以賽亞書 65 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

以賽亞書 65:1-25

懲罰與拯救

1耶和華說:「我向沒有求問我的人顯現,

讓沒有尋找我的人尋見,

對沒有求告我的國家說,

『我在這裡,我在這裡!』

2我整天伸出雙手招呼一群悖逆的百姓,

他們卻任意妄為,

不走正路,

3不斷地當面惹我發怒。

他們在園中獻祭,

在磚臺上燒香,

4坐在墳場裡,

宿在隱秘處。

他們吃豬肉,

用不潔之物做湯,

5還對人說,『站遠點,

別挨近我,因為我比你聖潔!』

我被這些人氣得鼻孔冒煙,

整天怒火難息。

6看啊,這些都記錄在我面前,

我不會再保持緘默,

我要報應他們,

7按他們和他們祖先的罪報應他們。

我必按他們的所作所為報應他們,

因為他們在山上燒香,

在丘陵上褻瀆我。

這是耶和華說的。」

8耶和華說:「人發現一串葡萄尚可釀造新酒時,

一定會說,『不要毀壞它,

裡面還有好葡萄。』

同樣,因我僕人的緣故,

我也不會把他們全部毀滅。

9「我必使雅各的後裔興起,

使猶大人興起,

繼承我的群山。

我揀選的子民必擁有那片土地,

我的僕人必在那裡安居。

10沙崙必成為牧放羊群的草場,

亞割谷必成為牛群休憩的地方,

這些地方必屬於尋求我的人。

11但至於你們這些背棄我、

忘記我的聖山、

擺宴供奉幸運之神、

調酒祭奠命運之神的人,

12我要使你們註定被殺,

喪身刀下。

因為我呼喚你們,你們不回應;

我講話,你們不聆聽。

你們做我視為惡的事,

專行令我不悅的事。」

13所以主耶和華說:

「看啊,我的僕人必有吃有喝,

你們卻要饑渴交加;

我的僕人必歡喜,

你們卻要受羞辱;

14我的僕人必歡喜快樂,

揚聲歌唱,

你們卻要傷心欲絕,

嚎啕大哭。

15我的選民必用你們的名字作咒詛,

主耶和華必殺死你們,

給祂的僕人另起名字。

16因此,在地上求福祉的人都必向信實的上帝祈求,

在地上起誓的人都必憑信實的上帝起誓。

因為過去的苦難已經被遺忘,

從我眼前消失了。

新天新地

17「看啊,我要創造新天新地,

過去的一切都要被遺忘,

從記憶中消失。

18你們要因我創造的一切而永遠歡喜快樂。

看啊,我要創造一個充滿喜樂的耶路撒冷

其中的居民個個歡欣。

19我必因耶路撒冷而歡喜,

因我的子民而快樂。

城裡再聽不見哭泣和哀號聲。

20再沒有只活幾天便夭折的嬰兒,

也沒有壽數未盡便死的老人,

因為滿了百歲便死的人不過算是青年,

不足百歲便死的人被視為受了咒詛。

21他們要建造房屋,安然居住,

栽種葡萄園,吃園中的果子。

22他們建的房屋再不會被別人居住,

他們種的果實再不會被別人享用。

我的子民必像樹木一樣長壽,

我揀選的人必長享自己親手勞碌的成果。

23他們不會徒勞,

他們的孩子也不會遇到災禍,

因為他們及其子孫是蒙上帝賜福的人。

24他們還沒有求告,

我就已經應允;

他們正要禱告,

我就已經垂聽。

25豺狼和綿羊必一起吃草,

獅子必像牛一樣吃草,

蛇必以塵土為食。

在我的整個聖山上,

牠們都不傷人,不害物。

這是耶和華說的。」

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 65:1-25

Hukumu Na Wokovu

165:1 Rum 10:20; Efe 2:12-13; Rum 9:30; Za 22:27; Hos 1:10; Rum 9:24-26; Isa 43:7“Nilijifunua kwa watu wale ambao hawakuniulizia.

Nimeonekana na watu wale ambao hawakunitafuta.

Kwa taifa lile ambalo halikuliita Jina langu,

nilisema, ‘Niko hapa, niko hapa.’

