1 Nyakati 9 – NEN & NVI

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Nyakati 9:1-44

19:1 1Nya 5:25Waisraeli wote waliorodheshwa katika koo zilizoandikwa kwenye kitabu cha wafalme wa Israeli.

Watu Katika Yerusalemu

Watu wa Yuda walichukuliwa mateka kwenda Babeli kwa sababu ya kukosa uaminifu kwa Mungu. 29:2 Yos 9:27; Ezr 2:70; 8:20; Neh 7:5; Law 26:33; 2Nya 33:11; 36:5Basi watu wa kwanza kurudi kukaa kwenye milki zao katika miji yao walikuwa baadhi ya Waisraeli, makuhani, Walawi na watumishi wa Hekalu.9:2 Yaani Wanethini.

39:3 Neh 11:1Wale waliotoka Yuda, Benyamini, Efraimu na Manase ambao waliishi Yerusalemu walikuwa:

Jamaa Za Yuda

49:4 Mwa 38:29; 46:12; Hes 26:20Uthai mwana wa Amihudi, mwana wa Omri, mwana wa Imri, mwana wa Bani, wa wana wa Peresi, mwana wa Yuda.

5Wazao wa Washiloni waliorudi ni:

Asaya mzaliwa wa kwanza na wanawe.

6Kwa wana wa Zera:

Yeueli.

Watu wa Yuda jumla yao walikuwa watu 690.

Jamaa Za Benyamini

7Kwa Benyamini walikuwa:

Salu mwana wa Meshulamu, mwana wa Hodavia, mwana wa Hasenua;

8Ibneya mwana wa Yerohamu, Ela mwana wa Uzi, mwana wa Mikri; na Meshulamu mwana wa Shefatia, mwana wa Reueli, mwana wa Ibniya.

9Watu kutoka Benyamini kama walivyoorodheshwa katika koo zao jumla yao ni 956. Watu hawa wote walikuwa viongozi wa jamaa zao.

Jamaa Za Makuhani

109:10 Neh 11:10; 12:19Wa jamaa za makuhani walikuwa:

Yedaya, Yehoyaribu na Yakini;

11Azaria mwana wa Hilkia, mwana wa Meshulamu, mwana wa Sadoki, mwana wa Merayothi, mwana wa Ahitubu aliyekuwa afisa kiongozi wa nyumba ya Mungu.

129:12 Neh 10:3; Yer 38:1Adaya mwana wa Yerohamu, mwana wa Pashuri, mwana wa Malkiya; Maasai, mwana wa Adieli, mwana wa Yahzera, mwana wa Meshulamu, mwana wa Meshilemithi, mwana wa Imeri.

13Makuhani waliokuwa viongozi wa jamaa zao walikuwa 1,760. Walikuwa watu wenye uwezo, waliowajibika kuhudumu katika nyumba ya Mungu.

Jamaa Za Walawi

149:14 1Nya 6:19; Neh 11:15-19Jamaa za Walawi walikuwa:

Shemaya, mwana wa Hashubu, mwana wa Azrikamu, mwana wa Hashabia, wa wana wa Merari. 159:15 2Nya 20:14; Neh 11:22Bakbakari, Hereshi, Galali na Matania mwana wa Mika, mwana wa Zikri, mwana wa Asafu. 169:16 Neh 12:28; 1Nya 2:54; Neh 7:26Obadia mwana wa Shemaya, mwana wa Galali, mwana wa Yeduthuni. Berekia mwana wa Asa, mwana wa Elikana, ambao waliishi katika vijiji vya Wanetofathi.

