이사야 51 – KLB & NEN

Korean Living Bible

이사야 51:1-23

예루살렘에 대한 위로의 말씀

1여호와께서 말씀하신다. “의를 추구하며 나 여호와를 찾는 자들아, 내 말을 들어라. 너희를 떠낸 반석과 너희를 파낸 51:1 또는 ‘우묵한 구덩이를’채석장을 생각해 보아라.

2너희 조상 아브라함과 너희를 낳은 사라를 생각해 보아라. 내가 아브라함을 부를 때 그에게는 자식이 없었지만 내가 그를 축복하여 그에게 자식을 주고 그 후손들을 번성하게 하였다.

3나 여호와가 이스라엘을 다시 축복하여 그 황폐한 땅을 에덴처럼 만들고 그 사막을 내 동산처럼 만들 것이니 이 땅에 기쁨과 즐거움이 있고 감사와 찬송이 있을 것이다.

4“내 백성아, 나에게 귀를 기울여 내가 하는 말을 들어라. 율법이 나에게서 나올 것이며 51:4 또는 ‘내 공의가’나의 의로운 진리가 만민의 빛이 될 것이다.

5구원의 때가 가까웠으므로 내가 속히 가서 그들을 구원하겠다. 내가 만민을 심판할 것이니 모든 51:5 원문에는 ‘섬들이’민족이 나를 바라보며 내가 구원해 주기를 기다릴 것이다.

6너희는 눈을 들어 하늘을 보고 그 아래 땅을 살펴보아라. 하늘이 연기처럼 사라지고 땅이 낡은 옷처럼 해어질 것이며 세상 사람들이 하루살이처럼 죽게 될 것이다. 그러나 내 구원은 영원하며 나의 의는 쇠하지 않을 것이다.

7“옳은 것이 무엇인지 아는 자들아, 마음 가운데 내 율법을 간직한 사람들아, 너희는 내 말을 들어라. 사람들이 너희를 조롱하고 비웃어도 너희는 두려워하거나 놀라지 말아라.

8그들은 옷처럼 좀에게 먹히고 양털처럼 벌레에게 먹힐 것이다. 그러나 나의 의는 영원히 지속되며 나의 구원은 대대에 미칠 것이다.”

9여호와여, 깨어 우리를 도우소서. 옛날처럼 주의 능력으로 우리를 구하소서. 나일강의 용과 같은 이집트를 난도질하신 분이 주가 아니십니까?

10바닷물을 말리시고 바다 깊은 곳에 길을 만들어 구출하신 자들을 건너가게 하신 분도 주가 아니었습니까?

11주께서 구출하신 자들이 노래하며 예루살렘으로 돌아와 영원한 기쁨과 즐거움을 누릴 것이니 슬픔과 탄식은 사라질 것입니다.

12여호와께서 말씀하신다. “너희를 위로하는 자는 나인데 어째서 너희는 풀잎에 불과한 죽을 인간을 두려워하느냐?

13너희는 어째서 하늘을 펼치고 땅의 기초를 놓은 너희 창조자, 나 여호와를 잊어버리고 너희를 괴롭히며 너희를 파멸시키려고 하는 자들의 분노를 항상 두려워하며 사느냐? 그들의 분노가 어디 있느냐?

14사로잡힌 자들이 곧 풀려 날 것이며 그들이 지하 감옥에서 죽거나 굶어 죽는 일이 다시는 없을 것이다.

15나는 바다를 휘저어 물결을 일으키는 너희 하나님 여호와이니 내 이름은 전능한 여호와이다.

16내가 너희에게 내 교훈을 가르치고 내 손으로 너희를 보호하였다. 나는 하늘을 펼치고 땅의 기초를 놓았으며 시온에게 ‘너는 내 백성이다’ 하고 말하는 자이다.”

여호와의 진노의 잔

17예루살렘아, 깨어라! 네가 여호와께서 주신 진노의 잔을 그 찌꺼기까지 다 마시고 비틀거리고 있구나.

18네 백성 가운데 너를 인도할 자가 아무도 없다.

19두 가지 재난이 너에게 밀어닥쳤으니 네 땅이 전쟁으로 황폐해졌고 네 백성이 기근으로 굶주렸다. 그러니 누가 너를 동정하고 위로할 수 있겠느냐?

20네 백성이 허약하여 사냥꾼의 그물에 걸린 사슴처럼 거리 모퉁이마다 쓰러져 누웠으니 여호와께서 그들에게 분노를 쏟아 그들을 책망하셨기 때문이다.

