1 Wafalme 8 – NEN & BDS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Wafalme 8:1-66

Sanduku La Agano Laletwa Hekaluni

(2 Nyakati 5)

18:1 Ezr 7:7Kisha Mfalme Solomoni akawaita mbele zake huko Yerusalemu wazee wa Israeli, viongozi wote wa makabila na wakuu wa jamaa za Waisraeli, ili walilete Sanduku la Agano la Bwana kutoka Sayuni, Mji wa Daudi. 28:2 1Nya 3:22Wanaume wote wa Israeli wakakusanyika kwa Mfalme Solomoni wakati wa sikukuu ya mwezi wa Ethanimu, ndio mwezi wa saba.

38:3 1Nya 3:22; Ezr 2:3Wazee wote wa Israeli walipofika, makuhani wakajitwika Sanduku la Agano, 48:4 Ezr 2:6nao wakalipandisha Sanduku la Bwana, na Hema la Kukutania pamoja na vyombo vyote vitakatifu vilivyokuwa ndani yake. Makuhani na Walawi wakavibeba, 5naye Mfalme Solomoni na kusanyiko lote la Israeli waliokusanyika kumzunguka walikuwa mbele ya hilo Sanduku, nao wakatoa dhabihu nyingi za kondoo na ngʼombe ambao idadi yao haikuwezekana kuandikwa au kuhesabiwa.

68:6 Ezr 2:15; Neh 7:20Makuhani wakalileta Sanduku la Agano la Bwana hadi mahali pake ndani ya sehemu takatifu ndani ya Hekalu, yaani Patakatifu pa Patakatifu, na kuliweka chini ya mabawa ya makerubi. 7Makerubi yalitandaza mabawa yao juu ya mahali pa Sanduku la Agano na kutia kivuli Sanduku pamoja na mipiko yake ya kubebea. 8Mipiko hiyo ilikuwa mirefu sana kiasi kwamba ncha zake zilionekana kutoka Mahali Patakatifu mbele ya Patakatifu pa Patakatifu, lakini sio nje ya Mahali Patakatifu. Hiyo mipiko ipo hata leo. 9Ndani ya Sanduku hapakuwepo kitu kingine chochote isipokuwa zile mbao mbili za mawe ambazo Mose alikuwa ameziweka ndani yake huko Horebu, mahali ambapo Bwana alifanya Agano na Waisraeli baada ya kutoka Misri.

10Makuhani walipoondoka katika Mahali Patakatifu, wingu likajaza Hekalu la Bwana. 11Nao makuhani hawakuweza kufanya huduma yao kwa sababu ya lile wingu, kwa kuwa utukufu wa Bwana ulijaza Hekalu lake.

12Ndipo Solomoni akasema, “Bwana alisema kwamba ataishi katika giza nene; 138:13 Ezr 2:13naam, hakika nimekujengea Hekalu zuri sana, mahali pako pa kuishi milele.”

Hotuba Ya Solomoni

(2 Nyakati 6:3-11)

14Kusanyiko lote la Israeli lilipokuwa limesimama hapo, mfalme akageuka na kuwabariki. 158:15 Ezr 2:40; 7:7; Mdo 16:13; 20:28; Za 137:1; Mit 27:23; Ebr 13:17; Ezr 7:7; Hes 8:1Kisha akasema:

“Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye kwa mkono wake mwenyewe ametimiza lile alilomwahidi Daudi baba yangu kwa kinywa chake mwenyewe. Kwa kuwa alisema, 16‘Tangu siku niliyowatoa watu wangu Israeli kutoka Misri, sikuchagua mji katika kabila lolote la Israeli ili Hekalu lijengwe humo ili Jina langu lipate kuwamo humo, bali nimemchagua Daudi kuwatawala watu wangu Israeli.’

178:17 Ezr 2:43“Ilikuwa moyoni mwa Daudi baba yangu kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana, Mungu wa Israeli. 188:18 Ezr 5:5; 7:28; Neh 8:7; Rum 8:28; Mit 3:6; Law 10:10-11; 2Nya 30:22Lakini Bwana akamwambia Daudi baba yangu, ‘Kwa sababu ilikuwa moyoni mwako kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina langu, ulifanya vyema kuwa na jambo hili moyoni mwako. 19Hata hivyo, sio wewe utakayenijengea hekalu, bali mwanao, ambaye ni nyama yako na damu yako mwenyewe, yeye ndiye atakayejenga Hekalu kwa ajili ya Jina langu.’

