箴言 28 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

箴言 28:1-28

1惡人未被追趕也逃竄,

義人坦然無懼如雄獅。

2國中有罪,君王常換;

國有哲士,長治久安。

3窮人28·3 窮人」有些抄本作「暴君」。欺壓貧民,

如暴雨沖毀糧食。

4背棄律法的稱讚惡人,

遵守律法的抗拒惡人。

5邪惡之人不明白公義,

尋求耶和華的全然明白。

6行為正直的窮人,

勝過行事邪僻的富人。

7遵守律法的是智慧之子,

與貪食者為伍令父蒙羞。

8人放高利貸牟利,

等於為扶貧者積財。

9人若不聽從律法,

他的禱告也可憎。

10引誘正直人走邪道,

必掉進自己設的陷阱;

但純全無過的人必承受福分。

11富人自以為有智慧,

卻被明智的窮人看透。

12義人得勝,遍地歡騰;

惡人當道,人人躲藏。

13自掩其罪,必不亨通;

痛改前非,必蒙憐憫。

14敬畏上帝必蒙福,

頑固不化必遭禍。

15暴虐的君王轄制窮人,

如咆哮的獅、覓食的熊。

16昏庸的君王殘暴不仁,

恨不義之財的享長壽。

17背負血債者必終生逃亡,

誰也不要幫他。

18純全無過的必蒙拯救,

行為邪僻的轉眼滅亡。

19勤奮耕耘,豐衣足食;

追求虛榮,窮困潦倒。

20忠信的人必大蒙祝福,

急於發財的難免受罰。

21徇私偏袒實不可取,

人卻為一餅而枉法。

22貪婪的人急於發財,

卻不知貧窮即將臨到。

23責備人的至終比諂媚者更受愛戴。

24竊取父母之財而不知罪者與匪類無異。

25貪得無厭的人挑起紛爭,

信靠耶和華的富足昌盛。

26愚人心中自以為是,

憑智慧行事的平安穩妥。

27賙濟窮人的一無所缺,

視而不見的多受咒詛。

28惡人當道,人人躲藏;

惡人滅亡,義人增多。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mithali 28:1-28

128:1 2Fal 7:7; Law 26:17; Za 53:5Mtu mwovu hukimbia ingawa hakuna yeyote anayemfukuza,

bali wenye haki ni wajasiri kama simba.

2Wakati nchi inapokuwa na uasi, inakuwa na viongozi wengi,

bali mwenye ufahamu na maarifa hudumisha utaratibu.

328:3 Mt 18:28Mtu maskini amwoneaye yeye aliye maskini zaidi

ni kama mvua ya dhoruba isiyosaza mazao.

428:4 1Fal 18:18; Mt 3:7; Efe 5:11; 1Tim 5:20Wale waiachao sheria huwasifu waovu,

bali wale waishikao sheria huwapinga.

528:5 Yn 7:17; 1Kor 2:15Watu wabaya hawaelewi haki,

bali wale wamtafutao Bwana wanaielewa kikamilifu.

628:6 Mit 19:1Afadhali maskini ambaye mwenendo wake hauna lawama

kuliko tajiri ambaye njia zake ni potovu.

728:7 Mit 23:19-21Yeye ashikaye sheria ni mwana mwenye ufahamu,

bali rafiki wa walafi humwaibisha baba yake.

828:8 Ay 27:16-17; Eze 18:8; Kut 18:21; Mit 13:22; Lk 14:12-14Yeye aongezaye utajiri wake kwa riba kubwa mno

hukusanya kwa ajili ya mwingine,

ambaye atawahurumia maskini.

928:9 Za 66:18; Zek 7:11; Isa 1:13; 2Tim 4:3Kama mtu yeyote akikataa kusikia sheria,

hata maombi yake ni chukizo.

1028:10 Za 34:9; 57:6; Mk 10:30; Mit 26:27; Rum 8:32Yeye ambaye humwongoza mwenye haki kwenye mapito mabaya,

ataanguka kwenye mtego wake mwenyewe,

bali wasio na lawama watapokea urithi mwema.

11Mtu tajiri anaweza kuwa na hekima machoni pake mwenyewe,

bali mtu maskini mwenye ufahamu atamfichua.

1228:12 2Fal 11:20; Ay 24:4; Mit 11:10Mwenye haki ashindapo, kuna furaha kubwa,

bali waovu watawalapo, watu hujificha.

1328:13 1Yn 1:8-10; 2Sam 12:13; Ay 31:33; Dan 4:27Yeye afichaye dhambi zake hatafanikiwa,

bali yeyote aziungamaye na kuziacha hupata rehema.

1428:14 Za 16:8; Mit 23:17; Rum 2:5; 11:20Amebarikiwa mtu ambaye siku zote humcha Bwana,

bali yeye afanyaye moyo wake kuwa mgumu

huangukia kwenye taabu.

15Kama simba angurumaye au dubu ashambuliaye,

ndivyo alivyo mtu mwovu atawalaye wanyonge.

16Mtawala dhalimu hana akili,

bali yeye achukiaye mapato ya udhalimu

atafurahia maisha marefu.

1728:17 Mwa 9:6; 1Sam 30:17Mtu mwenye kusumbuliwa na hatia ya kuua

atakuwa mtoro mpaka kufa;

mtu yeyote na asimsaidie.

1828:18 Es 6:13; Mit 10:9Yeye ambaye mwenendo wake hauna lawama

hulindwa salama,

bali yeye ambaye njia zake ni potovu

ataanguka ghafula.

1928:19 Mit 12:11Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele,

bali yule afuataye mambo ya upuzi atakuwa na umaskini wa kumtosha.

2028:20 Mit 13:11; 20:21; 23:4, 22; 1Tim 6:9Mtu mwaminifu atabarikiwa sana,

bali yeye atamaniye kupata utajiri kwa haraka

hataacha kuadhibiwa.

2128:21 Eze 13:19; Za 94:21; Mit 18:5Kuonyesha upendeleo si vizuri,

hata hivyo mtu atafanya kosa kwa kipande cha mkate.

2228:22 Mit 28:20Mtu mchoyo ana tamaa ya kupata utajiri,

naye hana habari kuwa umaskini unamngojea.

2328:23 Mit 27:5, 6Yeye amkemeaye mtu mwishoni hupata kibali zaidi,

kuliko mwenye maneno ya kusifu isivyostahili.

2428:24 Mit 18:9; 19:26Yeye amwibiaye babaye au mamaye

na kusema, “Si kosa,”

yeye ni mwenzi wa yule aharibuye.

2528:25 1Tim 6:6; Mit 29:25Mtu mwenye tamaa huchochea fitina,

bali yule amtegemeaye Bwana atafanikiwa.

2628:26 Za 4:5; Mit 3:5Yeye ajitumainiaye mwenyewe ni mpumbavu,

bali yeye atembeaye katika hekima hulindwa salama.

2728:27 Kum 15:7; Mit 19:17; 22:9Yeye ampaye maskini

hatapungukiwa na kitu chochote,

bali yeye awafumbiaye maskini macho

hupata laana nyingi.

2828:28 Mit 28:12; Ay 20:19Wakati waovu watawalapo,

watu huenda mafichoni,

bali waovu wanapoangamia,

wenye haki hufanikiwa.