哥林多前書 12 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

哥林多前書 12:1-31

聖靈的恩賜

1弟兄姊妹,談到聖靈的恩賜,我不希望你們無知。 2你們知道,自己在信主前曾受到迷惑和引誘去拜不會說話的偶像。 3因此我希望你們知道,一個被上帝的靈感動的人絕不會說「耶穌該受咒詛」;若不是受了聖靈的感動,沒有人會說「耶穌是主」。

4恩賜各有不同,但聖靈是同一位。 5事奉各有不同,但主是同一位。 6工作各有不同,但上帝是同一位,祂在眾人當中成就萬事。 7聖靈給各人不同的恩賜為要使眾人得益處。 8這人從聖靈領受智言,那人從聖靈領受知識; 9聖靈賜這人信心,賜那人醫病的恩賜; 10聖靈使這人能行神蹟,使那人能作先知講道;使這人能辨別諸靈,使那人能說方言12·10 方言」或譯「語言」。,又使另一人能翻譯方言。 11這一切都是同一位聖靈所賜的,是祂按自己的旨意分別賜給各人的。

同屬一個身體

12這如同一個身體有許多肢體,肢體雖多,仍同屬一個身體。基督的身體也是這樣。 13不論是猶太人或希臘人,是奴隸或自由人,我們都領受了同一位聖靈的洗禮,歸入了同一個身體,同飲一位聖靈。

14人的身體並非只有一個肢體,乃是由許多肢體組成的。 15如果腳說:「我不是手,所以我不屬於身體。」難道腳就因此不屬於身體嗎? 16如果耳朵說:「我不是眼睛,所以我不屬於身體。」難道耳朵就因此不屬於身體嗎? 17如果整個身體是一隻眼睛,哪裡有聽覺呢?如果整個身體是一隻耳朵,哪裡有嗅覺呢?

18但事實上,上帝按自己的旨意將各個肢體安置在身體上了。 19如果全身只有一個肢體,還會是身體嗎? 20如今肢體雖多,但身體只有一個。 21眼睛不能對手說:「我不需要你。」頭也不能對腳說:「我不需要你。」

22相反,看起來不太重要的肢體事實上是不可或缺的。 23我們認為身體上不體面的肢體,越要加以美化;不雅觀的肢體,越要精心呵護。 24我們身上體面的肢體用不著美化。上帝把身體的各肢體安排在一起,使那些不體面的肢體更體面, 25這樣身體各肢體才可以彼此相顧,不會分門別類。 26如果身體某個肢體感到痛苦,全身也一同受苦。如果某個肢體得到榮耀,全身也一同喜樂。

27你們正是基督身體的不同肢體。 28上帝在教會中設立的第一是使徒,第二是先知,第三是教師,其次是行神蹟的,然後是有醫病恩賜的,幫助別人的,管理事務的,說各種方言的。 29豈是都作使徒嗎?都作先知嗎?都作教師嗎?都行神蹟嗎? 30都有醫病的恩賜嗎?都懂得說方言嗎?都會翻譯方言嗎? 31你們應該熱心追求更大的恩賜。

現在,我要將一條奇妙無比的道路指示你們!

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Wakorintho 12:1-31

Karama Za Rohoni

112:1 Rum 1:11; 1Kor 1:7; 14:1, 37; Rum 11:25Basi ndugu zangu, kuhusu karama za rohoni, sitaki mkose kufahamu. 212:2 Efe 2:2; Za 115:5; Yer 10:5; Hab 2:18-19Mnajua kwamba mlipokuwa watu wasiomjua Mungu, kwa njia moja au ingine mlishawishika na kupotoshwa mkielekezwa kwa sanamu zisizonena. 312:3 Rum 9:3; 1Kor 16:22; Yn 13:13; 4:2-3Kwa hiyo nawaambieni ya kuwa hakuna mtu anayeongozwa na Roho wa Mungu anayeweza kusema, “Yesu na alaaniwe.” Pia hakuna mtu awezaye kusema, “Yesu ni Bwana,” isipokuwa ameongozwa na Roho Mtakatifu.

412:4 Rum 12:4-8; Efe 4:11; Ebr 2:4Kuna aina mbalimbali za karama, lakini Roho ni yule yule. 512:5 Rum 12:6; Efe 4:11Kuna huduma za aina mbalimbali, lakini Bwana ni yule yule. 612:6 Efe 4:6; Flp 2:13; Efe 1:23Kisha kuna tofauti za kutenda kazi, lakini ni Mungu yule yule atendaye kazi zote kwa watu wote.

