啟示錄 12 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

啟示錄 12:1-18

婦人與巨龍

1在天上出現了一個奇異的景象:有一個婦人,身披太陽,腳踏月亮,頭戴有十二顆星的冠冕。 2她懷了孕,正因產痛而呼叫。

3這時天上出現了另一個奇異的景象:有一條紅色巨龍出現,牠有七頭十角,每個頭上都戴著冠冕。 4牠的尾巴將天上三分之一的星掃落到地上。巨龍站在那正要生產的婦人面前,等著要吃掉她生下來的嬰孩。 5婦人生下一個男嬰,就是將來要用鐵杖治理列國的。那男嬰被提到了上帝的寶座那裡, 6婦人則逃到曠野,在上帝為她預備的地方安度一千二百六十天。

7天上起了戰爭,米迦勒和他的天使出戰巨龍。巨龍和牠的天使極力抵抗, 8那巨龍敗下陣來,天上再沒有牠們的立足之地, 9牠和牠的天使都一同從天上被摔到地上。巨龍就是那古蛇,又名魔鬼或撒旦,也就是那迷惑全人類的。

10我聽見天上有大響聲說:「我們上帝的救贖、權能、國度和祂所立的基督的權柄現在來臨了。因為那晝夜不停地在我們上帝面前控告我們弟兄的,已經被摔到地上了。 11弟兄們是靠著羔羊的血和自己所見證的道戰勝了牠,他們甘願犧牲,視死如歸。 12因此,諸天和其中的居民都要歡欣雀躍!但大地和海洋有禍了,因為魔鬼知道牠的時日不多了,就怒氣沖沖地下到你們那裡。」

13巨龍見自己被摔到地上,就迫害那先前產下男嬰的婦人。 14但那婦人得到一對巨鷹的翅膀,使她能飛到曠野,去上帝為她預備的地方避難,在那裡被照顧三年半。 15巨龍緊追不捨,張口吐出大量的水,如同江河一般,要沖走那婦人, 16大地卻幫助她,張口吞了巨龍口中吐出來的大水。 17巨龍大怒,轉而攻擊她的其他兒女,就是那些堅守上帝的誡命、為耶穌做見證的人。 18那時巨龍站在海邊的沙地上。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ufunuo 12:1-17

Mwanamke Na Joka

1Kukaonekana ishara kuu mbinguni: Palikuwa na mwanamke aliyevikwa jua, na mwezi ukiwa chini ya miguu yake, na taji ya nyota kumi na mbili ilikuwa kichwani mwake. 212:2 Gal 4:19Alikuwa na mimba naye akilia kwa uchungu kwa kuwa alikuwa anakaribia kuzaa. 312:3 Dan 7:7, 20; Ufu 13:1; 19:21Kisha ishara nyingine ikaonekana mbinguni: Likaonekana joka kubwa jekundu lenye vichwa saba na pembe kumi na taji saba katika vichwa vyake. 412:4 Ufu 8:7; Dan 8:10; Mt 22:16Mkia wake ukakokota theluthi ya nyota zote angani na kuziangusha katika nchi. Ndipo lile joka likasimama mbele ya yule mwanamke aliyekuwa karibu kuzaa ili lipate kumla huyo mtoto mara tu atakapozaliwa. 512:5 Za 2:9; Ufu 19:15Yule mwanamke akazaa mtoto mwanaume, atakayeyatawala mataifa yote kwa fimbo yake ya utawala ya chuma. Lakini huyo mtoto akanyakuliwa na kupelekwa kwa Mungu kwenye kiti chake cha enzi. 612:6 Ufu 11:2Yule mwanamke akakimbilia jangwani, ambako Mungu alikuwa amemtayarishia mahali ili apate kutunzwa huko kwa muda wa siku 1,260.

Malaika Mikaeli Amshinda Yule Joka

7Basi palikuwa na vita mbinguni: Mikaeli na malaika zake wakapigana na hilo joka, nalo joka pamoja na malaika zake likapigana nao. 8Lakini joka na malaika zake wakashindwa, na hapakuwa tena na nafasi yao huko mbinguni. 912:9 Mwa 3:1-7; Mt 25:41; Ufu 20:3, 8, 10; Lk 10:18; Yn 12:31Lile joka kuu likatupwa chini, yule nyoka wa zamani aitwaye ibilisi au Shetani, aupotoshaye ulimwengu wote. Akatupwa chini duniani, yeye pamoja na malaika zake.

Ushindi Mbinguni Watangazwa

1012:10 Ufu 11:15; Zek 3:1Kisha nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema:

“Sasa wokovu na uweza na Ufalme wa Mungu wetu umekuja

na mamlaka ya Kristo wake.

Kwa kuwa ametupwa chini

mshtaki wa ndugu zetu,

anayewashtaki mbele za Mungu

usiku na mchana.

1112:11 Ufu 7:14; 6:9; Lk 14:26Nao wakamshinda

kwa damu ya Mwana-Kondoo

na kwa neno la ushuhuda wao.

Wala wao hawakuyapenda maisha yao

hata kufa.

1212:12 Isa 44:23; Ufu 18:20; 8:13; 10:6Kwa hiyo, furahini ninyi mbingu

na wote wakaao humo!

Lakini ole wenu nchi na bahari,

kwa maana huyo ibilisi ameshuka kwenu,

akiwa amejaa ghadhabu,

kwa sababu anajua ya kuwa

muda wake ni mfupi!”

13Lile joka lilipoona kuwa limetupwa chini duniani, lilimfuatilia yule mwanamke aliyekuwa amezaa mtoto mwanaume. 1412:14 Kut 19:4; Dan 7:25Lakini huyo mwanamke akapewa mabawa mawili ya tai mkubwa, kusudi aweze kuruka mpaka mahali palipotayarishwa kwa ajili yake huko jangwani, ambako atatunzwa kwa wakati na nyakati na nusu,12:14 Maana yake ni miaka mitatu na nusu. ya wakati ambako yule joka hawezi kufika. 15Ndipo lile joka likamwaga maji kama mto kutoka kinywani mwake, ili kumfikia huyo mwanamke na kumkumba kama mafuriko. 16Lakini nchi ikamsaidia huyo mwanamke kwa kufungua kinywa na kuumeza huo mto ambao huyo joka alikuwa ameutoa kinywani mwake. 1712:17 Ufu 11:7; Mwa 3:15; Ufu 14:12; 1:2Kisha lile joka likapatwa na hasira kali kwa ajili ya huyo mwanamke na likaondoka ili kupigana vita na watoto waliosalia wa huyo mwanamke, yaani, wale wanaozitii amri za Mungu na kuushika ushuhuda wa Yesu Kristo. Lile joka likasimama kwenye mchanga wa bahari.