傳道書 3 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

傳道書 3:1-22

萬物有時

1天下萬物都有定期,

凡事都有定時。

2出生有時,死亡有時;

耕種有時,拔出有時;

3殺戮有時,醫治有時;

拆毀有時,建造有時;

4哭泣有時,歡笑有時;

哀傷有時,雀躍有時;

5拋石有時,堆石有時3·5 拋石有時,堆石有時」意義不明,有猶太拉比說是「同房有時,分房有時」。

擁抱有時,避開有時;

6尋找有時,遺失有時;

保存有時,丟棄有時;

7撕裂有時,縫合有時;

沉默有時,發言有時;

8愛慕有時,憎惡有時;

爭戰有時,和好有時。

9那麼,人勞碌做工有什麼益處呢? 10我察覺上帝給世人重擔,使他們忙碌不休。 11祂使萬事各按其時變得美好,又把永恆的意識放在人心裡,人卻不能測透上帝從始至終的作為。 12我認識到,人生在世沒有什麼比歡樂、享受更好。 13人人都該吃喝、享受自己勞苦的成果,這是上帝的恩賜。 14我知道,上帝所做的都會存到永遠,誰也不能增減。祂這樣安排是叫人敬畏祂。 15現在的事並不是新事,未來的事也早已發生過。上帝使過去的事再次出現。

世間的不公

16我又看到日光之下,即使在公道和正義之地也有邪惡。 17我心裡想:「不論義人或惡人,上帝必審判,因為萬事萬務都有受審之時。」 18我又想:「至於世人,上帝試驗他們,是要他們知道自己與獸類無異。 19因為人和獸的際遇並無分別,兩者都難逃一死,活著都靠一口氣。人並不比獸強,一切都是虛空。 20兩者都同歸一處,出於塵土,也歸於塵土。 21誰知道人的氣息3·21 氣息」或譯「靈」,本節同。會向上升,獸的氣息會降到地下呢?」 22因此,我覺得沒有什麼比人享受工作之樂更好,因為這是人當得的。人死後,誰能使他看到世間的事呢?

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mhubiri 3:1-22

Kila Jambo Lina Wakati Wake

13:1 Mhu 8:6Kuna wakati kwa ajili ya kila jambo,

nayo majira kwa kila tendo chini ya mbingu:

23:2 Mwa 47:29; Isa 28:24; 38:1wakati wa kuzaliwa na wakati wa kufa,

wakati wa kupanda na wakati wa kungʼoa yaliyopandwa,

33:3 Kum 5:17wakati wa kuua na wakati wa kuponya,

wakati wa kubomoa,

na wakati wa kujenga,

43:4 Kut 15:20; 2Sam 6:16wakati wa kulia na wakati wa kucheka,

wakati wa kuomboleza na wakati wa kucheza,

5wakati wa kutawanya mawe na wakati wa kukusanya mawe,

wakati wa kukumbatia na wakati wa kutokumbatia,

6wakati wa kutafuta na wakati wa kupoteza,

wakati wa kuweka na wakati wa kutupa,

73:7 Amo 5:13; Es 4:14wakati wa kurarua na wakati wa kushona,

wakati wa kunyamaza na wakati wa kuzungumza,

8wakati wa kupenda na wakati wa kuchukia,

wakati wa vita na wakati wa amani.

9Mfanyakazi anapata faida gani kutokana na taabu yake? 103:10 Mhu 1:13Nimeona mzigo Mungu alioweka juu ya wanadamu. 113:11 Kum 32:4; Mhu 8:17; Ay 11:7; 28:23; Rum 11:33Amefanya kila kitu kiwe kizuri kwa wakati wake. Pia ameiweka hiyo milele katika mioyo ya wanadamu, wala hawawezi kutambua kwa kina yale ambayo Mungu amefanya tangu mwanzo hadi mwisho. 12Ninajua kwamba hakuna kitu bora kwa wanadamu kuliko kuwa na furaha na kutenda mema wakati wanapoishi. 133:13 Za 34:12; Kum 12:7, 18; Mhu 2:3, 24; 5:19Tena ni karama ya Mungu kila mtu apate kula na kunywa na kujiburudisha kwa mema katika kazi yake yote. 143:14 Ay 23:15; Yak 1:17; Mhu 5:7; 7:18; 8:12-13Ninajua kwamba kila kitu anachokifanya Mungu kitadumu milele, hakuna kinachoweza kuongezwa au kupunguzwa. Mungu hufanya hivyo ili watu wamche yeye.

153:15 Mhu 6:10; 1:9Chochote kilichopo kilishakuwepo,

na kitakachokuwepo kimekwishakuwepo kabla;

naye Mungu huyaita yale yaliyopita yarudi tena.

16Pia nikaona kitu kingine tena chini ya jua:

Mahali pa kutolea hukumu,

uovu ulikuwepo,

mahali pa kupatia haki,

uovu ulikuwepo.

173:17 Ay 34:11; 19:29; Mt 16:27; Mhu 11:9; 12:14Nikafikiri moyoni mwangu,

“Mungu atawaleta hukumuni

wote wawili wenye haki na waovu,

kwa maana kutakuwako na wakati kwa ajili ya kila jambo,

wakati kwa ajili ya kila tendo.”

183:18 Za 73:22Pia nikafikiri, “Kuhusu wanadamu, Mungu huwajaribu ili wajione kwamba wao ni kama wanyama. 193:19 Mhu 2:14; Za 49:12Hatima ya mwanadamu ni kama ile ya wanyama; wote wana mwisho unaofanana: Jinsi anavyokufa mnyama, ndivyo anavyokufa mwanadamu. Wote wana pumzi inayofanana; mwanadamu hana cha zaidi kuliko mnyama. Kila kitu ni ubatili. 203:20 Mwa 2:7; 3:19-20; Ay 34:10Wote huenda mahali panapofanana; wote hutoka mavumbini, mavumbini wote hurudi. 213:21 Mhu 12:7Ni nani ajuaye kama roho ya mtu huenda juu na roho ya mnyama hushuka chini ardhini?”

223:22 Mhu 2:10, 24; 5:18; Ay 31:2Kwa hiyo nikaona kwamba hakuna kitu kilicho bora zaidi kwa mwanadamu kuliko kuifurahia kazi yake, kwa sababu hilo ndilo fungu lake. Kwa maana ni nani awezaye kumrudisha ili aje kuona kile kitakachotendeka baada yake?