli kupigana na Hazaeli mfalme wa Aramu huko Ramoth-Gileadi. Waaramu wakamjeruhi Yoramu. 622:6 1Fal 19:15; 2Fal 9:15Hivyo akarudi Yezreeli ili apate kuuguza majeraha aliyojeruhiwa huko Ramothi22:6 Yaani Rama kwa Kiebrania. alipopigana na Hazaeli mfalme wa Aramu.

Ndipo Ahazia mwana wa Yehoramu, mfalme wa Yuda, akashuka kwenda Yezreeli kumtazama Yoramu mwana wa Ahabu, kwa sababu alikuwa amejeruhiwa.

722:7 Amu 14:4; 2Nya 10:15; Amo 3:6; Mdo 2:23; 2Fal 9:16; 1Fal 12:15; Za 5:10; 9:16; 1Fal 19:16Mungu alikuwa ameamuru kwamba kuanguka kwa Ahazia kungetokea atakapokwenda kumwona Yoramu. Ahazia alipowasili, wakatoka pamoja na Yoramu ili kwenda kukutana na Yehu mwana wa Nimshi, ambaye Bwana alikuwa amemtia mafuta kuangamiza nyumba ya Ahabu. 822:8 2Fal 10:13Yehu alipokuwa anatekeleza hukumu juu ya nyumba ya Ahabu, akawakuta wakuu wa Yuda na wana wa jamaa ya Ahazia waliokuwa wanamhudumia Ahazia, naye akawaua. 922:9 Amu 9:5; 2Nya 17:4; 2Fal 9:27Ndipo akaenda kumsaka Ahazia, nao watu wake wakamkamata alipokuwa amejificha huko Samaria. Akaletwa kwa Yehu, naye Yehu akamuua. Wakamzika kwani walisema, “Alikuwa mwana wa Yehoshafati, ambaye alimtafuta Bwana kwa moyo wake wote.” Hivyo hapakuwa na mtu mwenye uwezo katika nyumba ya Ahazia aliyeweza kushika ufalme.

Athalia Na Yoashi

(2 Wafalme 11:1-3)

10Wakati Athalia mamaye Ahazia alipoona kuwa mwanawe amekufa, akainuka na kuiangamiza jamaa yote ya mfalme ya nyumba ya Yuda. 1122:11 2Fal 11:2Lakini Yehosheba, binti wa Mfalme Yehoramu, akamtwaa Yoashi mwana wa Ahazia kwa siri kutoka miongoni mwa wana wa mfalme waliokuwa karibu kuuawa. Akamweka Yoashi pamoja na yaya wake ndani ya chumba cha kulala. Kwa kuwa Yehosheba, aliyekuwa binti wa Mfalme Yehoramu, na pia alikuwa mke wa kuhani Yehoyada, alikuwa dada yake Ahazia, akamficha huyo mtoto ili Athalia asimuue. 12Alibaki amefichwa pamoja nao katika Hekalu la Mungu kwa muda wa miaka sita wakati Athalia alikuwa akitawala nchi.

New International Reader’s Version

2 Chronicles 22:1-12

Ahaziah King of Judah

1The people of Jerusalem made Ahaziah king in place of Jehoram. Ahaziah was Jehoram’s youngest son. Robbers had come with the Arabs into Jehoram’s camp. The robbers had killed all his older sons. So Ahaziah, the king of Judah, began to rule. He was the son of Jehoram.

2Ahaziah was 22 years old when he became king. He ruled in Jerusalem for one year. His mother’s name was Athaliah. She was a granddaughter of Omri.

3Ahaziah also followed the ways of the royal family of Ahab. That’s because Ahaziah’s mother gave him bad advice. She told him to do what was wrong. 4So he did what was evil in the eyes of the Lord. He did what the family of Ahab had done. After Ahaziah’s father died, the members of Ahab’s family became his advisers. That’s what destroyed him. 5He also followed their advice when he joined forces with Joram, the king of Israel. They went to war against Hazael at Ramoth Gilead. Joram was the son of Ahab. Hazael was king of Aram. The soldiers of Aram wounded Joram. 6So he returned to Jezreel to give his wounds time to heal. His enemies had wounded him at Ramoth in his battle against Hazael, the king of Aram.

Ahaziah, the son of Jehoram, went down to Jezreel. He went there to see Joram. That’s because Joram had been wounded. Ahaziah was king of Judah. Joram was the son of Ahab.

7Through Ahaziah’s visit to Joram, God caused Ahaziah to fall from power. When Ahaziah arrived, he rode out with Joram to meet Jehu, the son of Nimshi. The Lord had anointed Jehu to destroy the royal family of Ahab. 8So Jehu punished Ahab’s family, just as the Lord had told him to. While he was doing it, he found the officials of Judah and the sons of Ahaziah’s relatives. They had been serving Ahaziah. So Jehu killed them. 9Then he went to look for Ahaziah. Jehu’s men captured him while he was hiding in Samaria. Ahaziah was brought to Jehu and put to death. People buried him, because they said, “He was a grandson of Jehoshaphat, who followed the Lord with all his heart.” So no one in the royal family of Ahaziah was powerful enough to keep the kingdom.

Athaliah and Joash

10Athaliah was Ahaziah’s mother. She saw that her son was dead. So she began to wipe out the whole royal family of Judah. 11But Jehosheba went and got Joash, the son of Ahaziah. Jehosheba was the daughter of King Jehoram. She stole Joash away from among the royal princes. All of them were about to be murdered. She put Joash and his nurse in a bedroom. Jehosheba, the daughter of King Jehoram, was the wife of Jehoiada the priest. She was also Ahaziah’s sister. So Jehosheba hid the child from Athaliah. That’s why Athaliah couldn’t kill him. 12The child remained hidden with the priest and his wife at God’s temple for six years. Athaliah ruled over the land during that time.