1 Wafalme 6 – NEN & BPH

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Wafalme 6:1-38

Solomoni Ajenga Hekalu

(2 Nyakati 3)

16:1 Ezr 4:15; 5:17Katika mwaka wa 480 baada ya Waisraeli kutoka nchi ya Misri, katika mwaka wa nne wa utawala wa Solomoni katika Israeli, katika mwezi wa Zivu, ambao ndio mwezi wa pili, alianza kujenga Hekalu la Bwana.

2Hekalu hilo Mfalme Solomoni alilojenga kwa ajili ya Bwana lilikuwa na urefu wa dhiraa sitini,6:2 Dhiraa 60 ni sawa na mita 27. upana wa dhiraa ishirini6:2 Dhiraa 20 ni sawa na mita 9. na kimo cha dhiraa thelathini6:2 Dhiraa 30 ni sawa na mita 13.5. kwenda juu. 36:3 Ezr 3:10; Hag 2:3Baraza ya mbele ya Hekalu ilienea dhiraa ishirini kulingana na upana wa Hekalu na kujitokeza dhiraa kumi mbele ya Hekalu. 46:4 1Fal 6:36; Ezr 7:20; Isa 60:6; Za 68:29Akatengeneza madirisha membamba yenye vidirisha vidogo vya juu katika Hekalu. 56:5 1Nya 29:2; Yer 27:18-22; Ezr 5:14Akafanyiza vyumba vya pembeni kulizunguka Hekalu lote vikishikamana na kuta za Hekalu na za Patakatifu pa Patakatifu. 66:6 Ezr 5:3Ghorofa ya chini kabisa ilikuwa na upana wa dhiraa tano,6:6 Dhiraa 5 ni sawa na mita 2.25. ya kati ilikuwa dhiraa sita na ya tatu ilikuwa dhiraa saba.6:6 Dhiraa saba ni sawa na mita 3.15. Kuzunguka ukuta wa nje wa Hekalu akapunguza ukuta pande zote ili boriti zisishikane kwenye kuta za Hekalu.

7Katika kujenga Hekalu, yalitumika tu mawe yaliyochongwa huko machimboni, wala hakuna nyundo, patasi au chombo kingine chochote cha chuma kilichosikika sauti yake katika eneo la ujenzi wa Hekalu wakati lilipokuwa likijengwa.

86:8 1Sam 9:10Ingilio la ghorofa ya chini kabisa lilikuwa upande wa kusini wa Hekalu, ngazi ilielekea ghorofa ya kati na kutokea hapo ilielekea hadi ghorofa ya tatu. 9Basi Solomoni akajenga Hekalu na kulikamilisha, akiliweka paa za boriti na mbao za mierezi. 106:10 Ezr 7:23; Yer 29:7; Law 1:9; Mwa 8:21; 1Tim 2:1-2Mfalme Solomoni akajenga vyumba vya pembeni kuzunguka Hekalu lote. Kimo cha kila kimoja kilikuwa dhiraa tano. Navyo vilikuwa vimeunganishwa na Hekalu kwa boriti za mierezi.

116:11 Kum 21:22-23; Es 2:23; Ezr 7:26; Dan 2:5Neno la Bwana likamjia Solomoni kusema: 126:12 Kut 20:24; Kum 12:11; 1Fal 9:3; 2Nya 7:16; Za 132:13“Kwa habari ya Hekalu hili unalojenga, kama ukifuata amri zangu, ukatunza masharti yangu na kushika maagizo yangu yote na kuyatii, kwa kupitia wewe nitatimiza ahadi niliyomwahidi Daudi baba yako. 136:13 Ay 5:12; Ezr 4:9; Za 9:16; 1Kor 3:19Nami nitakaa miongoni mwa Waisraeli, nami sitawaacha watu wangu Israeli.”

146:14 Ezr 5:1; 7:1; Neh 2:1; Ezr 4:24Basi Solomoni akajenga Hekalu na kulikamilisha. 156:15 Zek 4:9Akazifunika kuta zake za ndani kwa mbao za mierezi, akizipigilia ukutani kuanzia sakafuni mwa Hekalu hadi kwenye dari na kufunika sakafu ya Hekalu kwa mbao za misunobari. 166:16 1Fal 8:63; 2Nya 7:15; Yn 10:22Akagawa dhiraa ishirini sehemu ya nyuma ya Hekalu kwa mbao za mierezi kuanzia kwenye sakafu hadi darini ili kufanya sehemu takatifu ya ndani, yaani Patakatifu pa Patakatifu. 176:17 2Sam 6:13; 1Nya 16:1-3; 2Nya 29:21; Hes 7:2-3; Ezr 8:25Ukumbi mkubwa uliokuwa mbele ya chumba hiki ndio ulikuwa na urefu wa dhiraa arobaini.6:17 Dhiraa 40 ni sawa na mita 18. 186:18 1Nya 24:1; 23:6; Hes 3:6-9; 8:9-11Hekalu ndani ilikuwa ya mierezi iliyonakshiwa mifano ya maboga na maua yaliyochanua. Kila kitu kilikuwa cha mwerezi, hakuna jiwe ambalo lilionekana.

