1 Nyakati 15 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Nyakati 15:1-29

Sanduku La Agano Laletwa Yerusalemu

(2 Samweli 6:12-22)

115:1 Za 132:1-5; 2Sam 6:17; 1Nya 17:1-5; Mdo 7:46Baada ya Daudi kujijengea nyumba zake katika Mji wa Daudi, akatengeneza sehemu kwa ajili ya Sanduku la Mungu, kisha akasimamisha hema kwa ajili yake. 215:2 Hes 3:6; Kum 31:9, 25; 2Nya 29:11; Hes 4:2, 15; Kum 10:5; Yos 3:3Kisha Daudi akasema, “Hakuna mtu yeyote anayeruhusiwa kulibeba Sanduku la Mungu isipokuwa Walawi peke yao, kwa sababu Bwana aliwachagua kulibeba Sanduku la Bwana na kuhudumu mbele zake milele.”

315:3 1Nya 13:5; 1Fal 8:1Daudi akawakusanya Israeli wote huko Yerusalemu ili kulipandisha Sanduku la Bwana na kulileta hadi kwenye sehemu aliyokuwa ametengeneza kwa ajili yake. 4Kisha Daudi akawakusanya pamoja wazao wa Aroni na Walawi:

515:5 Kut 6:16-18Kutoka wazao wa Kohathi,

Urieli kiongozi na ndugu zake 120,

6Kutoka wazao wa Merari,

Asaya kiongozi na ndugu zake 220.

7Kutoka wazao wa Gershoni,15:7 Namna nyingine ya kutaja Gershomu.

Yoeli kiongozi na ndugu zake 130.

815:8 Kut 6:22Kutoka wazao wa Elisafani,

Shemaya kiongozi na ndugu zake 200.

915:9 Hes 26:58; Kut 6:18Kutoka wazao wa Hebroni,

Elieli kiongozi na ndugu zake 80.

10Kutoka wazao wa Uzieli,

Aminadabu kiongozi na ndugu zake 112.

1115:11 1Nya 12:28; 1Sam 22:20Kisha Daudi akawaita makuhani Sadoki na Abiathari, pamoja na Walawi Urieli, Asaya, Yoeli, Shemaya, Elieli na Aminadabu. 1215:12 Kut 29:10; Law 11:44; Eze 48:11; Yn 17:17; Law 10:3; 2Nya 5:11; 29:5, 15; Rum 12:1-2Akawaambia, “Ninyi ndio viongozi wa jamaa za Walawi. Ninyi pamoja na Walawi wenzenu inawapasa mjitakase na kulipandisha Sanduku la Bwana, Mungu wa Israeli hadi mahali ambapo nimetengeneza kwa ajili yake. 1315:13 1Fal 8:4; 2Sam 6:3; 1Nya 13:11Ilikuwa ni kwa sababu hii, ninyi Walawi, hamkulipandisha Sanduku la Bwana mara ya kwanza, hata ikasababisha Bwana Mungu wetu kuwaka hasira dhidi yetu. Hatukumuuliza jinsi ya kufanya ili tupate kulileta jinsi alivyoagiza.” 14Kwa hiyo makuhani pamoja na Walawi wakajitakasa ili kulipandisha Sanduku la Bwana, Mungu wa Israeli. 1515:15 Kut 25:14; Hes 4:5-15Nao Walawi wakalichukua Sanduku la Mungu mabegani mwao wakitumia mipiko, kama vile Mose alivyoamuru sawasawa na neno la Bwana.

1615:16 Ezr 2:41; Neh 11:23; Amo 6:5; Ay 21:12; Za 68:25; 1Nya 6:31; 13:8; Za 33:2Daudi akawaambia viongozi wa Walawi kuwaweka ndugu zao waimbaji ili waimbe nyimbo za shangwe, wakiwa na vyombo vya uimbaji: zeze, vinubi na matoazi.

1715:17 1Nya 6:33-44Basi Walawi wakawaweka Hemani mwana wa Yoeli; kutoka miongoni mwa ndugu zake, Asafu mwana wa Berekia; kutoka miongoni mwa ndugu zao Wamerari, Ethani mwana wa Kushaiya; 1815:18 2Sam 6:10; 1Nya 26:4-5hawa ndio waliochaguliwa kuwa wasaidizi wao: Zekaria, Yaazieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni, Eliabu, Benaya, Maaseya, Matithia, Elifelehu, Mikneya, pamoja na mabawabu Obed-Edomu na Yehieli.

1915:19 1Nya 16:12-13; 29:26Waimbaji Hemani, Asafu na Ethani walichaguliwa kupiga matoazi ya shaba; 20Zekaria, Azieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni, Eliabu, Maaseya na Benaya walikuwa wapiga zeze kufuatana na sauti ya alamothi,15:20 Huenda ni aina ya uimbaji. 21na Matithia, Elifelehu, Mikneya, Obed-Edomu, Yehieli na Azazia walikuwa wapiga vinubi, wakiongozwa kwa kufuata sauti ya sheminithi.15:21 Huenda ni aina ya uimbaji. 22Kenania kiongozi wa Walawi alikuwa msimamizi wa uimbaji; huu ndio uliokuwa wajibu wake kwa sababu alikuwa stadi katika hilo.

23Berekia na Elikana walikuwa mabawabu kwa ajili ya Sanduku. 2415:24 2Nya 5:12; Hes 10:8; 2Nya 29:26; Za 81:3Shebania, Yoshafati, Nethaneli, Amasai, Zekaria, Benaya na Eliezeri, makuhani, walikuwa wapiga tarumbeta mbele ya Sanduku la Mungu. Obed-Edomu na Yehiya waliwekwa pia kuwa mabawabu wa Sanduku.

