罗马书 8 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

罗马书 8:1-39

随从圣灵而活

1因此,如今那些在基督耶稣里的人不被定罪, 2因为赐人生命之圣灵的律已经在基督耶稣里使我获得自由,脱离了罪与死的律。 3律法因为人性软弱而无法成就的事,上帝亲自成就了。祂差遣自己的儿子成为和罪人一样有血有肉的人,作了赎罪祭,废掉了罪的权势, 4使律法公义的要求实现在我们这些不随从罪恶本性,只随从圣灵而活的人身上。

5随从罪恶本性的人顾念罪恶本性的事,但随从圣灵的人顾念圣灵的事。 6顾念罪恶本性的人结局是死亡,但顾念圣灵的人却有生命和平安。 7因为顾念罪恶本性的人与上帝为敌,不服从上帝的律法,也无力服从。 8所以受罪恶本性控制的人无法令上帝喜悦。

9但如果上帝的灵住在你们里面,你们就不再受制于罪恶的本性,而是受圣灵管理。人若没有基督的灵,就不属于基督。 10如果基督在你们里面,你们的身体虽然因罪恶而死亡,灵魂却因上帝所赐的义而活着。 11如果使耶稣复活之上帝的灵住在你们里面,叫基督耶稣从死里复活的上帝,必借着住在你们里面的圣灵,使你们终有一死的身体活过来。

12弟兄姊妹,这样看来,我们不必随从罪恶本性活着。 13你们若随从罪恶本性活着,必定死亡;但若靠着圣灵除去身体的恶行,就必活着。

14因为凡有上帝的圣灵引导的人都是上帝的儿女。 15你们接受的圣灵不是使你们做奴隶,仍旧害怕,而是使你们做儿子,可以称上帝为“阿爸,父亲”。 16圣灵亲自与我们的心一同见证我们是上帝的儿女。 17既然我们是儿女,就是继承人,是上帝的后嗣,并且与基督同做后嗣。所以,如果现在我们和基督一同受苦,将来也必和祂一同得荣耀。

将来的荣耀

18我认为现在所受的痛苦与将来要显给我们的荣耀相比,简直微不足道。 19受造之物正热切等候上帝众子的显现, 20因为受造之物处在虚空之下并非出于情愿,而是出于上帝的旨意。 21不过,受造之物仍然盼望脱离衰亡之律的奴役,享受上帝儿女荣耀的自由。 22我们知道一切受造之物至今都在呻吟,如同经历分娩之痛。 23不但如此,就是我们这些首先得到圣灵的人也在心里叹息,热切等候得到儿子的名分8:23 儿子的名分”指被收养为义子,可以享受和亲生儿子一样的权利。,就是我们的身体得到救赎。 24我们得救的人有这个盼望。不过,看得见的盼望根本不算盼望,因为谁会盼望已经看见的呢? 25但我们若盼望那尚未看见的,就会忍耐等候。

26况且,我们软弱的时候,有圣灵帮助我们。我们本来不知道怎样祷告,但圣灵亲自用说不出来的叹息替我们祈祷。 27洞悉人心的上帝知道圣灵的意思,因为圣灵是照着上帝的旨意替圣徒祈祷。

28我们知道,上帝使万事互相效力8:28 上帝使万事互相效力”或译“万事都互相效力”。,使那些爱上帝,就是上帝按自己的旨意呼召的人得益处。 29因为上帝预先知道谁是属祂的人,并预定这些人要被塑造成祂儿子的形象,使祂的儿子在许多弟兄中成为长子。 30祂所预定的人,祂也呼召他们;祂所呼召的人,祂也称他们为义人;祂称为义人的,祂也使他们得荣耀。

上帝的爱

31对于这些事,我们还可以说什么呢?上帝若帮助我们,谁能与我们对抗? 32上帝既然连自己的儿子也不顾惜,让祂为我们牺牲,岂不也把万物和祂一同白白地赐给我们吗? 33谁能指控上帝拣选的人呢?上帝已经称他们为义人了。 34谁能定他们有罪呢?基督耶稣已经替他们死了,而且祂还从死里复活了,如今在上帝的右边替我们祈祷。 35谁能使我们与基督的爱分离呢?难道是患难吗?困苦吗?迫害吗?饥饿吗?赤身露体吗?危险吗?刀剑吗? 36正如圣经上说:“为了你,我们终日出生入死,被视为待宰的羊。”

