以弗所書 6 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

以弗所書 6:1-24

父慈子孝

1你們為人子女的,要按主的旨意聽從父母,這是理所當然的。 2因為第一條帶著應許的誡命就是:「要孝敬父母, 3使你在世上蒙祝福、享長壽。」 4你們為人父母的不要激怒兒女,要照主的教導和警戒養育他們。

主僕之間

5你們作奴僕的,要戰戰兢兢、誠誠實實、懷著敬畏的心服從你們肉身的主人,就像服從基督一樣。 6不要只做一些討好人的表面工夫,要像基督的奴僕一樣從心裡遵行上帝的旨意。 7要甘心樂意地工作,像是在事奉主,不是在服侍人。 8要知道:不管是奴僕還是自由人,每個人所做的善事都會得到主的獎賞。 9你們作主人的也一樣,要善待奴僕,不可威嚇他們。要知道你們主僕同有一位在天上的主人,祂不偏待人。

上帝所賜的軍裝

10最後,你們要靠著主和祂的大能大力作剛強的人, 11要穿戴上帝所賜的全副軍裝,以便能夠抵擋魔鬼的陰謀。 12因為我們爭戰的對象不是這世上的血肉之軀,而是在這黑暗世界執政的、掌權的、管轄的和天上屬靈的邪惡勢力。 13因此,你們要用上帝所賜的全副軍裝裝備自己,好在邪惡的時代抵擋仇敵,到爭戰結束後依舊昂首挺立。 14務要站穩,用真理當作帶子束腰,以公義當作護心鏡遮胸, 15把和平的福音當作鞋子穿在腳上準備行動。 16此外,還要拿起信心的盾牌,好滅盡惡者一切的火箭。 17要戴上救恩的頭盔,緊握聖靈的寶劍——上帝的話。 18要靠著聖靈隨時多方禱告和祈求,警醒不怠地為眾聖徒禱告。 19也請你們為我禱告,求上帝賜我口才,讓我勇敢地把福音的奧祕講解明白。 20我為傳福音成了披枷帶鎖的使者。請你們為我禱告,使我能盡忠職守,放膽傳福音。

問候

21至於我的近況,推基古會詳細告訴各位。他是主內親愛的弟兄和忠心的僕人。 22我特地派他去你們那裡,好讓你們知道我們的近況,並且叫他去安慰和鼓勵你們。

23願父上帝和主耶穌基督賜給各位弟兄姊妹平安、愛心和信心! 24願所有忠貞地愛我們主耶穌基督的人都蒙恩典!

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Waefeso 6:1-24

Mafundisho Kuhusu Watoto Na Wazazi

16:1 Kol 3:20; Mt 6:20Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana, kwa kuwa hili ni jema. 26:2 Kut 20:12; Kum 5:16; 27:16; Yer 35:18; Eze 22:7; Mal 1:6; Mt 15:4; Mk 7:10“Waheshimu baba yako na mama yako,” hii ndio amri ya kwanza yenye ahadi, 36:3 Kut 20; 12; Kum 5:16“upate baraka na uishi siku nyingi duniani.”

46:4 Kol 3:21; Mit 13:24; 22:6Ninyi akina baba, msiwachokoze watoto wenu, bali waleeni kwa nidhamu na mafundisho ya Bwana.

Mafundisho Kuhusu Watumwa Na Mabwana

56:5 Tit 2:9; Kol 3:22; Efe 5:22Ninyi watumwa, watiini hao walio mabwana zenu hapa duniani kwa heshima na kwa kutetemeka na kwa moyo mmoja, kama vile mnavyomtii Kristo. 66:6 Rum 6:22; Kol 3:22, 23Watiini, si tu wakati wakiwaona ili mpate upendeleo wao, bali mtumike kama watumwa wa Kristo, mkifanya mapenzi ya Mungu kwa moyo. 76:7 Kol 3:23Tumikeni kwa moyo wote, kama vile mnamtumikia Bwana na si wanadamu. 86:8 Kol 3:24Mkijua kwamba Bwana atampa kila mtu thawabu kwa lolote jema alilotenda, kama yeye ni mtumwa au ni mtu huru.

96:9 Ay 31:13, 14Nanyi mabwana, watendeeni watumwa wenu kwa jinsi iyo hiyo. Msiwatishe, kwa kuwa mnajua ya kwamba yeye aliye Bwana wenu na Bwana wao yuko mbinguni, naye hana upendeleo.

Silaha Za Mungu

106:10 Hag 2:4; Efe 1:19Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake. 116:11 Rum 13:12Vaeni silaha zote za Mungu ili kwamba mweze kuzipinga hila za ibilisi. 126:12 Efe 1:21; Rum 8:38; Efe 1:3Kwa maana kushindana kwetu si juu ya nyama na damu, bali dhidi ya falme, mamlaka, dhidi ya wakuu wa giza na majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho. 136:13 Efe 6:11; 2Kor 6:7; 10:4, 11; Efe 5:16Kwa hiyo vaeni silaha zote za Mungu ili mweze kushindana siku ya uovu itakapokuja nanyi mkiisha kufanya yote, simameni imara. 146:14 Isa 1:5; Za 132:9Kwa hiyo simameni imara mkiwa mmejifunga kweli kiunoni na kuvaa dirii ya haki kifuani, 156:15 Isa 52:7; Rum 10:15nayo miguu yenu ifungiwe utayari tuupatao kwa Injili ya amani. 166:16 1Yn 5:4; Mt 5:37Zaidi ya haya yote, twaeni ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu. 176:17 Isa 59:17; Ebr 4:12Vaeni chapeo ya wokovu na mchukue upanga wa Roho, ambao ni Neno la Mungu. 186:18 Lk 18:1; Mt 26:41; Flp 4:6Mkiomba kwa Roho siku zote katika sala zote na maombi, mkikesha kila wakati mkiwaombea watakatifu wote.

196:19 1The 5:25; Mdo 4:29; 2Kor 3:12Niombeeni na mimi pia, ili kila nifunguapo kinywa changu, nipewe maneno ya kusema, niweze kutangaza siri ya Injili kwa ujasiri, 206:20 2Kor 5:20; Mdo 21:23ambayo mimi ni balozi wake katika vifungo. Ombeni ili nipate kuhubiri kwa ujasiri kama inipasavyo.

Salamu Za Mwisho

216:21 Mdo 20:4Tikiko, aliye ndugu mpendwa na mtumishi mwaminifu katika Bwana, atawaambia kila kitu, ili pia mpate kujua hali yangu na kile ninachofanya sasa. 226:22 Kol 4:7-9Ninamtuma kwenu kwa ajili ya kusudi hili hasa, ili mpate kujua hali yetu, na awatie moyo.

236:23 Gal 6:16; 1Pet 5:14Amani iwe kwa ndugu, na pendo pamoja na imani kutoka kwa Mungu Baba na Bwana Yesu Kristo. 246:24 Tit 2:7; 1Pet 1:8Neema iwe na wote wampendao Bwana wetu Yesu Kristo kwa upendo wa dhati. Amen.