箴言 14 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

箴言 14:1-35

1智慧的女子建立家園,

愚昧的女子親手拆毀。

2行為正直的人敬畏耶和華,

行事邪僻的人輕視耶和華。

3愚人的狂言招來鞭打,

智者的唇舌保護自己。

4沒有耕牛槽頭淨,

五穀豐登需壯牛。

5忠實的證人不會撒謊,

虛假的證人謊話連篇。

6嘲諷者徒然尋智慧,

明哲人輕易得知識。

7你要遠離愚昧人,

他口中毫無知識。

8明哲憑智慧辨道,

愚人被愚昧欺騙。

9愚妄人戲看罪惡,

正直人彼此恩待。

10心頭的愁苦,唯有自己明白;

心中的喜樂,外人無法分享。

11惡人的房屋必遭毀滅,

正直人的帳篷必興盛。

12有的路看似正確,

最終卻通向死亡。

13歡笑難消內心的痛苦,

歡樂過後,悲傷猶在。

14背棄正道,自食惡果;

善人行善,必得善報。

15愚昧人什麼都信,

明哲人步步謹慎。

16智者小心謹慎,遠離惡事;

愚人驕傲自負,行事魯莽。

17急躁易怒的人做事愚昧,

陰險奸詐之人遭人痛恨。

18愚昧人得愚昧作產業,

明哲人得知識為冠冕。

19壞人俯伏在善人面前,

惡人俯伏在義人門口。

20窮人遭鄰舍厭,

富人朋友眾多。

21藐視鄰舍是罪過,

憐憫窮人蒙福樂。

22圖謀惡事的步入歧途,

行善的受愛戴和擁護。

23殷勤工作,帶來益處;

滿嘴空談,導致貧窮。

24智者以財富為冠冕,

愚人以愚昧為裝飾。

25誠實的證人挽救性命,

口吐謊言者欺騙他人。

26敬畏耶和華的信心堅定,

他的子孫也有庇護所。

27敬畏耶和華是生命的泉源,

可以使人避開死亡的陷阱。

28人民眾多,是君王的榮耀;

沒有臣民,君主必然敗亡。

29不輕易發怒者深明事理,

魯莽急躁的人顯出愚昧。

30心平氣和,滋潤生命;

妒火中燒,啃蝕骨頭。

31欺壓窮人等於侮辱造物主,

憐憫貧弱就是尊敬造物主。

32惡人因惡行而滅亡,

義人到死仍有倚靠。

33智慧存在哲士心裡,

愚人心中充滿無知。

34公義能叫邦國興盛,

罪惡是人民的恥辱。

35明智的臣子蒙王喜悅,

可恥的僕人惹王發怒。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mithali 14:1-35

114:1 Rut 3:11; Mit 24:3Mwanamke mwenye hekima huijenga nyumba yake,

bali mpumbavu huibomoa nyumba yake

kwa mikono yake mwenyewe.

214:2 Ay 12:4Yeye ambaye njia zake ni nyofu humcha Bwana,

bali yeye ambaye njia zake zimepotoka humdharau Mungu.

314:3 Mit 12:6; 10:13Mazungumzo ya mpumbavu huleta fimbo mgongoni mwake,

bali mwenye hekima hulindwa na maneno ya midomo yake.

414:4 Za 12:2; Mit 12:17Pale ambapo hakuna mafahali, hori ni tupu,

bali kutokana na nguvu za fahali huja mavuno mengi.

514:5 Kut 20:16; Za 12:2; Mit 6:19Shahidi mwaminifu hadanganyi,

bali shahidi wa uongo humimina uongo.

614:6 Mit 9:9; 17:24Mwenye mzaha huitafuta hekima na haipati,

bali maarifa huja kwa urahisi kwa anayepambanua.

7Kaa mbali na mtu mpumbavu,

kwa maana hutapata maarifa katika midomo yake.

814:8 Lk 12:20; 1Kor 3:19; Mit 15:28; 21:29Hekima ya mwenye busara ni kufikiria njia zake,

bali upumbavu wa wapumbavu ni udanganyifu.

914:9 Mit 1:22; 10:23Wapumbavu hudhihaki kujirekebisha kutoka dhambi,

bali wema hupatikana miongoni mwa wanyofu.

