1 Wakorintho 4 – NEN & SZ-PL

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Wakorintho 4:1-21

Mawakili Wa Siri Za Mungu

14:1 1Kor 3:5; 9:17; Tit 1:7; Rum 16:25Basi, watu na watuhesabu sisi kuwa tu watumishi wa Kristo na mawakili wa siri za Mungu. 24:2 Lk 12:42Tena, litakiwalo ni mawakili waonekane kuwa waaminifu. 3Lakini kwangu mimi ni jambo dogo sana kwamba nihukumiwe na ninyi au na mahakama yoyote ya kibinadamu. Naam, hata mimi mwenyewe sijihukumu. 44:4 Mdo 23:1; Rum 2:13; 2Kor 10:18Dhamiri yangu ni safi, lakini hilo halinihesabii kuwa asiye na hatia. Bwana ndiye anihukumuye. 54:5 Mt 7:12; 1The 2:19; Ay 12:22; Za 90:8; 1Kor 3:13; Rum 2:29Kwa hiyo msihukumu jambo lolote kabla ya wakati wake. Ngojeni mpaka Bwana atakapokuja. Yeye atayaleta nuruni mambo yale yaliyofichwa gizani, na kuweka wazi nia za mioyo ya wanadamu. Wakati huo kila mmoja atapokea sifa anayostahili kutoka kwa Mungu.

64:6 1Kor 1:19-31; 3:19-20; 1:21Basi ndugu zangu, mambo haya nimeyafanya kwangu binafsi na Apolo kwa faida yenu, ili mweze kujifunza kutoka kwetu maana ya ule usemi usemao, “Msivuke zaidi ya yale yaliyoandikwa.” Hivyo hamtajivunia mtu fulani na kumdharau mwingine. 74:7 Yn 3:27; Rum 12:3-6Kwa maana ni nani aliyewafanya kuwa tofauti na wengine? Ni nini mlicho nacho ambacho hamkupokea? Nanyi kama mlipokea, kwa nini mnajivuna kama vile hamkupokea?

84:8 Ufu 3:17-18Sasa tayari mnayo yale yote mnayohitaji! Tayari mmekwisha kuwa matajiri! Mmekuwa wafalme, tena bila sisi! Laiti mngekuwa wafalme kweli ili na sisi tupate kuwa wafalme pamoja nanyi! 94:9 Rum 8:36; Za 71:7; Ebr 10:33Kwa maana ninaona kwamba Mungu ametuweka sisi mitume katika nafasi ya mwisho kabisa, kama watu waliohukumiwa kufa kwenye uwanja wa tamasha, kwa sababu tumefanywa kuwa maonyesho kwa ulimwengu wote, kwa malaika na kwa wanadamu pia. 104:10 1Kor 1:18; Mdo 17:18; 26:24; 1Kor 3:18; 2Kor 11:19; 1Kor 2:3Kwa ajili ya Kristo sisi ni wajinga, lakini ninyi mna hekima sana ndani ya Kristo. Sisi tu dhaifu, lakini ninyi mna nguvu. Tunadharauliwa, lakini ninyi mnaheshimiwa. 114:11 Rum 8:35; 2Kor 11:23-27Mpaka saa hii tuna njaa na kiu, tu uchi, tumepigwa na hatuna makao. 124:12 Mdo 18:3; Rum 12:14; 1Pet 3:4; Mt 5:44Tunafanya kazi kwa bidii kwa mikono yetu wenyewe. Tunapolaaniwa, tunabariki, tunapoteswa, tunastahimili, 134:13 Yer 20:18; Mao 3:45; Kum 17:7; 22:24tunaposingiziwa, tunajibu kwa upole. Mpaka sasa tumekuwa kama takataka ya dunia na uchafu wa ulimwengu.

144:14 1Kor 6:5; 15:34; 2The 3:14; 1The 2:11Siwaandikii mambo haya ili kuwaaibisha, bali ili kuwaonya, kama wanangu wapendwa. 154:15 1Kor 9:12-23; 15:1Hata kama mnao walimu 10,000 katika Kristo, lakini hamna baba wengi. Mimi nilikuwa baba yenu katika Kristo Yesu kwa kuwaletea Injili. 164:16 1Kor 11:1; Flp 3:17; 4:9; 1The 1:6; 2The 3:7-9Basi nawasihi igeni mfano wangu. 174:17 1Kor 16:10; Mdo 16:1; 1Tim 1:2Kwa sababu hii ninamtuma Timotheo, mwanangu mpendwa na mwaminifu katika Bwana. Yeye atawakumbusha kuhusu njia za maisha yangu katika Kristo Yesu, ambayo yanakubaliana na mafundisho yangu ninayofundisha katika kila kanisa.