Jamaa Za Mabawabu

179:17 Ezr 2:42; Neh 7:4; 1Nya 23:5; 26:1; Za 84:10Mabawabu katika Hekalu la Bwana waliorudi walikuwa:

Shalumu, Akubu, Talmoni, Ahimani na ndugu zao. Shalumu alikuwa mlinzi wao mkuu. 189:18 Eze 43:1; 46:1; 2Fal 11:19; Eze 44:23Walikuwa wamewekwa katika lango la mfalme lililokuwa upande wa mashariki, mpaka wakati huu. Hawa walikuwa mabawabu wa kutoka kwenye kambi ya Walawi. 199:19 Yer 35:4; Hes 26:9-11Shalumu mwana wa Kore, mwana wa Ebiasafu, mwana wa Kora, pamoja na mabawabu wenzake kutoka jamaa yake ya Kora waliwajibika kulinda malango ya Hema, kama vile baba zao walivyokuwa wamewajibika kulinda ingilio la Maskani ya Bwana. 209:20 Hes 25:7-13; Kut 6:25; Hes 3:32; 31:6; Yos 22:30-31; Za 106:30Hapo zamani Finehasi mwana wa Eleazari alikuwa kiongozi wa mabawabu, naye Bwana alikuwa pamoja naye:

219:21 1Nya 26:2, 14Zekaria mwana wa Meshelemia alikuwa bawabu katika ingilio la Hema la Kukutania.

229:22 1Nya 26:1; 2Nya 31:15, 18; 1Sam 9:9Jumla ya waliochaguliwa kuwa mabawabu katika sakafu za kupuria nafaka walikuwa watu 212. Waliandikishwa kwa koo zao kwenye vijiji vyao. Mabawabu hawa waliwekwa katika nafasi zao za kuaminiwa na Daudi pamoja na mwonaji Samweli. 23Wao na wazao wao walikuwa viongozi wa kulinda malango ya nyumba ya Bwana, nyumba iliyoitwa Hema. 249:24 1Nya 26:13-19Mabawabu walikuwa pande zote nne: mashariki, magharibi, kaskazini na kusini. 259:25 2Fal 11:5; 2Nya 23:8Ndugu zao katika vijiji vyao walikuwa wakija mara kwa mara na kuwasaidia katika kazi zao kwa vipindi mbalimbali vya siku saba. 269:26 1Nya 26:22Lakini mabawabu wanne wakuu, waliokuwa Walawi, walikabidhiwa wajibu kwa ajili ya vyumba na hazina katika nyumba ya Mungu. 279:27 Hes 3:38; 1Nya 23:30-32; 1Sam 22:22Walikesha mahali walipowekwa kuizunguka nyumba ya Mungu, kwa sababu iliwapasa kuilinda. Pia walitunza funguo kwa ajili ya kufungua mlango kila siku asubuhi.

28Baadhi yao walikuwa viongozi wa kutunza vifaa vilivyotumika katika huduma ndani ya Hekalu; walivihesabu kila vilipoingizwa ndani na kila vilipotolewa. 299:29 Hes 3:23; 1Nya 23:29Wengine walipangiwa kutunza mapambo na vifaa vingine vya patakatifu, pamoja na unga, divai, mafuta, uvumba na vikolezo. 309:30 Kut 30:25; 37:29; Yer 6:20; Eze 27:19-22; Mk 14:3Lakini baadhi ya makuhani walifanya kazi ya kuchanganya vikolezo. 319:31 Law 24:5-8; 2Nya 13:11; Law 6:21Mlawi aliyeitwa Matithia, mwana mzaliwa wa kwanza wa Shalumu, wa ukoo wa Kora, alikabidhiwa wajibu kwa ajili ya kuoka mikate ya sadaka. 329:32 Kut 40:23; Ebr 9:2, 24; Yn 6:32, 33Baadhi ya ndugu zao wa ukoo wa Kohathi walikuwa viongozi wa kuandaa mikate ya Wonyesho kwa ajili ya kila Sabato, mikate iliyokuwa inawekwa mezani.

339:33 1Nya 25:1-31; 2Nya 5:12; Za 134:1; 1Nya 6:31; 13:8; 15:16Wale waliokuwa waimbaji, viongozi wa jamaa za Walawi, waliishi katika vyumba vya Hekalu, nao hawakufanya shughuli nyingine yoyote kwa sababu iliwapasa kuwajibika kwa kazi hiyo usiku na mchana.