37然而,靠着爱我们的主,我们在这一切事上已经得胜有余了。 38因为我深信无论是死、是生,是天使、是鬼魔,是现在的事、是将来的事, 39是高天之上的、是大地深处的或是其他受造之物,都不能使我们与上帝在主基督耶稣里赐下的爱分离。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Warumi 8:1-39

Maisha Katika Roho

18:1 Rum 16:3; 8:34, 39; 16:3Kwa hiyo, sasa hakuna hukumu ya adhabu kwa wale walio ndani ya Kristo Yesu, wale ambao hawaenendi kwa kuufuata mwili bali kwa kufuata Roho. 28:2 1Kor 15:45; Rum 6:18; 6:16; 7:4Kwa sababu sheria ya Roho wa uzima katika Kristo Yesu imeniweka huru mbali na sheria ya dhambi na mauti. 38:3 Mdo 13:39; Ebr 10:1-4; 2:14, 17Kwa maana kile ambacho sheria haikuwa na uwezo wa kufanya, kwa vile ilivyokuwa dhaifu katika mwili, Mungu kwa kumtuma Mwanawe mwenyewe kwa mfano wa mwanadamu mwenye mwili ulio wa dhambi na kwa ajili ya dhambi, yeye aliihukumu dhambi katika mwili, 48:4 Rum 2:26; Gal 5:16, 25ili kwamba haki ipatikanayo kwa sheria itimizwe ndani yetu sisi, ambao hatuenendi kwa kuufuata mwili bali kwa kufuata Roho.

58:5 Gal 5:19-21Kwa maana wale wanaoishi kwa kuufuata mwili huziweka nia zao katika vitu vya mwili, lakini wale wanaoishi kwa kufuata Roho, huziweka nia zao katika mambo ya Roho. 68:6 Rum 6:21, 23; 8:13; Gal 6:8Kwa maana kuwa na nia ya mwili ni mauti, bali kuwa na nia inayoongozwa na Roho ni uzima na amani. 78:7 Yak 4:4; Mt 12:34; Yn 8:43; 12:39Kwa kuwa ile nia ya mwili ni uadui na Mungu, kwa maana haiitii sheria ya Mungu, wala haiwezi kuitii. 88:8 Gal 5:24Wale wanaotawaliwa na mwili, hawawezi kumpendeza Mungu.

98:9 Kol 4:6; 2Tim 1:14; Mdo 16:7; 1Yn 4:13Lakini ninyi, hamtawaliwi na mwili, bali na Roho, ikiwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu. Mtu yeyote ambaye hana Roho wa Kristo, yeye si wa Kristo. 108:10 Kol 1:27; Ufu 3:20Lakini kama Kristo anakaa ndani yenu, miili yenu imekufa kwa sababu ya dhambi, lakini roho zenu zi hai kwa sababu ya haki. 118:11 Mdo 2:24; Yn 5:21; Rum 6:5Nanyi ikiwa Roho wa Mungu aliyemfufua Yesu kutoka kwa wafu anakaa ndani yenu, yeye aliyemfufua Kristo Yesu kutoka kwa wafu ataihuisha pia miili yenu ambayo hufa, kwa njia ya Roho wake akaaye ndani yenu.

128:12 Rum 6:7, 18Kwa hiyo ndugu zangu, sisi tu wadeni, si wa mwili, ili tuishi kwa kuufuata mwili, 138:13 Gal 6:8; Rum 6:23; 6; 2; 8:6; Gal 6:8kwa maana mkiishi kwa kuufuata mwili, mtakufa, lakini kama mkiyaua matendo ya mwili kwa Roho, mtaishi. 148:14 Gal 5:18; Hes 1:10; Efe 1:5Kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, hao ndio watoto wa Mungu. 158:15 2Tim 1:7; Ebr 2:15; Mk 14:36; Kol 4:5, 6Kwa maana hamkupokea roho ya utumwa iwaleteayo tena hofu, bali mlipokea roho ya kufanywa wana, ambaye kwa yeye twalia, “Abba,8:15 Abba ni neno la Kiaramu ambalo maana yake ni Baba; ni neno ambalo lingetumiwa na mtoto kwa yule ambaye amemzaa. yaani, Baba,” 168:16 2Kor 1:22; Efe 1:13Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu ya kwamba sisi tu watoto wa Mungu. 178:17 Efe 3:6; Tit 3:7; 2Tim 2:12; 1Pet 4:13Hivyo, ikiwa sisi ni watoto, basi tu warithi, warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo, naam, tukiteswa pamoja naye tupate pia kutukuzwa pamoja naye.