2515:25 2Sam 16:12-13; 2Nya 5:2; Yer 3:16; Kum 12:7, 18; Ezr 6:16Basi Daudi pamoja na wazee wa Israeli na majemadari wa vikosi vya elfu wakaenda ili kulipandisha Sanduku la Agano la Bwana kutoka nyumba ya Obed-Edomu kwa shangwe. 2615:26 Ay 42:8; Hes 23:1-4, 29Kwa sababu Mungu alikuwa amewasaidia Walawi waliokuwa wanalichukua Sanduku la Agano la Bwana, mafahali saba na kondoo dume saba walitolewa dhabihu. 27Basi Daudi alikuwa amevaa joho la kitani safi, kama walivyokuwa wamevaa Walawi wote waliokuwa wanalichukua lile Sanduku, waimbaji nao walivaa vivyo hivyo, pamoja na Kenania aliyekuwa anaongoza nyimbo za waimbaji. Daudi alivaa pia kisibau cha kitani safi. 2815:28 Kut 19:13; 1Nya 13:8Hivyo Israeli wote wakalipandisha Sanduku la Agano la Bwana kwa shangwe, wakipiga pembe za kondoo dume, tarumbeta, matoazi, wakipiga zeze na vinubi.

2915:29 2Sam 6:16; Mdo 2:13Sanduku la Agano la Bwana lilipokuwa linaingia katika Mji wa Daudi, Mikali binti Sauli akachungulia dirishani. Naye alipomwona Mfalme Daudi akicheza na kusherehekea, akamdharau moyoni mwake.

New International Version

1 Chronicles 15:1-29

The Ark Brought to Jerusalem

1After David had constructed buildings for himself in the City of David, he prepared a place for the ark of God and pitched a tent for it. 2Then David said, “No one but the Levites may carry the ark of God, because the Lord chose them to carry the ark of the Lord and to minister before him forever.”

3David assembled all Israel in Jerusalem to bring up the ark of the Lord to the place he had prepared for it. 4He called together the descendants of Aaron and the Levites:

5From the descendants of Kohath,

Uriel the leader and 120 relatives;

6from the descendants of Merari,

Asaiah the leader and 220 relatives;

7from the descendants of Gershon,15:7 Hebrew Gershom, a variant of Gershon

Joel the leader and 130 relatives;

8from the descendants of Elizaphan,

Shemaiah the leader and 200 relatives;

9from the descendants of Hebron,

Eliel the leader and 80 relatives;

10from the descendants of Uzziel,

Amminadab the leader and 112 relatives.

11Then David summoned Zadok and Abiathar the priests, and Uriel, Asaiah, Joel, Shemaiah, Eliel and Amminadab the Levites. 12He said to them, “You are the heads of the Levitical families; you and your fellow Levites are to consecrate yourselves and bring up the ark of the Lord, the God of Israel, to the place I have prepared for it. 13It was because you, the Levites, did not bring it up the first time that the Lord our God broke out in anger against us. We did not inquire of him about how to do it in the prescribed way.” 14So the priests and Levites consecrated themselves in order to bring up the ark of the Lord, the God of Israel. 15And the Levites carried the ark of God with the poles on their shoulders, as Moses had commanded in accordance with the word of the Lord.

16David told the leaders of the Levites to appoint their fellow Levites as musicians to make a joyful sound with musical instruments: lyres, harps and cymbals.

17So the Levites appointed Heman son of Joel; from his relatives, Asaph son of Berekiah; and from their relatives the Merarites, Ethan son of Kushaiah; 18and with them their relatives next in rank: Zechariah,15:18 Three Hebrew manuscripts and most Septuagint manuscripts (see also verse 20 and 16:5); most Hebrew manuscripts Zechariah son and or Zechariah, Ben and Jaaziel, Shemiramoth, Jehiel, Unni, Eliab, Benaiah, Maaseiah, Mattithiah, Eliphelehu, Mikneiah, Obed-Edom and Jeiel,15:18 Hebrew; Septuagint (see also verse 21) Jeiel and Azaziah the gatekeepers.

19The musicians Heman, Asaph and Ethan were to sound the bronze cymbals; 20Zechariah, Jaaziel,15:20 See verse 18; Hebrew Aziel, a variant of Jaaziel. Shemiramoth, Jehiel, Unni, Eliab, Maaseiah and Benaiah were to play the lyres according to alamoth,15:20 Probably a musical term 21and Mattithiah, Eliphelehu, Mikneiah, Obed-Edom, Jeiel and Azaziah were to play the harps, directing according to sheminith.15:21 Probably a musical term 22Kenaniah the head Levite was in charge of the singing; that was his responsibility because he was skillful at it.

23Berekiah and Elkanah were to be doorkeepers for the ark. 24Shebaniah, Joshaphat, Nethanel, Amasai, Zechariah, Benaiah and Eliezer the priests were to blow trumpets before the ark of God. Obed-Edom and Jehiah were also to be doorkeepers for the ark.

25So David and the elders of Israel and the commanders of units of a thousand went to bring up the ark of the covenant of the Lord from the house of Obed-Edom, with rejoicing. 26Because God had helped the Levites who were carrying the ark of the covenant of the Lord, seven bulls and seven rams were sacrificed. 27Now David was clothed in a robe of fine linen, as were all the Levites who were carrying the ark, and as were the musicians, and Kenaniah, who was in charge of the singing of the choirs. David also wore a linen ephod. 28So all Israel brought up the ark of the covenant of the Lord with shouts, with the sounding of rams’ horns and trumpets, and of cymbals, and the playing of lyres and harps.

29As the ark of the covenant of the Lord was entering the City of David, Michal daughter of Saul watched from a window. And when she saw King David dancing and celebrating, she despised him in her heart.