2 Nyakati 13 – NEN & PCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Nyakati 13:1-22

Abiya Mfalme Wa Yuda

(1 Wafalme 15:1-8)

1Katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Yeroboamu, Abiya akawa mfalme wa Yuda, 213:2 2Nya 11:20; 1Fal 15:6naye akatawala huko Yerusalemu miaka mitatu. Mama yake aliitwa Maaka, binti Urieli wa Gibea.

Basi kulikuwa na vita kati ya Abiya na Yeroboamu. 3Abiya aliingia vitani na jeshi la watu 400,000 wenye uwezo wa kupigana, naye Yeroboamu akapanga jeshi dhidi ya Abiya akiwa na jeshi la watu 800,000 wenye uwezo.

413:4 Yos 18:22; 1Nya 11:1Abiya akasimama juu ya Mlima Semaraimu, katika nchi ya vilima ya Efraimu, naye akasema, “Yeroboamu na Israeli yote, nisikilizeni mimi! 513:5 2Sam 7:13; 1Nya 17:12; Law 2:13; Hes 18:19; Amu 11:21-24; Eze 43:24; 1Sam 16:13; Za 89:20; Lk 1:31-33Hamfahamu kwamba Bwana, Mungu wa Israeli, alimpa Daudi na wazao wake ufalme juu ya Israeli milele kwa Agano la chumvi? 613:6 1Fal 11:26; 12:20; 2Nya 10:19Hata hivyo Yeroboamu mwana wa Nebati afisa wa Solomoni mwana wa Daudi, aliasi dhidi ya bwana wake. 713:7 Amu 9:4; Za 26:4; Mdo 17:5; Mit 12:11Baadhi ya watu wasiofaa kitu, wabaya kabisa walimkusanyikia na kumpinga Rehoboamu mwana wa Solomoni alipokuwa kijana mdogo asiyekuwa na uamuzi, asiye na nguvu za kuweza kupingana nao.

813:8 Za 68:25; 1Nya 25:10-24; 2Nya 29:2513:8 Kut 32:4; 1Fal 12:28; Hos 8:6“Hata sasa unapanga kupingana na ufalme wa Bwana ambao uko mikononi mwa wazao wa Daudi. Kweli ninyi ni jeshi kubwa nanyi mnazo ndama za dhahabu Yeroboamu alizozitengeneza kuwa miungu yenu. 913:9 2Nya 11:14-15; Kut 29:35-36; Gal 4:8; Yer 2:11Lakini je, hamkuwafukuza makuhani wa Bwana, wana wa Aroni na Walawi na kujifanyia makuhani wenu wenyewe kama yafanyavyo mataifa ya nchi nyingine? Yeyote anayekuja kujiweka wakfu akiwa na ndama dume na kondoo dume saba aweza kuwa kuhani wa kile ambacho ni miungu kwenu.

10“Lakini kwetu sisi, Bwana ndiye Mungu wetu, wala hatujamwacha. Makuhani wanaomtumikia Bwana ni wana wa Aroni, nao Walawi wakiwasaidia. 1113:11 Kut 29:39; 2Nya 2:4; Law 24:2-6; 1Nya 9:24; Kut 27:20-21Kila asubuhi na jioni wao hutoa sadaka za kuteketezwa na kufukiza uvumba wa harufu nzuri kwa Bwana. Wao huweka mikate juu ya meza safi kwa taratibu za kiibada na kuwasha taa kwenye kinara cha dhahabu kila jioni. Sisi tunazishika kanuni za Bwana Mungu wetu. Lakini ninyi mmemwacha Mungu. 1213:12 Hes 10:8-9; Amu 2:15; Mdo 5:39; Kum 20:4; Yos 5:4; Za 20:7; Ay 15:25-26; Mdo 9:4-5Mungu yu pamoja nasi, yeye ndiye kiongozi wetu. Makuhani wake wakiwa na tarumbeta zao watapiga baragumu ya vita dhidi yenu. Watu wa Israeli, msipigane dhidi ya Bwana, Mungu wa baba zenu, kwa maana hamtashinda.”

1313:13 2Nya 20:22; Yos 8:9Basi Yeroboamu alikuwa ametuma jeshi kuzunguka nyuma ya Yuda ili kwamba akiwa mbele ya Yuda, jeshi liwavizie kwa nyuma. 1413:14 1Nya 5:20; 2Nya 18:31Basi Yuda wakageuka na kuona kwamba wanashambuliwa mbele na nyuma. Ndipo wakamlilia Bwana. Makuhani wakapiga tarumbeta zao, 1513:15 2Nya 14:12; Hes 32:4nao watu wa Yuda wakapaza sauti ya kilio cha vita. Katika kupiga kelele za vita, Mungu akawafukuza Yeroboamu na Israeli wote mbele ya Mfalme Abiya na Yuda. 1613:16 2Nya 16:8Waisraeli wakakimbia mbele ya Yuda, naye Mungu akawatia Israeli mikononi mwao. 17Abiya na watu wake wakawachinja kwa machinjo makuu, hata wakawepo majeruhi 500,000 miongoni mwa watu wenye uwezo wa Israeli. 1813:18 1Nya 5:20; Za 22:5; Amu 8:28; 2Fal 18:5; 2Nya 16:8-9; 20:20Watu wa Israeli walitiishwa katika tukio lile, nao watu wa Yuda wakawa washindi kwa sababu walimtegemea Bwana, Mungu wa baba zao.

