馬太福音 7 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

馬太福音 7:1-29

責人先責己

1「不要論斷別人,免得你們被論斷。 2因為你們怎樣論斷別人,也必照樣被論斷;你們用什麼尺度衡量別人,也要用什麼尺度衡量你們。 3為什麼你只看見你弟兄眼中的小刺,卻看不見自己眼中的大樑呢? 4既然你自己眼中有大樑,又怎麼能對弟兄說『讓我除去你眼中的小刺』呢? 5你這偽君子啊!要先除掉自己眼中的大樑,才能看得清楚,好清除弟兄眼中的小刺。

6「不要把聖物給狗,免得狗轉過頭來咬你們,也不要把珍珠丟在豬前,免得豬踐踏了珍珠。

祈求、尋找、叩門

7「祈求,就會給你們;尋找,就會尋見;叩門,就會給你們開門。 8因為凡祈求的,就得到;尋找的,就尋見;叩門的,就給他開門。

9「你們做父親的,誰會在兒子要餅時給他石頭, 10要魚時給他毒蛇呢? 11你們雖然邪惡,尚且知道把好東西給兒女,你們的天父豈不更要把好東西賜給求祂的人嗎?

12「所以,你們希望人怎樣待你們,就要怎樣待人,這是律法和先知的教導。

辨別與抉擇

13「你們要進窄門,因為通向滅亡的門大,路寬,進去的人也多; 14但通向永生的門小,路窄,找到的人也少。

15「你們要提防假先知,他們披著羊皮到你們當中,骨子裡卻是凶殘的狼。 16你們可以憑他們結的果子認出他們。荊棘怎能結出葡萄呢?蒺藜怎能長出無花果呢? 17同樣,好樹結好果子,壞樹結壞果子; 18好樹結不出壞果子,壞樹也結不出好果子。 19凡不結好果子的樹,都要被砍下來丟在火裡。 20因此,你們可以憑他們結的果子認出他們。 21並不是所有稱呼我『主啊,主啊』的人都能進天國,只有遵行我天父旨意的人才能進去。 22在審判那天,很多人會對我說,『主啊,主啊,我們不是奉你的名傳道,奉你的名趕鬼,奉你的名行了許多神蹟嗎?』 23我會清楚地告訴他們,『我從來不認識你們,你們這些作惡的人走開!』

兩種蓋房子的人

24「所以,凡聽了我的這些話就去行的人,就像聰明人把房子建在磐石上。 25任由風吹雨打、洪水沖擊,房子仍屹立不倒,因為它建基在磐石上。 26凡聽了我這些話不去行的,就像愚昧人把房子建在沙土上。 27遇到風吹雨打、洪水沖擊,房子就倒塌了,而且倒塌得很厲害。」

28大家聽完耶穌這番教導,都很驚奇, 29因為祂教導他們時像位有權柄的人,不像他們的律法教師。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mathayo 7:1-29

Kuwahukumu Wengine

(Luka 6:37-38, 41-42)

17:1 1Kor 5:12; Yak 4:11-12“Usihukumu ili usije ukahukumiwa. 27:2 Lk 6:38; Rum 2:1Kwa maana jinsi unavyowahukumu wengine, ndivyo utakavyohukumiwa, na kwa kipimo kile upimiacho, ndicho utakachopimiwa.

37:3 Lk 6:41, 42“Mbona unatazama kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako, na wala huoni boriti iliyo ndani ya jicho lako mwenyewe? 4Au unawezaje kumwambia ndugu yako, ‘Acha nitoe kibanzi kwenye jicho lako,’ wakati kuna boriti kwenye jicho lako mwenyewe? 5Ewe mnafiki, ondoa boriti ndani ya jicho lako kwanza, ndipo utaweza kuona dhahiri jinsi ya kuondoa kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako.

67:6 Mt 9:7, 8; 23:9; Mdo 13:13, 45, 46; Mt 10:11“Msiwape mbwa vitu vilivyo vitakatifu; wala msitupie nguruwe lulu zenu. Kama mkifanya hivyo, watazikanyagakanyaga na kisha watawageukia na kuwararua vipande vipande.