21술을 마시지 않고서도 비틀거리며 고통당하는 예루살렘 사람들아,

22너희를 변호하시는 너희 하나님 여호와께서 말씀하신다. “내가 너희를 비틀거리게 한 내 진노의 그 큰 잔을 너희 손에서 거두겠다. 너희가 다시는 그것을 마시지 않을 것이다.

23그러나 너희를 괴롭히고 너희를 땅에 짓밟아 등을 밟고 걸어간 너희 원수들에게 내가 그 잔을 마시게 할 것이다.”

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 51:1-23

Wokovu Wa Milele Kwa Sayuni

151:1 Isa 46:3; Kum 7:13; Mit 26:27; Kum 16:20; Za 94:15; Isa 63:8; Rum 9:30-31; Isa 17:10“Nisikilizeni, ninyi mnaofuatia haki

na mnaomtafuta Bwana:

Tazameni mwamba ambako mlichongwa,

na mahali pa kuvunjia mawe ambako mlichimbwa;

251:2 Mwa 17:6; Ebr 11:11; Mwa 12:2; Isa 29:22; Rum 4:16mwangalieni Abrahamu, baba yenu,

na Sara, ambaye aliwazaa.

Wakati nilipomwita alikuwa mmoja tu,

nami nikambariki na kumfanya kuwa wengi.

351:3 Isa 40:1; Mwa 13:10; Yer 16:9; Za 102:13; Isa 44:26; Za 51:18; Isa 61:4Hakika Bwana ataifariji Sayuni,

naye atayaangalia kwa huruma magofu yake yote;

atayafanya majangwa yake yawe kama Edeni,

nazo sehemu zake zisizolimika ziwe kama bustani ya Bwana.

Shangwe na furaha zitakuwako ndani yake,

shukrani na sauti za kuimba.

451:4 Kut 6:7; Isa 26:18; 42:4-6; Za 50:7; Isa 3:15; 63:8“Nisikilizeni, watu wangu;

nisikieni, taifa langu:

Sheria itatoka kwangu;

haki yangu itakuwa nuru kwa mataifa.

551:5 Isa 35:4; 46:13; Za 98:1; 85:9; Mwa 49:10; Isa 52:10Haki yangu inakaribia mbio,

wokovu wangu unakuja,

nao mkono wangu utaleta hukumu kwa mataifa.

Visiwa vitanitegemea

na kungojea mkono wangu kwa matumaini.

651:6 Za 37:20; Lk 21:33; Za 102:25-26; Ebr 1:10-12; Mt 24:35; Isa 54:10Inueni macho yenu mbinguni,

mkaitazame dunia chini;

mbingu zitatoweka kama moshi,

dunia itachakaa kama vazi,

na wakazi wake kufa kama mainzi.

Bali wokovu wangu utadumu milele,

haki yangu haitakoma kamwe.

751:7 Za 37:31; Mt 10:28; Mdo 5:41; Za 119:39; Lk 6:22; Isa 54:4; 50:7“Nisikieni, ninyi mnaojua lililo sawa,

ninyi watu ambao mna sheria yangu mioyoni mwenu:

Msiogope mashutumu ya wanadamu

wala msitiwe hofu na matukano yao.

851:8 Ay 13:28; Yak 5:2; Isa 14:11Kwa maana nondo atawala kama vazi,

nao funza atawatafuna kama sufu.

Lakini haki yangu itadumu milele,

wokovu wangu kwa vizazi vyote.”

951:9 Kut 32:7; Za 68:30; Ay 26:12; Eze 29:3; Amu 5:12; Mwa 18:14; Za 65:6; 74:13Amka, Amka! Jivike nguvu,

ewe mkono wa Bwana,

Amka, kama siku zilizopita,

kama vile vizazi vya zamani.

Si ni wewe uliyemkata Rahabu vipande vipande,

uliyemchoma yule joka?

1051:10 Zek 10:11; Kut 14:21; Ufu 16:12; Kut 15:5, 8, 13; Ay 36:30Si ni wewe uliyekausha bahari,

maji ya kilindi kikuu,

uliyefanya barabara katika vilindi vya bahari

ili waliokombolewa wapate kuvuka?

1151:11 Isa 35:9; 44:23; 48:20; Ufu 7:17; Yer 31:13; 30:19; Sef 3:17; Isa 30:19Wale waliolipiwa fidia na Bwana watarudi.

Wataingia Sayuni wakiimba;

furaha ya milele itakuwa taji juu ya vichwa vyao.

Furaha na shangwe zitawapata,

huzuni na kulia kwa uchungu kutatoweka.

