1 Nyakati 16 – NEN & JCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Nyakati 16:1-43

Sanduku Lawekwa Ndani Ya Hema

116:1 2Sam 6:17-19Wakaleta Sanduku la Mungu na kuliweka ndani ya hema ambalo Daudi alikuwa amelisimamisha kwa ajili yake, na wakatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele za Mungu. 216:2 Kut 39:43; Hes 6:23-27Baada ya Daudi kumaliza kutoa hizo sadaka za kuteketezwa na hizo sadaka za amani, akawabariki watu katika jina la Bwana. 3Kisha akamgawia kila Mwisraeli mwanaume na mwanamke mkate, andazi la tende na andazi la zabibu kavu.

416:4 1Nya 15:1-2Akawaweka pia baadhi ya Walawi ili wahudumu mbele ya Sanduku la Bwana kufanya maombi, kumshukuru na kumsifu Bwana, Mungu wa Israeli: 5Asafu ndiye alikuwa mkuu wao, akisaidiwa na Zekaria, Yeieli, Shemiramothi, Yehieli, Matithia, Eliabu, Benaya, Obed-Edomu na Yeieli. Hawa ndio wangepiga zeze na vinubi, Asafu angepiga matoazi, 6nao Benaya na Yahazieli makuhani, ndio wangepiga tarumbeta mara kwa mara mbele ya Sanduku la Agano la Mungu.

Zaburi Ya Daudi Ya Shukrani

(Zaburi 105:1-15; 96:1-13; 106:1, 47-48)

716:7 2Sam 23:1; Za 47:7Siku ile, kitu cha kwanza Daudi alichofanya ni kumkabidhi Asafu na wenzake zaburi hii ya shukrani kwa Bwana:

816:8 Za 107:1; 118:1; 2Fal 19:19Mshukuruni Bwana, liitieni jina lake;

wajulisheni mataifa yale aliyoyatenda.

916:9 Za 100:1; Kut 15:1; Za 7:17; 95:1-2Mwimbieni yeye, mwimbieni yeye sifa;

waambieni matendo yake yote ya ajabu.

1016:10 Za 34:3; Isa 45:25Lishangilieni jina lake takatifu;

mioyo ya wale wamtafutao Bwana na ifurahi.

1116:11 Za 27:8; Mit 8:17; Amo 5:6-14Mtafuteni Bwana na nguvu zake;

utafuteni uso wake siku zote.

1216:12 Za 78:43; 103:2Kumbuka matendo ya ajabu aliyoyafanya,

miujiza yake na hukumu alizozitamka,

13enyi wazao wa Israeli mtumishi wake,

enyi wana wa Yakobo, wateule wake.

1416:14 Isa 29:9; 4:4Yeye ndiye Bwana Mungu wetu;

hukumu zake zimo duniani pote.

15Hulikumbuka agano lake milele,

neno ambalo aliamuru, kwa vizazi elfu,

1616:16 Mwa 17:2; Neh 9:8; Ebr 6:13-18; Za 105:8-10; Mwa 15:18; 26:3agano alilolifanya na Abrahamu,

kiapo alichomwapia Isaki.

1716:17 Mwa 35:9-12Alilithibitisha kwa Yakobo kuwa amri,

kwa Israeli liwe agano la milele:

1816:18 Mwa 13:14-17“Nitakupa wewe nchi ya Kanaani

kuwa sehemu utakayoirithi.”

1916:19 Mwa 34:30; Ebr 11:13; Kum 7:7Walipokuwa wachache kwa idadi,

wachache sana na wageni ndani yake,

20walitangatanga kutoka taifa moja hadi jingine,

kutoka ufalme mmoja hadi mwingine.

2116:21 Mwa 20:3; Kut 7:15-18; Za 9:5; Mwa 12:17Hakuruhusu mtu yeyote awaonee;

kwa ajili yao aliwakemea wafalme, akisema:

2216:22 Mwa 20:7; Za 105; 15; 1Yn 2:27“Msiwaguse niliowatia mafuta;

msiwadhuru manabii wangu.”

2316:23 Za 47:1; 96:1Mwimbieni Bwana dunia yote;

tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.

2416:24 Isa 12:4Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa,

matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.

2516:25 Za 18:3; 76:7; 89:7; Kut 18:11; Isa 40:25-26; Za 24:8Kwa kuwa Bwana ni mkuu,

mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote;

yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.

