1 Petro 5 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Petro 5:1-14

Kulichunga Kundi La Mungu

15:1 Mdo 11:30; Lk 24:48; 1Pet 4:13; Ufu 1:9Kwa wazee waliomo miongoni mwenu, nawasihi mimi nikiwa mzee mwenzenu, shahidi wa mateso ya Kristo, na mshiriki katika utukufu utakaofunuliwa: 25:2 Yn 21:6; 1Tim 3:3lichungeni kundi la Mungu mlilokabidhiwa, mkitumika kama waangalizi, si kwa kulazimishwa bali kwa hiari, kama Mungu anavyowataka mwe; si kwa tamaa ya fedha, bali mlio na bidii katika kutumika. 35:3 Eze 34:4; Mt 20:25-28; Flp 3:17; 1Tim 4:12Msijifanye mabwana juu ya wale walio chini ya uangalizi wenu, bali kuweni vielelezo kwa hilo kundi. 45:4 1Kor 9:25; Ebr 13:20; 1Kor 9:25; 2Tim 4:8; Yak 1:12; 1Pet 1:4Naye Mchungaji Mkuu atakapodhihirishwa, mtapokea taji ya utukufu isiyoharibika.

55:5 Efe 5:21; Mit 3:34; Yak 4:6Vivyo hivyo, ninyi mlio vijana watiini wazee. Nanyi nyote imewapasa kujivika unyenyekevu kila mtu kwa mwenzake, kwa kuwa,

“Mungu huwapinga wenye kiburi,

lakini huwapa wanyenyekevu neema.”

65:6 Yak 4:10Basi, nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake. 75:7 Mit 27:5; Mt 6:25; Ebr 13:5Mtwikeni yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana na mambo yenu.

85:8 Ay 1:7; Lk 21:34, 36; 1The 5:6; 1Pet 4:7; Ufu 12:12Mwe na kiasi na kukesha, maana adui yenu ibilisi huzungukazunguka kama simba angurumaye akitafuta mtu ili apate kummeza. 95:9 Yak 4:7; Kol 2:5; Mdo 14:22Mpingeni, mkiwa thabiti katika imani, mkijua ya kwamba mateso kama hayo yanawapata ndugu zenu pote duniani.

105:10 2Kor 4:17; 2The 2:17Nanyi mkiisha kuteswa kwa kitambo kidogo, Mungu wa neema yote, aliyewaita kuingia katika utukufu wake wa milele ndani ya Kristo, yeye mwenyewe atawarejesha na kuwatia nguvu, akiwaimarisha na kuwathibitisha. 115:11 Rum 11:36; 1Pet 4:11; Ufu 1:6Uweza una yeye milele na milele. Amen.

Salamu Za Mwisho

125:12 2Kor 1:19; Ebr 13:22Kwa msaada wa Silvano,5:12 Yaani Sila. ambaye ninamhesabu kuwa ndugu mwaminifu, nimewaandikia waraka huu mfupi ili kuwatia moyo, na kushuhudia kwamba hii ni neema halisi ya Mungu. Simameni imara katika neema hiyo.

135:13 Mdo 12:12Kanisa lililoko Babeli, lililochaguliwa pamoja nanyi, wanawasalimu; vivyo hivyo mwanangu Marko anawasalimu. 145:14 Rum 16:16; Efe 6:23Salimianeni kwa busu la upendo.

Amani iwe nanyi nyote mlio katika Kristo.

New International Version

1 Peter 5:1-14

To the Elders and the Flock

1To the elders among you, I appeal as a fellow elder and a witness of Christ’s sufferings who also will share in the glory to be revealed: 2Be shepherds of God’s flock that is under your care, watching over them—not because you must, but because you are willing, as God wants you to be; not pursuing dishonest gain, but eager to serve; 3not lording it over those entrusted to you, but being examples to the flock. 4And when the Chief Shepherd appears, you will receive the crown of glory that will never fade away.

5In the same way, you who are younger, submit yourselves to your elders. All of you, clothe yourselves with humility toward one another, because,

“God opposes the proud

but shows favor to the humble.”5:5 Prov. 3:34

6Humble yourselves, therefore, under God’s mighty hand, that he may lift you up in due time. 7Cast all your anxiety on him because he cares for you.

8Be alert and of sober mind. Your enemy the devil prowls around like a roaring lion looking for someone to devour. 9Resist him, standing firm in the faith, because you know that the family of believers throughout the world is undergoing the same kind of sufferings.

10And the God of all grace, who called you to his eternal glory in Christ, after you have suffered a little while, will himself restore you and make you strong, firm and steadfast. 11To him be the power for ever and ever. Amen.

Final Greetings

12With the help of Silas,5:12 Greek Silvanus, a variant of Silas whom I regard as a faithful brother, I have written to you briefly, encouraging you and testifying that this is the true grace of God. Stand fast in it.

13She who is in Babylon, chosen together with you, sends you her greetings, and so does my son Mark. 14Greet one another with a kiss of love.

Peace to all of you who are in Christ.