1 Wafalme 6 – NEN & NVI

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Wafalme 6:1-38

Solomoni Ajenga Hekalu

(2 Nyakati 3)

16:1 Ezr 4:15; 5:17Katika mwaka wa 480 baada ya Waisraeli kutoka nchi ya Misri, katika mwaka wa nne wa utawala wa Solomoni katika Israeli, katika mwezi wa Zivu, ambao ndio mwezi wa pili, alianza kujenga Hekalu la Bwana.

2Hekalu hilo Mfalme Solomoni alilojenga kwa ajili ya Bwana lilikuwa na urefu wa dhiraa sitini,6:2 Dhiraa 60 ni sawa na mita 27. upana wa dhiraa ishirini6:2 Dhiraa 20 ni sawa na mita 9. na kimo cha dhiraa thelathini6:2 Dhiraa 30 ni sawa na mita 13.5. kwenda juu. 36:3 Ezr 3:10; Hag 2:3Baraza ya mbele ya Hekalu ilienea dhiraa ishirini kulingana na upana wa Hekalu na kujitokeza dhiraa kumi mbele ya Hekalu. 46:4 1Fal 6:36; Ezr 7:20; Isa 60:6; Za 68:29Akatengeneza madirisha membamba yenye vidirisha vidogo vya juu katika Hekalu. 56:5 1Nya 29:2; Yer 27:18-22; Ezr 5:14Akafanyiza vyumba vya pembeni kulizunguka Hekalu lote vikishikamana na kuta za Hekalu na za Patakatifu pa Patakatifu. 66:6 Ezr 5:3Ghorofa ya chini kabisa ilikuwa na upana wa dhiraa tano,6:6 Dhiraa 5 ni sawa na mita 2.25. ya kati ilikuwa dhiraa sita na ya tatu ilikuwa dhiraa saba.6:6 Dhiraa saba ni sawa na mita 3.15. Kuzunguka ukuta wa nje wa Hekalu akapunguza ukuta pande zote ili boriti zisishikane kwenye kuta za Hekalu.

7Katika kujenga Hekalu, yalitumika tu mawe yaliyochongwa huko machimboni, wala hakuna nyundo, patasi au chombo kingine chochote cha chuma kilichosikika sauti yake katika eneo la ujenzi wa Hekalu wakati lilipokuwa likijengwa.

86:8 1Sam 9:10Ingilio la ghorofa ya chini kabisa lilikuwa upande wa kusini wa Hekalu, ngazi ilielekea ghorofa ya kati na kutokea hapo ilielekea hadi ghorofa ya tatu. 9Basi Solomoni akajenga Hekalu na kulikamilisha, akiliweka paa za boriti na mbao za mierezi. 106:10 Ezr 7:23; Yer 29:7; Law 1:9; Mwa 8:21; 1Tim 2:1-2Mfalme Solomoni akajenga vyumba vya pembeni kuzunguka Hekalu lote. Kimo cha kila kimoja kilikuwa dhiraa tano. Navyo vilikuwa vimeunganishwa na Hekalu kwa boriti za mierezi.

116:11 Kum 21:22-23; Es 2:23; Ezr 7:26; Dan 2:5Neno la Bwana likamjia Solomoni kusema: 126:12 Kut 20:24; Kum 12:11; 1Fal 9:3; 2Nya 7:16; Za 132:13“Kwa habari ya Hekalu hili unalojenga, kama ukifuata amri zangu, ukatunza masharti yangu na kushika maagizo yangu yote na kuyatii, kwa kupitia wewe nitatimiza ahadi niliyomwahidi Daudi baba yako. 136:13 Ay 5:12; Ezr 4:9; Za 9:16; 1Kor 3:19Nami nitakaa miongoni mwa Waisraeli, nami sitawaacha watu wangu Israeli.”

146:14 Ezr 5:1; 7:1; Neh 2:1; Ezr 4:24Basi Solomoni akajenga Hekalu na kulikamilisha. 156:15 Zek 4:9Akazifunika kuta zake za ndani kwa mbao za mierezi, akizipigilia ukutani kuanzia sakafuni mwa Hekalu hadi kwenye dari na kufunika sakafu ya Hekalu kwa mbao za misunobari. 166:16 1Fal 8:63; 2Nya 7:15; Yn 10:22Akagawa dhiraa ishirini sehemu ya nyuma ya Hekalu kwa mbao za mierezi kuanzia kwenye sakafu hadi darini ili kufanya sehemu takatifu ya ndani, yaani Patakatifu pa Patakatifu. 176:17 2Sam 6:13; 1Nya 16:1-3; 2Nya 29:21; Hes 7:2-3; Ezr 8:25Ukumbi mkubwa uliokuwa mbele ya chumba hiki ndio ulikuwa na urefu wa dhiraa arobaini.6:17 Dhiraa 40 ni sawa na mita 18. 186:18 1Nya 24:1; 23:6; Hes 3:6-9; 8:9-11Hekalu ndani ilikuwa ya mierezi iliyonakshiwa mifano ya maboga na maua yaliyochanua. Kila kitu kilikuwa cha mwerezi, hakuna jiwe ambalo lilionekana.