208:20 1Nya 9:2; Ezr 2:43Bwana ametimiza ahadi aliyoiweka: Nimeingia mahali pa Daudi baba yangu na sasa ninakikalia kiti cha ufalme cha Israeli, kama vile Bwana alivyoahidi, nami nimejenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana, Mungu wa Israeli. 218:21 2Nya 9:2; Ezr 2:438:21 2Nya 20:3; Za 27:11; Law 16:29; Za 5:8; 2Nya 20:3; Law 16:29; Isa 58:3-5Nimetenga nafasi humo kwa ajili ya Sanduku la Agano, ambamo ndani yake kuna lile Agano la Bwana alilofanya na baba zetu wakati alipowatoa Misri.”

Maombi Ya Solomoni Ya Kuweka Hekalu Wakfu

(2 Nyakati 6:12-42)

228:22 Neh 2:9; Yer 41:16; 2Nya 15:2; 1Kor 9:15; 1Nya 28:9; Ezr 7:6-9; Za 33:18-19; Isa 3:10; Rum 8:28; 1Pet 3:12; Za 34:16; 2Nya 15:2Kisha Solomoni akasimama mbele ya madhabahu ya Bwana machoni pa kusanyiko lote la Israeli, akakunjua mikono yake kuelekea mbinguni 238:23 2Nya 33:13; Kum 4:29; Mdo 14:23; 1Nya 5:20; Isa 19:22; Yer 29:12-13na kusema:

“Ee Bwana, Mungu wa Israeli, hakuna Mungu kama wewe juu mbinguni wala chini duniani, wewe unayetunza Agano lako la upendo na watumishi wanaodumu katika njia yako kwa moyo wote. 24Umetimiza ahadi yako kwa mtumishi wako Daudi baba yangu, kwa kinywa chako uliahidi na kwa mkono wako umetimiza, kama ilivyo leo.

258:25 Ezr 7:15-16“Sasa Bwana, Mungu wa Israeli, mtimizie mtumishi wako Daudi baba yangu ahadi zako ulizomwahidi uliposema, ‘Kamwe hutakosa kuwa na mtu atakayeketi mbele zangu kwenye kiti cha ufalme cha Israeli, kama wanao wakiangalia yote wayafanyayo kuenenda mbele zangu kama vile ulivyofanya.’ 26Sasa, Ee Mungu wa Israeli, acha neno lako lile ulilomwahidi mtumishi wako Daudi baba yangu litimie.

27“Lakini kweli, je, Mungu atafanya makao duniani? Mbingu, hata mbingu zilizo juu sana, haziwezi kukutosha wewe. Sembuse Hekalu hili nililojenga! 288:28 Kum 33:8; Law 21:6; 22:2-3; 2Nya 24:14; Hes 4:4; Isa 52:11; 1Nya 23:28Hata hivyo sikiliza dua ya mtumishi wako na maombi yake kwa huruma, Ee Bwana Mungu wangu. Sikia kilio na dua ambayo mtumishi wako anaomba mbele zako siku hii ya leo. 298:29 1Nya 26:20-26; Lk 12:38-39Macho yako na yafumbuke kuelekea Hekalu hili usiku na mchana, mahali hapa ambapo ulisema, ‘Jina langu litakuwako humo,’ ili kwamba upate kusikia maombi ambayo mtumishi wako ataomba kuelekea mahali hapa. 30Usikie maombi ya mtumishi wako na ya watu wako Israeli wakati wanapoomba kuelekea mahali hapa. Sikia kutoka mbinguni, mahali pa makao yako na usikiapo, samehe.

318:31 Ay 5:19-24; Isa 41:10-14; Ezr 7:6-7, 28“Mtu anapomkosea jirani yake na akatakiwa kuapa, akija na kuapa mbele ya madhabahu yako ndani ya Hekalu hili, 328:32 Mwa 40:13; Neh 2:11; Isa 56:6; 14:1basi, sikia kutoka mbinguni na ukatende. Hukumu kati ya watumishi wako, ukimhukumu yule mwenye hatia na kuleta juu ya kichwa chake yale aliyoyatenda. Umtangazie mwenye haki kwamba hana hatia, hivyo ukathibitishe kuwa haki kwake.

