1 Nyakati 29 – NEN & NVI

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Nyakati 29:1-30

Matoleo Kwa Ajili Ya Ujenzi Wa Hekalu

129:1 1Fal 3:7; 2Nya 13:7; Mit 4:3; 1Nya 22:5Ndipo Mfalme Daudi akaliambia kusanyiko lote: “Mwanangu Solomoni, yeye ambaye Mungu amemchagua, ni kijana mdogo na asiye na uzoefu. Kazi hii ni kubwa, kwa sababu Hekalu hili la fahari si kwa ajili ya mwanadamu bali ni kwa ajili ya Bwana. 229:2 Ezr 6:5; Ufu 21:18; Hag 2:8; Isa 54:11; 1Nya 22:2-5; Kut 28:9Kwa uwezo wangu wote nimetenga mali kwa ajili ya Hekalu la Mungu wangu: dhahabu kwa kazi za dhahabu, fedha kwa ajili ya fedha, shaba kwa kazi za shaba, chuma kwa kazi za chuma na miti kwa kazi za miti, vivyo hivyo vito vya shohamu kwa ajili ya kutia kwenye vijalizo, almasi, mawe ya rangi mbalimbali, aina zote za vito vya thamani na marmar; yote haya kwa wingi mno. 329:3 2Nya 24:10; Za 28:9; 2Nya 35:8; Za 26:8; 27:4; Mit 3:9Zaidi ya hayo, kwa kujitolea kwangu kwa ajili ya Hekalu la Mungu wangu, sasa ninatoa hazina zangu mwenyewe za dhahabu na fedha kwa ajili ya Hekalu la Mungu wangu, zaidi ya mali niliyotoa kwa ajili ya Hekalu hili takatifu: 429:4 Mwa 10:29; 1Nya 22:14; Ay 22:24; 1Fal 9:28; 2Nya 8:18talanta 3,00029:4 Talanta 3,000 za dhahabu sawa na tani 110. za dhahabu (dhahabu ya Ofiri) na talanta 7,00029:4 Talanta 7,000 za fedha ni sawa na tani 260. za fedha safi iliyosafishwa, kwa ajili ya kufunika kuta za Hekalu, 5kwa kazi ya dhahabu na kazi ya fedha na kwa kazi yote itakayofanywa na mafundi. Basi, ni nani anayependa kujitoa kwa Bwana leo?”

629:6 1Nya 28:1; Kut 36:2; Ezr 7:15Ndipo viongozi wa jamaa, maafisa wa kabila za Israeli, majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia, pamoja na maafisa waliokuwa wasimamizi wa kazi za mfalme wakatoa kwa hiari yao.

7Wakatoa kwa ajili ya kazi ya Hekalu la Mungu talanta 5,00029:7 Talanta 5,000 za dhahabu ni sawa na tani 190. na darkoni 10,00029:7 Darkoni 10,000 za dhahabu ni sawa na kilo 84. za dhahabu, talanta 10,00029:7 Talanta 10,000 za fedha ni sawa na tani 375. za fedha, talanta 18,00029:7 Talanta 18,000 za shaba ni sawa na tani 675. za shaba na talanta 100,00029:7 Talanta 100,000 za chuma ni sawa na tani 3,750. za chuma. 829:8 Kut 35:27; 1Nya 26:21Kila mmoja aliyekuwa na vito vya thamani akavitoa katika hazina ya Hekalu la Bwana chini ya uangalizi wa Yehieli Mgershoni. 929:9 1Fal 8:61; 2Kor 9:7Watu wakafurahi kwa sababu ya itikio la hiari la viongozi wao, kwa kuwa walikuwa wametoa kwa hiari na kwa moyo wote kwa Bwana. Mfalme Daudi pia akafurahi sana.

Maombi Ya Daudi

1029:10 1Fal 8:15-16; 2Nya 6:4; Za 72:18; Eze 3:12Daudi akamhimidi Bwana mbele ya kusanyiko lote, akisema:

“Uhimidiwe wewe, Ee Bwana,

Mungu wa Israeli baba yetu,

tangu milele hata milele.