Utukufu Ujao

188:18 1Pet 4:13Nayahesabu mateso yetu ya wakati huu kuwa si kitu kulinganisha na utukufu utakaodhihirishwa kwetu. 198:19 Rum 8:14Kwa maana viumbe vyote vinangoja kwa shauku kudhihirishwa kwa watoto wa Mungu. 208:20 Mwa 3:17-19; 5:29Kwa kuwa viumbe vyote viliwekwa chini ya ubatili, si kwa chaguo lao, bali kwa mapenzi yake yeye aliyevitiisha katika tumaini, 218:21 2Pet 3:13; Ufu 21:1ili kwamba viumbe vyote vipate kuwekwa huru kutoka kwa utumwa wa kuharibika na kupewa uhuru wa utukufu wa watoto wa Mungu.

228:22 Yer 12:4Kwa maana twajua ya kuwa hata sasa viumbe vyote vimekuwa vikilia kwa maumivu kama utungu wa mwanamke wakati wa kuzaa. 238:23 2Kor 5:5; 5:2, 4; Gal 5:5Wala si hivyo viumbe peke yao, bali hata sisi ambao ndio matunda ya kwanza ya Roho, kwa ndani tunalia kwa uchungu tukisubiri kwa shauku kufanywa wana wa Mungu, yaani, ukombozi wa miili yetu. 248:24 1The 5:8; Tit 3:7Kwa kuwa tuliokolewa kwa tumaini hili. Lakini kama kinachotumainiwa kikionekana hakiwi tumaini tena. Je, kuna mtu anayetumaini kupata kitu alicho nacho tayari? 258:25 Za 37:7Lakini tunapotumaini kupata kitu ambacho hatuna, basi twakingojea kwa saburi.

268:26 Efe 6:18Vivyo hivyo, Roho hutusaidia katika udhaifu wetu, kwa sababu hatujui kuomba ipasavyo. Lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa uchungu usioweza kutamkwa. 278:27 Ufu 2:23Naye Mungu aichunguzaye mioyo, anaijua nia ya Roho, kwa sababu Roho huwaombea watakatifu sawasawa na mapenzi ya Mungu.

Tunashinda Na Zaidi Ya Kushinda

288:28 Ebr 9:15; 1Pet 2:9Nasi tunajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hutenda kazi pamoja na wote wampendao, katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake. 298:29 Rum 11:2; 1Pet 1:2; Efe 1:5, 11; Flp 3:21; 1Yn 3:2Maana wale Mungu aliowajua tangu mwanzo, pia aliwachagua tangu mwanzo, wapate kufanana na mfano wa Mwanawe, ili yeye awe mzaliwa wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi. 308:30 Efe 1:5, 11; Rum 4:25; 1Kor 6:11; Rum 9:23Nao wale Mungu aliotangulia kuwachagua, akawaita, wale aliowaita pia akawahesabia haki, nao wale aliowahesabia haki, pia akawatukuza.

Upendo Wa Mungu

318:31 Rum 6:1; 7:7; Isa 8:10; Ebr 13:6Tuseme nini basi kuhusu haya? Ikiwa Mungu yuko upande wetu, ni nani awezaye kuwa kinyume chetu? 328:32 Mt 3:17; Yn 3:16Ikiwa Mungu hakumhurumia Mwanawe, bali alimtoa kwa ajili yetu sote, atakosaje basi kutupatia vitu vyote kwa ukarimu pamoja naye? 338:33 Isa 50:8, 9Ni nani atakayewashtaki wale ambao Mungu amewateua? Ni Mungu mwenyewe ndiye mwenye kuwahesabia haki. 348:34 Rum 5:6-8; Mk 16:19; Ay 16:20; Yn 2:1Ni nani basi atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu aliyekufa, naam, zaidi ya hayo, aliyefufuliwa kutoka kwa wafu, yuko mkono wa kuume wa Mungu, naye pia anatuombea. 358:35 1Kor 4:11; 2Kor 11:26, 27Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je, ni shida au taabu au mateso au njaa au uchi au hatari au upanga? 368:36 Za 44:22; 2Kor 6:9Kama ilivyoandikwa:

“Kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa;

tumehesabiwa kama kondoo wa kuchinjwa.”

378:37 1Kor 15:57; Efe 5:2; Ufu 3:9Lakini katika mambo haya yote tunashinda, naam na zaidi ya kushinda, kwa yeye aliyetupenda. 388:38 Kol 1:16; 1Pet 3:22Kwa maana nimekwisha kujua kwa hakika ya kuwa sio mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka, wala yaliyopo, wala yatakayokuja, wala wenye uwezo, 398:39 Rum 5:8wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kingine chochote zitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu, Bwana wetu.