1 Samweli 8 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Samweli 8:1-22

Israeli Waomba Mfalme

18:1 Kum 16:18-19; Amu 10:4; 12:14Samweli alipokuwa mzee, akaweka wanawe kuwa waamuzi wa Israeli. 28:2 1Nya 6:28; Mwa 22; 19; 1Fal 19:3; Amo 5:4-5Mzaliwa wa kwanza alikuwa Yoeli, na la wa pili lilikuwa Abiya, nao wakatumika huko Beer-Sheba. 38:3 1Sam 2:12; Neh 9:29; Ay 34:27; Za 14:3; 58:3; Isa 53:6; Kut 23:8; 1Sam 12:3; Mit 17:23; Kut 23:2; Kum 16:19Lakini wanawe hawakuenenda katika njia zake. Waliziacha wakageukia faida za udanganyifu nao wakapokea rushwa na kupotosha haki.

48:4 Amu 11:11; 1Sam 11:3; 7:17Basi wazee wote wa Israeli wakakusanyika pamoja na kumjia Samweli huko Rama. 58:5 Kum 17:14-20; 1Sam 10:19; 12:12-13; 3:20; 12:2; Hos 13:11Wakamwambia, “Wewe umekuwa mzee, nao wanao hawaenendi katika njia zako, sasa tuteulie mfalme wa kutuongoza, kama ilivyo kwa mataifa mengine yote.”

68:6 Hos 13:10; 1Sam 12:17; 15:11; 16:1Lakini wao waliposema, “Tupe mfalme wa kutuongoza,” hili lilimchukiza Samweli, hivyo akamwomba Bwana. 78:7 1Sam 12:1; Hes 11:20; Kut 16:8; Mt 10:24-25; Lk 10:16; Yn 13:16; 1Sam 10:19Naye Bwana akamwambia: “Sikiliza yale yote watu wanakuambia. Si wewe ambaye wamekukataa, bali wamenikataa mimi kuwa mfalme wao. 88:8 1Sam 12:10; 2Fal 21:22; Yer 2:17Kama vile walivyofanya tangu siku nilipowapandisha kutoka Misri mpaka siku hii ya leo; wakiniacha mimi na kutumikia miungu mingine, ndivyo wanavyokufanyia wewe. 98:9 Kum 17:14-20; 1Sam 8:11-18; 10:25Sasa wasikilize, lakini waonye kwa makini na uwafahamishe yale watakayotendewa na mfalme atakayewatawala.”

108:10 Kut 19:7Samweli akawaambia wale watu waliokuwa wakiomba wapewe mfalme maneno yote ya Bwana. 118:11 1Sam 10:25; 14:52; Mwa 41:46; Kum 17:16; 2Sam 15:1; 2Nya 1:14; 9:25; Wim 3:7; 1Nya 1:5Akasema, “Hivi ndivyo atakavyowatendea mfalme atakayewatawala. Atawachukua wana wenu na kuwafanya watumike kwa magari yake ya vita na farasi, nao watakimbia mbele ya magari yake. 128:12 Kum 1:15; 1Sam 22:7Baadhi yao atawaweka kuwa majemadari wa jeshi wa maelfu na majemadari wa jeshi wa hamsini, wengine kulima mashamba yake na kuvuna mavuno yake, pia na wengine kutengeneza silaha za vita na vifaa kwa ajili ya magari yake. 13Atawachukua binti zenu kuwa watengeneza manukato, wapishi na waokaji. 148:14 1Sam 28:6; Ay 27:9; 35:12-13; Za 18:41; 66:18; Mit 1:28; Isa 58:4; 59:2; Yer 14:12; Eze 8:18; Mik 3:4; 1Sam 10:25; 1Fal 12:4Atayachukua mashamba yenu yaliyo mazuri, mashamba ya mizabibu na mashamba yenu ya mizeituni na kuwapa watumishi wake. 158:15 Mwa 41:34; 1Sam 17:25Ataichukua sehemu ya kumi ya nafaka yenu na ya zabibu zenu na kuwapa maafisa wake na watumishi wake. 16Atawachukua watumishi wenu wa kiume na wa kike, na ngʼombe wenu walio wazuri sana na punda kwa matumizi yake mwenyewe. 17Atachukua sehemu ya kumi ya makundi yenu ya kondoo na mbuzi, na ninyi wenyewe mtakuwa watumwa wake. 188:18 1Sam 28:6; Ay 27:9; 35:12-13; Za 18:41; 66:18; Mit 1:28; Isa 58:4; 59:2; Yer 14:12; Eze 8:18; Mik 3:4; 1Sam 10:25; 1Fal 12:4Siku ile itakapowadia, mtalia kwa kutaka msaada kutokana na mfalme mliyemchagua, naye Bwana hatawajibu.”

