以賽亞書 11 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

以賽亞書 11:1-16

大衛的後裔做王

1就像樹墩上長出新的枝條,

大衛的後裔中必有一人做王。

2耶和華的靈必住在他身上,

使他有聰明和智慧、謀略和能力,

能認識並敬畏耶和華。

3他必以敬畏耶和華為樂。

他不憑眼見施行審判,

不憑耳聞斷定是非,

4而是按公義審判貧窮人,

以公正為受苦者斷案。

他必用口中的杖擊打世界,

以嘴裡的氣殺戮惡人。

5公義必作他的腰帶,

信實必作他肋下的帶子。

6那時,豺狼和綿羊羔同住,

豹子和山羊羔同臥,

牛犢和獅子同群,

小孩子可以照看牠們。

7牛與熊一起吃喝,

小牛和小熊一起躺臥,

獅子像牛一樣吃草。

8吃奶的嬰孩在毒蛇的洞口玩耍,

斷奶的孩子把手伸進蛇洞。

9在我的整個聖山上,

牠們都不傷人、不害物。

認識耶和華的人必充滿天下,

就像水充滿海洋一樣。

10到那日,耶西的根必成為引導萬民的旗幟,外族人都來尋求他,他的住處充滿榮耀。 11到那日,主必再次伸手從亞述埃及巴特羅古實以攔示拿哈馬和眾海島救回祂剩餘的子民。

12祂必向各國豎立旗幟,

召集被擄的以色列人,

把分散在世界各地的猶大人聚集起來。

13以色列必不再嫉妒猶大

猶大必不再與以色列為敵,

以色列的嫉妒和猶大的敵意必煙消雲散。

14他們必聯合起來,

向西征討非利士

向東征服以東摩押亞捫

15耶和華必使埃及的海乾涸,

揮手用焦熱的風使幼發拉底河分成七條溪流,

使人可以涉水而過。

16祂剩餘的子民必沿著大路從亞述歸回,

就像昔日以色列人離開埃及一樣。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 11:1-16

Tawi Kutoka Kwa Yese

111:1 Zek 6:12; Isa 9:7; Mdo 13:23; Ay 14:7; 2Fal 19:26-30; Isa 27:9; Ufu 5:5Chipukizi litatokea kutoka shina la Yese,

kutoka mizizi yake Tawi litazaa tunda.

211:2 Mt 3:16; Yoe 2:28; Yn 16:13; Kut 28:3; Kol 2:3; Amo 3:10; Isa 32:15; 48:16Roho wa Bwana atakaa juu yake,

Roho wa hekima na wa ufahamu,

Roho wa shauri na wa uweza,

Roho wa maarifa na wa kumcha Bwana

311:3 Isa 33:6; Yn 7:24; 2:25naye atafurahia kumcha Bwana.

Hatahukumu kwa yale ayaonayo kwa macho yake,

wala kuamua kwa yale ayasikiayo kwa masikio yake,

411:4 Ufu 19:11; Za 72:2-4; Zek 14:12; 2The 2:8; Za 18:8; Isa 14:30; Ufu 19:11; Ay 5:16bali kwa uadilifu atahukumu wahitaji,

kwa haki ataamua wanyenyekevu wa dunia.

Ataipiga dunia kwa fimbo ya kinywa chake,

kwa pumzi ya midomo yake atawaua waovu.

511:5 Isa 25:1; Efe 4:16; Kut 12:11; 1Fal 18:46Haki itakuwa mkanda wake

na uaminifu utakuwa mshipi kiunoni mwake.

611:6 Hos 2:18; Isa 65:25Mbwa mwitu ataishi pamoja na mwana-kondoo,

naye chui atalala pamoja na mbuzi,

ndama, mwana simba na ngʼombe wa mwaka mmoja watakaa pamoja,

naye mtoto mdogo atawaongoza.

711:7 Ay 40:15Ngʼombe na dubu watalisha pamoja,

watoto wao watalala pamoja,

na simba atakula majani makavu kama maksai.

811:8 Isa 65:20; 14:29; 30:6; 59:5Mtoto mchanga atacheza karibu na shimo la nyoka,

naye mtoto mdogo ataweka mkono wake

kwenye kiota cha fira.

911:9 Hab 2:14; Hes 25:12; Za 98:2-3; Ay 5:23; 1Sam 17:46; Isa 19:21; 52:10Hawatadhuru wala kuharibu

juu ya mlima wangu mtakatifu wote,

kwa kuwa dunia itajawa na kumjua Bwana

kama maji yajazavyo bahari.

1011:10 Yn 12:32; Rum 15:10-12; Mdo 11:18; Za 116:7; Isa 60:5, 10; 32:17-18; Yer 6:16Katika siku hiyo, Shina la Yese atasimama kama bendera kwa ajili ya mataifa. Mataifa yatakusanyika kwake, na mahali pake pa kupumzikia patakuwa utukufu. 1111:11 Mwa 10:22; Zek 10:10; Mik 7:12; Isa 66:19; 10:20; 19:24; Kum 30:4; Hos 11:11Katika siku hiyo Bwana atanyoosha mkono wake mara ya pili kurudisha mabaki ya watu wake waliosalia kutoka Ashuru, Misri, Pathrosi,11:11 Pathrosi ina maana Misri ya Juu. Kushi, Elamu, Babeli, Hamathi na kutoka visiwa vya baharini.

1211:12 Yn 7:35; Sef 3:10; Eze 28:25; Za 20:5; Isa 14:2; 43:5; Yer 16:15; 31:10Atainua bendera kwa mataifa

na kuwakusanya Waisraeli walioko uhamishoni;

atawakusanya watu wa Yuda waliotawanyika

kutoka pembe nne za dunia.

1311:13 2Nya 28:6; Hos 1:11; Gal 3:28; Yer 3:18; Eze 16:22; 37:16-17, 22Wivu wa Efraimu utatoweka,

na adui wa Yuda watakatiliwa mbali;

Efraimu hatamwonea Yuda wivu,

wala Yuda hatakuwa na uadui na Efraimu.

1411:14 Yoe 3:19; Sef 2:8-11; Yer 48:40; 2Nya 26:6; Amu 6:3; 11:14-18; Isa 25:3; Hes 24:18Watawashukia katika miteremko ya Wafilisti

hadi upande wa magharibi,

kwa pamoja watawateka watu nyara

hadi upande wa mashariki.

Watawapiga Edomu na Moabu,

na Waamoni watatawaliwa nao.

1511:15 Isa 19:16; 30:32; 7:20; Ufu 16:12; Kut 14:22, 29; Kum 11:10; Yer 50:38; Mwa 41:16Bwana atakausha

ghuba ya bahari ya Misri;

kwa upepo mkavu ataupeleka mkono wake

juu ya Mto Frati.

Ataugawanya katika vijito saba

ili watu waweze kuuvuka wakiwa wamevaa viatu.

1611:16 Kut 14:26-31; Yer 50:5; Isa 19:23; 35:8; 51:10; 62:10; Mwa 45:7Itakuwepo njia kuu kwa mabaki ya watu wake

wale waliosalia kutoka Ashuru,

kama ilivyokuwa kwa Israeli

walipopanda kutoka Misri.