约珥书 3 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

约珥书 3:1-21

上帝要审判万国

1“到那日,在我复兴犹大耶路撒冷的时候, 2我要聚集万国,带他们下到约沙法3:2 约沙法”意思是“耶和华审判”。谷,在那里审判他们,因为他们把我的子民,就是我的产业以色列,分散到各国,并瓜分我的土地。 3他们抽签分了我的子民,将男童换妓女,卖女童买酒喝。

4泰尔西顿非利士境内所有的人啊,你们为什么这样对我?你们要报复我吗?如果你们是报复我,我必速速使你们遭报应。 5你们夺去我的金银,抢走我的珍宝,拿去放在你们的庙中, 6并把犹大耶路撒冷的居民卖给希腊人,使他们远离家乡。 7然而,他们被卖到哪里,我要从哪里把他们带回来,并要使你们得到报应, 8我要把你们的儿女卖给犹大人,犹大人必把他们卖给远方的示巴人。这是耶和华说的。”

9你们去向万国宣告:

“要召集勇士,征调军队,

前去打仗!

10要将犁头打成刀剑,

把镰刀铸成矛头,

软弱的人也要做勇士!

11四围的列国啊,

你们快快聚集到那里吧!”

耶和华啊,

求你差遣大能的勇士降临。

12“万国都要起来,

上到约沙法谷受审判,

因为我要坐在那里审判他们。

13开镰吧,因为庄稼熟了;

踩踏吧,因为榨酒池的葡萄满了。

他们恶贯满盈,如酒池满溢。”

14千千万万的人聚集在审判谷,

因为耶和华的日子要临到那里。

15日月昏暗,

星辰无光。

16耶和华从锡安发出怒吼,

耶路撒冷发出雷声,

天地为之震动。

但耶和华却是祂子民的避难所,

以色列人的堡垒。

17“这样,你们就知道我是你们的上帝耶和华,

我住在锡安——我的圣山上。

耶路撒冷必成为圣地,

外族人必不再侵犯它。

18“到那日,群山要滴下甜酒,

丘陵要流出乳汁。

犹大的溪涧碧水常流,

必有清泉从耶和华的殿中流出,

浇灌什亭谷。

19埃及必一片荒凉,

以东必成为不毛之地,

因为他们曾残暴地对待犹大人,

犹大滥杀无辜。

20犹大必人口兴盛,

耶路撒冷必存到万代。

21我必追讨3:21 追讨”希伯来文是“洗净”。尚未追讨的血债,

因为耶和华住在锡安。”

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yoeli 3:1-21

Mataifa Yahukumiwa

13:1 Kum 30:3; Yer 16:15; 40:5; Eze 3:20; 38:8“Katika siku hizo na wakati huo,

nitakaporejesha neema ya Yuda na Yerusalemu,

23:2 Zek 14:2; Isa 13:9; 2Nya 20:26; Isa 66:16; Yer 2:35; Sef 3:8; Mwa 11:4; Law 26:33nitayakusanya mataifa yote na kuyaleta

katika Bonde la Yehoshafati3:2 Yehoshafati maana yake Bwana huhukumu.

Hapo nitaingia kwenye hukumu dhidi yao

kuhusu urithi wangu, watu wangu Israeli,

kwa kuwa waliwatawanya watu wangu

miongoni mwa mataifa

na kuigawa nchi yangu.

33:3 Oba 1:11; Amo 2:6; Ay 6:27; Eze 24:6Wanawapigia kura watu wangu

na kuwauza wavulana ili kupata makahaba;

waliwauza wasichana

ili wapate kunywa mvinyo.

43:4 Mwa 10:15; Mt 11:21; Yak 2:13; Lk 18:7; Amo 1:6-9; Isa 14:29-31; 34:8; Za 87:4; Eze 25:15-17“Sasa una nini dhidi yangu, ee Tiro na Sidoni, nanyi nchi zote za Ufilisti? Je, mnanilipiza kwa yale niliyoyafanya? Kama mnalipa, mimi nitalipiza juu ya vichwa vyenu kwa kasi na kwa haraka yale mliyoyatenda. 53:5 1Fal 15:18; 2Nya 21:16-17Kwa kuwa mlichukua fedha na dhahabu yangu pia mkabeba hazina zangu nzuri sana mkapeleka kwenye mahekalu yenu. 63:6 Eze 27:13; Zek 9:13Mliwauza watu wa Yuda na Yerusalemu kwa Wayunani, ili kwamba mpate kuwapeleka mbali na nchi yao.

