歷代志下 20 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

歷代志下 20:1-37

約沙法禱告退敵

1後來摩押人、亞捫人同一些米烏尼20·1 米烏尼人」出現在古希臘譯本,但希伯來文是「亞捫人」。一起來攻打約沙法2有人稟告約沙法說:「有一支大軍從死海對岸的以東20·2 以東」希伯來文是「亞蘭」。殺來,已經攻到哈洗遜·他瑪。」哈洗遜·他瑪就是隱·基底3約沙法很害怕,決定尋求耶和華,在整個猶大宣告禁食。 4猶大人聚集起來尋求耶和華。他們從猶大各城前來尋求耶和華。

5約沙法站在耶和華殿的新院裡,在猶大耶路撒冷的民眾面前, 6說:「我們祖先的上帝耶和華啊,你不是住在天上的上帝嗎?你主宰萬邦萬國,你手中有權柄和能力,無人能抵擋你。 7我們的上帝啊,你不是曾經在你的以色列子民面前驅逐這地方的居民,把這片土地賜給你的朋友亞伯拉罕的後裔永遠作產業嗎? 8你的子民在這裡居住,為你的名建造殿宇,說, 9『如果我們遭遇禍患,無論是戰禍、瘟疫或饑荒,當我們在急難中站在這殿前向你呼求時,你必定垂聽,施行拯救,因為你的名在這殿裡。』

10「從前以色列人離開埃及的時候,你不准他們侵犯亞捫人、摩押人和來自西珥山的人,他們就繞道而行,沒有毀滅這些人。 11但現在這些人要報復我們,把我們從你賜給我們作產業的地方趕走。 12我們的上帝啊,難道你不懲罰他們嗎?面對前來攻擊的大軍,我們無力抵擋,不知道該怎麼辦,我們只有仰望你。」

13猶大人與他們的妻子、兒女和嬰孩都站在耶和華面前。 14這時,耶和華的靈降在雅哈悉身上。雅哈悉利未亞薩的後裔、瑪探雅的玄孫、耶利的曾孫、比拿雅的孫子、撒迦利雅的兒子。 15他說:「全體猶大人、耶路撒冷的居民和約沙法王啊,你們要留心聽!耶和華對你們如此說,『你們不要因敵軍強大而恐懼驚慌,因為戰爭的勝敗不在乎你們,而在乎上帝。 16明天你們下去迎敵,敵軍會從洗斯坡上來,你們一定會在耶魯伊勒曠野前面的谷口遇見他們。 17你們不用與他們交戰,只要守住陣勢,站立不動,看耶和華為你們施行拯救。猶大人和耶路撒冷人啊,不要恐懼,不要驚慌,明天只管出去迎敵,耶和華必與你們同在!』」

18於是,約沙法面伏於地,所有猶大人和耶路撒冷的居民也都俯伏在耶和華面前敬拜祂。 19哥轄族和可拉族的利未人都站起來,高聲讚美以色列的上帝耶和華。 20第二天清晨,眾人起來去提哥亞的曠野。他們出發的時候,約沙法站著說:「猶大人和耶路撒冷的居民啊,請聽我說!要信靠你們的上帝耶和華,你們就必堅立;要相信祂的先知,你們就必得勝。」 21約沙法與眾人商議後,就派歌樂手穿上聖潔的禮服走在軍隊前面,讚美耶和華,說:「你們要稱謝耶和華,因祂的慈愛永遠長存!」

22他們開始唱歌讚美的時候,耶和華就派伏兵擊殺前來攻打猶大亞捫人、摩押人和來自西珥山的人,打敗了他們。 23原來亞捫人和摩押人攻擊來自西珥山的人,消滅了他們,然後亞捫人和摩押人又自相殘殺。

24猶大人來到曠野的瞭望塔俯瞰那支大軍,發現敵軍屍橫遍野,無一倖免。 25約沙法和他的百姓前去拾財物,發現屍體中有許多財物、衣服和貴重物品,多得拿不完。他們拾了三天才拾完。 26第四天,他們聚集到一個山谷,一起稱頌耶和華。那裡從此名叫比拉迦20·26 比拉迦」就是稱讚的意思。 谷,直到今天。