338:33 Neh 3:3, 21-24“Wakati watu wako Israeli watakapokuwa wameshindwa na adui kwa sababu ya dhambi walizofanya dhidi yako, watakapokugeukia na kulikiri jina lako, wakiomba na kufanya dua kwako katika Hekalu hili, 34basi usikie kutoka mbinguni, ukasamehe dhambi ya watu wako Israeli na kuwarudisha katika nchi uliyowapa baba zao.

358:35 Ezr 6:17“Wakati mbingu zitakapokuwa zimefungwa kusiwe na mvua kwa sababu watu wako wametenda dhambi dhidi yako, watakapoomba kuelekea mahali hapa na kulikiri jina lako nao wakageuka kutoka dhambi zao kwa sababu umewaadhibu, 368:36 Ezr 7:21-24; Zek 8:1-23; Es 9:3basi usikie kutoka mbinguni na usamehe dhambi ya watumishi wako, watu wako Israeli. Wafundishe njia sahihi ya kuishi na ukanyeshe mvua juu ya nchi uliyowapa watu wako kuwa urithi.

37“Wakati njaa au tauni vikija juu ya nchi, au koga au kawa, nzige au panzi, au wakati adui atakapowazingira katika mji wao wowote, maafa ya namna yoyote au ugonjwa wowote unaoweza kuwajia, 38wakati dua au maombi yatakapofanywa na mmojawapo wa watu wako Israeli, kila mmoja akitambua taabu za moyo wake mwenyewe, naye akainyoosha mikono yake kuelekea Hekalu hili: 39basi usikie kutoka mbinguni, katika makao yako. Usamehe na utende, umpe kila mtu kulingana na matendo yake, kwa kuwa unaujua moyo wake (kwa kuwa ni wewe peke yako ujuaye mioyo ya watu wote), 40ili wakuogope kwa wakati wote watakaoishi katika nchi uliyowapa baba zetu.

41“Kwa habari ya mgeni ambaye si miongoni mwa watu wako Israeli, lakini amekuja kutoka nchi ya mbali kwa sababu ya jina lako, 42kwa maana watu watasikia juu ya Jina lako kuu na juu ya mkono wako wenye nguvu na mkono wako ulionyooshwa, atakapokuja na kuomba kuelekea Hekalu hili, 43basi na usikie kutoka mbinguni, mahali pa makao yako, ukafanye lolote ambalo mgeni huyo anakuomba, ili mataifa yote ya dunia wapate kujua jina lako na wakuogope kama wafanyavyo watu wako Israeli nao wapate pia kujua kwamba nyumba hii niliyoijenga imeitwa kwa Jina lako.

44“Wakati watu wako watakapokwenda vitani dhidi ya adui zao, popote utakapowapeleka, wakati watakapoomba kwa Bwana kuelekea mji ambao umeuchagua, na Hekalu nililolijenga kwa ajili ya Jina lako, 45basi usikie dua na maombi yao kutoka mbinguni, ukawatetee haki yao.

46“Watakapotenda dhambi dhidi yako, kwa kuwa hakuna mtu yeyote ambaye hatendi dhambi, nawe ukachukizwa nao na kuwakabidhi kwa adui, ambaye atawachukua utumwani katika nchi yake mwenyewe, mbali au karibu; 47na kama watabadilika mioyo yao katika nchi wanakoshikiliwa mateka, nao wakatubu na kukulilia katika nchi ya wale waliowashinda na kusema, ‘Tumetenda dhambi, tumefanya makosa, tumetenda uovu’; 48kama wakikugeukia kwa moyo wao wote na nafsi zao katika nchi ya adui zao ambao waliwachukua mateka, wakakuomba kuelekea nchi uliyowapa baba zao, kuelekea mji uliouchagua na Hekalu nililolijenga kwa ajili ya Jina lako; 49basi kutoka mbinguni, mahali pa makao yako, usikie dua yao na maombi yao na kuitetea haki yao. 50Uwasamehe watu wako, waliotenda dhambi dhidi yako; uwasamehe makosa yote waliyoyatenda dhidi yako, ukawafanye wale waliowashinda kuwaonea huruma; 51kwa maana ni watu wako na urithi wako, uliowatoa Misri, kutoka kwenye lile tanuru la kuyeyushia chuma.

52“Macho yako na yafumbuke juu ya ombi la mtumishi wako na ombi la watu wako Israeli, nawe uwasikilize wakati wowote wanapokulilia. 53Kwa maana uliwachagua wao kutoka mataifa yote ya ulimwengu kuwa urithi wako mwenyewe, kama ulivyotangaza kupitia mtumishi wako Mose wakati wewe, Ee Bwana Mwenyezi, ulipowatoa baba zetu kutoka Misri.”

