雅歌 3 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

雅歌 3:1-11

1我夜晚躺在床上,

思念著我心愛的人;

我尋找他,卻找不到。

2我要起來尋遍城裡的大街小巷,

我要尋找我心愛的人。

我尋找他,卻尋不到。

3遇上了城中巡邏的守衛,

我就問他們:「你們看到我心愛的人了嗎?」

4我剛離開他們,便找到了我心愛的人。

我拉著他,不讓他走;

我把他帶回娘家,

到懷我者的臥室。

5耶路撒冷的少女啊!

我指著羚羊和田野的母鹿吩咐你們,

不要叫醒或驚動愛情,

等它自發吧。

耶路撒冷的少女:

6那從曠野上來,形狀像煙柱,

散發著商人販賣的沒藥、乳香等各樣芬芳之氣的是什麼呢?

7看啊,是所羅門的轎子,

周圍是六十名勇士,

都是以色列的精兵。

8他們個個驍勇善戰,手持利劍,

腰配戰刀,防備夜間的偷襲。

9所羅門王用黎巴嫩木為自己製造了一頂轎子。

10銀轎柱、金靠背、紫錦坐墊,

轎子裡面的裝飾都是耶路撒冷少女們用愛情編織的。

11錫安的少女啊,

出去看看所羅門王的風采吧!

他頭上的王冠是他母親在他成婚那天,

在他心中歡快之日為他戴上的。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Wimbo 3:1-11

13:1 Isa 26:9; Wim 5:6Usiku kucha kwenye kitanda changu

nilimtafuta yule moyo wangu umpendaye;

nilimtafuta, lakini sikumpata.

2Sasa nitaondoka na kuzunguka mjini,

katika barabara zake na viwanja;

nitamtafuta yule moyo wangu umpendaye.

Kwa hiyo nilimtafuta lakini sikumpata.

33:3 Wim 5:7; Isa 21:6-11Walinzi walinikuta

walipokuwa wakizunguka mji.

Nikawauliza, “Je, mmemwona

yule moyo wangu umpendaye?”

43:4 Wim 8:2; 6:9; 8:5; Rum 8:35-39; Mit 8:17; 4:13Kitambo kidogo tu baada ya kuwapita

nilimpata yule moyo wangu umpendaye.

Nilimshika na sikumwachia aende

mpaka nilipomleta katika nyumba ya mama yangu,

katika chumba cha yule aliyenichukua mimba.

53:5 Wim 2:7; 8:4Binti za Yerusalemu, ninawaagiza

kwa paa na kwa ayala wa shambani:

Msichochee wala kuamsha mapenzi

hata yatakapotaka yenyewe.

Shairi La Tatu

Mpenzi

63:6 Wim 8:6; 4:6, 14; Kut 30:34; Yer 2:2Ni nani huyu anayekuja kutoka jangwani

kama nguzo ya moshi,

anayenukia manemane na uvumba

iliyotengenezwa kwa vikolezo vyote

vya mfanyabiashara?

73:7 1Sam 8:11Tazama! Ni gari la Solomoni

lisindikizwalo na mashujaa sitini,

walio wakuu sana wa Israeli,

83:8 Ay 15:22; Za 91:5wote wamevaa panga,

wote wazoefu katika vita,

kila mmoja na upanga wake pajani,

wamejiandaa kwa ajili ya hofu za usiku.

9Mfalme Solomoni alijitengenezea gari;

alilitengeneza kwa mbao kutoka Lebanoni.

103:10 Mt 22:37; Efe 3:19; Rum 5:8Nguzo zake alizitengeneza kwa fedha,

kitako chake kwa dhahabu.

Kiti chake kilipambwa kwa zambarau,

gari lake likanakshiwa njumu kwa upendo

na binti za Yerusalemu.

113:11 Isa 3:16; 54:5; 32:9-13; 62:5; Yer 3:14Tokeni nje, ninyi binti za Sayuni,

mkamtazame Mfalme Solomoni akiwa amevaa taji,

taji ambalo mama yake alimvika

siku ya arusi yake,

siku ambayo moyo wake ulishangilia.