2616:26 Law 19:4; Isa 45:20; 1Kor 8:4; Za 115:4-8; Yer 10:3Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu,

lakini Bwana aliziumba mbingu.

27Fahari na enzi viko mbele yake;

nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.

2816:28 Za 29:1-2; 8:1Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa,

mpeni Bwana utukufu na nguvu,

29mpeni Bwana utukufu

unaostahili jina lake.

Leteni sadaka na mje katika nyua zake;

mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake.

3016:30 Za 2:11; 33:8Dunia yote na itetemeke mbele zake!

Ulimwengu ameuweka imara; hauwezi kusogezwa.

3116:31 Isa 44:23; 35:10; 49:13; Mao 5:19; Isa 52:7; Lk 2:13; Ufu 14:2Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi;

semeni katikati ya mataifa, “Bwana anatawala!”

3216:32 Kut 20:11; Za 98:7; 96:10Bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake;

mashamba na yashangilie, na vyote vilivyomo ndani yake.

3316:33 Isa 14:8; 55:12; Za 110:6Kisha miti ya msituni itaimba,

itaimba kwa furaha mbele za Bwana,

kwa maana anakuja kuihukumu dunia.

3416:34 Isa 12:4; Za 25:7; Ezr 3:11; Yer 33:1Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema;

upendo wake wadumu milele.

3516:35 Kum 32:15; Mik 7:7; Ezr 3:11; Yer 33:11; Za 106:47Mlilieni, “Ee Mungu Mwokozi wetu, tuokoe.

Tukusanye tena na utukomboe kutoka kwa mataifa,

ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu,

na kushangilia katika sifa zako.”

3616:36 Kum 27:15; 1Fal 8:15; Neh 8:6; 10:27; 2Nya 8:14; Za 72:18-19Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli,

tangu milele na hata milele.

Nao watu wote wakasema, “Amen,” na “Msifuni Bwana.”

37Daudi akamwacha Asafu na wenzake mbele ya Sanduku la Agano la Bwana ili wahudumu humo mara kwa mara, kulingana na mahitaji ya kila siku. 3816:38 1Nya 13:13; 26:4-10Pia akamwacha Obed-Edomu pamoja na wenzake sitini na wanane wahudumu pamoja nao. Obed-Edomu mwana wa Yeduthuni na pia Hosa walikuwa mabawabu wa lango.

3916:39 1Sam 2:35; 1Nya 21:29; 2Sam 8:17; Yos 9:3; 1Fal 3:4Daudi akamwacha kuhani Sadoki pamoja na makuhani wenzake mbele ya hema ya ibada ya Bwana katika mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni 4016:40 Kut 29:38; Hes 28:1-8ili kutoa sadaka za kuteketezwa kwa Bwana kwenye madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa mara kwa mara, asubuhi na jioni, sawasawa na kila kitu kilichoandikwa katika sheria ya Bwana ambayo alikuwa amempa Israeli. 4116:41 1Nya 15:19; 2Nya 5:13; Yak 5:11; Ezr 3:11; Neh 9:17; Za 25:10; 33:5; Yer 33:11; Yoe 2:13; Lk 3:36Waliohudumu pamoja nao walikuwa Hemani, Yeduthuni na wale wote waliochaguliwa na kutajwa kwa jina kumpa Bwana shukrani, “Kwa maana fadhili zake zadumu milele.” 4216:42 2Nya 7:6Hemani na Yeduthuni walikuwa na wajibu wa kupiga tarumbeta, matoazi na kutumia vyombo vingine kwa ajili ya nyimbo za sifa kwa Mungu. Wana wa Yeduthuni waliwekwa langoni.

4316:43 2Sam 6:19-20; Mwa 18:19; Yos 24:15Kisha watu wote wakaondoka, kila mmoja akarudi nyumbani kwake, naye Daudi akarudi nyumbani kuibariki jamaa yake.

