الْمَزْمُورُ الأَرْبَعُونَ
لِقَائِدِ الْمُنْشِدِينَ، مَزْمُورٌ لِدَاوُدَ
1انْتَظَرْتُ الرَّبَّ صَابِراً، فَالْتَفَتَ إِلَيَّ وَسَمِعَ صُرَاخَ اسْتِغَاثَتِي، 2وَانْتَشَلَنِي مِنْ هُوَّةِ الْهَلاكِ، مِنْ طِينِ الْمُسْتَنْقَعِ. وَأَوْقَفَ قَدَمَيَّ عَلَى أَرْضٍ صَخْرِيَّةٍ، فَصِرْتُ أَمْشِي بِخُطُوَاتٍ ثَابِتَةٍ. 3وَضَعَ فِي فَمِي تَرْنِيمَةً جَدِيدَةً، قَصِيدَةَ تَسْبِيحٍ لإِلَهِنَا. يَرَى ذَلِكَ كَثِيرُونَ فَيَخَافُونَ الرَّبَّ.
4طُوبَى لِرَجُلٍ وَضَعَ فِي الرَّبِّ ثِقَتَهُ، وَلَمْ يَلْتَفِتْ إِلَى الْمُتَكَبِّرِينَ وَالْمُنْحَرِفِينَ إِلَى الْكَذِبِ. 5أَيُّهَا الرَّبُّ إِلَهِي، مَا أَكْثَرَ أَعْمَالَكَ الْعَجِيبَةَ! إِنْ تَحَدَّثْتُ عَنْ خُطَطِكَ الرَّائِعَةِ لَنَا فَلَنْ أَقْدِرَ أَنْ أُحْصِيَهَا. زَادَتْ عَنْ أَنْ تُعَدَّ. 6لَمْ تُرِدْ أَوْ تَطْلُبْ ذَبَائِحَ وَمُحْرَقَاتٍ عَنِ الْخَطِيئَةِ، لَكِنَّكَ وَهَبْتَنِي أُذُنَيْنِ مُصْغِيَتَيْنِ مُطِيعَتَيْنِ. 7عِنْدَئِذٍ قُلْتُ: «هَا أَنَا أَجِيءُ، كَمَا هُوَ مَكْتُوبٌ عَنِّي فِي دَرْجِ الْكِتَابِ: 8إِنَّ مَسَرَّتِي أَنْ أَعْمَلَ مَشِيئَتَكَ الصَّالِحَةَ يَا إِلَهِي، وَشَرِيعَتُكَ فِي صَمِيمِ قَلْبِي. 9أَعْلَنْتُ بِرَّكَ وَسَطَ جَمَاعَةِ شَعْبِكَ الْعَظِيمِ، وَأَنْتَ يَا رَبُّ عَلِمْتَ أَنَّنِي لَمْ أُلْجِمْ شَفَتَيَّ. 10لَمْ أُخْفِ بِرَّكَ دَاخِلَ قَلْبِي، بَلْ أَعْلَنْتُ أَمَانَتَكَ وَخَلاصَكَ. لَمْ أَكْتُمْ رَحْمَتَكَ وَحَقَّكَ عَنْ جَمَاعَةِ شَعْبِكَ الْعَظِيمِ».
11فَأَنْتَ يَا رَبُّ لَنْ تَمْنَعَ مَرَاحِمَكَ عَنِّي. تَنْصُرُنِي دَائِماً رَحْمَتُكَ وَحَقُّكَ. 12إِنَّ شُرُوراً لَا تُحْصَى قَدْ أَحَاطَتْ بِي، وَآثَامِي قَدْ أَطْبَقَتْ عَلَيَّ فَأَعْمَتْنِي لأَنَّهَا أَكْثَرُ مِنْ شَعْرِ رَأْسِي، وَقَلْبِي قَدْ خَذَلَنِي. 13يَا رَبُّ، ارْتَضِ أَنْ تُنَجِّيَنِي. أَسْرِعْ يَا رَبُّ لإِغَاثَتِي. 14لِيَخْزَ وَلْيَخْجَلْ مَعاً الَّذِينَ يَسْعَوْنَ إِلَى قَتْلِي. لِيُدْبِرْ وَلْيَخْزَ الْمَسْرُورُونَ بِأَذِيَّتِي. 15لِيَذْهَلْ خِزْياً السَّاخِرُونَ مِنِّي. 16وَلْيَفْرَحْ وَيَبْتَهِجْ بِكَ جَمِيعُ طَالِبِيكَ، وَلْيَقُلْ كُلَّ حِينٍ مُحبُّو خَلاصِكَ: «يَتَعَظَّمُ الرَّبُّ». 17أَمَّا أَنَا فَمِسْكِينٌ وَبَائِسٌ. الرَّبُّ يَهْتَمُّ بِي. عَوْنِي وَمُنْقِذِي أَنْتَ. فَلَا تَتَوَانَ يَا إِلَهِي.
