马可福音 8 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

马可福音 8:1-38

耶稣使四千人吃饱

1那时,又有一大群人聚在一起,他们没有东西吃。耶稣就叫来门徒,说: 2“我怜悯这些人,他们跟我在一起已经三天,没有任何吃的了。 3如果让他们饿着肚子回家,他们在路上会体力不支,因为有些人是远道而来的。”

4门徒说:“在这荒野,如何找到足够的食物给这些人吃呢?”

5耶稣问:“你们有多少饼?”

门徒答道:“七个。”

6耶稣便吩咐大家坐在地上,然后拿着那七个饼祝谢了,掰开,递给门徒,让门徒分给大家,门徒就把饼分给大家。 7他们还有几条小鱼。耶稣祝谢了,叫门徒分给众人。 8大家都吃了,并且吃饱了,剩下的零碎装满了七个筐子。 9吃的人约有四千。耶稣让众人回家后, 10随即和门徒上船,来到大玛努他地区。

11法利赛人出来盘问耶稣,要求祂从天上显一个神迹给他们看看,借此试探祂。 12耶稣深深叹息道:“这世代的人为什么总是要看神迹呢?我实在告诉你们,没有神迹给这世代的人看。” 13然后,耶稣离开他们,乘船回对岸去了。

防备法利赛人和希律的酵

14门徒忘了带饼,船上只有一个饼。 15耶稣警告他们:“你们要谨慎,要提防法利赛人和希律的酵!”

16他们彼此议论说:“老师这样说,是不是因为我们没有带饼呢?”

17耶稣知道他们的心思,就说:“你们为什么议论没有带饼的事呢?难道你们还不明白、不领悟吗?你们的心还是愚顽吗? 18你们有眼不会看,有耳不会听吗?你们不记得吗? 19我掰开五个饼分给五千人吃的时候,你们捡了多少篮的零碎呢?”

门徒答道:“十二篮。”

20耶稣又说:“我用七个饼喂饱四千人的时候,你们捡了多少筐零碎呢?”

门徒答道:“七筐。”

21耶稣接着说:“你们还不明白吗?”

治好伯赛大的瞎子

22他们到了伯赛大,有人带来一个瞎子,求耶稣摸他。 23耶稣拉着瞎子的手带他走到村外,吐唾沫在他的眼睛上,并把手按在他身上,问他:“你看见什么了?”

24他抬头看了看,说:“我看见人们好像一棵棵的树,走来走去。”

25耶稣把手按在他的眼睛上,他定睛一看,便恢复了视力,什么都看得清清楚楚。 26耶稣叫他回家,并对他说:“不要再进这个村子了。”

彼得宣告耶稣是基督

27耶稣和门徒前往凯撒利亚·腓立比境内的村庄。在路上,祂问门徒:“别人说我是谁?”

28他们说:“有人说你是施洗者约翰,有人说你是以利亚,有人说你是众先知中的一位。”

29耶稣又问他们:“那么,你们说我是谁?”

彼得回答说:“你是基督!”

30耶稣吩咐他们不要泄露祂的身份。

耶稣预言自己的受难和复活

31从此,耶稣便告诉他们,人子必须受许多苦,被长老、祭司长和律法教师弃绝,杀害,但必在三天之后复活。 32耶稣清楚地把这些事告诉了他们,彼得就把祂拉到一边,劝阻祂。 33耶稣转身看了看门徒,斥责彼得说:“撒旦,退到我后面去!因为你不考虑上帝的意思,只考虑人的意思。”

34祂叫众人和门徒一起过来,对他们说:“如果有人要跟从我,就应当舍己,背起他的十字架跟从我。 35因为想救自己生命的,必失去生命;但为了我和福音而失去生命的,必得到生命。 36人就是赚得全世界,却丧失自己的生命,又有什么益处呢? 37他还能用什么换回生命呢?

38“在这淫乱、罪恶的世代,如果有人以我和我的道为耻,人子在父的荣耀中与圣天使再来的时候,也要以他为耻。”

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Marko 8:1-38

Yesu Alisha Wanaume 4,000

(Mathayo 15:32-39)

18:1 Mt 15:32Katika siku hizo, umati mkubwa wa watu ulikusanyika tena. Kwa kuwa walikuwa hawana chakula, Yesu akawaita wanafunzi wake akawaambia, 28:2 Mt 9:36“Ninauhurumia huu umati wa watu, kwa sababu sasa wamekuwa nami kwa muda wa siku tatu na hawana chakula. 3Nikiwaaga waende nyumbani bila kula, watazimia njiani kwa sababu baadhi yao wametoka mbali.”

4Wanafunzi wake wakamjibu, “Lakini hapa nyikani tutapata wapi mikate ya kutosha kuwalisha?”

58:5 Mt 15:34; Mk 6:38Yesu akawauliza, “Mna mikate mingapi?”

Wakajibu, “Tuna mikate saba.”

6Akawaambia watu waketi chini. Akiisha kuichukua mikate saba na kushukuru, akaimega na kuwapa wanafunzi wake ili wawagawie watu. Wanafunzi wake wakafanya hivyo. 78:7 Mt 14:19Walikuwa pia na visamaki vichache, Yesu akavibariki, akawaamuru wanafunzi wake wawagawie watu. 88:8 Mk 8:20Wale watu walikula na kutosheka. Baadaye wanafunzi wakakusanya vipande vilivyosalia, wakajaza vikapu saba. 9Watu waliokula walikuwa wapata 4,000. Akiisha kuwaaga, 108:10 Mt 15:39aliingia kwenye mashua pamoja na wanafunzi wake, akaenda sehemu za Dalmanutha.