Omba, Tafuta, Bisha

(Luka 11:9-13)

77:7 1Fal 3:5; Mk 11:24; Yer 29:13-14“Ombeni nanyi mtapewa; tafuteni nanyi mtapata; bisheni nanyi mtafunguliwa mlango. 87:8 Mit 8:17; 29:12-13Kwa kuwa kila aombaye hupewa; naye kila atafutaye hupata; na kila abishaye hufunguliwa mlango.

9“Au ni nani miongoni mwenu ambaye mwanawe akimwomba mkate atampa jiwe? 10Au mwanawe akimwomba samaki atampa nyoka? 117:11 Yak 1:17Ikiwa ninyi basi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vitu vizuri, si zaidi sana Baba yenu aliye mbinguni atawapa vitu vizuri wale wamwombao? 127:12 Lk 6:31; Rum 13:8-10; Gal 5:14Kwa hiyo chochote mnachotaka mtendewe na watu, ninyi nanyi watendeeni vivyo hivyo. Kwa kuwa hii ndiyo Sheria na Manabii.

Njia Nyembamba Na Njia Pana

137:13 Lk 13:24; Yn 10:7-9“Ingieni kupitia mlango mwembamba, kwa maana lango ni pana na njia ni pana ielekeayo upotevuni, nao ni wengi waingiao kwa kupitia lango hilo. 147:14 Mt 19:24; Mdo 14:22Lakini mlango ni mwembamba na njia ni finyu ielekeayo kwenye uzima, nao ni wachache tu waionao.

Mti Na Tunda Lake

(Luka 6:43-44)

157:15 Yer 23:16; Mk 13:22; Eze 22:27; Mdo 20:29; Isa 1:23“Jihadharini na manabii wa uongo, wanaowajia wakiwa wamevaa mavazi ya kondoo, lakini ndani ni mbwa mwitu wakali. 167:16 Mt 12:33; Lk 6:44Mtawatambua kwa matunda yao. Je, watu huchuma zabibu kwenye miiba, au tini kwenye michongoma? 177:17 Mt 12:33Vivyo hivyo, mti mwema huzaa matunda mazuri, na mti mbaya huzaa matunda mabaya. 187:18 Lk 6:43Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mbaya hauwezi kuzaa matunda mazuri. 197:19 Mt 3:10Kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni. 20Hivyo, mtawatambua kwa matunda yao.

Mwanafunzi Wa Kweli

(Luka 13:25-27)

217:21 Hos 8:2; Yn 13:13; Yak 1:22; 1Yn 3:18; Rum 2:13“Si kila mtu aniambiaye, ‘Bwana, Bwana,’ atakayeingia katika Ufalme wa Mbinguni, bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni. 227:22 Mt 10:15; Lk 10:20; Mdo 19:13Wengi wataniambia siku ile, ‘Bwana, Bwana, hatukutoa unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo wachafu na kufanya miujiza mingi?’ 237:23 Za 6:8; Lk 13:25-27Ndipo nitakapowaambia wazi, ‘Sikuwajua kamwe. Ondokeni kwangu, ninyi watenda maovu!’

Msikiaji Na Mtendaji

(Luka 6:47-49)

247:24 Mt 7:21; Yak 1:22-25“Kwa hiyo kila mtu ayasikiaye haya maneno yangu na kuyatenda, ni kama mtu mwenye busara aliyejenga nyumba yake kwenye mwamba. 25Mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, na upepo ukavuma ukaipiga hiyo nyumba. Lakini haikuanguka; kwa sababu msingi wake ulikuwa kwenye mwamba. 26Naye kila anayesikia haya maneno yangu wala asiyatende, ni kama mtu mjinga aliyejenga nyumba yake kwenye mchanga. 277:27 Eze 13:10, 11Mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, nao upepo ukavuma ukaipiga hiyo nyumba, nayo ikaanguka kwa kishindo kikubwa.”

287:28 Mt 19:1; 26:1; Mk 11:18; Yn 7:46Yesu alipomaliza kusema maneno haya, makutano ya watu wakashangazwa sana na mafundisho yake, 297:29 Yn 7:46kwa sababu alifundisha kama yeye aliye na mamlaka, wala si kama walimu wao wa sheria.