712:7 1Kor 14:12; Efe 4:12Basi kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa faida ya wote. 812:8 1Kor 2:6; 2Kor 8:7Maana mtu mmoja kwa Roho hupewa neno la hekima na mwingine neno la maarifa kwa Roho huyo huyo. 912:9 Mt 17:19-20; 1Kor 13:2; Mt 10:1Mtu mwingine imani kwa huyo Roho na mwingine karama za kuponya kwa huyo Roho mmoja. 1012:10 Gal 3:5; Efe 4:11; 1Yn 4:1; Mk 16:17Kwa mwingine matendo ya miujiza, kwa mwingine unabii kwa mwingine kupambanua roho, kwa mwingine aina mbalimbali za lugha, na kwa mwingine bado, tafsiri za lugha. 1112:11 1Kor 11:4; Rum 12:3; Efe 4:7; 1Kor 7:7Haya yote hufanywa na huyo huyo Roho mmoja, Roho naye humgawia kila mtu, kama apendavyo.

Mwili Mmoja, Wenye Viungo Vingi

1212:12 Rum 12:5; 1Kor 11:27Kama vile mwili ulivyo mmoja nao una viungo vingi, navyo viungo vyote vya mwili ingawa ni vingi, ni mwili mmoja, vivyo hivyo na Kristo. 1312:13 Efe 2:18; Gal 3:28; Kol 3:11; Yn 7:37-38Kwa maana katika Roho mmoja wote tulibatizwa katika mwili mmoja, kama ni Wayahudi au Wayunani, kama ni watumwa au watu huru, nasi sote tulinyweshwa Roho mmoja.

1412:14 1Kor 12:12, 20Basi mwili si kiungo kimoja, bali ni viungo vingi. 15Kama mguu ungesema, “Kwa kuwa mimi si mkono basi mimi si wa mwili,” hiyo isingefanya huo mguu usiwe sehemu ya mwili. 16Na kama sikio lingesema, “Kwa kuwa mimi si jicho, basi mimi si wa mwili,” hiyo isingefanya hilo sikio lisiwe sehemu ya mwili. 17Kama mwili wote ungelikuwa jicho, kusikia kungekuwa wapi? Au kama mwili wote ungelikuwa sikio, kunusa kungekuwa wapi? 1812:18 1Kor 12:28; 12:11Lakini kama ilivyo, Mungu ameweka viungo katika mwili, kila kimoja kama alivyopenda. 19Kama vyote vingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi? 20Kama ulivyo, una viungo vingi, lakini mwili ni mmoja.

21Jicho haliwezi kuuambia mkono, “Sina haja nawe!” Wala kichwa hakiwezi kuiambia miguu, “Sina haja na ninyi!” 22Lakini badala yake, vile viungo vya mwili vinavyoonekana kuwa dhaifu, ndivyo ambavyo ni vya muhimu sana. 23Navyo vile viungo tunavyoviona havina heshima, ndivyo tunavipa heshima maalum. Vile viungo vya mwili ambavyo havina uzuri, tunavipa heshima ya pekee; 24wakati vile viungo vyenye uzuri havihitaji utunzaji wa pekee. Lakini Mungu ameviweka pamoja viungo vya mwili na akavipa heshima zaidi vile vilivyopungukiwa, 25ili pasiwe na mafarakano katika mwili, bali viungo vyote vihudumiane kwa usawa kila kimoja na mwenzake. 26Kama kiungo kimoja kikiumia, viungo vyote huumia pamoja nacho, kama kiungo kimoja kikipewa heshima, viungo vyote hufurahi pamoja nacho.

2712:27 Efe 1:23; 4:12; Kol 1:18, 24; Rum 12:5Sasa ninyi ni mwili wa Kristo na kila mmoja wenu ni sehemu ya huo mwili. 2812:28 1Kor 10:32; Efe 4:11; Mk 16:17; Rum 12:6-8Mungu ameweka katika kanisa, kwanza mitume, pili manabii, tatu walimu, kisha watenda miujiza, pia karama za kuponya, karama za kusaidiana, karama za uongozi, aina mbalimbali za lugha. 29Je, wote ni mitume? Je, wote ni manabii? Je, wote ni walimu? Je, wote wanatenda miujiza? 3012:30 1Kor 12:10Je, wote wana karama ya kuponya? Je, wote hunena kwa lugha mpya? Je, wote wanatafsiri? 3112:31 1Kor 14:1, 39Basi tamanini sana karama zilizo kuu.

Nami nitawaonyesha njia iliyo bora zaidi.