27猶大人和耶路撒冷人在約沙法的帶領下,歡歡喜喜地返回耶路撒冷,因為耶和華使他們戰勝了仇敵。 28他們一路彈琴、鼓瑟、吹號回到耶路撒冷,進入耶和華的殿。 29列邦列國聽聞耶和華打敗了以色列的敵人,都很懼怕。 30因此,約沙法執政期間國家太平,因為他的上帝賜他四境平安。

約沙法逝世

31約沙法三十五歲登基做猶大王,在耶路撒冷執政二十五年。他母親叫阿蘇巴,是示利希的女兒。 32約沙法效法他父親亞撒,做耶和華視為正的事,不偏不離。 33然而,他沒有拆除邱壇,民眾還沒有全心歸向他們祖先的上帝。

34約沙法其他的事蹟自始至終都記在哈拿尼的兒子耶戶的史記上。耶戶的史記收錄在以色列的列王史上。

35後來,猶大約沙法與作惡多端的以色列亞哈謝修好。 36他們在以旬·迦別造船,要去他施37瑪利沙多大瓦的兒子以利以謝約沙法預言說:「因為你與亞哈謝修好,耶和華必破壞你所造的船隻。」那些船隻果然壞了,無法前往他施

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Nyakati 20:1-37

120:1 1Nya 4:41Ikawa baada ya jambo hili, Wamoabu na Waamoni, pamoja na baadhi ya Wameuni wakaja ili wapigane vita na Yehoshafati.

220:2 Mwa 14:7; Wim 1:14; Yos 15:62; 1Sam 23:29Watu fulani wakaja wakamwambia Yehoshafati, “Jeshi kubwa linakuja dhidi yako kutoka Edomu tokea ngʼambo ile nyingine ya Bahari.20:2 Yaani Bahari ya Chumvi. Tayari liko Hasason-Tamari” (yaani En-Gedi). 320:3 Es 4:16; Isa 58:6; Amu 20:26; Ezr 8:21-23; 1Sam 7:6; Yer 36:9; Yn 3:5Yehoshafati akaogopa, akaazimu kumtafuta Bwana, na akatangaza kwa Yuda wote kufunga. 420:4 Yoe 1:14Watu wa Yuda wakakusanyika pamoja ili kutafuta msaada kutoka kwa Bwana. Wakaja kutoka kila mji wa Yuda ili kumtafuta.

5Kisha Yehoshafati akasimama katika kusanyiko la Yuda na Yerusalemu katika Hekalu la Bwana, mbele ya ua mpya, 620:6 Mt 6:9; Kum 4:39; 1Fal 8:23; 1Nya 29:11-12; Yos 2:11; Isa 57:15; Za 47:2; 62:11; Yer 27:5; Dan 4:17; Mt 6:13akasema:

“Ee Bwana, Mungu wa baba zetu, si wewe ndiwe uliye Mungu mbinguni? Si wewe ndiwe utawalaye juu ya falme zote za mataifa? Uweza na nguvu viko mkononi mwako, wala hakuna yeyote awezaye kushindana nawe. 720:7 Isa 41:8; Yak 2:23; Mwa 17:7; Kut 6:7Je, si wewe, Ee Mungu wetu, uliyewafukuza wenyeji wa nchi hii mbele ya watu wako Israeli, ukawapa wazao wa Abrahamu, rafiki yako, hata milele? 820:8 2Nya 6:20-28Wameishi ndani yake na humo wamekujengea mahali patakatifu kwa ajili ya Jina lako, wakisema: 920:9 1Fal 8:33-37; 2Nya 6:28-29‘Kama maafa yakitujia, ikiwa ni upanga, hukumu, tauni, au njaa, tutasimama mbele zako, mbele ya Hekalu hili ambalo limeitwa kwa Jina lako na kukulilia katika shida yetu, nawe utatusikia na kutuokoa.’