34Hawa wote walikuwa viongozi wa jamaa za Walawi, wakuu kama walivyoorodheshwa katika koo zao, nao waliishi Yerusalemu.

Ukoo Wa Sauli

(1 Nyakati 8:29-38)

359:35 1Nya 8:29Yeieli alikuwa baba yake Gibeoni naye aliishi huko Gibeoni. Mke wake aliitwa Maaka, 36mwanawe mzaliwa wa kwanza alikuwa Abdoni, akafuatiwa na Suri, Kishi, Baali, Neri, Nadabu, 37Gedori, Ahio, Zekaria na Miklothi. 38Miklothi akamzaa Shimeamu. Wao pia waliishi karibu na jamaa zao huko Yerusalemu.

399:39 1Nya 8:33; 1Sam 9:1; 13:22; 2Sam 2:8Neri akamzaa Kishi, Kishi akamzaa Sauli. Sauli akamzaa Yonathani, Malki-Shua, Abinadabu na Esh-Baali.9:39 Anajulikana pia kwa jina la Ish-Boshethi, maana yake Mtu wa Aibu (2Sam 2:8).

409:40 2Sam 4:4Yonathani akamzaa Merib-Baali,9:40 Pia anajulikana kwa jina la Mefiboshethi.

naye Merib-Baali akamzaa Mika.

419:41 2Sam 9:12; 1Nya 8:35Wana wa Mika walikuwa:

Pithoni, Meleki, Tarea, na Ahazi.

42Ahazi akamzaa Yara, Yara akawazaa Alemethi, Azmawethi na Zimri, naye Zimri akamzaa Mosa. 43Mosa akamzaa Binea, Binea akamzaa Refaya, na mwanawe huyo ni Eleasa, na mwanawe huyo ni Aseli.

44Aseli alikuwa na wana sita, na haya ndiyo majina yao:

Azrikamu, Bokeru, Ishmaeli, Shearia, Obadia na Hanani. Hawa ndio waliokuwa wana wa Aseli.

Nueva Versión Internacional

1 Crónicas 9:1-44

1Todos los israelitas fueron registrados en las listas genealógicas e inscritos en el libro de los reyes de Israel.

Por causa de su infidelidad a Dios, Judá fue llevado cautivo a Babilonia.

Los que regresaron a Jerusalén

9:1-17Neh 11:3-19

2Los primeros en ocupar nuevamente sus posesiones y ciudades fueron israelitas, sacerdotes, levitas y servidores del Templo.

3Algunos de los descendientes de Judá, Benjamín, Efraín y Manasés habitaron en Jerusalén.

4De los judíos: Utay, hijo de Amiud, descendiente en línea directa de Omrí, Imrí, Baní y Fares, hijo de Judá.

5De los silonitas:

Asaías, el primogénito, con sus hijos.

6De los zeraítas:

Jeuel y el resto de sus parientes.

En total seiscientas noventa personas.

7De los benjamitas:

Salú, hijo de Mesulán, hijo de Hodavías, hijo de Senuá;9:7 Senuá. Alt. Hasenuá.

8Ibneías, hijo de Jeroán;

Elá, hijo de Uzi, hijo de Micri;

Mesulán, hijo de Sefatías, hijo de Reuel, hijo de Ibnías.

9Sus parientes, según sus registros genealógicos, eran en total novecientos cincuenta y seis, todos ellos jefes de sus familias patriarcales.

10De los sacerdotes:

Jedaías, Joyarib, Jaquín,

11Azarías, hijo de Jilquías, que era descendiente en línea directa de Mesulán, Sadoc, Merayot y Ajitob, quien estuvo a cargo del Templo de Dios;

12Adaías, hijo de Jeroán, hijo de Pasur, hijo de Malquías;

Masay, hijo de Adiel, que era descendiente en línea directa de Jazera, Mesulán, Mesilemit e Imer,

13y sus parientes, en total mil setecientos sesenta jefes de familias patriarcales y hombres muy capacitados para el servicio en el Templo de Dios.