196:19 Kut 12:11; Hes 28:16Ndani ya Hekalu akatengeneza sehemu takatifu ya ndani, kwa ajili ya kuweka Sanduku la Agano la Bwana. 206:20 2Nya 30:15-17; 35:11; Kut 12:25; 2Nya 29:34Sehemu takatifu ya ndani ilikuwa na upana, urefu na kimo cha dhiraa ishirini ndani kwa ndani. Akaifunika ndani kwa dhahabu safi, pia akaifunika madhabahu ya mierezi vivyo hivyo. 216:21 Kut 12:48; Za 93:5Solomoni akaifunika sehemu ya ndani ya Hekalu kwa dhahabu safi, naye akaitandaza mikufu ya dhahabu kutoka upande moja hadi ule mwingine mbele ya Patakatifu pa Patakatifu, ambako palifunikwa kwa dhahabu. 226:22 Kut 12:17; Mit 21:1; Ezr 1:1Basi akafunika sehemu yote ya ndani kwa dhahabu. Pia akafunika madhabahu yale yaliyokuwa ndani ya Patakatifu pa Patakatifu kwa dhahabu.

23Katika Patakatifu pa Patakatifu akatengeneza makerubi wawili kwa mzeituni, kila moja likiwa na dhiraa kumi6:23 Dhiraa 10 ni sawa na mita 4.5. kwenda juu. 24Bawa moja la kerubi wa kwanza lilikuwa na urefu wa dhiraa tano na bawa jingine dhiraa tano, hivyo urefu kutoka ncha ya bawa moja hadi ncha ya bawa jingine ulikuwa dhiraa kumi. 25Kerubi wa pili alikuwa na urefu wa dhiraa kumi pia, hivyo makerubi hao wawili walifanana kwa vipimo na kwa umbo. 26Kimo cha kila kerubi kilikuwa dhiraa kumi. 27Aliwaweka makerubi hao ndani ya Patakatifu pa Patakatifu pa Hekalu, mabawa yake yakiwa yamekunjuliwa. Bawa la kerubi mmoja liligusa ukuta mmoja, wakati bawa la yule mwingine liligusa ukuta mwingine, nayo mabawa yao mengine yaligusana katikati ya chumba. 28Akafunika wale makerubi kwa dhahabu.

29Juu ya kuta zote zilizozunguka Hekalu, za vyumba vya ndani na vya nje, zilipambwa kwa nakshi zilizokatwa za makerubi, miti ya mitende na maua yaliyochanua. 30Pia alifunika sakafu zote za vyumba vya ndani na vya nje vya Hekalu kwa dhahabu.

31Kwa ingilio la Patakatifu pa Patakatifu akatengeneza milango ya mbao za mzeituni, zikiwa na miimo na vizingiti vyenye umbo la pembe tano. 32Juu ya milango miwili ya mbao za mzeituni alinakshi makerubi, miti ya mitende pamoja na maua yaliyochanua na kufunika makerubi na miti ya mitende kwa dhahabu iliyofuliwa. 33Kwa njia iyo hiyo akatengeneza miimo yenye pande nne ya miti ya mizeituni, kwa ajili ya ingilio la ukumbi mkubwa. 34Kulikuwa na milango miwili iliyoweza kukunjuka iliyotengenezwa kwa mbao za msunobari na kila mmoja ulikuwa na bawaba ambazo zingeuwezesha kujikunja kila kipande juu ya kingine. 35Akanakshi makerubi, miti ya mitende na maua yaliyochanua juu yake na kufunika kwa dhahabu iliyonyooshwa vizuri juu ya michoro.

36Tena akajenga ua wa ndani safu tatu za mawe yaliyochongwa na safu moja ya boriti za mierezi zilizorembwa.

37Msingi wa Hekalu la Bwana uliwekwa katika mwaka wa nne, katika mwezi wa Zivu, ndio mwezi wa tano. 38Katika mwaka wa kumi na moja, mwezi wa Buli, ndio mwezi wa nane, Hekalu lilikamilika katika hatua zake zote kwa kufuatana na maelekezo yake Solomoni. Alilijenga kwa miaka saba.

Nueva Versión Internacional

1 Reyes 6:1-38

Salomón construye el templo

6:1-292Cr 3:1-14

1Salomón comenzó a construir el templo del Señor en el cuarto año de su reinado en Israel, en el mes de zif, que es el mes segundo. Habían transcurrido cuatrocientos ochenta años desde que los israelitas salieron de Egipto.

