1 Wakorintho 8 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Wakorintho 8:1-13

Chakula Kilichotolewa Sadaka Kwa Sanamu

18:1 Mdo 15:20; Rum 15:14Sasa kuhusu chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu, tunajua kwamba “sisi sote tuna ujuzi.” Lakini ujuzi hujivuna, bali upendo hujenga. 28:2 1Kor 3:8-12; 1Tim 6:4Mtu yeyote anayedhani kwamba anajua kitu, bado hajui kama impasavyo kujua. 38:3 Yer 1:5; Rum 8:29; Gal 4:9Lakini mtu ampendaye Mungu, hujulikana naye Mungu.

48:4 Kut 34:15; Mdo 14:15; 1Kor 10:19; Gal 4:8; Kum 6:4; Za 86:10; Efe 4:6; 1Tim 2:5Hivyo basi, kuhusu kula chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu: Tunajua kwamba “Sanamu si kitu chochote kabisa duniani,” na kwamba “Kuna Mungu mmoja tu.” 58:5 2The 2:4; Za 82:6; Yn 10:34Kwa kuwa hata kama wapo hao wanaoitwa miungu, kama wakiwa mbinguni au duniani (kama ilivyo kweli wapo “miungu” wengi na “mabwana” wengi), 68:6 Mal 2:10; Rum 11:36; Efe 4:5; Yn 1:3kwetu sisi yuko Mungu mmoja, aliye Baba, ambaye vitu vyote vyatoka kwake na kwa ajili yake sisi twaishi; na kuna Bwana mmoja tu, Yesu Kristo, ambaye kwa yeye vitu vyote vimekuwepo na kwa yeye tunaishi.

78:7 Rum 14:14; 1Kor 10:28Lakini si wote wanaojua jambo hili. Baadhi ya watu bado wamezoea sanamu kuwa halisi hivi kwamba wanapokula chakula kama hicho wanadhani kimetolewa sadaka kwa sanamu na kwa kuwa dhamiri zao ni dhaifu, dhamiri yao inanajisika. 88:8 Rum 14:17Lakini chakula hakituleti karibu na Mungu, wala hatupotezi chochote tusipokula, wala hatuongezi chochote kama tukila.

98:9 2Kor 6:3; Gal 5:13; Rum 14:1Lakini angalieni jinsi mnavyotumia uhuru wenu usije ukawa kikwazo kwao walio dhaifu. 108:10 1Kor 8:1, 4, 7; 10:28, 32Kwa maana kama mtu yeyote mwenye dhamiri dhaifu akiwaona ninyi wenye ujuzi huu mkila katika hekalu la sanamu, je, si atatiwa moyo kula chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu? 118:11 Rum 14:15-20Kwa njia hiyo, huyo ndugu mwenye dhamiri dhaifu, ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake, ataangamia kwa sababu ya ujuzi wenu. 128:12 Mt 18:6; 25:40-45Mnapotenda dhambi dhidi ya ndugu zenu kwa njia hii na kujeruhi dhamiri zao zilizo dhaifu, mnamkosea Kristo. 138:13 Mt 5:29; Rum 14:21; 2Kor 11:29Kwa hiyo, kama kile ninachokula kitamfanya ndugu yangu aanguke katika dhambi, sitakula nyama kamwe, nisije nikamfanya ndugu yangu aanguke.

New International Version

1 Corinthians 8:1-13

Concerning Food Sacrificed to Idols

1Now about food sacrificed to idols: We know that “We all possess knowledge.” But knowledge puffs up while love builds up. 2Those who think they know something do not yet know as they ought to know. 3But whoever loves God is known by God.8:2,3 An early manuscript and another ancient witness think they have knowledge do not yet know as they ought to know. 3 But whoever loves truly knows.

4So then, about eating food sacrificed to idols: We know that “An idol is nothing at all in the world” and that “There is no God but one.” 5For even if there are so-called gods, whether in heaven or on earth (as indeed there are many “gods” and many “lords”), 6yet for us there is but one God, the Father, from whom all things came and for whom we live; and there is but one Lord, Jesus Christ, through whom all things came and through whom we live.

7But not everyone possesses this knowledge. Some people are still so accustomed to idols that when they eat sacrificial food they think of it as having been sacrificed to a god, and since their conscience is weak, it is defiled. 8But food does not bring us near to God; we are no worse if we do not eat, and no better if we do.

9Be careful, however, that the exercise of your rights does not become a stumbling block to the weak. 10For if someone with a weak conscience sees you, with all your knowledge, eating in an idol’s temple, won’t that person be emboldened to eat what is sacrificed to idols? 11So this weak brother or sister, for whom Christ died, is destroyed by your knowledge. 12When you sin against them in this way and wound their weak conscience, you sin against Christ. 13Therefore, if what I eat causes my brother or sister to fall into sin, I will never eat meat again, so that I will not cause them to fall.