196:19 Kut 12:11; Hes 28:16Ndani ya Hekalu akatengeneza sehemu takatifu ya ndani, kwa ajili ya kuweka Sanduku la Agano la Bwana. 206:20 2Nya 30:15-17; 35:11; Kut 12:25; 2Nya 29:34Sehemu takatifu ya ndani ilikuwa na upana, urefu na kimo cha dhiraa ishirini ndani kwa ndani. Akaifunika ndani kwa dhahabu safi, pia akaifunika madhabahu ya mierezi vivyo hivyo. 216:21 Kut 12:48; Za 93:5Solomoni akaifunika sehemu ya ndani ya Hekalu kwa dhahabu safi, naye akaitandaza mikufu ya dhahabu kutoka upande moja hadi ule mwingine mbele ya Patakatifu pa Patakatifu, ambako palifunikwa kwa dhahabu. 226:22 Kut 12:17; Mit 21:1; Ezr 1:1Basi akafunika sehemu yote ya ndani kwa dhahabu. Pia akafunika madhabahu yale yaliyokuwa ndani ya Patakatifu pa Patakatifu kwa dhahabu.

23Katika Patakatifu pa Patakatifu akatengeneza makerubi wawili kwa mzeituni, kila moja likiwa na dhiraa kumi6:23 Dhiraa 10 ni sawa na mita 4.5. kwenda juu. 24Bawa moja la kerubi wa kwanza lilikuwa na urefu wa dhiraa tano na bawa jingine dhiraa tano, hivyo urefu kutoka ncha ya bawa moja hadi ncha ya bawa jingine ulikuwa dhiraa kumi. 25Kerubi wa pili alikuwa na urefu wa dhiraa kumi pia, hivyo makerubi hao wawili walifanana kwa vipimo na kwa umbo. 26Kimo cha kila kerubi kilikuwa dhiraa kumi. 27Aliwaweka makerubi hao ndani ya Patakatifu pa Patakatifu pa Hekalu, mabawa yake yakiwa yamekunjuliwa. Bawa la kerubi mmoja liligusa ukuta mmoja, wakati bawa la yule mwingine liligusa ukuta mwingine, nayo mabawa yao mengine yaligusana katikati ya chumba. 28Akafunika wale makerubi kwa dhahabu.

29Juu ya kuta zote zilizozunguka Hekalu, za vyumba vya ndani na vya nje, zilipambwa kwa nakshi zilizokatwa za makerubi, miti ya mitende na maua yaliyochanua. 30Pia alifunika sakafu zote za vyumba vya ndani na vya nje vya Hekalu kwa dhahabu.

31Kwa ingilio la Patakatifu pa Patakatifu akatengeneza milango ya mbao za mzeituni, zikiwa na miimo na vizingiti vyenye umbo la pembe tano. 32Juu ya milango miwili ya mbao za mzeituni alinakshi makerubi, miti ya mitende pamoja na maua yaliyochanua na kufunika makerubi na miti ya mitende kwa dhahabu iliyofuliwa. 33Kwa njia iyo hiyo akatengeneza miimo yenye pande nne ya miti ya mizeituni, kwa ajili ya ingilio la ukumbi mkubwa. 34Kulikuwa na milango miwili iliyoweza kukunjuka iliyotengenezwa kwa mbao za msunobari na kila mmoja ulikuwa na bawaba ambazo zingeuwezesha kujikunja kila kipande juu ya kingine. 35Akanakshi makerubi, miti ya mitende na maua yaliyochanua juu yake na kufunika kwa dhahabu iliyonyooshwa vizuri juu ya michoro.

36Tena akajenga ua wa ndani safu tatu za mawe yaliyochongwa na safu moja ya boriti za mierezi zilizorembwa.

37Msingi wa Hekalu la Bwana uliwekwa katika mwaka wa nne, katika mwezi wa Zivu, ndio mwezi wa tano. 38Katika mwaka wa kumi na moja, mwezi wa Buli, ndio mwezi wa nane, Hekalu lilikamilika katika hatua zake zote kwa kufuatana na maelekezo yake Solomoni. Alilijenga kwa miaka saba.

