啟示錄 6 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

啟示錄 6:1-17

羔羊揭開前六印

1然後,我看見羔羊揭開七印中的第一印,那時我聽見四個活物中的一個用如雷的聲音說:「來!」 2我便觀看,見有一匹白馬,馬上的騎士拿著弓,他接受了賞賜給他的冠冕後,便四處征戰,戰無不勝。

3羔羊揭開第二印時,我聽見第二個活物說:「來!」 4這次出現了一匹紅馬,馬上的騎士獲得權柄和一把大刀,要奪取地上的和平,使人類互相廝殺。

5揭開第三印的時候,我聽見第三個活物說:「來!」我便看見一匹黑馬,馬上的騎士手裡拿著天平。 6我又聽見四個活物中好像有聲音說:「一升小麥值一個銀幣6·6 一個銀幣相當於一天的工錢。,三升大麥也同價,油和酒都不要糟蹋。」

7羔羊揭開第四印的時候,我聽到第四個活物說:「來!」 8這次我看到一匹淺灰色的馬,馬上騎士的名字叫死亡,陰府緊跟在他後面。他們得到權力可以用刀劍、饑荒、瘟疫和野獸消滅全人類的四分之一。

9羔羊揭開第五印的時候,我看到一個祭壇,祭壇下有許多靈魂,都是為傳揚上帝的道、為祂做見證而被殺的。 10他們大聲喊著說:「聖潔真實的主宰啊,還要等多久呢?為什麼你還不審判地上那些屠殺我們的人,為我們伸冤呢?」 11這時有白袍賜給他們,有聲音告訴他們要再稍候片刻,直到和他們同作奴僕的弟兄被殺害的數目滿了為止。

12羔羊揭開第六印的時候,我看見大地震發生了,太陽變得像黑毛布一樣黑,整個月亮變成血紅色, 13天上的星辰都墜落,好像未成熟的無花果被狂風吹落一般。 14天空也像書卷被捲起來,所有的山嶺和海島都被挪離原位。 15地上的君王、顯貴、將領、富豪、有勢力的、一切奴隸和自由人都躲藏在山洞裡和岩穴間。 16他們哀求群山和岩石,說:「倒下來遮蓋我們,將我們藏起來吧!我們不敢面對寶座上的那位和羔羊的烈怒啊! 17因為祂們發烈怒的大日子到了,誰能站得住呢?」

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ufunuo 6:1-17

Mwana-Kondoo Avunja Lakiri Saba

16:1 Ufu 5:6; 5:1; 19:6; 4:6-7; 14:2Kisha nikaangalia wakati Mwana-Kondoo akivunja ile lakiri ya kwanza miongoni mwa zile saba. Ndipo nikasikia mmoja wa wale viumbe wanne wenye uhai akisema kwa sauti kama ya radi: “Njoo!” 26:2 Zek 1:8; 6:11; Ufu 19:11-12; Za 45:4Nikatazama, na hapo mbele yangu alikuwepo farasi mweupe! Yeye aliyempanda alikuwa na upinde, naye akapewa taji, akampanda akatoka akiwa kama mshindi aelekeaye katika kushinda.

36:3 Ufu 4:7Alipoivunja ile lakiri ya pili, nikamsikia yule kiumbe wa pili mwenye uhai akisema, “Njoo!” 46:4 Zek 1:8; 6:2; Mt 10:34Ndipo akatokea farasi mwingine mwekundu sana. Yeye aliyempanda akapewa uwezo wa kuondoa amani duniani na kuwafanya watu wauane. Yeye akapewa upanga mkubwa.

56:5 Ufu 4:7Mwana-kondoo alipoivunja ile lakiri ya tatu, nikamsikia yule kiumbe wa tatu mwenye uhai akisema, “Njoo!” Nikatazama, na mbele yangu alikuwepo farasi mweusi! Yeye aliyempanda alikuwa na mizani mkononi mwake. 66:6 Ufu 4:6-7; 7:1-3Ndipo nikasikia kile kilichokuwa kama sauti katikati ya wale viumbe wanne wenye uhai ikisema, “Kipimo kimoja6:6 Ni kama lita moja. cha ngano kwa mshahara wa kibarua wa siku moja,6:6 Sawa na dinari moja. na vipimo vitatu vya shayiri kwa mshahara wa kibarua cha siku moja. Lakini usiharibu mafuta wala divai!”

76:7 Zek 6:3; Hos 13:14; Yer 24:10; Eze 5:12-17Alipovunja ile lakiri ya nne, nikasikia sauti ya yule kiumbe wa nne mwenye uhai ikisema, “Njoo!” 86:8 Zek 6:3; Hos 13:14; Ufu 1:18; 20:13; 14; Yer 15:2, 3; 24:10; Eze 5:12, 17Nikatazama, na hapo mbele yangu alikuwepo farasi mwenye rangi ya kijivujivu! Yeye aliyempanda aliitwa Mauti, naye Kuzimu6:8 Kuzimu linalotokana na neno Hades la Kiyunani au Sheol kwa Kiebrania. alikuwa akimfuata nyuma yake kwa karibu. Wakapewa mamlaka juu ya robo ya dunia, kuua kwa upanga, njaa, tauni na kwa wanyama wakali wa dunia.

96:9 Ufu 14:18; 16:17; 20:4Mwana-kondoo alipoivunja ile lakiri ya tano, nikaona chini ya madhabahu, roho za wale waliochinjwa kwa ajili ya neno la Mungu na kwa ajili ya ushuhuda walioutunza. 106:10 Za 119:84; 79:10; Zek 1:12; Ufu 3:7; 18:20Wakalia kwa sauti kuu, wakisema, “Hata lini, Ee Bwana Mwenyezi, uliye mtakatifu na mwaminifu, hutawahukumu na kulipiza kisasi juu ya watu waishio duniani kwa ajili ya damu yetu?” 116:11 Ufu 3:4; Ebr 11:40Kisha kila mmoja wao akapewa joho jeupe na wakaambiwa wangoje kwa muda kidogo zaidi, mpaka idadi ya ndugu zao na watumishi wenzao watakaouawa kama wao walivyouawa, itakapotimia.

126:12 Isa 29:6; Ufu 16:18; Mt 24:29Nikatazama akiivunja ile lakiri ya sita. Pakatokea tetemeko kuu la nchi, na jua likawa jeusi kama nguo ya gunia iliyotengenezwa kwa singa za mbuzi, na mwezi wote ukawa mwekundu kama damu. 136:13 Ufu 9:1; Isa 34:4Nyota zilizo angani zikaanguka ardhini kama vile matunda ya mtini yasiyokomaa yaangukavyo wakati mti wake unapotikiswa na upepo mkali. 146:14 Isa 54:10; Ufu 21:1Anga ikatoweka kama vile karatasi isokotwavyo, na kila mlima na kila kisiwa kikaondolewa mahali pake.

156:15 Isa 2:10-21Ndipo wafalme wa dunia, wakuu wote, majemadari, matajiri, wenye nguvu na kila mtu, mtumwa na mtu huru, wakajificha katika mapango na kwenye miamba ya milima. 166:16 Hos 10:8; Lk 23:30Wakaiita milima na miamba wakisema, “Tuangukieni, mkatufiche na uso wake yeye aketiye kwenye kiti cha enzi, na mkatuepushe na ghadhabu ya Mwana-Kondoo! 176:17 Yoe 1:15; Ufu 16:14; Nah 1:6; Mal 3:2Kwa maana siku ile kuu ya ghadhabu yao imewadia. Je, ni nani awezaye kustahimili?”