2El templo que el rey Salomón construyó para el Señor medía sesenta codos de largo por veinte de ancho y treinta de alto.6:2 Es decir, aprox. 27 m de largo, 9 m de ancho y 14 m de alto. 3El vestíbulo de la nave central del templo medía también veinte codos6:3 Es decir, aprox. 9 m. de ancho y por el frente del templo sobresalía diez codos.6:3 Es decir, aprox. 4.5 m; también en vv. 23-26. 4Salomón también mandó colocar en el templo ventanales con celosías. 5Alrededor del edificio, y contra las paredes de la nave central y del santuario interior, construyó un anexo con cámaras laterales. 6El piso inferior del anexo medía cinco codos6:6 Es decir, aprox. 2.3 m; también en vv. 10 y 24. de ancho; el piso intermedio, seis codos,6:6 Es decir, aprox. 2.7 m. y el piso más alto, siete codos.6:6 Es decir, aprox. 3.2 m. Salomón había mandado hacer salientes en el exterior del templo para que las vigas no se empotraran en la pared misma.

7En la construcción del templo solo se emplearon piedras de cantera ya labradas, así que durante las obras no se oyó el ruido de martillos ni de piquetas, ni de ninguna otra herramienta.

8La entrada al piso inferior6:8 inferior (LXX y Targum); intermedio (TM). se hallaba en el lado sur del templo; una escalera de caracol conducía al nivel intermedio y a la planta alta. 9Salomón terminó de construir el templo techándolo con vigas y tablones de cedro. 10A lo largo del templo construyó el anexo, el cual tenía una altura de cinco codos y quedaba unido a la pared del templo por medio de vigas de cedro.

11La palabra del Señor vino a Salomón y le dio este mensaje: 12«Ya que estás construyendo este templo, quiero decirte que, si andas según mis estatutos, y obedeces mis leyes y todos mis mandamientos, yo cumpliré por medio de ti la promesa que hice a tu padre David. 13Entonces viviré entre los israelitas y no abandonaré a mi pueblo Israel».

14Cuando Salomón terminó de construir la estructura del templo, 15revistió las paredes interiores con tablas de cedro, artesonándolas desde el piso hasta el techo; el piso lo recubrió con tablones de ciprés. 16En el santuario interior, al fondo del templo, acondicionó el Lugar Santísimo, recubriendo el espacio de veinte codos con tablas de cedro desde el piso hasta el techo. 17Frente al Lugar Santísimo estaba la nave central, la cual medía cuarenta codos.6:17 Es decir, aprox. 18 m. 18El interior del templo lo recubrió de cedro tallado con figuras de calabazas y flores abiertas. No se veía una sola piedra, pues todo era de cedro.

19Salomón dispuso el santuario interno del templo para que se colocara allí el arca del pacto del Señor. 20El interior de este santuario, que medía veinte codos de largo por veinte de ancho por veinte de alto, lo recubrió de oro puro, y también recubrió de cedro el altar. 21Además, Salomón recubrió de oro puro el interior del templo, y tendió cadenas de oro a lo largo del frente del santuario interno, el cual estaba recubierto de oro. 22En efecto, recubrió de oro todo el santuario interior y así mismo el altar que estaba delante de este.

23Salomón mandó esculpir para el santuario interior dos querubines de madera de olivo, cada uno de los cuales medía diez codos de altura. 24De una punta a otra, las alas extendidas del primer querubín medían diez codos, es decir, cada una de sus alas medía cinco codos. 25Las del segundo querubín también medían diez codos, pues los dos eran idénticos en tamaño y forma. 26Cada querubín medía diez codos de altura. 27Salomón puso los querubines con sus alas extendidas en medio del recinto interior del templo. Con una de sus alas, cada querubín tocaba una pared, mientras que sus otras alas se tocaban en medio del santuario. 28Luego Salomón recubrió de oro los querubines.

29Sobre las paredes que rodeaban el templo, lo mismo por dentro que por fuera, talló figuras de querubines, palmeras y flores abiertas. 30Además, recubrió de oro los pisos de los cuartos interiores y exteriores del templo.

31Para la entrada del santuario interior, Salomón hizo puertas de madera de olivo, con jambas y postes pentagonales. 32Sobre las dos puertas de madera de olivo talló figuras de querubines, palmeras y flores abiertas, y todas ellas las recubrió de oro. 33Así mismo, para la entrada de la nave central hizo postes cuadrangulares de madera de olivo. 34También hizo dos puertas de madera de ciprés, cada una con dos hojas giratorias. 35Sobre ellas talló figuras de querubines, palmeras y flores abiertas, y las recubrió de oro bien ajustado al relieve.

36Las paredes del atrio interior las construyó con tres hileras de piedra labrada por cada hilera de vigas de cedro.

37Los cimientos del templo del Señor se habían echado en el mes de zif del cuarto año del reinado de Salomón, 38y en el mes de bul del año undécimo, es decir, en el mes octavo de ese año, se terminó de construir el templo siguiendo al pie de la letra todos los detalles del diseño. Siete años le llevó a Salomón la construcción del templo.