73:7 Isa 43:5-6; 66:6; Yer 23:8“Tazama nitawaamsha kutoka zile sehemu mlizowauza, nami nitawalipiza juu ya vichwa vyenu kile mlichofanya. 83:8 Eze 23:42; Isa 14:2; 60:14; Mwa 10:7; Yer 30:16; 2Nya 9:1Nitawauza wana wenu na binti zenu kwa watu wa Yuda, nao watawauza kwa Waseba, taifa lililo mbali.” Bwana amesema.

93:9 Isa 8:9; Yer 46:4Tangazeni hili miongoni mwa mataifa:

Jiandaeni kwa vita!

Amsha askari!

Wanaume wote wapiganaji

wasogee karibu na kushambulia.

103:10 Zek 12:8; Isa 2:4; Mik 4:3; Hes 25:7Majembe yenu yafueni yawe panga

na miundu yenu ya kukatia iwe mikuki.

Aliye dhaifu na aseme,

“Mimi nina nguvu!”

113:11 Eze 38:15-16; Sef 3:8; Isa 13:3Njooni haraka, ninyi mataifa yote kutoka pande zote,

kusanyikeni huko.

Shusha wapiganaji wako, Ee Bwana!

123:12 Za 96:13; 82:1; 2Nya 20:26; Isa 2:4“Mataifa na yaamshwe;

na yasonge mbele kuelekea Bonde la Yehoshafati,

kwa kuwa nitaketi mahali pale

kuhukumu mataifa yote yaliyoko kila upande.

133:13 Isa 17:5; Ufu 14:15-20; Amu 6:11; Mt 13:39; Mk 4:29; Yer 51:33; Hos 6:11Tia mundu,

kwa kuwa mavuno yamekomaa.

Njooni, mkanyage zabibu,

kwa kuwa shinikizo la kukamua zabibu limejaa

na mapipa yanafurika:

kwa kuwa uovu wao ni mkubwa!”

143:14 Isa 2:4; 13:4; 34:2-8; Sef 1:7; Yoe 1:15; Eze 36:5Umati mkubwa, umati mkubwa

katika bonde la uamuzi!

Kwa kuwa siku ya Bwana ni karibu

katika bonde la uamuzi.

15Jua na mwezi vitatiwa giza,

na nyota hazitatoa mwanga wake tena.

163:16 Amu 5:4; Isa 14:16; 25:4; 42:13; 2Sam 22:3; Zek 9:12; Eze 38:19Bwana atanguruma kutoka Sayuni

na mshindo wa ngurumo kutoka Yerusalemu;

dunia na mbingu vitatikisika.

Lakini Bwana atakuwa kimbilio la watu wake,

ngome imara kwa ajili ya watu wa Israeli.

Baraka Kwa Watu Wa Mungu

173:17 Yoe 2:27; Za 74:2; Isa 4:3; 35:8; Ufu 21:27; Nah 1:15; Kut 6:7; Yer 31:40; Eze 44:9“Ndipo mtakapojua kwamba Mimi, Bwana Mungu wenu,

nakaa Sayuni, mlima wangu mtakatifu.

Yerusalemu utakuwa mtakatifu;

kamwe wageni hawatavamia tena.

183:18 Kut 3:8; Eze 47:1; Zek 13:1; Wim 5:1; Isa 25:6; 30:25; 35:6; 44:3; Ufu 22:1-2; Hes 25:1; Yoe 2:24“Katika siku hiyo milima itadondosha divai mpya,

na vilima vitatiririka maziwa;

mabonde yote ya Yuda yatatiririka maji.

Chemchemi itatiririka kutoka kwenye nyumba ya Bwana

na kunywesha Bonde la Shitimu.3:18 Au: Bonde la Migunga.

193:19 Yer 51:35; Oba 1:10; Isa 11:14; 34:11Lakini Misri itakuwa ukiwa,

Edomu itakuwa jangwa tupu,

kwa sababu ya jeuri waliofanya kwa watu wa Yuda,

ambao katika nchi yao

walimwaga damu isiyo na hatia.

203:20 Ezr 9:12; Amo 9:15Yuda itakaliwa na watu milele

na Yerusalemu itadumu vizazi vyote.

213:21 Eze 36:25; 48:35; Isa 1:15; 59:20; Za 74:2; Zek 8:3Hatia yao ya damu, ambayo sijasamehe,

nitasamehe.”

Bwana anakaa Sayuni!