184:18 Yer 43:2Baadhi yenu mmekuwa na jeuri mkidhani kuwa sitafika kwenu. 194:19 1Kor 16:5-6; 2Kor 1:15; Mdo 18:21Lakini kama Bwana akipenda, nitafika kwenu mapema, nami nitapenda kujua, si tu kile wanachosema hawa watu jeuri, bali pia kujua nguvu yao. 204:20 Rum 14:17; 15:13Kwa kuwa Ufalme wa Mungu si maneno matupu tu bali ni nguvu. 214:21 2Kor 1:23; 2:1; 13:2-10Ninyi amueni. Je, nije kwenu na fimbo, au nije kwa upendo na kwa roho ya upole?

Słowo Życia

1 Koryntian 4:1-21

Apostołowie Chrystusa

1Traktujcie nas więc jako tych, którzy służą Chrystusowi i wyjaśniają innym Boże tajemnice. 2Naszym najważniejszym obowiązkiem jest lojalność wobec Tego, któremu służymy. 3Dlatego nie martwię się tym, jak mnie ocenicie lub co myślą o mnie inni ludzie. Zresztą nawet ja sam nie oceniam mojej służby. 4Wprawdzie niczego nie mogę sobie zarzucić, ale to nie wystarcza. Ocenić musi mnie sam Pan. 5Nie osądzajcie więc nikogo przedwcześnie—zanim On nie powróci i nie rozświetli tego, co ukryte w ciemnościach, i nie ujawni prawdziwych ludzkich zamiarów. Wtedy każdy z nas otrzyma od Boga należną pochwałę.

6Na przykładzie własnym i Apollosa pokazałem wam, że nie wolno wykraczać ponad to, co mówi Pismo, i wywyższać jednych nauczycieli, poniżając drugich. 7Jaki masz powód do dumy? Czy masz coś, czego nie otrzymałeś w darze? A skoro wszystko, co masz, jest darem, dlaczego szczycisz się tym tak, jakbyś sam to zdobył?

8Wszystko już macie? Jesteście bogaci? Nie czekając na nas, zaczynacie już królować? Chciałbym, abyście rzeczywiście królowali—a my z wami. 9Jestem przekonany, że nas, apostołów, Bóg umieścił na samym końcu. Jesteśmy jak skazańcy czekający na egzekucje, wystawieni na widok publiczny przed całym światem—przed ludźmi i aniołami. 10My z powodu Chrystusa jesteśmy uważani za głupców—wy staliście się dzięki Niemu mądrzy; my słabniemy—wy nabieracie sił; my jesteśmy pogardzani—wy otaczani szacunkiem. 11Stale jesteśmy głodni i spragnieni, pozbawieni ubrań, poniżani i bezdomni. 12Ciężko pracujemy, aby zarobić na życie. Gdy ludzie nas znieważają—my życzymy im szczęścia, gdy nas prześladują—znosimy to, 13gdy nas zniesławiają—modlimy się za nich. Wciąż jesteśmy jak śmieci i odpadki tego świata.

Prośba i ostrzeżenie

14Nie piszę o tym wszystkim, aby was zawstydzić, ale żeby was pouczyć jako ukochane dzieci. 15Bo chociaż możecie mieć tysiące nauczycieli, to duchowych ojców macie niewielu. Przecież to ja „zrodziłem” was dla Chrystusa, głosząc wam dobrą nowinę. 16Gorąco więc proszę was: Naśladujcie nas! 17Dlatego właśnie posyłam Tymoteusza, żeby wam w tym pomógł. On jest wiernym sługą Pana i kocham go jak własnego syna. On przypomni wam to, czego nauczam we wszystkich kościołach, które odwiedzam.

18Ponieważ nie odwiedzałem was, niektórzy zaczęli popadać w pychę. 19Jeśli jednak Pan pozwoli, już niebawem do was przyjadę, a wtedy będę mógł stwierdzić czy ci, którzy tak się przechwalają, potrafią tylko dużo mówić, czy też naprawdę mają moc od Boga. 20Królestwo Boże nie opiera się bowiem na słowach, ale na mocy. 21Sami wybierzcie: Czy mam do was przyjść ze słowami nagany, czy też z miłością i łagodnością?