1251:12 Za 118:6; 2Kor 1:3-4; 1Pet 1:24; Isa 15:6; 2Fal 1:15; Isa 2:22; 40:6-7“Mimi, naam mimi,

ndimi niwafarijie ninyi.

Ninyi ni nani hata kuwaogopa

wanadamu wanaokufa,

wanadamu ambao ni majani tu,

1351:13 Ay 8:13; 4:17; Isa 17:10; 7:4; Ay 20:7; Isa 45:11; 48:13; 9:4kwamba mnamsahau Bwana Muumba wenu,

aliyezitanda mbingu

na kuiweka misingi ya dunia,

kwamba mnaishi katika hofu siku zote

kwa sababu ya ghadhabu ya mdhalimu,

ambaye nia yake ni kuangamiza?

Iko wapi basi ghadhabu ya mdhalimu?

1451:14 Isa 49:10; Zek 9:11; Isa 42:7Wafungwa waliojikunyata kwa hofu

watawekwa huru karibuni;

hawatafia kwenye gereza lao,

wala hawatakosa chakula.

1551:15 Kut 14:21; Isa 43:16; Za 74:13; Yer 31:35; Za 93:3; Isa 13:4Kwa maana Mimi ndimi Bwana, Mungu wako,

ambaye huisukasuka bahari ili mawimbi yake yangurume:

Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake.

1651:16 Kut 4:12-15; 2Pet 3:13; Kum 18:18; 33:22; Zek 8:8; Eze 14:11; Yer 7:23; 24:7Nimeweka maneno yangu kinywani mwako

na kukufunika kwa uvuli wa mkono wangu:

Mimi niliyeweka mbingu mahali pake,

niliyeweka misingi ya dunia,

niwaambiaye Sayuni,

‘Ninyi ni watu wangu.’ ”

Kikombe Cha Ghadhabu Ya Bwana

1751:17 Amu 5:12; Ay 21:20; Ufu 16:19; Za 60:3; 16:5; Mt 20:22; Isa 42:25Amka, amka!

Simama, ee Yerusalemu,

wewe uliyekunywa kutoka mkono wa Bwana

kikombe cha ghadhabu yake,

wewe uliyekunywa mpaka kufikia machujo yake,

kikombe kile cha kunywea

kiwafanyacho watu kuyumbayumba.

1851:18 Ay 31:18; Za 88:18; Isa 49:21; 41:13Kati ya wana wote aliowazaa

hakuwepo hata mmoja wa kumwongoza,

kati ya wana wote aliowalea

hakuwepo hata mmoja wa kumshika mkono.

1951:19 Isa 40:2; 47:9; 49:13; Yer 14:12; 24:10Majanga haya mawili yamekuja juu yako:

ni nani awezaye kukufariji?

Maangamizi, uharibifu, njaa na upanga:

ni nani awezaye kukutuliza?

2051:20 Yer 14:16; Mao 2:19; Isa 5:25; Ay 18:10; Yer 44:6; Ay 40:11; Kum 28:20Wana wako wamezimia,

wamelala kwenye mwanzo wa kila barabara,

kama swala aliyenaswa kwenye wavu.

Wamejazwa na ghadhabu ya Bwana

na makaripio ya Mungu wako.

2151:21 Isa 14:32; 29:9; Mao 3:15Kwa hiyo sikiliza hili, wewe uliyeteswa,

uliyelewa, lakini si kwa mvinyo.

2251:22 Yer 50:34; Hab 2:16; Isa 49:25; Yer 25:15; Mt 20:2251:22 Yer 50:34; Hab 2:16; Isa 49:25; Yer 25:15; Mt 20:22Hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi wako,

Mungu wako, yeye ambaye huwatetea watu wake:

“Tazama, nimeondoa mkononi mwako

kikombe kilichokufanya uyumbayumbe;

kutoka kikombe hicho,

kikombe cha kunywa cha ghadhabu yangu,

kamwe hutakunywa tena.

2351:23 Yer 49:12; Zek 12:3; Yos 10:24; Isa 14:4; 49:26; Yer 25:15-17, 26; Mik 7:1051:23 Yer 49:12; Zek 12:3; Yos 10:24; Isa 14:4; 49:26; Yer 25:15-17, 26; Mik 7:10Nitakiweka mikononi mwa watesi wako,

wale waliokuambia,

‘Anguka kifudifudi

ili tuweze kutembea juu yako.’

Ukaufanya mgongo wako kama ardhi,

kama njia yao ya kupita.”