歷代志上 10 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

歷代志上 10:1-14

掃羅之死

1非利士人與以色列人交戰,以色列人敗逃,許多人在基利波山被殺。 2非利士人窮追掃羅及其眾子,殺了掃羅的兒子約拿單亞比拿達麥基舒亞3掃羅周圍的戰鬥非常猛烈,他被弓箭手發現、射成重傷, 4就對為他拿兵器的人說:「拔出你的刀來刺死我吧!免得那些未受割禮的人來凌辱我。」但拿兵器的人非常害怕,不敢動手,掃羅就自己伏刀自盡。 5拿兵器的人看見掃羅已死,也伏刀自盡了。 6這樣,掃羅和他的三個兒子及全家都死了。 7住在山谷中的以色列人看見以色列軍敗逃、掃羅及其眾子已死,都棄城而逃。於是,非利士人佔領了那些城邑。 8次日,非利士人來剝陣亡者的衣物,發現掃羅及其眾子橫屍基利波山, 9就剝下掃羅的盔甲,割下他的頭顱,並派人到非利士四境向他們的偶像和民眾通告消息。 10他們將掃羅的盔甲放在他們的神廟裡,把他的頭顱掛在大袞神廟中。 11基列·雅比人聽見非利士人對掃羅的所作所為, 12他們所有的勇士就去把掃羅和他兒子們的屍體運到雅比,葬在雅比的橡樹下,並禁食七天。 13掃羅死了,因為他對耶和華不忠,不聽從祂的教誨,甚至去求問靈媒, 14而不求問耶和華。因此,耶和華使他被殺,把王位交給了耶西的兒子大衛

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Nyakati 10:1-14

Sauli Ajiua

(1 Samweli 31:1-13)

110:1 1Sam 7:7; 13:5; 31:1Basi Wafilisti wakapigana na Israeli. Waisraeli wakawakimbia, na wengi wakauawa katika mlima Gilboa. 2Wafilisti wakawafuatia kwa bidii Sauli na wanawe, wakawaua Yonathani, Abinadabu na Malki-Shua. 3Mapigano yakawa makali kumzunguka Sauli na wakati wapiga mishale walipompata, wakamjeruhi.

410:4 Amu 16:21Sauli akamwambia mbeba silaha wake, “Futa upanga wako unichome nao, la sivyo hawa watu wasiotahiriwa watakuja na kunidhalilisha.”

Lakini mbeba silaha wake akaogopa sana wala hakuweza kufanya hivyo. Kwa hiyo Sauli akachukua upanga wake mwenyewe na kuuangukia. 5Mbeba silaha wake alipoona kwamba Sauli amekufa, naye pia akauangukia upanga wake akafa. 6Kwa hiyo Sauli na wanawe watatu wakafa, pamoja na nyumba yake yote.

7Waisraeli wote waliokuwa bondeni walipoona kwamba jeshi limekimbia na kwamba Sauli na wanawe wamekufa, waliacha miji yao wakakimbia. Nao Wafilisti wakaja na kukaa humo.

8Kesho yake Wafilisti walipokuja kuwavua maiti silaha, walimkuta Sauli na wanawe wameanguka katika Mlima Gilboa. 9Wakamvua mavazi, wakachukua kichwa chake pamoja na silaha zake, wakawatuma wajumbe katika nchi yote ya Wafilisti kutangaza habari hizi miongoni mwa sanamu zao na watu wao. 1010:10 Amu 16:23; 1Sam 31:10; Isa 48:5Waliweka silaha zake katika hekalu la miungu yao, wakatundika kichwa chake katika hekalu la Dagoni.

1110:11 Amu 21:8Wakazi wote wa Yabeshi-Gileadi waliposikia yote Wafilisti waliyomtendea Sauli, 12mashujaa wao wote wakaondoka, wakautwaa mwili wa Sauli na miili ya wanawe, wakaileta Yabeshi. Wakaizika mifupa yao chini ya mti mkubwa huko Yabeshi, nao wakafunga kwa siku saba.

1310:13 2Sam 1; 1; 15:23; 1Nya 5:25; 1Sam 13:13; Kum 18:9-14; 1Sam 28:7; 1Fal 18:18; 2Nya 16:9; Kut 22:18; Law 19:31; 20:27; 2Fal 21:6Sauli alikufa kwa sababu hakuwa mwaminifu kwa Bwana. Hakulishika neno la Bwana, hata akataka shauri kwa mwaguzi kwa ajili ya uongozi, 1410:14 1Nya 12:23; 1Sam 13:14; 15:28hakumuuliza Bwana. Kwa hiyo Bwana alimuua, na ufalme akampa Daudi mwana wa Yese.