1 Samweli 29 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Samweli 29:1-11

Akishi Amrudisha Daudi Huko Siklagi

129:1 1Sam 28:1; 4:1; Yos 17:16; 1Fal 18:45; 21:1; 2Fal 9:30; Yer 50:5; Hos 1:4; 5:11; 2:22; Yos 12:18Wafilisti wakakusanya majeshi yao yote huko Afeki, nao Waisraeli wakapiga kambi karibu na chemchemi iliyoko Yezreeli. 229:2 1Sam 28:2Watawala wa Wafilisti walipokuwa wakipita pamoja na vikosi vyao vya mamia na vya maelfu, Daudi na watu wake walikuwa wakitembea huko nyuma pamoja na Akishi. 329:3 1Nya 12:19; 1Sam 27:7; Dan 6:5; Yn 19:6; 1Pet 3:16Majemadari wa Wafilisti wakauliza, “Vipi kuhusu hawa Waebrania?”

Akishi akajibu, “Huyu si Daudi, aliyekuwa afisa wa Sauli mfalme wa Israeli? Ameshakuwa pamoja nami kwa zaidi ya mwaka, naye tangu alipomwacha Sauli hadi sasa, sikuona kosa lolote kwake.”

429:4 1Nya 12:19; 1Sam 14:21Lakini majemadari wa Wafilisti wakamkasirikia na kusema, “Mrudishe mtu huyu, apate kurudi mahali pale ulipompangia. Haimpasi kufuatana pamoja nasi vitani, asije akageuka, akawa kinyume chetu vitani. Ni kwa njia ipi bora zaidi angeweza kujipatia tena kibali kwa bwana wake, isipokuwa kwa vichwa vya watu wetu wenyewe? 529:5 1Sam 18:7; 21:11Je, huyu si ndiye Daudi walioimba kumhusu katika ngoma zao, wakisema:

“ ‘Sauli amewaua elfu zake,

naye Daudi makumi elfu yake’?”

629:6 1Sam 27:8-12; Hes 27:17; 2Sam 3:25; 2Fal 19:27; Za 121:8; Isa 37:28Basi Akishi akamwita Daudi na kumwambia, “Kama vile Bwana aishivyo, wewe umekuwa mtu mwaminifu, nami ningependa utumike pamoja nami katika jeshi. Tangu siku ile uliyofika kwangu hadi sasa, sijaona kosa lolote kwako, lakini hao watawala hawakukubali. 7Rudi na uende kwa amani; usifanye chochote cha kuwakasirisha watawala wa Kifilisti.”

8Daudi akamuuliza Akishi, “Lakini mimi nimefanya nini? Je, umeona nini kibaya juu ya mtumishi wako tangu siku ile niliyokuja kwako hadi leo? Kwa nini nisirudi na kupigana na adui za bwana wangu mfalme?”

929:9 2Sam 14:17, 20; 19:27Akishi akamjibu Daudi, “Mimi ninajua ya kuwa wewe umekuwa wa kupendeza machoni pangu kama vile malaika wa Mungu. Lakini hao majemadari wa Wafilisti wamesema, ‘Huyu haimpasi kwenda vitani pamoja nasi.’ 1029:10 1Nya 12:19Sasa amka mapema, pamoja na watumishi wa bwana wako waliofuatana nawe, nanyi ondokeni asubuhi mara kutakapopambazuka.”

1129:11 Za 37:23; 73:2; Mit 16:9; 20:24; Isa 30:21; Yer 10:23; 1Kor 10:23; 10:13; 2Sam 4:4Hivyo Daudi na watu wake wakaamka asubuhi na mapema, wakaenda zao kurudi katika nchi ya Wafilisti, nao Wafilisti wakapanda kwenda Yezreeli.

King James Version

1 Samuel 29:1-11

1Now the Philistines gathered together all their armies to Aphek: and the Israelites pitched by a fountain which is in Jezreel. 2And the lords of the Philistines passed on by hundreds, and by thousands: but David and his men passed on in the rereward with Achish. 3Then said the princes of the Philistines, What do these Hebrews here? And Achish said unto the princes of the Philistines, Is not this David, the servant of Saul the king of Israel, which hath been with me these days, or these years, and I have found no fault in him since he fell unto me unto this day? 4And the princes of the Philistines were wroth with him; and the princes of the Philistines said unto him, Make this fellow return, that he may go again to his place which thou hast appointed him, and let him not go down with us to battle, lest in the battle he be an adversary to us: for wherewith should he reconcile himself unto his master? should it not be with the heads of these men? 5Is not this David, of whom they sang one to another in dances, saying, Saul slew his thousands, and David his ten thousands?

6¶ Then Achish called David, and said unto him, Surely, as the LORD liveth, thou hast been upright, and thy going out and thy coming in with me in the host is good in my sight: for I have not found evil in thee since the day of thy coming unto me unto this day: nevertheless the lords favour thee not.29.6 the lords…: Heb. thou art not good in the eyes of the lords 7Wherefore now return, and go in peace, that thou displease not the lords of the Philistines.29.7 displease…: Heb. do not evil in the eyes of the lords

8¶ And David said unto Achish, But what have I done? and what hast thou found in thy servant so long as I have been with thee unto this day, that I may not go fight against the enemies of my lord the king?29.8 with…: Heb. before thee 9And Achish answered and said to David, I know that thou art good in my sight, as an angel of God: notwithstanding the princes of the Philistines have said, He shall not go up with us to the battle. 10Wherefore now rise up early in the morning with thy master’s servants that are come with thee: and as soon as ye be up early in the morning, and have light, depart. 11So David and his men rose up early to depart in the morning, to return into the land of the Philistines. And the Philistines went up to Jezreel.