以賽亞書 47 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

以賽亞書 47:1-15

巴比倫的覆滅

1巴比倫的少女啊,

下來坐在塵土中吧!

迦勒底的姑娘啊,

坐在沒有寶座的地上吧!

因為你必不再嬌柔細嫩。

2你要推磨磨麵,

揭下面紗,掀起裙子,

露出大腿,涉水過河。

3你必赤身裸體,

露出羞處。

我必報仇,不放過一人。

4我們的救贖主是以色列的聖者,

祂名叫萬軍之耶和華。

5迦勒底的姑娘啊,

要靜靜地坐著,進入黑暗中,

因為你不再被稱為列國之後。

6我曾向我的子民發怒,

讓我的產業被玷污,

把他們交在你手中。

你對他們毫不留情,

甚至讓老人負極重的軛。

7你聲稱要永遠做王后,

不把這些事放在心上,

也不思想以後的結局。

8「淫逸安舒的人啊,聽著!

你以為天地間唯你獨尊,

你必不致寡居,

也不會遭喪子之痛。

9誰知寡居、喪子二事卻忽然在同一天臨到你身上。

即使你懂得許多邪術和符咒,

也於事無補。

10「你肆無忌憚地行惡,

自以為沒有人看見。

你被自己的聰明智慧欺騙,

自以為天下無雙。

11你必大禍臨頭,

不知如何祛災避禍。

災禍必落在你身上,

無可挽回。

你意想不到的禍患必突然來到。

12「你自幼就勤練符咒和五花八門的邪術,繼續施展吧!

也許會有用處,

也許會令人害怕。

13眾多的計謀使你疲憊不堪,

讓那些觀天象、

每月說預言的占星家來救你脫離將臨的災禍吧!

14「看啊,他們不過像枯草,

必遭焚燒,

無法救自己脫離烈焰。

這火並非取暖的炭火,

也不是人可以靠近的火。

15你自幼交往的占星家幫不上你,

他們都四散奔逃,無人救你。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 47:1-15

Anguko La Babeli

147:1 Mao 2:10; Isa 21:9; 23:12; Yer 51:33; Zek 2:7; Ay 2:13; Isa 29:4“Shuka uketi mavumbini,

ee Bikira Binti Babeli;

keti chini pasipo na kiti cha enzi,

ee binti wa Wakaldayo.

Hutaitwa tena mwororo wala wa kupendeza.

247:2 Mt 24:41; Kut 11:5; Amu 16:21; Mwa 24:65; Isa 32:11Chukua mawe ya kusagia, usage unga,

vua shela yako.

Pandisha mavazi yako, ondoa viatu vyako,

vuka vijito kwa shida.

347:3 Mwa 2:25; Rum 12:19; Neh 3:5; Isa 13:18-19; 20:4; 34:8; Eze 16:37Uchi wako utafunuliwa

na aibu yako itaonekana.

Nitalipa kisasi;

sitamhurumia hata mmoja.”

447:4 Yer 50:34; Amo 4:13; Isa 48:2, 17; Ay 19:25Mkombozi wetu: Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake;

ndiye yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.

547:5 Dan 2:37; Isa 13:10, 19; 9:2; 21:9; Ufu 17:18; Ay 2:13; Ufu 18:7“Keti kimya, ingia gizani,

Binti wa Wakaldayo,

hutaitwa tena malkia wa falme.

647:6 2Nya 28:9; Isa 10:13; Zek 1:15; Kum 13:15; Yer 50:11; Isa 14:6; 42:24Niliwakasirikia watu wangu

na kuaibisha urithi wangu;

niliwatia mikononi mwako,

nawe hukuwaonea huruma.

Hata juu ya wazee

uliweka nira nzito sana.

747:7 Ufu 18:7; Kum 32:29; Isa 10:13; Dan 4:30; Isa 42:23-25Ukasema, ‘Nitaendelea

kuwa malkia milele!’

Lakini hukutafakari mambo haya

wala hukuwaza juu ya kile kingeweza kutokea.

847:8 Isa 32:9; 45:6; 49:21; 54:4; Sef 2:15; Ufu 18:7“Sasa basi, sikiliza, ewe kiumbe mpenda anasa,

ukaaye mahali pako pa salama,

na kujiambia mwenyewe,

‘Mimi ndiye, wala hakuna mwingine zaidi yangu.

Kamwe sitakuwa mjane,

wala sitafiwa na watoto.’

947:9 1The 5:3; Isa 13:8; Nah 3:4; Za 55:15; Mal 3:5; Kum 18:10-11; Ufu 9:21; 18:8-10Haya mawili yatakupata, kufumba na kufumbua,

katika siku moja:

kufiwa na watoto, na ujane.

Yote yatakupata kwa kipimo kikamilifu,

ijapokuwa uchawi wako ni mwingi,

na uaguzi wako ni mwingi.

1047:10 Ay 15:31; 2Fal 21:16; Isa 5:21; 29:15; Za 52:7; 62:10Umeutegemea uovu wako,

nawe umesema, ‘Hakuna yeyote anionaye.’

Hekima yako na maarifa yako vinakupoteza

unapojiambia mwenyewe,

‘Mimi ndiye, wala hakuna mwingine zaidi yangu.’

1147:11 Dan 5:30; Za 55:15; 1The 5:3; Isa 10:3; 14:15; 21:9; Lk 17:27; Isa 17:14Maafa yatakujia,

nawe hutaweza kuyaondoa kwa uaguzi.

Janga litakuangukia,

wala hutaweza kulikinga kwa fidia;

msiba mkuu usioweza kuutabiri

utakujia ghafula.

1247:12 Kut 7:11“Endelea basi na uaguzi wako,

na wingi wa uchawi wako,

ambao umeutumikia tangu utoto wako.

Labda utafanikiwa,

labda unaweza ukasababisha hofu kuu.

1347:13 Yer 51:58; Hab 2:13; Isa 19:3; 5:29; 43:13; 57:10; 46:7; Dan 2:2Ushauri wote uliopokea umekuchosha bure!

Wanajimu wako na waje mbele,

wale watazama nyota watabiriao mwezi baada ya mwezi,

wao na wawaokoe na lile linalokuja juu yenu.

1447:14 Isa 5:24; Nah 1:10; Yer 50:30-32; Isa 30:30; 10:17Hakika wako kama mabua makavu;

moto utawateketeza.

Hawawezi hata kujiokoa wao wenyewe

kutokana na nguvu za mwali wa moto.

Hapa hakuna makaa ya kumtia mtu yeyote joto;

hapa hakuna moto wa kuota.

1547:15 Ufu 18:11; Isa 44:17Hayo ndiyo yote wanayoweza kuwatendea ninyi,

hawa ambao umetaabika nao

na kufanya nao biashara tangu utoto.

Kila mmoja atatoroka;

hakuna yeyote awezaye kukuokoa.