198:19 Mit 1:24; Isa 50:2; 66:4; Yer 7:13; 8; 12; 13; 10; 44:16; Mdo 13:21Lakini watu wakakataa kumsikiliza Samweli wakasema, “Hapana! Tunataka mfalme wa kututawala. 20Kisha tutakuwa kama mataifa mengine yote, tukiwa na mfalme wa kutuongoza na kwenda mbele yetu na kutupigania vita vyetu.”

218:21 Amu 11:11Samweli aliposikia yote watu waliyosema, akarudia kuyasema mbele za Bwana. 228:22 Hos 13:11Bwana akamjibu, “Wasikilize na uwape mfalme.”

Kisha Samweli akawaambia watu wa Israeli, “Kila mmoja arudi mjini kwake.”

Swedish Contemporary Bible

1 Samuelsboken 8:1-22

Samuel och Saul

(8:1—15:35)

Saul blir Israels kung

Folket vill ha en kung

1När Samuel blev äldre, tillsatte han sina söner som domare över Israel. 2Hans äldste son Joel och hans näst äldste son Avia dömde i Beer Sheva, 3men de följde inte alls i sin fars fotspår utan sökte egen orätt vinning: de tog emot mutor och vrängde rättvisan. 4Alla Israels äldste möttes i Rama hos Samuel. 5De sa: ”Du har blivit gammal och dina söner följer inte i dina fotspår. Ge oss en kung som kan styra oss, så som alla andra folk har!”

6Samuel blev besviken när han hörde att de ville ha en kung och bad till Herren. 7Men Herren svarade: ”Låt dem få vad de vill ha! Det är mig de förkastar, inte dig. De vill inte längre ha mig till kung. 8Ända sedan jag förde dem ut ur Egypten har de gång på gång vänt mig ryggen och följt andra gudar och nu behandlar de dig på samma sätt. 9Gör som folket vill, men varna dem för hur det kommer att bli att lyda under en kung!”

10Samuel berättade allt vad Herren sagt till dem som begärde en kung. 11Han sa: ”En kung som ska härska över er kommer att ha rätt att ta ut era söner till krigstjänst, som ryttare eller vagnsförare eller till att springa framför hans vagnar. 12Några kommer han att sätta till befäl över tusen eller femtio man. Andra kommer att tvingas plöja hans åkrar och ta in hans skördar eller sättas att tillverka hans vapen och vagnar. 13Han kommer att ta era döttrar till att bereda salvor och parfymer och till att arbeta i hans kök och bageri. 14Han kommer att ta era bästa åkrar, vingårdar och olivträd och ge dem till sina tjänstemän. 15Han kommer att kräva en tiondel av er skörd åt sina hovmän och tjänstemän. 16Han kommer att kräva att få era tjänare, de bästa åsnorna och det bästa av er boskap för sina personliga behov. 17Han kommer att kräva en tiondel av era hjordar och ni kommer att bli hans slavar. 18Ni kommer att ångra er och gråta bittert på grund av den kung som ni valt, men då ska Herren inte hjälpa er.”

19Men folket vägrade lyssna till Samuels varningar och sa: ”Nej, vi måste ha en kung! 20Vi vill vara som alla andra folk. Vi vill ha en kung som kan skipa rätt åt oss och leda oss och kämpa för oss i strid.”

21Samuel berättade sedan för Herren vad folket hade sagt 22och Herren svarade: ”Gör som de säger och ge dem en kung!” Då sa Samuel till dem att de skulle gå hem, var och en till sin stad.