265:2 Za 78:8; Rum 10:21; Za 81:11-12; Mit 24:2; Isa 66:18Mchana kutwa nimeinyoosha mikono yangu

kwa watu wakaidi,

wanaokwenda katika njia ambazo si nzuri,

wafuatao mawazo yao wenyewe:

365:3 Isa 1:29; Law 17:5; Ay 1:11; Yer 41:5; Eze 23:41; Yer 44:17taifa ambalo daima hunikasirisha

machoni pangu,

wakitoa dhabihu katika bustani

na kufukiza uvumba juu ya madhabahu za matofali;

465:4 Law 11:7; Isa 8:19; Law 19:31; Kum 18:11watu waketio katikati ya makaburi

na kukesha mahali pa siri,

walao nyama za nguruwe,

nazo sufuria zao zina mchuzi wa nyama zilizo najisi,

565:5 Za 40:4; Lk 7:39; Yud 19; Mt 9:11; Lk 18:9-12; Mit 10:26wasemao, ‘Kaa mbali; usinikaribie,

kwa maana mimi ni mtakatifu mno kwako!’

Watu wa aina hiyo ni moshi katika pua zangu,

ni moto uwakao mchana kutwa.

665:6 2Nya 6:23; Kum 32:34; Za 50:3; Yer 16:18; Lk 6:38; Isa 59:18; Za 79:12; Eze 9:10“Tazama, jambo hili hubakia limeandikwa mbele zangu:

sitanyamaza, bali nitalipiza kwa ukamilifu;

nitalipiza mapajani mwao:

765:7 Kut 20:5; Yer 32:18; Law 26:39; Isa 22:14; Mit 10:24; Isa 10:12; 57:7dhambi zenu na dhambi za baba zenu,”

asema Bwana.

“Kwa sababu walitoa dhabihu za kuteketezwa juu ya milima

na kunichokoza mimi juu ya vilima,

nitawapimia mapajani mwao

malipo makamilifu kwa matendo yao ya zamani.”

865:8 Isa 5:2; 54:17; Kut 4:22; Yer 3:4; Isa 29:16; Rum 9:20-21; Ay 10:3Hili ndilo asemalo Bwana:

“Kama vile divai mpya ingali bado inapatikana

katika kishada cha zabibu,

nao watu husema, ‘Usikiharibu,

kwa kuwa bado kuna kitu kizuri ndani yake,’

hivyo ndivyo nitakavyofanya kwa ajili ya watumishi wangu;

sitawaangamiza wote.

965:9 Isa 45:19; Hes 34:13; Amo 9:11-15; Isa 32:18; Yer 50:19Nitawaleta wazao kutoka kwa Yakobo,

na kutoka kwa Yuda wale watakaomiliki milima yangu,

nao watu wangu wateule watairithi,

nako huko wataishi watumishi wangu.

1065:10 1Nya 27:29; Hos 2:15; Mdo 9:35; Yos 7:26; Isa 35:2; Yer 31:12; Eze 34:13-14Sharoni itakuwa malisho

kwa ajili ya makundi ya kondoo,

na Bonde la Akori mahali pa kupumzikia

kwa makundi ya ngʼombe,

kwa ajili ya watu wangu wanaonitafuta.

1165:11 Eze 23:41; Yer 19:4; 1Kor 10:21; Kum 29:24-25; 32:15; Yer 2:13; 19:4“Bali kwenu ninyi mnaomwacha Bwana

na kuusahau mlima wangu mtakatifu,

ninyi mnaoandaa meza kwa ajili ya Bahati,65:11 Bahati alikuwa mungu wa Wakaldayo ambaye pia alijulikana kama Gadi.

na kujaza mabakuli ya mvinyo uliochanganywa

kwa ajili ya Ajali,65:11 Ajali au Meni alikuwa mungu wa majaliwa.

1265:12 Mit 1:24-25; Yer 7:27; 2Nya 36:15-16; Yer 13:11; Isa 1:20; 30:25; Mik 5:15nitawaagiza mfe kwa upanga,

nanyi nyote mtainama chini ili kuchinjwa;

kwa kuwa niliwaita lakini hamkuitika,

nilisema lakini hamkusikiliza.

Mlitenda maovu machoni pangu,

nanyi mkachagua mambo yale yanayonichukiza.”

1365:13 Isa 1:19; Ay 18:12; Lk 6:25; Isa 33:16; 60:5; 44:9Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi:

“Watumishi wangu watakula,

lakini ninyi mtaona njaa;

watumishi wangu watakunywa

lakini ninyi mtaona kiu;

watumishi wangu watafurahi,

lakini ninyi mtaona haya.