54Wakati Solomoni alipomaliza dua hizi zote na maombi kwa Bwana, akainuka kutoka mbele ya madhabahu ya Bwana, mahali alipokuwa amepiga magoti, mikono yake ikawa imekunjuliwa kuelekea juu mbinguni. 55Akasimama na kubariki kusanyiko lote la Israeli kwa sauti kubwa akisema:

56“Ahimidiwe Bwana, aliyewapa pumziko watu wake Israeli kama vile alivyokuwa ameahidi. Hakuna hata neno moja lililopunguka kati ya ahadi zote nzuri alizozitoa kupitia mtumishi wake Mose. 57Bwana Mungu wetu na awe pamoja nasi kama alivyokuwa na baba zetu, kamwe asituache wala kutukataa. 58Yeye na aielekeze mioyo yetu kwake, ili tutembee katika njia zake zote na kuzishika amri na maagizo na masharti aliyowapa baba zetu. 59Nami maneno yangu haya, ambayo nimeyaomba mbele za Bwana, yawe karibu na Bwana Mungu wetu usiku na mchana, ili kwamba atetee shauri la mtumishi wake na la watu wake Israeli kulingana na hitaji lao la kila siku, 60ili kwamba mataifa yote ya dunia wajue kwamba Bwana ndiye Mungu na kwamba hakuna mwingine. 61Lakini ni lazima mwiweke mioyo yenu kikamilifu kwa Bwana Mungu wetu, kuishi kwa maagizo yake na kutii amri zake, kama ilivyo wakati huu.”

Kuwekwa Wakfu Hekalu

(2 Nyakati 7:4-10)

62Kisha mfalme na Israeli wote pamoja naye wakatoa dhabihu mbele za Bwana. 63Solomoni akatoa dhabihu sadaka za amani kwa Bwana: ngʼombe 22,000, pamoja na kondoo na mbuzi 120,000. Hivyo ndivyo mfalme na Waisraeli wote walivyoweka wakfu Hekalu la Bwana.

64Siku iyo hiyo mfalme akaweka wakfu sehemu ya katikati ya ua uliokuwa mbele ya Hekalu la Bwana na hapo akatoa sadaka za kuteketezwa, sadaka za nafaka na mafuta ya sadaka za amani, kwa sababu madhabahu ya shaba iliyokuwa mbele za Bwana ilikuwa ndogo sana kuweza kubeba sadaka hizo za kuteketezwa, sadaka za nafaka na mafuta ya sadaka ya amani.

65Hivyo Solomoni akaiadhimisha sikukuu kwa wakati ule, na Israeli wote pamoja naye. Walikuwa kusanyiko kubwa sana, watu kutoka Lebo-Hamathi hadi Kijito cha Misri. Wakaiadhimisha mbele za Bwana Mungu wetu kwa siku saba na siku saba zaidi, yaani, jumla siku kumi na nne. 66Siku iliyofuata, aliwaruhusu watu waondoke. Wakambariki mfalme, kisha wakaenda nyumbani, wakiwa na mashangilio na furaha rohoni kwa ajili ya mambo yote mema ambayo Bwana ametenda kwa ajili ya Daudi mtumishi wake na watu wake Israeli.

La Bible du Semeur

1 Rois 8:1-66

L’inauguration du Temple

L’Eternel vient habiter dans le Temple

(2 Ch 5.2 à 6.11)

1Alors Salomon rassembla auprès de lui à Jérusalem tous les responsables d’Israël, tous les chefs des tribus et les chefs de familles des Israélites pour faire transporter le coffre de l’alliance de l’Eternel depuis la Cité de David8.1 Voir 2 S 6.12-16 ; 1 Ch 15.25-29., qui est Sion. 2Tous les hommes d’Israël s’assemblèrent auprès du roi Salomon, au mois d’Etanim, qui est le septième mois8.2 Septembre-octobre., pendant la fête des Cabanes8.2 Voir Lv 23.33-43..

3Tous les responsables d’Israël vinrent, et les prêtres se chargèrent de porter le coffre sacré. 4Les prêtres et les lévites transportèrent le coffre de l’Eternel ainsi que la tente de la Rencontre et tous les ustensiles sacrés qu’elle contenait. 5Le roi Salomon et toute la communauté d’Israël rassemblée auprès de lui, devant le coffre, offrirent en sacrifice un très grand nombre de petit et de gros bétail qu’on ne pouvait évaluer.