Bibelen på hverdagsdansk

1. Kongebog 6:1-38

Salomon bygger templet

1I Salomons fjerde regeringsår, i måneden ziv, det vil sige årets anden måned,6,1 Måneden ziv svarer til dansk april-maj. (Året menes at være 996 f.Kr.) påbegyndte han tempelbyggeriet—480 år efter, at Israels folk havde forladt Egypten. 2Templet blev 27 m langt, 9 m bredt og 13,5 m højt. 3Foran indgangen til templet blev der bygget en forhal, 9 m på den lange led svarende til templets bredde og 4,5 m på den korte led. 4Hele vejen rundt på tempelbygningen var der smalle vinduesåbninger.

5-6Rundt langs templets ydermur byggede Salomon en række mindre rum i tre etager. Stueetagen var 2,25 m bred, førstesalen var 2,7 m bred, og andensalen var 3,15 m bred. De bjælker der dannede gulv og loft, hvilede på nogle fremspring i tempelmuren, således at man ikke behøvede at bryde hul i muren for at lave denne tilbygning.

7Tempelbygningens sten var blevet færdighugget i stenbruddet, hvilket betød, at bygningen blev rejst i stilhed uden støj fra hamre, mejsler eller andre jernredskaber.

8Der var kun adgang til den udvendige tilbygning gennem en dør, der vendte mod syd, og trapper førte op til første og anden sal.

9Templets tag bestod af tværbjælker og planker af cedertræ. 10Det var også tværbjælker og planker af cedertræ, der forbandt tilbygningen med templet. Hver etage i tilbygningen var 2,25 m høj.

11-12Herren talte til Salomon om det tempel, han var i færd med at bygge. „Hvis du nøje følger mine instrukser og adlyder mine befalinger,” sagde han, „vil jeg opfylde det løfte, jeg gav din far, David. 13Jeg vil tage bolig iblandt mit folk Israel og ikke forlade dem.”

14Da selve tempelbygningen var færdig, fortsatte Salomon med den indvendige indretning. 15Væggene blev beklædt med cedertræspaneler fra gulv til loft, og gulvbrædderne var af cyprestræ. 16-22Der blev lavet et inderrum på 9 m gange 9 m gange 9 m. Det var det allerhelligste rum. Også det rum blev beklædt på alle sider med cedertræsplanker. Det største rum i templet, som kaldtes det hellige, blev således 18 m langt. Cedertræspaneler dækkede alle murene fuldstændigt, og de blev dekoreret med udskårne figurer af blomsterknopper og udsprungne blomster.

I templets inderste rum, det allerhelligste, blev pagtens ark anbragt. Røgelsesalteret, som skulle stå foran indgangen til det allerhelligste rum, blev lavet af cedertræ. Templets indersider blev derefter belagt med rent guld, både i det hellige og det allerhelligste. Også cedertræsalteret blev belagt med guld.

23-28I det allerhelligste rum anbragte Salomon to keruber, udskåret af vildt oliventræ. De var 4,5 m høje. Hver vinge var 2,25 m lang, og hver kerubs vingefang var således 4,5 m. De to keruber var nøjagtig ens, og de var begge belagt med guld. De var anbragt således, at deres udbredte vinger tilsammen nåede fra væg til væg, og det sted, hvor deres vingespidser rørte hinanden, var nøjagtig midt i rummet.

29Figurer, der skulle forestille keruber, palmetræer og blomster, var sirligt udskåret i panelerne i begge tempelrum, 30og selv gulvet i begge rum blev belagt med guld.

31-32Salomon lod fremstille to dørfløje af vildt oliventræ til at lukke af for det allerhelligste rum, og rammen omkring døråbningen blev lavet med en gavl, så den var en femkant.6,31-32 Teksten er vanskelig at forstå i versene 31-34. Dørene blev udsmykket med udskårne keruber, palmetræer og blomster, og det hele blev belagt med guld.

33Ved indgangen til det hellige rum lod han også lave en dørramme af vildt oliventræ, men den var firkantet. 34Der blev lavet to fløjdøre af cyprestræ, hvor hver fløj havde to dørflader, som drejede på hængsler. 35På fløjdørene lod han udskære keruber, palmetræer og blomster, som blev belagt med guld.

36Han lod bygge en mur rundt om den indre forgård med tre lag sten og et lag cedertræsbjælker.

37Tempelbyggeriet startede som sagt i årets anden måned i Salomons fjerde regeringsår, 38og det var færdigt til mindste detalje i bul måned, det vil sige den ottende måned, i Salomons 11. regeringsår. Det tog altså godt syv år at opføre templet.