詩篇 36 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

詩篇 36:1-12

第 36 篇

人的邪惡與上帝的美善

耶和華的僕人大衛的詩,交給樂長。

1罪惡在惡人內心深處說話,

他們眼中毫無對上帝的畏懼。

2他們自以為是,渾然不知自己的罪,

也不憎惡自己的罪。

3他們滿口惡言謊話,

毫無智慧和善行。

4他們躺在床上盤算作惡,

執意走罪惡的道路,

無惡不作。

5耶和華啊,你的慈愛廣及諸天,

你的信實高達穹蒼。

6你的公義穩如高山,

你的判斷深不可測。

耶和華啊,你保護人類,

也保護牲畜。

7上帝啊,

你的慈愛無比寶貴!

世人都在你的翅膀下尋求蔭庇。

8你讓他們飽享你殿裡的美食,

暢飲你樂河中的水。

9因為你是生命的泉源,

在你的光中我們得見光明。

10求你常施慈愛給認識你的人,

以公義恩待心地正直的人。

11別讓驕傲人的腳踐踏我,

別讓兇惡人的手驅趕我。

12看啊!惡人已經摔倒在地,

再也爬不起來。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 36:1-12

Zaburi 36

Uovu Wa Mwanadamu

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana.

136:1 Ay 21:16; 23:15; Yer 2:19; 36:16, 24; Rum 3:18; Mit 8:13; Mwa 20:11; Mhu 12:3Kuna neno moyoni mwangu

kuhusu hali ya dhambi ya mwovu.

Hakuna hofu ya Mungu

mbele ya macho yake.

236:2 Kum 29:19Kwa kuwa machoni pake mwenyewe hujisifu mno

hata hawezi kugundua au kuichukia dhambi yake.

336:3 Yer 4:22; 13:23; Za 10:7; 5:6, 9; 43:1; 144:8, 11; 94:8; Ay 5:13; Isa 44:20; Amo 3:10Maneno ya kinywa chake ni maovu na ya udanganyifu,

ameacha kuwa mwenye hekima na kutenda mema.

436:4 Mik 2:1; Rum 12:9; Isa 65:2; Za 52:3Hata kitandani mwake hupanga hila mbaya,

hujitia katika njia ya dhambi

na hakatai lililo baya.

536:5 Za 89:1; 119:90; 108:4; 57:10; 89:2; 71:19; 103:11Upendo wako, Ee Bwana, unafika hadi mbinguni,

uaminifu wako hadi kwenye anga.

636:6 Za 5:8; 68:15; Mwa 1:2; Za 104:14; 7:11; 145:9; Neh 9:6; Rum 11:33; Ay 7:20; 11:8Haki yako ni kama milima mikubwa,

hukumu zako ni kama kilindi kikuu.

Ee Bwana, wewe huwahifadhi

mwanadamu na mnyama.

736:7 Za 6:4; 17:8; 57:1; 91:4; Rut 2:12Upendo wako usiokoma

ni wa thamani mno!

Watu wakuu na wadogo

hujificha uvulini wa mbawa zako.

836:8 Za 65:4; 23:2; 63:5; Yer 31:12, 14; Ufu 22:1; Isa 25:6; Ay 20:17Wanajifurahisha katika wingi nyumbani mwako,

nawe utawanywesha katika mto wa furaha zako.

936:9 Isa 12:3; 2:5; 9:2; 60:1, 19; Yer 2:13; Zek 13:1; Yn 1:4; 4:10, 14; Ufu 21:6; Mdo 26:18; Efe 5:8; Kol 1:13; 1Pet 2:9; Mit 10:11; 16:22; Za 87:7; 4:6; 27:1; 76:4; 104:2Kuwa pamoja nawe ni kijito cha uzima,

katika nuru yako twaona nuru.

1036:10 Yer 31:3; 9:24; 22:16; Za 7:10; 11:2; 94:15; 125:4Dumisha upendo wako kwa wale wanaokujua wewe,

haki yako kwa wale walio wanyofu wa moyo.

1136:11 Za 71:4; 140:4Mguu wa mwenye kiburi usije dhidi yangu,

wala mkono wa mwovu usinifukuze.

1236:12 Za 18:38Angalia jinsi watenda mabaya walivyoanguka:

wametupwa chini, hawawezi kuinuka!