1 Nyakati 13 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Nyakati 13:1-14

Kurudishwa Kwa Sanduku La Mungu

(2 Samweli 6:1-11)

113:1 1Nya 12:14; Za 132:1; Mit 15:22Daudi alishauriana na kila afisa wake, majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia. 213:2 1Nya 10:7; Isa 37:4Ndipo Daudi akaliambia kusanyiko lote la Israeli, “Kama mkiona ni vyema, na kama ni mapenzi ya Bwana Mungu wetu, tupeleke ujumbe kwa ndugu zetu wengine walio mbali na walio karibu katika nchi yote ya Israeli, pia kwa makuhani na Walawi walio pamoja nao katika miji yao na katika sehemu zao za malisho yao, waje waungane na sisi. 313:3 1Sam 7:1-2; 2Nya 1:5; 1Sam 23:2-4Sisi na tulirudishe Sanduku la Mungu wetu kwetu kwa maana hatukujali wakati wa utawala wa Sauli.” 4Kusanyiko lote likakubaliana kufanya hivyo, kwa sababu ilionekana vyema kwa watu wote.

513:5 1Nya 11:1; 15:3; Yos 13:3; Hes 13:21; 1Sam 6:21; 7:2Basi Daudi akawakusanya Waisraeli wote, kuanzia Mto Shihori ulioko Misri hadi Lebo-Hamathi, ili kulileta Sanduku la Mungu kutoka Kiriath-Yearimu. 613:6 Yos 15:9; 2Sam 6:2; Kut 25:22; 2Fal 19:15; 1Sam 4:4Daudi akiwa pamoja na Waisraeli wote wakaenda Baala ya Yuda (yaani Kiriath-Yearimu) kulipandisha Sanduku la Mungu Bwana, yeye anayeketi katika kiti cha enzi kati ya makerubi: Sanduku linaloitwa kwa Jina lake, kutoka huko.

713:7 Hes 4:15; 1Sam 7:1Wakalisafirisha Sanduku la Mungu kwa gari jipya la kukokotwa na maksai kutoka nyumba ya Abinadabu, Uza na Ahio wakiliongoza gari hilo. 813:8 2Sam 6:5; Za 92:3Daudi pamoja na Waisraeli wote walikuwa wanasifu kwa nguvu zao zote mbele za Mungu, kwa nyimbo na kwa vinubi, zeze, matari, matoazi na tarumbeta.

913:9 2Sam 6:6Walipofika kwenye uwanja wa kupuria nafaka wa Kidoni, Uza akaunyoosha mkono wake ili kulizuia Sanduku, kwa sababu maksai walijikwaa. 1013:10 1Nya 15:13, 15; Law 10:2; Hes 4:15Hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya Uza, akampiga kwa sababu aliuweka mkono wake kwenye Sanduku. Kwa hiyo akafa pale mbele za Mungu.

1113:11 1Nya 15:13; Za 7:11Ndipo Daudi akakasirika kwa sababu ghadhabu ya Bwana ilifurika dhidi ya Uza, mahali pale pakaitwa Peres-Uza13:11 Maana yake ni Gadhabu dhidi ya Uza. hadi leo.

12Siku ile Daudi akamwogopa Mungu naye akauliza. “Nitawezaje kulichukua Sanduku la Mungu kwangu?” 1313:13 1Nya 15:18, 24; 16:38; 26:4-5, 15Hakulichukua hilo Sanduku akae nalo katika Mji wa Daudi. Badala yake, akalipeleka nyumbani kwa Obed-Edomu, Mgiti. 1413:14 2Sam 6:11; 1Nya 26:4-5; Mwa 30:27; 39:5; 1Nya 26:5; Za 37:22; Mit 3:9; 10:22; Mal 3:10Sanduku la Mungu likabaki pamoja na jamaa ya Obed-Edomu, nyumbani kwake kwa miezi mitatu, naye Bwana akaibariki nyumba yake pamoja na kila kitu alichokuwa nacho.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

历代志上 13:1-14

运回约柜

1大卫跟千夫长、百夫长等所有的首领商议, 2然后对以色列全体会众说:“如果你们赞成,而且这是我们上帝耶和华的旨意,我们就派人到以色列各地把其他同胞,包括住在城邑及草场的祭司和利未人召集来。 3我们要将我们上帝的约柜运到这里来,因为在扫罗执政期间,我们忽视了它。” 4会众都表示赞同,认为这样做很好。

5于是,大卫召集了从埃及西曷河一直到哈马口的全体以色列人,要将上帝的约柜从基列·耶琳运来。 6大卫率领以色列众人到巴拉,即犹大基列·耶琳,要将上帝的约柜运回来。这约柜以坐在基路伯天使上面的耶和华的名字命名。 7他们把上帝的约柜从亚比拿达家抬出来,放在一辆新车上,由乌撒亚希约赶车。 8大卫以色列众人就在上帝面前用琴、瑟、鼓、钹和号奏乐,尽情歌舞。 9他们来到基顿麦场的时候,拉车的牛失蹄,乌撒就伸手去扶约柜。 10因他伸手碰了约柜,上帝便向他发怒,击杀了他,他就死在上帝面前。 11大卫因耶和华击杀乌撒而烦恼,就称那地方为毗列斯·乌撒13:11 毗列斯·乌撒”意思是“向乌撒发怒”。,沿用至今。 12那天,大卫惧怕上帝,他说:“我怎能将上帝的约柜运到我这里?” 13因此,大卫没有将约柜运到大卫城,而是把它运到迦特俄别·以东家。 14上帝的约柜在俄别·以东家存放了三个月。耶和华使俄别·以东家及其拥有的一切都蒙福。