約書亞記 4 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

約書亞記 4:1-24

堆石為證

1民眾都過河之後,耶和華對約書亞說: 2「你去從民眾中選出十二個人,每支派選一人, 3吩咐他們從約旦河床祭司站立的地方取十二塊石頭,放在你們今天晚上住宿的地方。」 4約書亞便召來他從以色列人中選的十二個人,對他們說: 5「你們到約旦河床你們的上帝耶和華的約櫃前面,每人扛一塊石頭回來,每個支派一塊,一共十二塊。 6這些石頭要在你們中間作記號。以後,倘若你們的子孫問你們,『這些石頭是什麼意思?』 7你們就告訴他們,『約旦河水在耶和華的約櫃前曾經被截斷,當約櫃過河的時候,河水被截斷了。這些石頭要在以色列人當中作為永久的紀念。』」

8以色列人就照約書亞的吩咐,也就是照耶和華對約書亞的吩咐,按以色列人支派的數目,從約旦河中取了十二塊石頭,搬來放在住宿的地方。 9約書亞又在約旦河床抬約櫃的祭司站立的地方立了十二塊石頭。石頭至今還在那裡。 10抬約櫃的祭司站在約旦河中間,一直站到耶和華吩咐約書亞交待民眾做的每一件事都完成了,正如摩西約書亞的吩咐。民眾迅速過了河。 11所有人都過河以後,祭司才抬著耶和華的約櫃在民眾注視之下過了河。 12呂便支派、迦得支派和瑪拿西半個支派的人照摩西從前的囑咐,帶著兵器走在以色列人的前面。 13大約有四萬全副武裝的以色列人在耶和華面前過了河,前往耶利哥平原,準備作戰。 14那一天,耶和華使約書亞以色列眾人面前受尊重,他像摩西一樣終生受民眾敬畏。

15耶和華對約書亞說: 16「你去吩咐抬約櫃的祭司從約旦河裡上來。」 17約書亞便吩咐他們上來。 18抬耶和華約櫃的祭司從河床上來,腳剛一踏上岸,約旦河的水立刻恢復了原狀,像以往一樣漲過兩岸。

19那天是一月十日。以色列人從約旦河上來之後,就在耶利哥東邊的吉甲紮營。 20約書亞把從約旦河取來的十二塊石頭立在吉甲21並對以色列人說:「以後,你們的子孫問你們這堆石頭是什麼意思, 22你們就告訴他們,『這是代表以色列人曾在乾地上走過約旦河。』 23因為你們的上帝耶和華為了讓你們過河而使約旦河成為乾地,就像祂從前為了讓我們過紅海而使海成為乾地一樣。 24這是要讓天下萬民都知道耶和華有無比的能力,要讓你們永遠敬畏你們的上帝耶和華。」

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yoshua 4:1-24

Ukumbusho Wa Kuvuka Mto Yordani

14:1 Kum 27:2; Yos 2:17Wakati taifa lote lilipokwisha kuvuka Mto Yordani, Bwana akamwambia Yoshua, 24:2 Yos 3:17; Hes 13:1; 34:18; Yos 1:4-15; 1Fal 18:31“Chagua watu kumi na wawili miongoni mwa watu, kila kabila mtu mmoja, 3nawe uwaambie wachukue mawe kumi na mawili katikati ya Mto Yordani, palepale makuhani waliposimama, wayachukue na kuyaweka mahali mtakapokaa usiku huu wa leo.”

44:4 Yos 3:12Basi Yoshua akawaita watu kumi na wawili ambao alikuwa amewachagua kutoka miongoni mwa Waisraeli, mtu mmoja kutoka kila kabila, 54:5 Yos 3:17naye akawaambia, “Mtangulie mbele ya Sanduku la Bwana Mungu wenu, mwende katikati ya Mto Yordani. Kila mmoja wenu atainua jiwe begani mwake, kufuatana na hesabu ya makabila ya Waisraeli, 64:6 Yos 2:12; Kut 10:2; 12:26; 13:14; Kum 6:20; Za 78:3-6; Isa 38:16kuwa kama ishara katikati yenu. Siku zijazo, wakati watoto wenu watakapowauliza, ‘Ni nini maana ya mawe haya?’ 74:7 Yos 3:13; Kut 28:12; 12:14waambieni kwamba maji ya Mto Yordani yaliyokuwa yakitiririka yalitindika mbele ya Sanduku la Agano la Bwana. Wakati lilipovuka Yordani, maji ya Yordani yalitindika. Mawe haya yatakuwa kumbukumbu kwa watu wa Israeli milele.”