6Les prêtres installèrent le coffre de l’alliance de l’Eternel à la place qui lui était destinée dans la salle du fond du Temple, c’est-à-dire dans le lieu très saint, sous les ailes des chérubins. 7Car les chérubins avaient leurs ailes déployées au-dessus de l’emplacement du coffre, de sorte qu’ils formaient un dais protecteur au-dessus du coffre et de ses barres. 8On avait donné à ces barres une longueur telle que leurs extrémités se voyaient depuis le lieu saint qui précédait le sanctuaire intérieur, mais elles ne se voyaient pas de l’extérieur. Elles sont restées là jusqu’à ce jour. 9Dans le coffre, il y avait seulement les deux tablettes de pierre que Moïse y avait déposées à Horeb8.9 Voir Ex 25.16 ; 40.20 ; Dt 10.5., lorsque l’Eternel conclut une alliance avec les Israélites à leur sortie d’Egypte.

10Au moment où les prêtres sortirent du lieu saint, la nuée lumineuse remplit le temple de l’Eternel. 11Les prêtres ne purent pas y rester pour accomplir le service, à cause de la nuée, car la gloire de l’Eternel remplissait son temple8.11 Voir Ex 40.34-35..

12Alors Salomon dit : L’Eternel a déclaré qu’il demeurerait dans un lieu obscur. 13J’ai enfin bâti pour toi une résidence, un lieu où tu habiteras éternellement !

Salomon loue l’Eternel

14Puis le roi se retourna et bénit toute l’assemblée d’Israël qui se tenait debout.

15Il dit : Béni soit l’Eternel, le Dieu d’Israël qui a, de sa propre bouche, parlé à mon père David et qui a agi pour accomplir la promesse qu’il lui avait faite. Il lui avait dit : 16« Depuis le jour où j’ai fait sortir mon peuple Israël d’Egypte, je n’ai jamais choisi une ville particulière parmi toutes les tribus d’Israël pour qu’on y bâtisse un temple où je sois présent, mais j’ai choisi David pour gouverner mon peuple Israël8.16 Voir 2 S 7.4-11 ; 1 Ch 17.3-10.. » 17Mon père David avait à cœur de bâtir un temple en l’honneur de l’Eternel, le Dieu d’Israël. 18Mais l’Eternel lui a déclaré : « Ton projet de bâtir un temple en mon honneur est une excellente chose : tu as bien fait de prendre cela à cœur. 19Toutefois, ce n’est pas toi qui bâtiras ce temple, c’est ton propre fils qui le bâtira pour moi8.19 Voir 2 S 7.1-3 ; 1 Ch 17.1-2.. » 20L’Eternel a tenu sa promesse : j’ai succédé à mon père David et j’occupe le trône d’Israël comme l’Eternel l’avait annoncé, et j’ai construit ce temple en l’honneur de l’Eternel, le Dieu d’Israël. 21J’y ai réservé un emplacement pour le coffre qui contient le code de l’alliance de l’Eternel, cette alliance qu’il a conclue avec nos ancêtres quand il les a fait sortir d’Egypte.

Prière d’intercession de Salomon

(2 Ch 6.12-40)

22Puis Salomon se plaça devant l’autel de l’Eternel, en faisant face à toute l’assemblée d’Israël. Il leva les mains vers le ciel 23et pria : Eternel, Dieu d’Israël ! Il n’y a pas de Dieu semblable à toi, ni là-haut dans le ciel, ni ici-bas sur la terre ! Tu es fidèle à ton alliance et tu conserves ta bonté à tes serviteurs qui se conduisent selon ta volonté de tout leur cœur. 24Ainsi tu as tenu la promesse que tu avais faite à ton serviteur David, mon père, oui, tu as agi pour que soit accompli aujourd’hui ce que tu lui avais déclaré de ta propre bouche. 25A présent, Eternel, Dieu d’Israël, veuille aussi tenir l’autre promesse que tu lui as faite lorsque tu lui as dit : « Il y aura toujours l’un de tes descendants qui siégera sous mon regard sur le trône d’Israël, à condition qu’ils veillent sur leur conduite pour vivre selon ma volonté comme tu as toi-même vécu8.25 Voir 1 R 2.4.. » 26Oui, maintenant, Dieu d’Israël, daigne réaliser cette promesse que tu as faite à ton serviteur, mon père David.