1129:11 Za 24:8; 89:11; Mt 6:13; Ufu 5:12-13; Dan 4:34-35; 1Tim 1:17Ukuu na uweza, ni vyako, Ee Bwana,

na utukufu na enzi na uzuri,

kwa kuwa kila kilichoko mbinguni na duniani

ni chako wewe.

Ee Bwana, ufalme ni wako;

umetukuzwa kuwa mkuu juu ya yote.

1229:12 Ezr 7:27; Mhu 5:19; 2Nya 20:6; Rum 11:36; Kum 8:18; 1Sam 2:7-8; Za 75:6; Mit 10:22; Yak 1:17Utajiri na heshima vyatoka kwako;

wewe ndiwe utawalaye vitu vyote.

Mikononi mwako kuna nguvu na uweza

ili kuinua na kuwapa wote nguvu,

13Sasa, Mungu wetu, tunakushukuru

na kulisifu Jina lako tukufu.

14“Lakini mimi ni nani, nao watu wangu ni nani, hata tuweze kukutolea kwa ukarimu namna hii? Vitu vyote vyatoka kwako, nasi tumekutolea tu vile vitokavyo mkononi mwako. 1529:15 Mwa 47:9; 23:4; Ebr 11:13; Mhu 6:12; Za 102:11; Ay 14:2; Za 39:12; 1Pet 2:11; Za 90:9; 144:4Sisi ni wageni na wapitaji machoni pako, kama walivyokuwa baba zetu wote. Siku zetu duniani ni kama kivuli, bila tumaini. 16Ee Bwana Mungu wetu, kwa wingi wote huu ambao tumekutolea kwa kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina lako Takatifu, vimetoka mkononi mwako, navyo vyote ni mali yako. 1729:17 Mit 17:3; Yer 11:20; Za 15:1-5; Mit 11:20; Ebr 4:13; Kum 8:2; 1Sam 16:7; 1Nya 28:9; Za 7:9; Yer 17:10; Mit 16:2Ninajua, Mungu wangu, kwamba wewe huujaribu moyo na unapendezwa na unyofu. Vitu hivi vyote nimetoa kwa hiari na kwa moyo mnyofu. Nami sasa nimeona kwa furaha jinsi watu wako walioko hapa kwa hiari yao walivyokutolea wewe. 1829:18 Za 10:17; Yer 10:23Ee Bwana, Mungu wa baba zetu Abrahamu, Isaki na Israeli, weka shauku hii ndani ya mioyo ya watu wako daima na uifanye mioyo yao iwe na uaminifu kwako. 1929:19 1Fal 8:61; Isa 38:3; 1Nya 22:14; Za 72:1Nawe umpe mwanangu Solomoni kujitolea kwako kwa moyo wote ili kuzishika amri zako, masharti yako, maagizo yako na kufanya kila kitu ili kujenga Hekalu hili la fahari ambalo kwa ajili yake nimetoa.”

20Ndipo Daudi akaliambia kusanyiko lote, “Mhimidini Bwana Mungu wenu.” Hivyo wote wakamhimidi Bwana, Mungu wa baba zao. Wakasujudu na kuanguka kifudifudi mbele za Bwana na mfalme.

Solomoni Akubalika Kuwa Mfalme

21Siku ya pili yake wakamtolea Bwana dhabihu na sadaka za kuteketezwa: mafahali 1,000, kondoo dume 1,000 na wana-kondoo dume 1,000, pamoja na sadaka za kinywaji na sadaka nyingine nyingi sana kwa ajili ya Israeli. 2229:22 1Nya 12:40; 1Sam 2:35; 1Fal 1:33-39Wakala na kunywa kwa furaha kubwa mbele za Bwana siku ile.