10Kila moyo hujua uchungu wake wenyewe,

wala hakuna yeyote awezaye kushiriki furaha yake.

1114:11 Za 72:7; Ay 8:15; Mit 3:33Nyumba ya mwovu itaangamizwa,

bali hema la mnyofu litastawi.

1214:12 Rum 6:21; Mit 12:15; 16:25Iko njia ionekanayo kuwa sawa kwa mtu,

bali mwisho wake huelekeza mautini.

1314:13 Mhu 2:2; 7:3-6Hata katika kicheko moyo waweza kuuma,

nayo furaha yaweza kuishia katika majonzi.

1414:14 2Nya 15:7; Mit 12:14Wasio na imani watapatilizwa kikamilifu kwa ajili ya njia zao,

naye mtu mwema atapewa thawabu kwa ajili ya njia yake.

1514:15 Mit 14:8Mtu mjinga huamini kila kitu,

bali mwenye busara hufikiria hatua zake.

1614:16 Kut 20:20; Mit 22:3Mtu mwenye hekima humcha Bwana na kuepuka mabaya,

bali mpumbavu hukasirika kwa hamaki na uzembe.

1714:17 Mit 28:25; 29:22Mtu anayekasirika kwa haraka hufanya mambo ya upumbavu,

naye mtu wa hila huchukiwa.

18Mjinga hurithi upumbavu,

bali wenye busara huvikwa maarifa kichwani kama taji.

1914:19 Mit 11:29Watu wabaya watasujudu mbele ya watu wema,

nao waovu kwenye malango ya wenye haki.

2014:20 Mit 19:4, 7Maskini huepukwa hata na majirani zao,

bali matajiri wana marafiki wengi.

2114:21 Mit 11:12; 19:17; Za 41:1Yeye anayemdharau jirani yake hutenda dhambi,

bali amebarikiwa yeye aliye na huruma kwa mhitaji.

2214:22 Mit 4:16-17Je, wale wanaopanga ubaya hawapotoki?

Bali wale wanaopanga kilicho chema

hupata upendo na uaminifu.

23Kazi zote zinazofanywa kwa bidii huleta faida,

bali mazungumzo matupu huelekea umaskini tu.

2414:24 Mit 14:8Utajiri wa wenye hekima ni taji yao,

bali upumbavu wa wapumbavu huzaa upumbavu.

2514:25 Mit 12:17Shahidi wa kweli huokoa maisha,

bali shahidi wa uongo ni mdanganyifu.

2614:26 Mit 19:23; Isa 33:6Yeye amchaye Bwana ana ngome salama,

na kwa watoto wake itakuwa kimbilio.

2714:27 Za 18:5; Mit 13:14Kumcha Bwana ni chemchemi ya uzima,

ili kumwepusha mtu na mitego ya mauti.

2814:28 2Sam 19:7Wingi wa watu ni utukufu wa mfalme,

bali pasipo watu mkuu huangamia.

2914:29 Mhu 7:8-9; Mit 15:18; Yak 1:19Mtu mwenye subira ana ufahamu mwingi,

bali anayekasirika haraka huonyesha upumbavu.

3014:30 Ay 5:2; Mdo 7:9; Mit 12:4Moyo wenye amani huupa mwili uzima,

bali wivu huozesha mifupa.

3114:31 Ay 31:15-16; Mit 17:5Yeye amwoneaye maskini huonyesha dharau kwa Muumba wao,

bali yeyote anayemhurumia mhitaji humheshimu Mungu.

3214:32 Za 34:21; Mit 6:15; Ay 13:15; 2Tim 4:18Waovu huangamizwa kwa matendo yao maovu,

bali hata katika kifo wenye haki hupata kimbilio.

3314:33 Mit 2:6-10Hekima hukaa katika moyo wa mwenye ufahamu

bali haijulikani miongoni mwa wapumbavu.

3414:34 Mit 11:11Haki huinua taifa,

bali dhambi ni aibu kwa watu wote.

3514:35 Es 8:2; Mt 25:14-30Mfalme hupendezwa na mtumishi mwenye hekima,

bali ghadhabu yake humwangukia

mtumishi mwenye kuaibisha.