1020:10 Hes 20:14-21; Kum 2:4-6, 9, 18-19“Lakini sasa hawa watu wa kutoka Amoni, Moabu na Mlima Seiri, ambao hukuwaruhusu Israeli wazivamie nchi zao wakati walitoka Misri, hivyo wakageukia mbali nao na hawakuwaangamiza, 1120:11 Za 83:1-12tazama jinsi wanavyotulipa kwa kuja kututupa nje ya milki uliyotupa sisi kuwa urithi. 1220:12 2Kor 3:5; Amu 11:27; Mik 7:7; Za 12:1-2; 1Sam 3:13; Za 46:7-11; Ufu 19:11; Za 25:15Ee Mungu wetu, je, wewe hutawahukumu? Kwa kuwa sisi hatuna uwezo wa kukabiliana na jeshi hili kubwa linalokuja kutushambulia. Sisi hatujui la kufanya, bali macho yetu yanakutazama wewe.”

13Watu wote wa Yuda pamoja na wake zao, watoto wao na wadogo wao wakasimama pale mbele za Bwana.

1420:14 Hes 11:25; 24:2; 1Nya 12:18; 2Nya 15:1; 24:20Ndipo Roho wa Bwana akaja juu ya mtu mmoja jina lake Yahazieli mwana wa Zekaria, mwana wa Benaya, Mwana wa Yeieli, mwana wa Matania, Mlawi mzao wa Asafu alipokuwa amesimama katika kusanyiko.

1520:15 2Nya 32:7; Kut 14:13-14; Za 91:8; Kum 1:29; 31:6-8Akasema: “Sikilizeni, enyi Yuda wote nanyi nyote mkaao Yerusalemu, nawe Mfalme Yehoshafati! Hili ndilo Bwana asemalo kwenu, ‘Msiogope wala msifadhaike kwa sababu ya jeshi hili kubwa. Kwa maana vita hivi si vyenu, bali ni vya Mungu. 16Kesho shukeni kukabiliana nao. Watakwea kwa kupandia Genge la Sisi, nanyi mtawakuta mwisho wa bonde, kabla ya Jangwa la Yerueli. 1720:17 Hes 14:9; 2Nya 15:2; Kut 14:13; 2Nya 32:8; Za 46:7-11; Isa 8:10; Amo 5:14Hamtahitaji kupigana vita hivi. Kaeni kwenye nafasi zenu, simameni imara na mkaone wokovu Bwana atakaowapatia, enyi Yuda na Yerusalemu. Msiogope, wala msifadhaike. Kesho tokeni mwende mkawakabili, naye Bwana atakuwa pamoja nanyi.’ ”

1820:18 Mwa 24:26; Kut 4:31Yehoshafati akainamisha uso wake chini, nao watu wote wa Yuda na Yerusalemu wakaanguka chini ili kuabudu mbele za Bwana. 19Ndipo baadhi ya Walawi kutoka kwa Wakohathi na kwa wana wa Kora wakasimama na kumsifu Bwana, Mungu wa Israeli, kwa sauti kuu sana.

2020:20 Isa 7:9; Mwa 39:3; Mit 16:3; Rum 8:31; Isa 26:3; Yn 11:40; 14:1Asubuhi na mapema wakaondoka kuelekea Jangwa la Tekoa. Walipoanza safari, Yehoshafati akasimama akasema, “Nisikilizeni, enyi Yuda, na watu wa Yerusalemu! Mwaminini Bwana Mungu wenu, hivyo mtathibitika, wasadikini manabii wake nanyi mtafanikiwa. 2120:21 1Nya 16:29; 2Nya 5:13; Za 136:1Alipomaliza kushauriana na watu, Yehoshafati akawaweka watu wa kumwimbia Bwana na kumsifu katika utukufu wa utakatifu wake walipokuwa wametangulia mbele ya jeshi, wakisema:

“Mshukuruni Bwana

kwa kuwa upendo wake wadumu milele.”