Mafarisayo Waomba Ishara

(Mathayo 12:38-42; 16:1-4)

118:11 Mt 12:38Mafarisayo wakaja, wakaanza kumhoji Yesu. Ili kumtega, wakamwomba awaonyeshe ishara kutoka mbinguni. 128:12 Mk 7:34Akahuzunika moyoni, akawaambia, “Kwa nini kizazi hiki kinataka ishara? Amin nawaambieni, hakitapewa ishara yoyote.” 13Kisha akawaacha, akarudi kwenye mashua, akavuka hadi ngʼambo.

Chachu Ya Mafarisayo Na Ya Herode

(Mathayo 16:5-12)

148:14 Mt 16:5Wanafunzi walikuwa wamesahau kuchukua mikate ya kutosha. Walikuwa na mkate mmoja tu kwenye mashua. 158:15 1Kor 5:6-8; Lk 12:1; Mt 14:1; Mk 12:13Yesu akawaonya: “Jihadharini na chachu ya Mafarisayo na ya Herode.”

168:16 Mt 16:7Wakajadiliana wao kwa wao, na kusema, “Anasema hivi kwa sababu hatukuleta mikate.”

178:17 Isa 6:9-10; Mk 6:52Yesu, akifahamu majadiliano yao, akawauliza: “Mbona mnajadiliana kuhusu kutokuwa na mikate? Je, bado hamtambui wala hamwelewi? Je, mbona mioyo yenu ni migumu kiasi hicho? 188:18 Yer 5:21; Eze 12:2Je, mna macho lakini mnashindwa kuona, na mna masikio lakini mnashindwa kusikia? Je, hamkumbuki? 198:19 Lk 9:17; Yn 6:13Nilipoimega ile mikate mitano kuwalisha watu 5,000, mlikusanya vikapu vingapi vilivyojaa vya masazo?”

Wakamjibu, “Kumi na viwili.”

208:20 Mk 8:6-9; Mt 15:37“Je, nilipoimega ile mikate saba kuwalisha watu 4,000, mlikusanya vikapu vingapi vilivyojaa vya masazo?”

Wakamjibu, “Saba.”

218:21 Mk 6:52Ndipo akawauliza, “Je, bado hamwelewi?”

Yesu Amponya Kipofu Huko Bethsaida

228:22 Mt 11:21; Mk 10:46; Yn 9:1Wakafika Bethsaida na baadhi ya watu wakamleta mtu mmoja kipofu wakamsihi Yesu amguse. 238:23 Mk 7:33; 5:23Yesu akamshika mkono huyo kipofu akampeleka nje ya kijiji. Baada ya kuyatemea mate macho ya yule kipofu na kumwekea mikono, Yesu akamuuliza, “Unaona chochote?”

24Yule kipofu akaangalia, akasema, “Ninaona watu, wanaonekana kama miti inayotembea.”

25Yesu akamwekea tena mikono machoni. Kisha macho yake yakafunguka, kuona kwake kukarejea naye akaona kila kitu dhahiri. 268:26 Mt 8:14; Mk 5:43Yesu akamuaga aende nyumbani kwake, akimwambia, “Hata kijijini usiingie.”

Petro Amkiri Yesu Kuwa Ndiye Kristo

(Mathayo 16:13-20; Luka 9:18-21)

278:27 Mt 16:13; Lk 9:18Yesu na wanafunzi wake wakaondoka kwenda katika vijiji vya Kaisaria-Filipi. Walipokuwa njiani, Yesu akawauliza, “Watu husema mimi ni nani?”

288:28 Mt 3:1; Mal 4:5Wakamjibu, “Baadhi husema wewe ni Yohana Mbatizaji, wengine husema ni Eliya, na bado wengine husema wewe ni mmojawapo wa manabii.”

298:29 Yn 6:69; 11:27Akawauliza, “Je, ninyi mnasema mimi ni nani?”

Petro akajibu, “Wewe ndiwe Kristo.”8:29 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta.

308:30 Mt 17:9; Lk 9:21Yesu akawaonya wasimwambie mtu yeyote habari zake.

Yesu Atabiri Kifo Chake

(Mathayo 16:21-28; Luka 9:22-27)

318:31 Mt 8:20; 16:21; 27:1-2; Mdo 2:23Ndipo akaanza kuwafundisha wanafunzi wake kuwa Mwana wa Adamu lazima atapata mateso mengi na kukataliwa na wazee, viongozi wa makuhani, na walimu wa sheria, na kwamba itampasa auawe lakini baada ya siku tatu afufuke. 328:32 Yn 18:20Aliyasema haya waziwazi, ndipo Petro akamchukua kando na akaanza kumkemea.

338:33 Mt 4:10Lakini Yesu alipogeuka na kuwaangalia wanafunzi wake, akamkemea Petro. Akasema, “Rudi nyuma yangu, Shetani! Moyo wako hauwazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu.”

348:34 Mt 10:38; Lk 14:27Ndipo akauita ule umati wa watu pamoja na wanafunzi wake, akasema, “Mtu yeyote akitaka kunifuata, ni lazima ajikane mwenyewe, auchukue msalaba wake, anifuate. 358:35 Yn 12:25Kwa maana yeyote anayetaka kuyaokoa maisha yake atayapoteza, lakini yeyote atakayeyapoteza maisha yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili atayaokoa. 36Je, itamfaidi nini mtu kuupata ulimwengu wote, lakini akayapoteza maisha yake? 37Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake? 388:38 Mt 8:20; 10:33; Lk 12:9; 1The 2:19Mtu yeyote akinionea aibu mimi na maneno yangu katika kizazi hiki cha uzinzi na dhambi, Mwana wa Adamu naye atamwonea aibu wakati atakapokuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu.”