1 Nyakati 23 – NEN & JCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Nyakati 23:1-32

Jamaa Za Walawi Na Utendaji Wao

123:1 1Fal 1:30-33; 1Nya 28:5; 29:28; 29:22-25Daudi alipokuwa mzee aliyeshiba siku, akamfanya Solomoni mwanawe kuwa mfalme juu ya Israeli.

2Pia akawakusanya pamoja viongozi wote wa Israeli, pamoja na makuhani na Walawi. 323:3 Hes 8:24; 4:3-49Walawi waliokuwa na umri wa miaka thelathini au zaidi walihesabiwa, nayo hesabu ya wanaume ilikuwa 38,000. 423:4 Ezr 3:8; 2Nya 19:8; Kum 16:18; Eze 44:24; Kum 16:18; 1Nya 26:29Daudi akasema, “Miongoni mwa hawa, 24,000 watasimamia kazi ya Hekalu la Bwana na 6,000 watakuwa maafisa na waamuzi, 523:5 1Nya 15:16; Za 92:3; Neh 12:45; Amo 6:5; 2Nya 29:25-26na 4,000 watakuwa mabawabu, na wengine 4,000 watamsifu Bwana kwa ala za uimbaji nilizotoa kwa ajili ya kusudi hilo.”

623:6 2Nya 23:18; 29:25; 8:14; Kut 6:16; Hes 26:57; 2Nya 35:10; 31:2; Ezr 6:18Daudi akawagawa Walawi katika makundi kufuatana na wana wa Lawi: Gershoni, Kohathi na Merari.

Wagershoni

7Wana wa Wagershoni walikuwa wawili:

Ladani na Shimei.

8Wana wa Ladani walikuwa watatu:

Yehieli wa kwanza, Zethamu na Yoeli.

9Wana wa Shimei walikuwa watatu:

Shelomothi,23:9 Yaani Shelomithi; maana yake ni Mpenda amani. Hazieli na Harani.

Hawa watatu walikuwa viongozi wa jamaa za Ladani.

10Nao wana wa Shimei walikuwa wanne:

Yahathi, Zina,23:10 Tafsiri zingine zinamwita Ziza. Yeushi na Beria.

11Yahathi alikuwa wa kwanza na Ziza wa pili, lakini Yeushi na Beria hawakuwa na wana wengi; kwa hiyo walihesabiwa kama jamaa moja, wakapewa wajibu kwa pamoja.

Wakohathi

1223:12 Mwa 46:11; Kut 6:18-20; 1Nya 6:2Wana wa Kohathi walikuwa wanne:

Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.

1323:13 Kut 30:7-10; 28:1; Kum 21:5; Hes 6:23; 16:40; Ebr 5:4; Hes 16:40; 1Sam 2:28Wana wa Amramu walikuwa:

Aroni na Mose.

Aroni waliwekwa wakfu, yeye na wazao wake milele, wawe wakiweka wakfu vitu ambavyo ni vitakatifu mno, kutoa dhabihu mbele za Bwana, kuhudumu mbele zake na kutamka baraka katika Jina la Bwana milele. 1423:14 Kum 33:1Wana wa Mose mtu wa Mungu walihesabiwa kama sehemu ya kabila la Lawi.

1523:15 Kut 18:4; 2:22Wana wa Mose walikuwa:

Gershomu na Eliezeri.

1623:16 1Nya 26:24-28Wazao wa Gershomu:

Shebueli alikuwa wa kwanza.

17Wazao wa Eliezeri:

Rehabia alikuwa wa kwanza.

Eliezeri alikuwa na mwana mmoja tu, lakini wana wa Rehabia walikuwa wengi sana.

18Wana wa Ishari:

Shelomithi alikuwa wa kwanza.

1923:19 1Nya 24:23; 26:31Wana wa Hebroni walikuwa:

Yeria alikuwa wa kwanza, wa pili Amaria, wa tatu Yahazieli, na wa nne Yekameamu.

20Wana wa Uzieli walikuwa:

Mika wa kwanza na Ishia wa pili.

Wamerari

2123:21 1Nya 6:19; 24:26Wana wa Merari walikuwa:

Mahli na Mushi.

Wana wa Mahli walikuwa:

Eleazari na Kishi.

2223:22 Hes 36:6Eleazari akafa bila ya kuwa na wana: alikuwa na binti tu. Binamu zao, wana wa Kishi, wakawaoa.

2323:23 1Nya 24:30Wana wa Mushi:

Mahli, Ederi na Yeremothi; wote walikuwa watatu.

2423:24 Hes 4:3; 10:17-21Hawa walikuwa wazao wa Lawi kwa jamaa zao. Wakuu wa jamaa kama walivyoandikwa kwa majina yao na kuhesabiwa kila mmoja, yaani, wenye uwezo wa kufanya kazi kuanzia miaka ishirini au zaidi, waliohudumu katika Hekalu la Bwana. 25Kwa maana Daudi alikuwa amesema, “Kwa vile Bwana, Mungu wa Israeli amewapa watu wake raha na amekuja kuishi Yerusalemu milele, 26Walawi hawahitaji tena kubeba Maskani wala chombo chochote cha utumishi wake.” 27Kulingana na maagizo ya mwisho ya Daudi, Walawi waliohesabiwa ni wale wa kuanzia umri wa miaka ishirini au zaidi.