27Mais est-ce qu’en vérité Dieu habiterait sur la terre, alors que le ciel dans toute son immensité ne saurait le contenir ? Combien moins ce temple que je viens de te construire ! 28Toutefois, Eternel, mon Dieu, veuille être attentif à la prière et à la supplication de ton serviteur et écouter l’appel que je t’adresse en ce jour. 29Que tes yeux veillent nuit et jour sur ce temple, ce lieu dont tu as toi-même dit : « Là, je serai présent8.29 Voir Dt 12.11.. » Et exauce la prière que ton serviteur t’adresse en ce lieu. 30Daigne écouter ma supplication et celle de ton peuple Israël lorsqu’il viendra prier ici. Depuis le lieu où tu demeures, depuis le ciel, entends notre prière et veuille pardonner !

31Lorsque quelqu’un sera accusé d’avoir commis une faute envers son prochain et qu’on exigera de lui qu’il prête serment avec des imprécations ici devant ton autel dans ce temple, 32sois attentif depuis le ciel, interviens et juge tes serviteurs pour condamner le coupable, afin qu’il reçoive le châtiment que mérite sa conduite et pour faire reconnaître l’innocence du juste afin qu’il soit traité selon son innocence.

33Quand ton peuple Israël aura été battu par un ennemi, parce que ses membres auront péché contre toi, si ensuite ils reviennent à toi, s’ils t’adressent leurs louanges, te prient et t’expriment leurs supplications dans ce temple, 34écoute-les depuis le ciel, pardonne le péché de ton peuple Israël et ramène-les dans le pays que tu as donné à leurs ancêtres !

35Quand le ciel sera fermé et refusera de donner la pluie, parce que ton peuple aura péché contre toi, si ce peuple prie en ce lieu, s’il te loue et se détourne de ses fautes, après que tu l’as affligé, 36écoute-le depuis le ciel, pardonne le péché de tes serviteurs et de ton peuple Israël, indique-leur la bonne ligne de conduite à suivre, et fais tomber la pluie sur ton pays que tu as donné en possession à ton peuple !

37Quand la famine ou la peste sévira dans le pays, quand les céréales seront atteintes de maladie, quand surviendra une invasion de sauterelles ou de criquets, ou quand l’ennemi assiégera ton peuple dans les villes fortifiées du pays, quand quelque maladie ou quelque malheur s’abattra sur lui, 38-39si, considérant sa peine, chacun tend les mains vers ce temple, veuille exaucer du ciel, le lieu où tu demeures, les prières et les supplications que t’adressera tout homme ou tout ton peuple Israël. Pardonne-leur et traite chacun selon sa conduite, puisque tu connais le cœur de chacun. En effet, toi seul tu connais le cœur de tous les humains. 40De cette manière, ils te craindront tout le temps qu’ils vivront sur l’étendue du territoire que tu as donné à nos ancêtres.

41Et même si un étranger qui ne fait pas partie de ton peuple Israël entend parler de toi et vient d’un pays lointain 42– car les étrangers apprendront que tu es un grand Dieu qui agit en déployant sa puissance – quand un étranger viendra prier dans ce temple, 43veuille l’écouter depuis le ciel, la demeure où tu habites, et lui accorder tout ce qu’il t’aura demandé. De cette manière, tous les peuples du monde te connaîtront, ils te craindront comme le fait ton peuple Israël et ils reconnaîtront que le temple que j’ai construit t’appartient.

44Lorsque ton peuple partira pour combattre son ennemi, sur le chemin où tu l’enverras, s’il prie l’Eternel en se tournant vers la ville que tu as choisie et vers ce temple que j’ai construit en ton honneur, 45daigne écouter, depuis le ciel, leurs prières et leurs supplications et défendre leur cause !

46Il se peut qu’ils commettent un péché contre toi – car quel est l’homme qui ne commet jamais de péché ? Alors tu seras irrité contre eux, tu les livreras au pouvoir de leurs ennemis, qui les emmèneront en captivité dans un pays ennemi, proche ou lointain. 47S’ils se mettent à réfléchir dans le pays où ils auront été déportés, s’ils reviennent en arrière et t’adressent leurs supplications dans le pays de leurs vainqueurs et qu’ils disent : « Nous avons péché, nous avons mal agi, nous sommes coupables », 48s’ils reviennent à toi de tout leur cœur et de tout leur être, dans le pays des ennemis qui les auront déportés, et s’ils te prient en se tournant vers le pays que tu as donné à leurs ancêtres, vers la ville que tu as choisie et vers le temple que j’ai construit en ton honneur, 49alors, depuis le ciel, la demeure où tu habites, veuille écouter leur prière et leur supplication et défendre leur cause !