1465:14 Isa 15:2; Lk 13:28; Za 109:28; Sef 3:14-20; Yak 5:13; Mt 8:12Watumishi wangu wataimba

kwa furaha ya mioyo yao,

lakini ninyi mtalia

kutokana na uchungu wa moyoni,

na kupiga yowe kwa sababu

ya uchungu wa roho zenu.

1565:15 Hes 5:27; Mdo 11:26; Zek 8:13; Za 102:8; Mwa 32:28; Ufu 2:17Mtaliacha jina lenu

kuwa laana kwa watu wangu waliochaguliwa;

Bwana Mwenyezi atawaua ninyi,

lakini watumishi wake atawapa jina jingine.

1665:16 Za 31:5; Ufu 3:14; Isa 19:18; Kum 29:19; Ay 11:16; Za 63:11Yeye aombaye baraka katika nchi

atafanya hivyo kwa Mungu wa kweli;

yeye aapaye katika nchi

ataapa kwa Mungu wa kweli.

Kwa kuwa taabu za zamani zitasahaulika

na kufichwa kutoka machoni pangu.

Mbingu Mpya Na Dunia Mpya

1765:17 2Kor 5:17; 2Pet 3:13; Yer 3:16; Ufu 7:17; Isa 41:22; 43:18“Tazama, nitaumba

mbingu mpya na dunia mpya.

Mambo ya zamani hayatakumbukwa,

wala hayatakuja akilini.

1865:18 Kum 32:43; Za 98:1-9; Isa 25:9; Ufu 21:2Lakini furahini na kushangilia daima

katika hivi nitakavyoumba,

kwa kuwa nitaumba Yerusalemu uwe wa kupendeza,

nao watu wake wawe furaha.

1965:19 Isa 35:10; 62:5; Ufu 7:17; Kum 30:9; Isa 25:8Nami nitaifurahia Yerusalemu

na kuwafurahia watu wangu;

sauti ya maombolezo na ya kilio

haitasikika humo tena.

2065:20 Mwa 15:15; Mhu 8:12; Zek 8:4; Isa 11:8; Mwa 5:1-32“Kamwe hatakuwepo tena ndani yake

mtoto mchanga atakayeishi siku chache tu,

au mzee ambaye hataishi akatimiza miaka yake.

Yeye atakayekufa akiwa na umri wa miaka mia moja

atahesabiwa kwamba ni kijana tu,

yeye ambaye hatafika miaka mia moja,

atahesabiwa kuwa amelaaniwa.

2165:21 Isa 32:18; 2Fal 19:29; Eze 28:26; Isa 61:4; 37:30; Amo 9:14Watajenga nyumba na kuishi ndani yake;

watapanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake.

2265:22 Za 92:12-14; 21:4; 91:16; Kum 28:30; Isa 14:1Hawatajenga nyumba, nao watu wengine waishi ndani yake,

au kupanda mazao na wengine wale.

Kwa kuwa kama zilivyo siku za mti,

ndivyo zitakavyokuwa siku za watu wangu,

wateule wangu watafurahia kwa siku nyingi

kazi za mikono yao.

2365:23 Mwa 12:2; Kum 28:3-12; Mdo 2:39; Hos 9:12; Isa 49:4; 1Kor 15:58; Yer 3:4Hawatajitaabisha kwa kazi bure,

wala hawatazaa watoto ili wapatwe na majanga,

kwa kuwa watakuwa taifa lililobarikiwa na Bwana,

wao na wazao wao pamoja nao.

2465:24 Dan 9:20-23; 10:12; Mt 6:8; Isa 55:6; Ay 8:6; Zek 10:6; Isa 30:19Kabla hawajaita, nitajibu,

nao wakiwa katika kunena, nitasikia.

2565:25 Mwa 3:14; Rum 16:20; Mik 7:17; Isa 11:6; Dan 2:35; Ay 40:15; 5:23; Isa 2:4Mbwa mwitu na mwana-kondoo watalisha pamoja,

naye simba atakula nyasi kama maksai,

lakini mavumbi yatakuwa chakula cha nyoka.

Hawatadhuru wala kuharibu

katika mlima wangu mtakatifu wote,”

asema Bwana.