2823:28 Neh 13:9; Mal 3:3Wajibu wa Walawi ulikuwa kuwasaidia wazao wa Aroni kuhudumu katika Hekalu la Bwana: Kuwa wasimamizi wa nyua, vyumba vya pembeni, kutakasa vyombo vitakatifu na utendaji mwingine wowote katika nyumba ya Mungu. 2923:29 Kut 25:30; Law 2:4-7; 6:20-23; 19:35-36; 1Nya 9:29-32Walikuwa wasimamizi wa mikate iliyowekwa mezani, unga kwa ajili ya sadaka za nafaka, mikate isiyotiwa chachu, uokaji na uchanganyaji, pamoja na vipimo vyote vya wingi na ukubwa. 3023:30 1Nya 9:33; Ufu 5:8-14; 2Nya 31:2; 1Nya 6:31-33; Za 135:1-3; Ufu 14:3Pia ulikuwa wajibu wao kila asubuhi kumshukuru na kumsifu Bwana. Iliwapasa pia kufanya hivyo jioni 3123:31 2Fal 4:23; Law 23:4; Kol 2:16; Hes 10:10; Za 81:3; Isa 1:13-14na wakati wowote sadaka za kuteketezwa zilipotolewa kwa Bwana siku za Sabato na kwenye sikukuu za Mwezi Mwandamo na katika sikukuu nyingine zilizoamriwa. Iliwapasa kuhudumu mbele za Bwana mara kwa mara kwa idadi maalum na kwa namna waliyokuwa wamepewa maelekezo.

3223:32 Hes 1:53; 1Nya 6:48; Hes 3:6-8; 2Nya 31:2; Eze 44:14Hivyo Walawi wakafanya wajibu wao katika Hema la Kukutania, katika Mahali Patakatifu chini ya uongozi wa ndugu zao wazao wa Aroni, kwa ajili ya utumishi katika Hekalu la Bwana.

Japanese Contemporary Bible

歴代誌Ⅰ 23:1-32

23

レビ人の組み分け

1すっかり年老いたダビデはソロモンに王位を譲り、 2その即位式にイスラエルのすべての政治的、宗教的指導者を召集しました。 3レビ族で三十歳以上の男の人数を数えたところ、その合計は三万八千でした。

4-5ダビデはこのように指示しました。「そのうち、二万四千人は神殿の仕事を監督しなさい。六千人は管理者と裁判官、四千人は門衛となり、あとの四千人は私の作った楽器で主を賛美しなさい。」

6ダビデは彼らを、レビの三人の息子の名にちなんで、ゲルションの組、ケハテの組、メラリの組に分けました。

7ゲルションの組は、さらに二人の子の名にちなんで、ラダンの班とシムイの班に分けられました。 8-9その班がまた、ラダンとシムイの子たちの名にちなんで、六つのグループに分けられました。ラダンの子は、指導者エヒエル、ゼタム、ヨエル。シムイの子はシェロミテ、ハジエル、ハラン。

10-11シムイの各氏族には、四人の子の名がつけられました。長はヤハテで、次がジザ。エウシュとベリアは子どもが少なかったので、合わせて一つの氏族を構成しました。

12ケハテの組は、その子の名にちなんで、アムラム、イツハル、ヘブロン、ウジエルの四つの班に分けられました。

13アムラムはアロンとモーセの父です。アロンとその子たちは、人々のささげ物を主に奉納する奉仕に取り分けられました。アロンはいつも主に仕え、御名によって人々を祝福したからです。

14-15神の人モーセについて言えば、その子ゲルショムとエリエゼルはレビ族に入れられました。 16ゲルショムの子たちの長はシェブエルです。 17エリエゼルのひとり息子のレハブヤは子どもが大ぜいいたので、氏族の長となりました。

18イツハルの子たちの長はシェロミテ。

19ヘブロンの子たちの長はエリヤ。第二はアマルヤ、第三はヤハジエル、第四はエカムアム。

20ウジエルの子らの長はミカで、第二はイシヤ。

21メラリの子はマフリとムシ。マフリの子はエルアザルとキシュ。 22エルアザルには息子がなく、娘たちが、いとこに当たるキシュの息子たちと結婚しました。 23ムシの子はマフリ、エデル、エレモテ。

24人口調査の時、二十歳以上のレビ人はみな、以上の氏族やその一族に組み入れられ、神殿の奉仕を割り当てられました。 25ダビデがこう言ったからです。「イスラエルの神、主は平和を与えてくださった。これからは、主はエルサレムにお住みになる。 26レビ人はもう、幕屋や礼拝の器具をいちいち運ばなくてもよい。」

27このレビ族の人口調査は、ダビデが死ぬ前に行った最後のものでした。 28レビ人の仕事は、神殿でいけにえをささげるアロンの子孫である祭司を補佐することでした。また、神殿の管理に当たり、きよめの儀式を行う手伝いもしました。 29供えのパン、穀物のささげ物用の小麦粉、それにオリーブ油で揚げたり、オリーブ油を混ぜ合わせたりした、パン種(イースト菌)を入れない薄焼きのパンなどを用意しました。また、すべての物の重さや大きさをはかり、 30毎日、朝と夕方には、主の前に立って感謝をささげ、賛美しました。 31さらに、焼き尽くすいけにえ、安息日のいけにえ、新月の祝いや各種の例祭用のいけにえも用意しました。そのときに応じて必要な数のレビ人がこれに当たりました。 32彼らは幕屋や神殿の管理を行い、求められることは何でも行って、祭司たちを助けました。