84:8 Kut 28:21; Yos 3:17Hivyo Waisraeli wakafanya kama Yoshua alivyowaagiza. Wakachukua mawe kumi na mawili kutoka katikati ya Mto Yordani, kulingana na hesabu ya kabila za Waisraeli kama Bwana alivyomwambia Yoshua, nao wakayabeba hadi kambini mwao, mahali walipoyatua chini. 94:9 Mwa 28:18; Yos 24:26; 1Sam 7:12; Mwa 35:20Yoshua akayasimamisha yale mawe kumi na mawili ambayo yalikuwa katikati ya Mto Yordani, mahali pale ambapo miguu ya makuhani waliobeba Sanduku la Agano iliposimama. Nayo yako huko mpaka leo.

10Makuhani waliobeba lile Sanduku walibakia wakiwa wamesimama katikati ya Mto Yordani mpaka kila kitu Bwana alichomwamuru Yoshua kilipokuwa kimefanywa na watu, sawasawa na vile Mose alivyokuwa amemwamuru Yoshua. Watu wakafanya haraka kuvuka, 11na mara tu watu wote walipokwisha kuvuka, Sanduku la Bwana na makuhani wakavuka watu wakiwa wanatazama. 124:12 Mwa 29:32; 30:11; 41:51; Hes 32:27-29Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase wakavuka mbele ya Waisraeli, wakiwa wamevaa silaha, kama Mose alivyowaamuru. 134:13 Kut 13:18; Hes 32:17Kiasi cha watu 40,000 waliojiandaa kwa vita walivuka mbele za Bwana hadi nchi tambarare za Yeriko kwa ajili ya vita.

144:14 Yos 3:7; 1Sam 2:30; 2Nya 32:23; 1Nya 29:12Siku ile Bwana akamtukuza Yoshua mbele ya Israeli yote, nao wakamheshimu siku zote za maisha yake, kama vile walivyomheshimu Mose.

15Basi Bwana akamwambia Yoshua, 164:16 Kut 25:22; Ufu 11:19; Yos 3:15“Waamuru hao makuhani wanaolibeba Sanduku la Ushuhuda, wapande kutoka ndani ya Mto Yordani.”

17Kwa hiyo Yoshua akawaamuru hao makuhani akisema, “Pandeni kutoka ndani ya Mto Yordani.”

184:18 Kut 14:27; Yos 3:15Nao makuhani wakapanda kutoka ndani ya Mto Yordani wakilibeba hilo Sanduku la Agano la Bwana. Mara tu walipoiweka miguu yao penye kingo, nje ya mto, maji ya Yordani yakarudi kufurika kama ilivyokuwa kabla.

194:19 Kum 11:30; Yos 5:9; 15:17; 1Sam 11:14-15; Amo 4:4; 5:5; Mik 6:5Siku ya kumi ya mwezi wa kwanza watu walipanda kutoka Yordani na kupiga kambi huko Gilgali, kwenye mpaka wa mashariki ya Yeriko. 20Naye Yoshua akayasimamisha huko Gilgali yale mawe kumi na mawili ambayo walikuwa wameyachukua katikati ya Mto Yordani. 21Akawaambia Waisraeli, “Wazao wenu watakapowauliza baba zao siku zijazo wakisema, ‘Mawe haya maana yake ni nini?’ 224:22 Kut 14:22; Yos 3:17Basi waambieni, ‘Israeli ilivukia mahali pakavu katika Mto Yordani.’ 234:23 Kut 14:19-22; Neh 9:11; Za 77:16-19; Isa 43:16; 63:12Kwa maana Bwana Mungu wenu alikausha maji ya Yordani mbele yenu, hadi mlipomaliza kuvuka. Bwana Mungu wenu alifanya haya kwa Mto Yordani sawasawa na kile alichoifanyia Bahari ya Shamu wakati alipoikausha mbele yetu hadi tulipomaliza kuvuka. 244:24 1Fal 8:60; 18:36; 2Fal 5:15; Za 67:2; 83:18; 106:8; Isa 37:20; 52:10; Kut 15:16; 1Nya 29:12; Za 44:3; 89:13; 98:1; 118:15-16; Kut 14:31Alifanya hivi ili kwamba mataifa yote ya dunia yapate kujua kuwa mkono wa Bwana ni wenye nguvu, na ili kwamba kila wakati mpate kumcha Bwana Mungu wenu.”