14De los levitas:

Semaías, hijo de Jasub, que descendía en línea directa de Azricán, Jasabías y Merari;

15Bacbacar, Heres, Galal y Matanías, hijo de Micaías, hijo de Zicrí, hijo de Asaf;

16Abdías, hijo de Semaías, hijo de Galal, hijo de Jedutún;

Berequías, hijo de Asá, hijo de Elcaná, que habitó en las aldeas de los netofatitas.

17Los porteros:

Salún, Acub, Talmón y Ajimán y sus parientes; Salún era el jefe. 18Hasta ahora custodian la puerta del rey, que está al oriente, y han sido porteros de los campamentos levitas.

19Además, Salún, hijo de Coré, hijo de Ebiasaf, hijo de Corah, y sus parientes coreítas de la misma familia patriarcal estaban encargados de custodiar la entrada de la Tienda, tal como sus antepasados habían custodiado la entrada del campamento del Señor.

20En el pasado, Finés, hijo de Eleazar, fue el oficial a cargo de ellos, y el Señor estuvo con él.

21Zacarías, hijo de Meselemías, era el portero de la Tienda de reunión.

22Los escogidos como porteros fueron un total de doscientos doce. En sus aldeas se encuentran sus registros genealógicos.

David y Samuel, el vidente, asignaron sus funciones. 23Los porteros y sus hijos estaban encargados de custodiar la entrada de la Tienda que se usaba como Templo del Señor. 24Había porteros en los cuatro puntos cardinales. 25Cada siete días, sus parientes que vivían en las aldeas se turnaban para ayudarlos. 26Los cuatro porteros principales estaban en servicio permanente. Eran levitas y custodiaban las salas y los tesoros del Templo de Dios. 27Durante la noche, montaban guardia alrededor del Templo de Dios y en la mañana abrían sus puertas.

28Algunos de ellos estaban encargados de los utensilios que se usaban en el servicio del Templo, y debían contarlos al sacarlos y al guardarlos. 29Otros estaban a cargo de los utensilios, de todos los vasos sagrados, de la harina refinada, el vino, el aceite, el incienso y los perfumes. 30Algunos de los sacerdotes preparaban la mezcla de los perfumes. 31El levita Matatías, primogénito del coreíta Salún, estaba encargado de hacer las tortas para las ofrendas. 32Algunos de sus parientes coatitas preparaban el pan que se ponía cada sábado en la mesa.

33También había cantores que eran jefes de familias patriarcales de los levitas, los cuales vivían en las habitaciones del Templo. Estos estaban exentos de cualquier otro servicio, porque de día y de noche tenían que ocuparse de su ministerio.

34Según sus registros genealógicos, estos eran jefes de las familias patriarcales de los levitas y vivían en Jerusalén.

Genealogía de Saúl

9:35-441Cr 8:28-38

35Jehiel, padre de Gabaón, vivía en Gabaón.

Su esposa se llamaba Macá. 36Sus hijos fueron Abdón, el primogénito; Zur, Quis, Baal, Ner, Nadab, 37Guedor, Ajío, Zacarías y Miclot, 38padre de Simeia. Estos también vivían en Jerusalén con sus parientes.

39Ner fue el padre de Quis, y este fue padre de Saúl, quien a su vez lo fue de Jonatán, Malquisúa, Abinadab y Esbaal.

40El hijo de Jonatán fue

Meribaal, y este fue padre de Micaías.

41Los hijos de Micaías fueron:

Pitón, Mélec, Tarea y Acaz.9:41 y Acaz (mss. de LXX, Siríaca, Targum y Nova Vulgata; véase 8:35); TM no incluye este nombre aquí.

42Acaz fue el padre de Jará, y este lo fue de Alemet, Azmávet y Zimri. Zimri fue el padre de Mosá; 43Mosá fue el padre de Biná, y este lo fue de Refaías. Refaías fue el padre de Elasá, y este lo fue de Azel.

44Azel tuvo seis hijos, cuyos nombres fueron:

Azricán, Bocrú, Ismael, Searías, Abdías y Janán. Estos fueron los hijos de Azel.