Zaburi 40
Wimbo Wa Sifa
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.
140:1 Za 37:7; 116:1; 6:9; 31:22; 34:15; 7:15; 145:19Nilimngoja Bwana kwa saburi,
naye akaniinamia, akasikia kilio changu.
240:2 Ay 9:31; 30:19; Za 7:15; 69:14; 31:8; 27:5Akanipandisha kutoka shimo la uharibifu,
kutoka matope na utelezi;
akaiweka miguu yangu juu ya mwamba
na kunipa mahali imara pa kusimama.
340:3 Za 28:7; 52:6; 64:9; Ufu 5:9; Kut 14:31Akaweka wimbo mpya kinywani mwangu,
wimbo wa sifa kwa Mungu wetu.
Wengi wataona na kuogopa
na kuweka tumaini lao kwa Bwana.
440:4 Za 2:12; 34:8; 84:12; 101:5; 4:2; 138:6; Kum 31:20; Mit 3:34; 16:5; Isa 65:5; 1Pet 5:5Heri mtu yule amfanyaye Bwana kuwa tumaini lake,
asiyewategemea wenye kiburi,
wale wenye kugeukia miungu ya uongo.
540:5 Kum 4:34; Isa 55:8; Za 75:1; 105:5; 136:4; 139:18; 71:15; 139:15Ee Bwana Mungu wangu,
umefanya mambo mengi ya ajabu.
Mambo uliyopanga kwa ajili yetu
hakuna awezaye kukuhesabia;
kama ningesema na kuyaelezea,
yangekuwa mengi mno kuyaelezea.
640:6 1Sam 15:22; Isa 1:11; Hos 6:6; Yer 6:20; Mt 9:13; Amo 5:22; Kut 21:6; Za 50:8; 51:16Dhabihu na sadaka hukuvitaka,
lakini umefungua masikio yangu;40:6 Au: bali mwili uliniandalia.
sadaka za kuteketezwa na sadaka za dhambi
hukuzihitaji.
740:7 Ay 19:23; Yn 5:39; Yer 36:2; 45:1; Eze 2:9; Lk 24:44; Mdo 10:43; Ebr 10:7Ndipo niliposema, “Mimi hapa, nimekuja:
imeandikwa kunihusu katika kitabu.
840:8 Mt 26:39; Yn 4:34; Ebr 10:5-7; Kum 6:6; Yer 15:16; Rum 7:22; Ay 22:22; 23:12Ee Mungu wangu,
natamani kuyafanya mapenzi yako;
sheria yako iko ndani ya moyo wangu.”
940:9 Za 22:25, 31; 139:2; Yos 22:22Nimehubiri haki katika kusanyiko kubwa,
sikufunga mdomo wangu,
Ee Bwana, kama ujuavyo.
1040:10 Za 89:1; 22:22; Mdo 20:20; Flp 3:9; Rum 1:16, 17Sikuficha haki yako moyoni mwangu;
ninasema juu ya uaminifu wako na wokovu wako.
Sikuficha upendo wako na kweli yako
mbele ya kusanyiko kubwa.
1140:11 Zek 1:12; Za 26:3; 61:7; 43:3; Mit 20:28Ee Bwana, usizuilie huruma zako,
upendo wako na kweli yako daima vinilinde.
1240:12 Za 25:17; 38:4; 65:3; 69:4; 73:26Kwa maana taabu zisizo na hesabu zimenizunguka,
dhambi zangu zimenikamata, hata nisiweze kuona.
Zimekuwa nyingi kuliko nywele za kichwa changu,
nao moyo unazimia ndani yangu.
1340:13 Za 22:19; 38:22Ee Bwana, uwe radhi kuniokoa;
Ee Bwana, njoo hima unisaidie.
1440:14 1Sam 20:1; Es 9:2; Za 35:26; 35:4Wote wanaotafuta kuuondoa uhai wangu,
waaibishwe na kufadhaishwa;
wote wanaotamani kuangamizwa kwangu,
warudishwe nyuma kwa aibu.
1540:15 Za 35:21Wale waniambiao, “Aha! Aha!”
wafadhaishwe na iwe aibu yao.
1640:16 Kum 4:29; 1Nya 28:9; Za 9:10; 119:2; 9:2; 35:27Lakini wote wakutafutao
washangilie na kukufurahia,
wale wapendao wokovu wako siku zote waseme,
“Bwana atukuzwe!”
1740:17 Neh 5:19; Mk 10:21; Za 86:1; 109:22; 144:3; 20:2; 18:2; 119:60Lakini bado mimi ni maskini na mhitaji;
Bwana na anifikirie.
Wewe ndiwe msaada wangu na Mwokozi wangu;
Ee Mungu wangu, usikawie.