Wakamtawaza Solomoni mwana wa Daudi mara ya pili kuwa mfalme, wakamtia mafuta kwa ajili ya Bwana ili awe mfalme na Sadoki kuwa kuhani. 2329:23 1Fal 2:12; 1Nya 17:14Solomoni akaketi kwenye kiti cha enzi cha Bwana kuwa mfalme mahali pa Daudi baba yake. Akafanikiwa sana na Israeli wote wakamtii. 2429:24 Mwa 24:2; 47:29; Eze 17:18; 2Nya 30:8Maafisa wote na mashujaa, pamoja na wana wote wa Daudi, wakaahidi kumtii Mfalme Solomoni.

2529:25 1Fal 10:7; 3:13; Mhu 2:9; 2Nya 1:12; Dan 5:18-19; Ebr 2:9Bwana akamtukuza sana Solomoni mbele ya Israeli wote na kumvika fahari ya kifalme ambayo hakuna mfalme yeyote wa Israeli kabla yake aliwahi kuwa nayo.

Muhtasari Wa Utawala Wa Daudi

2629:26 1Nya 18:14Daudi mwana wa Yese alikuwa mfalme wa Israeli yote. 2729:27 2Sam 5:4-5; 1Fal 2:11Alitawala Israeli kwa miaka arobaini: huko Hebroni alitawala miaka saba, na katika Yerusalemu akatawala miaka thelathini na mitatu.

2829:28 Mwa 15:15; Mdo 13:36; 1Nya 23:1; Mwa 25:8; Hes 23:10; Ay 5:26Daudi akafa akiwa mzee mwenye umri mwema, akiwa ameshiba siku, utajiri na heshima. Naye Solomoni mwanawe akawa mfalme baada yake.

2929:29 1Sam 9:9; 22:5; 2Sam 7:2; Ay 5:26Kuhusu matukio ya utawala wa Mfalme Daudi, kuanzia mwanzo hadi mwisho, yameandikwa katika kumbukumbu za mwonaji Samweli, na kumbukumbu za nabii Nathani na kumbukumbu za mwonaji Gadi, 3029:30 Dan 2:21pamoja na habari zote za utawala wake, nguvu zake na matukio yaliyompata yeye, na Israeli, na falme za nchi nyingine zote.

Nueva Versión Internacional

1 Crónicas 29:1-30

Ofrendas para el templo

1El rey David dijo a toda la asamblea: «Dios ha escogido a mi hijo Salomón, pero para una obra de esta magnitud todavía le falta experiencia. El templo no es para un hombre, sino para Dios el Señor. 2Con mucho esfuerzo he hecho los preparativos para el templo de Dios. He conseguido oro para los objetos de oro, plata para los de plata, bronce para los de bronce, hierro para los de hierro, madera para los de madera; y piedras de ónice para engastar piedras de turquesa,29:2 El significado hebreo de esta palabra es incierto. piedras para mosaicos, piedras preciosas de toda clase y mármol en abundancia. 3Además, aparte de lo que ya he conseguido, por amor al templo de mi Dios entrego para su templo todo el oro y la plata que poseo: 4tres mil talentos29:4 Es decir, aprox. 102 t. de oro de Ofir y siete mil talentos29:4 Es decir, aprox. 238 t. de plata refinada, para recubrir las paredes de los edificios, 5para todos los objetos de oro y de plata, y para toda clase de trabajo que hagan los orfebres. ¿Quién de ustedes quiere hoy dar una ofrenda al Señor?».

6Entonces los líderes de familia, los oficiales de las tribus de Israel, los comandantes de mil y de cien soldados, y los oficiales encargados de las obras del rey hicieron sus ofrendas voluntarias. 7Donaron para las obras del templo de Dios cinco mil talentos29:7 Es decir, aprox. 170 t. y diez mil dáricos29:7 Es decir, aprox. 84 kg. de oro, diez mil talentos29:7 Es decir, aprox. 340 t. de plata, y dieciocho mil talentos29:7 Es decir, aprox. 612 t. de bronce y cien mil talentos29:7 Es decir, aprox. 3,400 t. de hierro. 8Los que tenían piedras preciosas las entregaron a Jehiel el guersonita para el tesoro del templo del Señor. 9El pueblo estaba muy contento de poder dar voluntariamente29:9 voluntariamente. Lit. con corazón perfecto. sus ofrendas al Señor; también el rey David se sentía muy feliz.