1913:19 Yos 15:9; Yn 11:54Abiya akamfuatia Yeroboamu na kuteka miji ya Betheli, Yeshana na Efroni kutoka kwake, pamoja na vijiji vinavyoizunguka miji hiyo. 2013:20 1Sam 25:38; Eze 24:16; Mdo 12:23; 1Sam 26:10; 1Fal 14:20Yeroboamu hakupata nguvu tena wakati wa utawala wa Abiya. Naye Bwana akampiga Yeroboamu akafa.

21Lakini Abiya akapata nguvu. Alioa wanawake kumi na wanne na alikuwa na wana ishirini na wawili na binti kumi na sita.

2213:22 2Nya 9:29; 12:15Matukio mengine ya utawala wa Abiya, pamoja na mambo aliyofanya na aliyosema, yameandikwa katika kitabu cha maelezo cha nabii Ido.

Persian Contemporary Bible

دوم تواريخ 13:1‏-22

جنگ ابيا با يربعام

(اول پادشاهان 15‏:1‏-8)

1‏-2در هجدهمين سال سلطنت يربعام پادشاه اسرائيل، ابيا پادشاه يهودا شد و سه سال در اورشليم سلطنت كرد. مادرش معكه دختر13‏:1‏و2 «دختر» يا «نوه».‏ اوری‌ئيل جبعه‌ای بود.

بين ابيا و يربعام جنگ درگرفت. 3سپاه يهودا كه از ۴۰۰,۰۰۰ مرد جنگی و كارآزموده تشكيل شده بود به فرماندهی ابيای پادشاه به جنگ سپاه اسرائيل رفت كه تعداد آن دو برابر سپاه يهودا بود و افرادش همه سربازانی كارآزموده و قوی بودند و فرماندهی آنها را يربعام پادشاه به عهده داشت.

4وقتی دو لشكر در كوهستان افرايم به همديگر رسيدند، ابيای پادشاه از كوه صمارايم بالا رفته و با صدای بلند به يربعام پادشاه و لشكر اسرائيل گفت: 5«به من گوش دهيد! مگر نمی‌دانيد كه خداوند، خدای اسرائيل عهد ابدی با داوود بسته است كه پسران او هميشه بر اسرائيل سلطنت كنند؟ 6پادشاه شما يربعام، غلام سليمان پسر داوود بود و به ارباب خود خيانت كرد. 7عده‌ای از اراذل و اوباش دور او جمع شدند و بر ضد رحبعام، پسر سليمان شورش كردند. رحبعام چون جوان و كم‌تجربه بود، نتوانست در برابر آنها ايستادگی كند. 8حال خيال می‌كنيد می‌توانيد سلطنت خداوند را كه در دست فرزندان داوود است، سرنگون كنيد؟ قشون شما بزرگ است و گوساله‌های طلا را كه يربعام برای پرستش ساخته است نيز نزد شماست. 9شما كاهنان خداوند را كه از نسل هارون هستند و لاويان را از ميان خود رانده و مانند مردمان سرزمينهای ديگر، كاهنان بت‌پرست برای خويش تعيين كرده‌ايد. هر كسی را كه با يک گوساله و هفت قوچ برای كاهن شدن نزد شما بيايد، او را به عنوان كاهن بتهايتان قبول می‌كنيد.

10«ولی خداوند، خدای ماست و ما او را ترک نكرده‌ايم. كاهنان ما كه خداوند را خدمت می‌كنند از نسل هارون هستند و لاويان نيز آنها را در انجام وظيفه‌ای كه دارند ياری می‌كنند. 11آنها هر روز صبح و عصر قربانیهای سوختنی و بخور معطر به خداوند تقديم می‌كنند و نان مقدس را روی ميز مخصوص می‌گذارند. هر شب چراغدان طلا را روشن می‌كنند. ما دستورات خداوند، خدای خود را اطاعت می‌كنيم، ولی شما، او را ترک نموده‌ايد. 12خدا با ماست و او رهبر ماست. كاهنان خدا با نواختن شيپور، ما را برای جنگ با شما رهبری خواهند كرد. ای مردم اسرائيل بر ضد خداوند، خدای اجدادتان نجنگيد، زيرا پيروز نخواهيد شد.»

13در اين ضمن، يربعام قسمتی از نيروهای خود را فرستاد تا از پشت سر به نيروهای يهودا حمله كنند و خود با بقيهٔ قشون از روبرو به آنها حمله كرد. 14قشون يهودا وقتی ديدند دشمن از پس و پيش آنها را محاصره كرده است، به سوی خداوند دعا كردند و كاهنان شيپورها را نواختند. 15‏-16مردان يهودا شروع كردند به فرياد زدن. وقتی آنها فرياد می‌زدند، خدا ابيای پادشاه و مردان يهودا را ياری كرد تا يربعام و قشون اسرائيل را تار و مار كرده، شكست دهند. 17آنها در آن روز ۵۰۰,۰۰۰ سرباز اسرائيلی را كشتند. 18به اين ترتيب، يهودا با اتكاء و اعتماد بر خداوند، خدای اجداد خود، اسرائيل را شكست داد.

19ابيا به تعقيب يربعام پرداخت و از شهرهای او بيت‌ئيل، يشانه، افرون و روستاهای اطراف آنها را گرفت. 20يربعام، پادشاه اسرائيل در تمام عمر ابيا ديگر هرگز به قدرت نرسيد و سرانجام خداوند او را كشت.

21اما ابيا قویتر می‌شد. او چهارده زن و بيست و دو پسر و شانزده دختر داشت. 22شرح بقيه رويدادهای دوران سلطنت ابيا و كردار و گفتار او در كتاب «تاريخ عدوی نبی» نوشته شده است.