50Pardonne à ton peuple les péchés qu’il aura commis contre toi et toutes ses fautes contre toi ! Inspire à leurs vainqueurs qui les retiennent captifs de la compassion pour eux, et qu’ils aient compassion d’eux. 51En effet, Israël n’est-il pas ton peuple, celui qui t’appartient, depuis que tu l’as fait sortir d’Egypte, de cette fournaise à fondre le fer ?

52Veuille considérer favorablement la supplication de ton serviteur et celle de ton peuple Israël pour les exaucer chaque fois qu’ils te prieront. 53Car c’est toi, ô Seigneur Eternel, qui as choisi ce peuple pour toi parmi tous les autres peuples de la terre pour en faire le peuple qui t’appartient, comme tu l’as déclaré par l’intermédiaire de ton serviteur Moïse quand tu as fait sortir nos ancêtres d’Egypte.

Bénédiction de l’assemblée

54Or, lorsque Salomon eut terminé toute cette prière de supplication à l’Eternel, il se releva de devant l’autel de l’Eternel, où il était resté agenouillé, les mains levées vers le ciel. 55Il se releva et, d’une voix forte, il bénit toute l’assemblée d’Israël, en disant : 56Béni soit l’Eternel qui a accordé la paix à son peuple Israël, conformément à ses promesses. En effet, aucune promesse de bienfait qu’il nous a faite par l’intermédiaire de son serviteur Moïse n’a manqué de se réaliser8.56 Voir Dt 12.10 ; Jos 21.44-45.. 57Que l’Eternel, notre Dieu, soit avec nous, comme il a été avec nos ancêtres ! Qu’il ne nous abandonne jamais, qu’il ne nous délaisse pas, 58mais qu’il incline notre cœur vers lui, pour que nous marchions dans les voies qu’il a prescrites pour nous, en obéissant à ses commandements, ses ordonnances et ses lois qu’il a donnés à nos ancêtres. 59Puisse l’Eternel notre Dieu prendre en considération jour et nuit toutes les prières de supplication que je viens de lui présenter et défendre jour après jour la cause de son serviteur et de son peuple Israël. 60Ainsi tous les peuples de la terre reconnaîtront que c’est l’Eternel qui est Dieu et qu’il n’y en a pas d’autre. 61Quant à vous, que votre cœur soit attaché sans réserve à l’Eternel notre Dieu, pour que vous viviez d’une manière conforme à ses lois et que vous obéissiez à ses commandements, comme c’est le cas aujourd’hui.

La première fête célébrée au Temple

(2 Ch 7.4-10)

62Le roi et tout Israël offrirent des sacrifices devant l’Eternel. 63Salomon offrit à l’Eternel un sacrifice de communion pour lequel il immola 22 000 bœufs et 120 000 moutons. C’est de cette manière que le roi et tous les Israélites inaugurèrent le temple de l’Eternel. 64Ce même jour, le roi consacra l’intérieur de la cour qui s’étend devant le temple de l’Eternel pour y offrir les holocaustes, les offrandes et les graisses des sacrifices de communion, car l’autel de bronze qui se trouvait devant l’Eternel était trop petit pour recevoir tous les holocaustes, les offrandes et les graisses des sacrifices de communion.

65Salomon et tout Israël célébrèrent la fête. Une grande assemblée de gens venus depuis la région de Lebo-Hamath jusqu’au torrent d’Egypte8.65 C’est-à-dire du nord (Lebo-Hamath) au sud (le torrent d’Egypte) du royaume. se tint devant l’Eternel, notre Dieu, pendant sept jours puis encore sept autres jours, soit quatorze jours en tout8.65 Les mots puis encore sept autres jours… en tout manquent dans l’ancienne version grecque.. 66Après cela, le huitième jour de la seconde semaine, Salomon renvoya le peuple. Les gens vinrent le bénir, puis chacun rentra chez soi. Tous étaient joyeux et avaient le cœur content à cause de tous les bienfaits que l’Eternel avait accordés à son serviteur David et à Israël.