Oración de David

10Entonces David bendijo así al Señor en presencia de toda la asamblea:

«¡Bendito seas, Señor,

Dios de nuestro padre Israel,

desde siempre y para siempre!

11Tuyos son, Señor, la grandeza y el poder,

la gloria, la victoria y la majestad.

Tuyo es todo cuanto hay en el cielo y en la tierra.

Tuyo también es el reino

y estás por encima de todo.

12De ti proceden la riqueza y el honor;

tú lo gobiernas todo.

En tus manos están la fuerza y el poder;

y eres tú quien engrandece y fortalece a todos.

13Por eso, Dios nuestro, te damos gracias

y a tu glorioso nombre tributamos alabanzas.

14»Pero ¿quién soy yo y quién es mi pueblo, para que podamos darte estas ofrendas voluntarias? En verdad, tú eres el dueño de todo y lo que te hemos dado, de ti lo hemos recibido. 15Ante ti, somos extranjeros que están de paso, como lo fueron nuestros antepasados. Nuestros días sobre la tierra son solo una sombra sin esperanza. 16Señor y Dios nuestro, de ti procede todo cuanto hemos conseguido para construir un templo a tu santo Nombre. ¡Todo es tuyo! 17Yo sé, mi Dios, que tú pruebas los corazones y amas la rectitud. Por eso, con honestidad29:17 honestidad. Lit. con rectitud de corazón. En la Biblia, corazón se usa para designar el asiento de las emociones, pensamientos y voluntad, es decir, el proceso de toma de decisiones del ser humano. te he ofrecido voluntariamente todas estas cosas y he visto con júbilo que tu pueblo, aquí presente, te ha traído sus ofrendas. 18Señor, Dios de nuestros antepasados Abraham, Isaac e Israel, conserva por siempre estos pensamientos en el corazón de tu pueblo y dirige su pensamiento hacia ti. 19Dale también a mi hijo Salomón un corazón sincero, para que obedezca y ponga en práctica tus mandamientos, estatutos y mandatos. Permítele construir el templo para el cual he hecho esta provisión».

20Luego David animó a toda la asamblea: «¡Alaben al Señor su Dios!». Entonces toda la asamblea alabó al Señor, Dios de sus antepasados, y se postró ante el Señor y ante el rey.

Coronación de Salomón

29:21-251R 1:28-53

21Al día siguiente, ofrecieron sacrificios y holocaustos al Señor por todo Israel: mil novillos, mil carneros y mil corderos, con sus respectivas ofrendas líquidas, y numerosos sacrificios. 22Ese día comieron y bebieron con gran regocijo en presencia del Señor.

Luego, por segunda vez, proclamaron como rey a Salomón, hijo de David, y lo consagraron ante el Señor como soberano y a Sadoc lo ungieron como sacerdote. 23Y Salomón se sentó en el trono del Señor como rey en lugar de su padre David y tuvo éxito. Todo Israel le obedeció. 24Todos los oficiales, los guerreros y los hijos del rey David rindieron pleitesía al rey Salomón.

25El Señor engrandeció en extremo a Salomón ante todo Israel y le otorgó un reinado glorioso, como jamás lo tuvo ninguno de los reyes de Israel.

Muerte de David

29:26-281R 2:10-12

26David, hijo de Isaí, reinó sobre todo Israel. 27Había reinado siete años en Hebrón y treinta y tres en Jerusalén, así que en total reinó en Israel cuarenta años. 28Y murió muy anciano y entrado en años, en medio de grandes honores y riquezas, y su hijo Salomón lo sucedió en el trono.

29Todos los hechos del rey David, desde el primero hasta el último, están escritos en las crónicas del vidente Samuel, del profeta Natán y del vidente Gad. 30Allí también se registra lo que tiene que ver con su reinado y su poder; también lo que les sucedió a él, a Israel y a los pueblos vecinos.