Japanese Contemporary Bible

歴代誌Ⅰ 16:1-43

16

神の箱の前での奉仕

1こうして神の箱は、ダビデがあらかじめ用意しておいた幕屋に運び込まれました。イスラエルの指導者たちは、神の前に、焼き尽くすいけにえと和解のいけにえをささげました。 2いけにえをささげ終わると、ダビデは主の名によって民を祝福し、 3集まっていた全員にパンとぶどう酒と干しぶどうの菓子を配りました。

4また、レビ人の中から、契約の箱の前で仕える者を選び、イスラエルの神、主を絶えず覚えて感謝し、ほめたたえ、そして民への祝福を祈り求めるようにさせました。この務めに任じられたのは次の人々です。 5かしらはアサフで、彼はシンバルを鳴らし、彼の同僚には、ゼカリヤ、エイエル、シェミラモテ、エヒエル、マティテヤ、エリアブ、ベナヤ、オベデ・エドム、エイエルがいて、みな十弦の琴と竪琴を弾きました。 6祭司のベナヤとヤハジエルは、契約の箱の前で決まった時間にラッパを吹き鳴らしました。

7この時からダビデ王は、幕屋での主への賛美にアサフの指揮する祭司の合唱隊を用い始めたのです。

8彼らは歌いました。

「さあ、主に感謝し、主に祈れ。

世界の人々に、偉大なみわざを伝えよ。

9主をたたえ、そのすばらしいみわざを告げ知らせよ。

10主の聖なる名を誇れ。

主を慕い求める者すべてを喜ばせよ。

11主とその御力とを尋ね求めよ。

絶えず御顔を慕い求めよ。

12-13主のしもべアブラハムの子孫よ。

主に選ばれたヤコブの子らよ。

偉大なみわざと、驚くべき奇跡と御力とを思い起こせ。

14このお方こそ、私たちの神、主!

その御力は全世界にわたる。

15主の契約を、いつまでも忘れるな。

そのことばは千代にも及ぶ。

16主はアブラハムと契約を結び、

イサクに誓いを立て、

17ヤコブにも確証して、

イスラエルへの永遠の契約とされた。

18『あなたがたの相続地として

カナンの地を与える。』

19その時、イスラエルの数はごくわずかで、

しかも、約束の地では外国人であった。

20彼らは、国から国へと渡り歩いた。

21神はだれにも手を出すことを許さず、

彼らを害する者は、たとえ王でも殺された。

22『わたしが選んだ民を害するな。

わたしの預言者だから、ふれてはいけない。』

23全地よ、主に歌え。

日ごと、主が救い主であることを宣べ伝えよ。

24主の栄光を国々に知らせ、

すばらしいみわざを、すべての人に語り告げよ。

25主は偉大で、高らかにほめたたえられるべきお方、

すべての神々にまさって恐れられるべきお方。

26他国で、神々と呼ばれるものはみな悪霊で

主こそが天をお造りになった。

27尊厳と栄誉は御前にあり、

力と歓喜はみそばにある。

28国々の民よ、

主の大いなる力と栄光とをたたえよ。

29御名にふさわしく、ほめたたえよ。

ささげ物を携えて、御前に出よ。

聖なる衣を着けて、主を礼拝せよ。

30全地よ、主の御前におののけ。

世界はびくとも動じない。

31天は喜び、地は楽しめ。

諸国の民は言え。『主が王である』と。

32大海は鳴りとどろけ。

野とその中にあるものは喜び躍れ。

33森の木々も、主の御前で喜び歌え。

主が地をさばきに来られるからだ。

34主に感謝せよ。

その恵みは深く、愛といつくしみは限りない。

35主に叫べ。

『私たちの救いの神よ、どうかお救いください。

私たちを国々から呼び集め、

安全に救い出してください。

そうすれば、あなたのきよい御名に感謝し、

声の限りほめたたえます。』

36イスラエルの神は、永遠にほむべきかな。」

この歌にすべての民は「アーメン」と和し、主をほめたたえました。

37ダビデは、レビ人のアサフと同僚たちを幕屋で仕えさせ、毎日の日課として決められたことを規則正しく行わせました。 38この中には、エドトンの子オベデ・エドム、ホサ、同じ門衛の六十八人がいました。

39一方、ギブオンの丘にある古い幕屋も、そのままになっていました。ダビデは、そこで祭司ツァドクと同僚の祭司たちを仕えさせました。 40彼らは、主がイスラエルに命じられたとおり、毎朝毎夕、焼き尽くすいけにえを祭壇の上でささげました。 41王はまた、絶えず注がれる主の愛と恵みに感謝をささげる務めに、ヘマンとエドトンをはじめ数人の者を指名しました。 42彼らはラッパを吹き、シンバルを鳴らし、合唱隊に合わせて、高らかに主をほめたたえました。エドトンの子らは門衛に任じられました。

43祝いが終わり、民がそれぞれ自分の家へ帰って行ったので、ダビデも家族を祝福するために戻って行きました。