2220:22 Amu 7:22; 2Nya 13:13; 1Sam 14:20Walipoanza kuimba na kusifu, Bwana akaweka waviziao dhidi ya watu wa Amoni, Moabu na wale wa Mlima Seiri waliokuwa wamekuja kuishambulia Yuda, nao wakashindwa. 2320:23 Mwa 19:38; 2Nya 21:8; Eze 38:21Watu wa Amoni na Moabu wakawainukia watu wa Mlima Seiri ili kuwaua na kuwaangamiza kabisa. Baada ya kumaliza kuwachinja watu wa Seiri, wakaangamizana wao kwa wao.

2420:24 Isa 37:36; Yer 33:5; Kut 14:13Yuda walipofika katika mnara wa ulinzi wa jangwani, wakaliangalia lile jeshi kubwa, wakaona ni maiti tupu zimetapakaa ardhini, wala hakuna yeyote aliyenusurika. 25Hivyo Yehoshafati na watu wake wakaenda kujitwalia nyara kutoka kwao, nao wakakuta humo wingi wa mifugo, mali, nguo na vitu vya thamani, ambavyo vilikuwa vingi zaidi ya vile walivyoweza kuchukua. Wakakusanya nyara kwa siku tatu kwa sababu zilikuwa nyingi mno. 26Siku ya nne wakakusanyika katika Bonde la Beraka20:26 Bonde la Beraka maana yake Bonde la Kusifu. kwa maana huko ndiko walikomsifu Bwana. Ndiyo sababu linaitwa Bonde la Beraka mpaka leo.

2720:27 Neh 12:43Kisha watu wote wa Yuda na Yerusalemu, wakiongozwa na Yehoshafati, wakarudi Yerusalemu wakiwa na furaha kwa kuwa Bwana alikuwa amewasababisha wafurahi juu ya adui zao. 28Wakaingia Yerusalemu na kwenda hekaluni mwa Bwana wakiwa na vinubi, zeze na tarumbeta.

2920:29 Mwa 35:5; Kum 2:25; 14:14; 2Nya 17:10Hofu ya Mungu ikazipata falme zote za nchi waliposikia jinsi Bwana alivyokuwa amepigana dhidi ya adui za Israeli. 3020:30 2Nya 15:15; 1Nya 22:9; Ay 34:29Ufalme wa Yehoshafati ukawa na amani, kwa kuwa Mungu wake alikuwa amemstarehesha pande zote.

Mwisho Wa Utawala Wa Yehoshafati

(1 Wafalme 22:41-50)

3120:31 1Fal 22:41Hivyo Yehoshafati akatawala Yuda. Alikuwa na umri wa miaka thelathini na mitano alipoanza kutawala, akatawala katika Yerusalemu kwa miaka ishirini na mitano. Mama yake aliitwa Azuba binti Shilhi. 32Alienenda katika njia za Asa baba yake wala hakwenda kinyume chake. Alifanya yaliyo mema machoni pa Bwana. 3320:33 2Nya 12:14; 17:6Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa, na watu wakawa bado hawajaelekeza mioyo yao kwa Mungu wa baba zao.

3420:34 1Fal 16:1-3Matukio mengine ya utawala wa Yehoshafati, kuanzia mwanzo hadi mwisho, yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu cha Yehu mwana wa Hanani, ambazo zimeandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli.

3520:35 2Nya 16:3; 19:1-3Hatimaye Yehoshafati mfalme wa Yuda akafanya urafiki na Ahazia mfalme wa Israeli ambaye alifanya maovu sana. 3620:36 1Fal 22:49Akaungana naye kutengeneza meli nyingi za kwenda Tarshishi,20:36 Au: za biashara (ona pia 1Fal 10:22; 22:48; 2Nya 9:21; Isa 2:16; 60:9). nazo zilitengenezwa huko Esion-Geberi. 3720:37 1Fal 9:26; 2Nya 9:21; Mwa 10:4; 1Fal 10:22Ndipo Eliezeri mwana wa Dodavahu wa Maresha akatoa unabii dhidi ya Yehoshafati, akasema, “Kwa kuwa umeungana na Ahazia, Bwana ataangamiza vile mlivyotengeneza.” Zile meli zikavunjika na hazikuweza kungʼoa nanga ili kwenda Tarshishi.